Tuesday, 12 December 2017

Majonzi miili 14 ya Wanajeshi wa Jeshi la Wananchi (JWTZ) ikipokelewa.

Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam jana ulikuwa eneo la majonzi makubwa baada ya miili ya askari 14 wa Jeshi la Wananchi (JWTZ), waliouawa na waasi wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC), kufika nchini hatimaye.

Miili hiyo ilirejeshwa majira ya jioni na kupokelewa na umati wa askari wa JWTZ wakiongozwa na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk. Hussein Mwinyi pamoja na Mkuu wa Majeshi, Jenerali Venance Mabeyo.

Ni mara ya kwanza kwa wanajeshi wengi kiasi hicho wa JWTZ kuuawa katika misheni ya kulinda amani, kwa mujibu wa Jenerali Mabeyo aliyekuwa akijibu maswali ya waandishi wa habari uwanjani hapo.

Miili hiyo ililetwa na ndege maalum ya Umoja wa Mataifa huku ikiwa imefunikwa bendera ya UN.

Baada ya kuwasili, kwa huzuni wanajeshi walianza kuchukua mwili mmoja baada ya mwingine na kuhamishia katika magari maalum yaliyokuwa yameandaliwa.

Kila mwili ulibebwa na wanajeshi nane wakati wa kuhamishia katika magari hayo kwa ajili ya kusafirisha kwenda kuilaza katika Hospitali Kuu ya Jeshi ya Lugalo, jijini.

Jumla ya magari saba yalitumika kubebea miili hiyo, kila moja ikibeba miili miwili na kusindikizwa na kundi la wanajeshi.

Akizungumza kabla ya kuanza safari hiyo ya kwenda Hospitali ya Lugalo, Dk. Mwinyi alisema miili hiyo inatarajiwa kuagwa Alhamisi katika viwanja vya Wizara ya Ulinzi, eneo la Upanga.

Pia alisema tukio la kuuawa kwa wanajeshi hao wamelipokea kwa masikitiko makubwa na kwamba wataendelea kuchukua tahadhari ili kuzuia kutokea kwa tukio kama hilo tena.

Kwa upande wake, Jenerali Mabeyo alisema tukio kama hilo ni la kwanza kutokea na kwamba hawajatetereka.

“Unavyolinda amani, lazima utegemee lolote, na tukio hili ni la kwanza katika kipindi cha miaka mitano," alisema Jenerali Mabeyo. "Hatuna hofu."

"Isipokuwa unaposhambuliwa, unajitazama umekosea wapi halafu unajirekebisha."

Aidha, mkuu wa majeshi alisema hali ya wanajeshi waliojeruhiwa ambao wako Kinshansa, DRC na nchini Uganda inaendelea vizuri na kwamba mmoja aliyepotea kati ya wawili amepatikana.

Kufuatia vifo hivyo, Rais John Magufuli ambaye pia ni Amiri Jeshi Mkuu alituma salamu za rambirambi kwa Waziri Mwinyi, Jenerali Mabeyo, maofisa wote wa Jeshi na kwa familia zote za marehemu mwishoni mwa wiki iliyopita.

Katika salamu hizo Rais Magufuli alisema: “Nimepokea kwa mshtuko mkubwa taarifa za kuuawa askari wetu kumi na wanne na wengine arobaini na wanne kujeruhiwa, na wawili hawajapatikana huko DRC wakati wakitekeleza majukumu ya ulinzi wa amani.

"Natoa pole sana kwa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania na familia, (na) wakati tukisubiri taarifa kamili kutoka DRC niwaombe Watanzania tuwe na subira."Mungu wetu yuko pamoja nasi."

Taarifa ya Umoja wa Mataifa iliyotolewa na Katibu Mkuu wa UN, Antonio Guterres Ijumaa ilisema shambulio hilo ndilo baya zaidi kuwahi kutekelezwa dhidi ya walinda amani wa umoja huo katika historia yake miaka ya karibuni.Pia alielezea kusikitishwa na tukio hilo.

“Ningependa kueleza kusikitishwa kwangu na shambulio hilo lililotekelezwa usiku wa jana (Alhamisi) dhidi ya walinda amani wa Umoja wa Mataifa nchini DRC," alisema katika taarifa hiyo.

"Shambulio hilo lilitekelezwa kwenye kambi ya jeshi ya Semuliki, eneo la Beni katika mkoa wa Kivu Kaskazini.Taarifa ya UN ilisema pia wanajeshi watano wa Jeshi la DRC (FARDC) waliuawa kwenye shambulio hilo.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Msagasumu Awakata Ngebe Wanawake Wanaomshobokea " Nina Mke Wangu Acheni Shobo".

NGULI wa Muziki wa Singeli, Selemani Jabir ‘Msaga Sumu’, amewakata ngebe wanawake ambao wamekuwa wakimshobokea wakati yeye ana mke na watoto wawili.

Akizungumza na Full Shangwe, Msaga Sumu anayebamba na Ngoma ya Mwanaume Mashine alisema kuwa hana mpango na wanawake wanaomshobokea na haitakuja kutokea kwani ana ndoa yake anayoipenda.

“Imekuwa kero sasa, ninachoweza kuwaambia ni kwamba wanawake waache kunishobokea, Kwanza watambue kuwa ninaipenda familia yangu na kwa sasa ninatimiza miaka nane ya ndoa yangu, na nina watoto wawili, inshallah Mungu kanijalia,”alisema Msaga Sumu na kuongeza;

“Kwa sasa najipanga kuzindua rasmi Mwanaume Mashine ndani ya Dar Live hivyo soon nitatangaza.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Dully Sykse Atokwa Povu Kisa Bomberdier Atangaza Vita kwa Wasanii Wenzake.

ETI kisa Bombardier! Mkongwe wa Bongo Fleva nchini, Dully Sykse ametoa povu ikiwemo kutangaza vita na wasanii wa kizazi kipya kwa sababu ya kushindwa kumsapoti kwenye wimbo wake mpya.

Dully Sykes ambaye ameachia wimbo mpya wa Bombardier, alisema wasanii wa sasa ambao wengi ni wapya wana roho mbaya na yeye yuko tayari kupambana nao.

“Wasanii wa sasa wana roho mbaya, hawasapotiani kama wasanii wa zamani, ndiyo maana Bombadier yangu hawajanisaidia kuitangaz, hiyo inaonesha muziki ni vita na mimi niko tayari kupambana nao,” alisema Dully 

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Shamsa Ford Amfunda Shilole "Kuwa Mke Bora kwa Mumeo Ustar Weka Pembeni".

STAA wa Filamu nchini, Shamsa Ford amefungukia uamuzi wa msanii mwenzake wa Muziki, Zuwena Mohammed maarufu kama Shilole kwa kuamua kufunga ndoa tena ya Kidini na mpenzi wake, Uchebe ndoa iliyoshuhudiwa hivi karibuni na kutikisa kwenye mitandao na vyombo vya habari huku ikiwaacha midomo wazi kwa wale walidhani kuwa angerudiana na mpenzi wake wa zamani, Nuh Mziwanda.
Shamsa ambaye pia alifunga ndoa mwaka huu na mpenzi wake, Chidi Mapenzi ametumia ukurasa wake wa Instagram kumsihi Shilole atulie, aweke umaarufu pembeni, aitunze ndoa yake na hatimaye atafaidi matunda ya ndoa iliyo bora.
Shamsa ameandika;
“Hongera sana mamy. Umefanya maamuzi sahihi ya kumpendeza Mwenyezi Mungu.Cha muhimu uwe mke bora wa Kitanzania kwa mumeo na ustar uweke pembeni.
“Mumuweke Mungu mbele, uvumilivu na kuheshimiana inshaallah mtazikana.Karibu kwenye Chama mama….Sasa nyie mnao subili matajiri wawaoe wakati hao matajiri wana wake zao wameanza nao moja mtasubili sana mpaka uso uote sugu.Uzuri na Ustar una mwisho wake. Iitafika muda hata inzi hakusogelei……HONGERA MAMA @shilolekiuno_badgirlshishi,” ameadika Shamsa.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Monday, 11 December 2017

Hili ndilo Kombora jipya la korea Kaskazini Linaloweza Kuitandika Marekani.

Korea Kaskazini imetoa picha za jaribio la kombora lake jipya ambalo inadai kuwa linaweza kushambulia popote pale nchini Marekani.

Picha hizo zinaonyesha kiongozi wa Korea Kaskazini Ki Jong un na maafisa wengine kadha ya ngazi za juu jeshini wakisherehekea kombora la Hwasong-15 wakati likipaa.

Wengi wameshangazwa na ukubwa wa kombora hilo. Picha hii ambayo haijulikanai ilichukuliwa lini na iliyotolewa na vyombo vya habari vya taifa inaonyesha Kim akilikagua kombora hilo.

Michael Duitsman, mtafiti katika kituo kimoja alisema kuwa kombora hilo ni kubwa kuliko kombora la kwanza la Hwasong-14 "ni nchi chache tu zinaweza kuunda kombora kama hilo na Korea Kaskazini imejiunga nazo."

Pia linaonekana kuwa na kichwa kikubwa ikimaanisha kuwa linaweza kubeba bomu zito la nyuklia kwenye kichwa chake.

Yote haya yanaashiria kuwa kombora hilo lina uwezo kwa kusafirisha bomu la nyuklia kwa muda mrefu.

Lilisherehekewa kwa sigara

Kim mwenye furaha anaonekana akicheka kwa furaha  wakati kombora hilo linapaa. Linaaminiwa kuwa kombora la kwanza la Korea Kaskazini lililopaa mbali zaidi katika kilomita 4,475.

Bw Kim na wenzake walionekana wakisherehekea  mafanikio ya jaribio hilo kwa sigara.

Credit: BBC

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

“Timu ya Taifa si Sehemu ya Kujifunzia Ukocha”-Mwambusi Arusha Dongo.

Kocha aliyetamba na kikosi cha Mbeya City Juma Mwambusi ametoa maoni yake kuhusiana na timu ya taifa ya Tanzania bara ‘Kilimanjaro Stars’ kufanya vibaya kwenye mashindano ya Chalenji 2017 ambapo amesema, timu ya taifa sio mahali pa kujifunzia ukocha.

Mwambusi ambaye amewahi kufanya kazi kama kocha msaidizi kwenye timu ya Yanga ameonesha kusikitishwa na matokeo mabovu ya Kili Stars kwenye mashindano ya mwaka huu na kuongeza huenda ugeni wa mwalimu ukawa moja ya tatizo kwa timu hiyo kushindwa kufanya vyema.

“Kinachosikitisha watanzania ni timu yetu kufanya vibaya sana katika mashindano ya Chalenji yanayoendelea kule Kenya. Kubwa kama mwalimu ni kuelezana ukweli, watanzania wanataka matokeo mazuri kitu ambacho kocha aliyeteuliwa na wachezaji lazima wajitume na kujitolea kwa ajili ya nchi yao.”

“Timu ya Taifa watu wanaitegemea ni kigezo gani TFF wanakitumia kuteua kocha ni swali ambalo nimekuwa nikiulizwa na wadau wengi wa soka kwa sababu wanaamini kutokana na taaluma yangu na uzoefu huenda nikawa najua, lakini hata mimi sifahamu TFF ndio wenye majibu na wanatakiwa kuwajibu watanzania wapenda michezo kwamba ni vigezo vipi wanavyovitumia.”

“Mwalimu huyu ni mgeni katika soka la Tanzania labda kama alicheza lakini hajafundisha kwa sababu lazima ufundishe vilabu vya ligi kuu ili uweze kuteuliwa mwalimu wa timu ya taifa, lakini sio kufundisha tu umefanya nini katika klabu au vilabu ulivyofundisha. Una wasifu mzuri unawajua watanzania unajua utamaduni wa wachezaji wetu, kwa sababu mwalimu anaweza kuwa mzuri lakini anafundisha katika mazingira yapi na yeye katoka mazingira gani?”

“Watanzania wataendelea kuumia hadi lini kutokana na matokeo ya timu yao ya taifa? Isiwe sehemu ya kujaribia makocha ni kutowapa thamani watanzania ambao mioyo yao inapenda sana matokeo mazuri kutoka kwa timu yetu.”

“Nakumbuka Rais mstaafu wa awamu ya pili Ali Hassani Mwinyi aliwahi kusema “timu yetu imekuwa kichwa cha mwendawazimu” kwa hiyo kuifuta hii kauli ni lazima tufanye vizuri. Inatakiwa timu iwe na mwelekeo, naishauri TFF kwamba walimu wapo waliofundisha ligi kuu wamefanya vizuri wanatakiwa wapewe nafasi wafundishe timu ya taifa tumechoka kuumia, timu ya taifa sio sehemu ya kwenda kujifunzia au kujaribia.”

“Wachezaji tutawalaumu lakini labda waliletewa utamaduni ambao hawajauzoea na wao wanatakiwa kujituma katika timu yao kwa sababu sisi watanzania tunaumia.” 
Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Monday, 4 December 2017

Simba Kicheko Tu....Haya Ndo Mambo 10 Bilionea Mohammed Dewji Atakayoanza Nayo Baada ya Kukabidhiwea Timu Hiyo.

Bilionea Mohammed Dewji ameipokea kwa mikono miwili ishu yake ya ushindi kuwa mwekezaji mpya Simba na ametoa ahadi zake 10 kuhakikisha zinafanyika kuleta mabadiliko makubwa.

Mo Dewji ameshinda zabuni ya kuwa mwekezaji wa Simba kwa dau la Sh bilioni 20 alizoweka ‘mezani’ na hakukuwa na mtu yoyote aliyejitokeza kushindana naye kama ilivyokuwa ikielezwa awali.

MOJA:
Kambi ya Simba itajengwa upya kabisa na itakuwa ni hosteli ya kisasa yenye vyumba hadi 35. 30 vitakuwa kwa ajili ya wachezaji na vitano kwa ajili ya benchi la ufundi.
 
MBILI:
Simba sasa itafaidika kwa kuwa na gym yake ya kisasa, bwawa kubwa la kuogelea kwa ajili ya mazoezi na sehemu ya kupumzika kwa wachezaji.
 
TATU:
Wachezaji, makocha na viongozi watakuwa na mgahawa wao wa kisasa kabisa.
 
NNE:
Mo Dewji anaamini timu lazima iwe na viwanja vya mazoezi. Hivyo ataanza na viwanja viwili, kimoja nyasi asilia na kingine nyasi bandia.
 
TANO:
Mo Dewji ameahidi kuwekeza katika soka la vijana akianza na wale wenye umri wa chini ya miaka 14, 16 na 18 na lengo ni kuwakuza.
 
SITA:
Mo Dewji amesema atasimamia wachezaji kuitambua thamani ya Simba kwa kujituma hasa.

SABA:
Simba itaanza kufanya mambo kimataifa kwa kuitangaza na kuikuza brand ikiwa ni pamoja na kutengeneza vifaa mbalimbali kama fulana, kofia, vishika ufunguo na kadhalika.

NANE:
Ameahidi kutenga kitita cha  Sh milioni 500 ambazo zitatumiwa na benchi la ufundi katika mipango yao kama kambi na kadhalika pia Sh bilioni moja kwa ajili ya usajili.

TISA:
Kushindana na timu kubwa Afrika na sio Tanzania pekee.

KUMI:
Kurejesha Simba katika historia ya kimataifa

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

MENEJA WA ULIMWENGU AELEZA NAMNA ALIVYOVUNJA MKATABA NA TIMU YA NDEMLA SWEDEN.

Jamal Kisongo ambaye ni meneja wa straika, Thomas Ulimwengu, yupo kwenye mchakato wa kuvunja mkataba wa mteja wake huyo dhidi ya timu ya AFC Eskilstuna iliyokuwa ikishiriki Ligi Kuu ya Sweden kufuatia kushuka daraja.

Timu hiyo ndiyo inayojiandaa kumchukua Said Ndemla ambaye amefuzu majaribio akitokea klabu ya Simba ya nchini.

Ulimwengu alijiunga na timu hiyo msimu uliopita ambapo alisaini mkataba wa miaka mitatu na hadi anafikia uamuzi huu hakuwahi kucheza mechi yoyote ya ligi kutokana na kusumbuliwa na majeraha ya goti anayouguza mpaka sasa.

Kisongo alisema kuwa kwa sasa yupo kwenye mchakato wa kumtafutia timu nyingine Ulimwengu ambapo anaamini mpaka Januari, mwakani, atakuwa amepata timu kubwa inayoshiriki ligi kuu na hatarejea Sweden tena.

Meneja huyo aliongeza kuwa kwa sasa Ulimwengu yupo nchini hapa akifanya mazoezi binafsi ya kujiimarisha baada ya kutoka Ubelgiji alikokuwa kwa mapumziko binafsi.

“Nipo kwenye mchakato wa kumtafutia timu Ulimwengu na ninaamini hadi kufika Januari nitakuwa nimepata ile ambayo inashiriki ligi kuu na hatarudi tena Sweden. Tunataka kuvunja mkataba na wale AFC Eskilstuna kwa kuwa imeshuka daraja licha ya kuwa tumebakiza miaka mawili kwenye mkataba,” alisema Kisongo.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

KOCHA NINJE AELEZA KIKOSI CHAKE KILIVYOJITAHIDI CHALENJI..

Kocha Mkuu wa Tanzania Bara ‘Kilimanjaro Stars’, Ammy Conrad Ninje amepanga kesho Jumanne Desemba 5, 2017 kuanza kufanyia kazi upungufu ulioonekana kwenye mchezo dhidi ya Libya  uliofanyika Jumapili Desemba 3, mwaka huu.

Katika mchezo huo uliofanyika Uwanja wa Kenyatta ulioko Machakos hapa nchini Kenya, Tanzania Bara ilipata sare katika safari ya kuwania Kombe la Cecafa – michuano inayofanyika hapa Kenya.

Ninje amesema katika mchezo huo wa kwanza waliecheza katika kiwango cha kuridhisha na kikubwa anataka kuangalia namna ya kufanyia kazi upungufu ikiwa ni pamoja na pale timu inapopoteza mpira.

Anasema kwenye mchezo dhidi ya Libya timu ilicheza kuanzia nyuma kupitia sehemu ya kiungo na kuunganisha sehemu ya ushambuliaji – jambo ambalo limemfurahisha kwa namna timu ilivyotengeneza nafasi.

Akizungumzia mchezo unaofuata dhidi ya Zanzibar Heroes, Ninje amesema ni mchezo mgumu kama ambavyo historia inaonesha wakati timu hizo mbili zinapokutana.

“Lakini kuanzia mazoezi ya kesho nitaiandaa timu kupata ushindi na nimepanga kwenda kuitazama Zanzibar itakapocheza mchezo wake wa kesho dhidi ya Rwanda,” amesema.

Amesema ataiangalia Zanzibar Heroes kiufundi ili kubaini upungufu wao ili naye ajue namna atakavyoweza kutumia nafasi hizo kwenye mchezo unaofuata.

“Ni fahari kwa timu zetu hizi mbili kila mmoja kupambana kupata pointi bahati nzuri wao wanacheza kesho kwa hiyo mchezo wao nitautumia kutazama mapungufu (upungufu wao) yao yatakayoweza kutusaidia," alisema Ninje.

Leo Desemba 4, mwaka huu asubuhi kikosi cha Kilimanjaro Stars kimefanya mazoezi ya kuondoa uchovu baada ya mechi ya jana kabla ya hapo kesho kuanza rasmi kujiandaa kwa mchezo huo unaofuata.

Mbarak Yusuph ndiye mchezaji pekee ambaye hakufanya mazoezi hayo baada ya kuumia misuli kwenye mchezo wa jana dhidi ya Libya.
Mbarak atapumzishwa kwenye mchezo unaofuata ili kuwa tayari kuikabili Rwanda.

Leo jioni Kocha Ninje atakutana na wachezaji kuutathmini mchezo wa Libya ambao ulimalizika kwa sare ya bila kwenye Uwanja wa Kenyatta, Machakos.

Kilimanjaro Stars ipo kundi A pamoja na timu za Zanzibar, Libya, Rwanda na wenyeji Kenya.


Kenya wana pointi tatu baada ya kuifunga Rwanda mabao 2-0 wakati Kilimanjaro Stars na Libya wana pointi 1 kila mmoja baada ya kutoka sare ya bila kufungana kwenye mchezo wao wa kwanza wakati Zanzibar na Rwanda wenyewe hawana pointi huku Zanzibar ikiwa haijashuka dimbani katika kundi hilo.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Bunduki ya Nassari Yachunguzwa na Polisi Mkoani Arusha.

Wakati mbunge wa Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Nassari akilihusisha tukio la kuvamiwa nyumbani kwake na watu wasiojulikana na masuala ya kisiasa, polisi inashikilia bunduki ya mwanasiasa huyo kwa uchunguzi.

Polisi mkoani Arusha imesema imeanza uchunguzi wa kina wa kuwasaka washukiwa, huku ikichunguza silaha ya Nassari aina ya shotgun, ikisema tukio hilo lina utata kutokana na mazingira lilivyotokea.

Kamanda wa polisi wa mkoa, Charles Mkumbo aliliambia gazeti hili kuwa wameanza uchunguzi wa kina ili kubaini endapo kulikuwa na tukio au la.

“Tunaifanyia uchunguzi bunduki yake, tunataka kujiridhisha endapo kulikuwa na tukio au la,” alisema Mkumbo.

Hata hivyo, kamanda huyo alisema msako unaendelea ili kuwabaini washukiwa na kwamba hawajapata maganda ya risasi zinazodaiwa kutumika katika uvamizi huo.

Juzi Nassari aliwaambia waandishi wa habari kuwa nusu saa baada ya kuwasili nyumbani kwake alisikia hali isiyo ya kawaida ndani ya uzio wa nyumba na baadaye kulisikika milio ya risasi. Alisema mbwa wake aliyekuwa akibweka alinyamaza, hali iliyomfanya achukue silaha yake kujihami.

“Nilipiga risasi tano, kisha kukawa kimya nikaenda kuwaamsha vijana wanaonisaidia hapa nyumbani kuwaeleza tukio lililotokea kisha nikaondoka.”

Alisema waliofanya tukio hilo hawakujua kama ana silaha kwa sababu mwaka 2014 wakati wa uchaguzi wa Serikali za mitaa, bastola yake ilichukuliwa na polisi na hadi leo haijarudishwa, hivyo kuwa na silaha nyingine kulimsaidia kujibu mapigo.

Katika tukio hilo, Nassari alisema aliwajibu watu hao kwa kupiga risasi tano hewani huku wenyewe wakipiga 12 na moja ilimpata mbwa wake ambaye alimzika juzi katika maeneo ya nyumba anayoishi.

Hivi karibuni mbunge huyo aliwasilisha makao makuu ya Takukuru ushahidi wa CD aliodai kuwa unawahusisha madiwani wa Chadema mkoani Arusha kushawishiwa kuhamia chama taw 

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Soma Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo Jumatatu.

26 Job Opportunities at Tanesco Tanzania

Job Opportunity at Tigo Tanzania, Regional Distribution Coordinator

Job Opportunity at EGPAF, Project Coordinator

Job Opportunity at EGPAF, Health Information System (HIS) Officer

Job Opportunity at EGPAF, Technical Officer TB services

Sales Jobs at METL (2 Vacancies)

Nafasi zingine Bonyeza www.ajirayako.co.tz

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Diamond, Tudd Thomas Washinda Tuzo Nigeria.

Msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz na Muandaaji wa muziki, Tudd Thomas wote kutoka Tanzania wameshinda tuzo za African Entertainment Legends Awards (AELA) jana Desemba 3, 2017 jijini Lagos, nchini Nigeria.

Diamond Platnumz ameshinda tuzo ya kolabo bora ya mwaka 2017 kupitia wimbo wake wa FIRE aliomshirikisha msanii kutoka Nigeria Tiwa Savage huku producer Tuddy Thomas akinyakua tuzo ya Muandaaji bora wa muziki kwa mwaka 2017 barani Afrika.

Wengine walioshinda tuzo hizo ni Davido kupitia wimbo wake wa Coolest Kid in Afrika kwenye kipengele cha ‘Best Music Video of the Year’, RunTown, Black Coffee na wengine wengi.

Tazama orodha kamili ya washindi wa Tuzo hizo za (African Entertainment Legends Awards 2017) . 

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Shilole Harusi Yangu Ipo Pale Pale Mwezi Huu.

Zikiwa zimesalia siku kadhaa mwaka 2017 kumalizika, msanii Shilole amezidi kusisitiza azma yake ya kufunga ndoa kwa mwaka huu ipo pale pale.

Mwishoni mwa weendend iliyomalizika katika sherehe ya ndoa ya Dj wa Clouds Media, Dj Zero shilole katika kutoa nasaha zake alisema mwezi huu atafunga ndoa.

Pia hivi karibuni kupitia ukurasa wake wa mtandao wa Instagram, Shilole alimweleza msanii wa filamu Bongo, Steven Nyerere kuwa harusi yake ipo pale pale.

Shilole ambaye yupo katika mahusiano na mpenzie, Uchebe hivi karibuni walioneka wakiwa wote Igonga, Tabora nyumbani kwa kina Shilole.  July Mwaka huu ndio Shilole alimuweka wazi mpenzi wake huyo na kueleza mwaka watafunga ndoa. 

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa