Tuesday, 19 June 2018

LIVE: DIAMOND Anazungumza na Waandishi Muda Huu Fatilia sasa.



Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Wednesday, 18 April 2018

Kimenuka: Jeshi la Polisi Limeshikilia Hati za Kusafiria na Simu za Wasanii Nandy, Billnass, Hamissa Mobetto na Diamond.

DAR: Jeshi la Polisi linashikilia hati za kusafiria pamoja na simu za wasanii Diamond Platnumz, Nandy, Billnass na Hamisa Mobetto kwa uchunguzi zaidi

Wasanii hao walikamatwa na kuhojiwa juzi na jana katika Kituo Kikuu cha Polisi kisha kuachiwa kwa dhamana wakitakiwa kuripoti tena Ijumaa Aprili 20

Wasanii hao walikamatwa na kuhojiwa kutokana na kusambaa kwa video zao zisizo na maadili katika mitandao ya kijamii

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Saturday, 14 April 2018

Video ya utupu ya Nandy na Bill Nass yawawekea uzibe Harmonize na Diamond Platnumz.

Kwa wafuatiliaji wa mitandao ya kijamii nchini Tanzania, hususani kwa wale ambao wanamfuatilia Diamond Platnumz utagundua kuwa jana Aprili 12, 2018 aliahidi kuachia video ya wimbo wa ‘Kwa ngwaru’ ambayo amemshirikishwa na Harmonize lakini mpaka sasa hivi hakuna chochote kile walichofanya.

Diamond kupitia kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii jana aliahidi kuachia video ya Kwa ngwaru kwa kuahidi kuwa endapo angepata maoni (Comments) 10,000 kwenye posti yake aliyochapisha kwenye mtandao wa instagram, basi wangeachia video ya wimbo huo ambao umetokea kupendwa sana na mashabiki wa wakali hao lakini posti hiyo hadi sasa imefikisha comments elfu 13 na video hiyo bado haija achiwa.

Hii haina ubishi kuwa video ya utupu ya Nandy na Bill Nass imepoteza attention kwa mashabiki wengi wa muziki nchini Tanzania kutokana na ukubwa wa wasanii hao ambao kila Mtanzania alikuwa anaamini kuwa ndio zao jipya la wasanii wa kizazi kipya.

Hata hivyo, mpaka sasa hivi si Diamond wala Harmonize aliyetoa kauli yoyote ile kuhusiana na kuachia video hiyo ingawaje mashabiki wengi walitazamia kuona video hiyo kwa siku ya jana.

Kwa mujibu wa maelezo ya Nandy na Bill Nass kuhusu video yao ya utupu iliyovuja siku ya jana hadi sasa bado haijajulikana ni nani aliyevujisha kwani wamekuwa wakitupiana lawama kila mmoja.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Video ya Utupu ya Bilnass na Nandy Yaizima Kwangaru ya Daimond.

Kwa wafuatiliaji wa mitandao ya kijamii nchini Tanzania, hususani kwa wale ambao wanamfuatilia Diamond Platnumz utagundua kuwa jana Aprili 12, 2018 aliahidi kuachia video ya wimbo wa ‘Kwa ngwaru’ ambayo amemshirikishwa na Harmonize lakini mpaka sasa hivi hakuna chochote kile walichofanya.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Tuesday, 27 March 2018

Augustine Mrema Akunwa na Muziki wa Daimond "Nampenda sana Daimond Huyu Mtoto Anajua Kuimba".

Mwenyekiti wa Chama cha TLP, Augustine Mrema amesema yeye ni miongoni kwa watu ambao wamekuwa wakifuatilia muziki wa wasanii wa hapa nchini na kati ya watu ambao wanamkuna ni Naseeb Abdul maarufu kama Diamond.

Mrema amesema kwamba anapenda sana nyimbo za mwanamuzi huyo na kwa muda mrefu amekuwa akizifuatilia.

“Nampenda sana Diamond si ndiyo yule aliyeimba ‘zilipendwa huku akitutaja mimi na Lipumba? Huyu mtoto anajua kuimba,”anasisitiza.

Mrema amesema kuwa wimbo huo ametokea kuupenda kwa kwa sababu unaonyesha hali halisi ya maisha yake sasa kwa kuwa ni ukweli usiopingika kwamba yeye na Lipumba sasa ni zilipendwa.

“Kweli tumekuwa wazeee, wakati wetu umefika na sasa tunatakiwa kuwapisha vijana waendeleze gurudumu lakini usifikirie mimi mzee ukajua sisikilizi muziki wa kizazi kipya nasikiliza zote na ninafurahi sana wanafanya kazi nzuri,”ameongeza. 

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Monday, 26 March 2018

Mange Kimambi Atabiri Roma Mkatoliki Kuhamia CCM Kama Alivyotabiri Wema Kuhama na Ikawa.

ANAYO ENDELEA MTANDAONI :
Unakumbuka kabla ya wema sepetu kurudi ccm Mange Kimambi aliandika kwenye page yake ya instagram na kutoa sababu mbili nzito zilizomfanya Wema kurudi CCM?

Awamu hii kamuibukia Roma Mkatoliki, anadai mda wowote anajiunga CCM

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

TCRA Kutoa Hatima ya Times Fm Maojiano na Diamond Wiki Hii.

Hatima ya Kituo cha Redio Times cha jijini Dar es Salaam kilichotakiwa kuwasilisha kipindi cha mahojiano waliyoyafanya na mwanamuziki Diamond Platinumz kwa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kwa ajili ya uchunguzi zaidi, itajulikana wiki hii.

Taarifa zilizoifikia MCL Digital leo Jumatatu Machi 26, 2018 zinaeleza kuwa kamati ya maudhui ya TCRA iliyokuwa ikifanya uchunguzi huo inakaribia kumaliza kazi hiyo.

Machi 22, 2018, Times ilipokea barua ya kuwataka wawasilishe kipindi hicho kilichorushwa Machi 19, 2018 na kutii agizo hilo.

Mwanamuzi Diamond alizua mjadala baada ya kuzungumzia suala la nyimbo za wasanii hao kufungiwa akimlalamikia Naibu Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Juliana Shonza kutowatendea haki wasanii.

Ofisa Mkuu Idara ya Utangazaji wa mamlaka hiyo, Andrew Kisaka ameieleza MCL Digital leo kwamba tayari kamati ya maudhui inakaribia kumaliza kazi yake ya kupitia maudhui ya kipindi hicho.
chanzo: Mwananchi 

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Irene Amvaa Wema Sepetu Amtupia Dongo Zito Kisa ni Diamond.

Video vixen aliye jizolea umaarufu baada ya kuonekana kwenye video ya ‘Kwetu’ ya msanii Rayvanny Irene, amemtolea povu zito staa wa Bongo movie Wema Sepetu huku ikidaiwa kisa ni penzi la Diamond.

Tangu Zari aweke wazi kuwa kaachana na Diamond na kuwa single Kumekuwa na tetesi nyingi sana kwenye social media juu ya nani hasa anayechukua nafasi ya Zari na moja kati ya Wanawake waliotajwa kuwa na uhusiano na Diamond kwa sasa ni Irene na Wema.

Kuna stori ili trend sana kwenye mitandao ya kijamii siku za nyuma kidogo ambapo ilisemekana kuwa Irene na Wema wamepeana kichapo cha maana baada ya kugongana Madale nyumbani kwa Diamond.

Stori hiyo ilidai kuwa Diamond anatoka na Irene na Wema kwa wakati mmoja na wikiendi hii Irene kamtupia dongo Wema ambapo amemcheka kuwa anajiita African beauty wakati hata kiwanja hana!.

African beauty ni wimbo mpya wa Diamond na siku wimbo huo ulipotoka wasanii mbali mbali wa WCB akiwemo Harmonize alimtunuku Wema jina la African beauty jambo ambalo lilimfanya Wema ajitambe kuwa ni African beauty.

Fununu za Irene kuwa na Mahusiano na Diamond zilianza siku nyingi sana wakati bado Diamond yuko na Zari ingawa Diamond alikuwa anakataa kuwa hana Mahusiano naye.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Saturday, 24 March 2018

Diamond amtaka Lulu Diva kumzalia mtoto Rich Mavoko.

Baada ya kukanusha kwa muda mrefu, hatimaye imebainika kuwa Rich Mavoko na Lulu Diva ni wapenzi.

Aliyeweka wazi hilo ni Diamond Platnumz ambaye anafanya kazi na Rich Mavoko kupitia label yake ya WCB. Katika kumtakia kheri ya siku ya kuzaliwa Lulu Diva, Diamond amemwandika haya mrembo huyo.

We @luludivatz nae Utulete Mtoto sasa, Tushachoka picha zenu za Kuviziwa kwenye ma Parties😏👌🏼#AfricanBeauty

Utakumbuka Fiesta ya Dar es Salaam iliyofanyika November, 2017 kuna picha zilisambaa mtaandaoni zikiwaonyesha Rich Mavoko na Lulu Diva katika mapozi ya kimahaba ingawa wenyewe walikanusha na hilo pia ila kwa kauli hii ya Diamond ni wazi lilokuwa likisema lipo. 

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Wednesday, 21 March 2018

Khadija Khopa Achoka Kuwa Single Ataka Mwanaume wa Kumuoa "Nataka Mume Sipendi Dhambi".

Malkia wa Mipasho nchini Tanzania asiyekuwa na mshindani, Khadija Kopa ametangaza rasmi kuhitaji mume wa kumuoa ili aweze kuishi naye huku akiweka vigezo vyake kuwa hataki aliyechini ya miaka 40 kwa madai hawezi kufundisha tution.


Khadija Kopa ametoa kauli hiyo wakati alipokuwa anazungumza kwenye kipindi cha KIKAANGONI kinachorushwa mubashara kupitia kurasa za EATV kila siku ya Jumatano kuanzia saa 8:00 mchana hadi 10:00 alasiri.

"Sijaolewa ila sitaki kusomesha tuition, nataka mwanaume aliyekuwa na umri mkubwa kuanzia 40 kwenda juu, mwenye mapenzi ya dhati na huba, mwenye kujali na kujua ninataka nini, atakayeweza kuijali familia yangu pamoja na watoto wangu, awe mnene kidogo na sio mwembamba, awe na rangi yeyote na kabila lolote lile kwasababu mimi sina ubaguzi katika vitu hivyo", amesema Khadija Kopa.

Pamoja na hayo, Khadija Kopa ameendelea kwa kusema "napenda mwanaume mfanyakazi maana kupata pesa ni majaliwa ila asiwe mwanaume wa kulala nyumbani akanitegemea mimi nikafanye kazi ili yeye aje kula maana maisha ni kusaidia nasio kuegemea upande mmoja tena wa mwanamke".

Aidha, Khadija Kopa amesema sababu kubwa iliyompelekea mpaka sasa kutoolewa ndoa nyingine baada ya aliyekuwa mume wake kufariki ni kutokana na kuwa na wasiwasi na wanaume wa sasa.

"Nina wasiwasi kwa mwanaume atakayekuja kunioa kwa sasa, maana najiuliza mengi je atakuwa na huba kama marehemu mume wangu ndio maana mpaka sasa sijaolewa kwa kuwa nafikiria sana. Mume wangu aliyefariki alikuwa ni mwenye huba, mwenye kunijali, nimekaa naye miaka yote sijawahi kugombana naye, nilikuwa natamani kumuona akinuna ananuna vipi, alikuwa na vigezo vyote", amesisitiza Khadija Kopa.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Mwakyembe Amshukia Diamond, Asema Umarufu Utamkosti, Awezi Bishana na Shonza na Atapotea Kubishana na Serikali.

Waziri wa Habari Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe ameeleza kukerwa na mwanamuziki Diamond Platnumz kutokana na kumdharirisha naibu wake Juliana Shonza wakati akihojiwa katika kipindi cha The Play List cha Times FM na mitandaoni.

Katika maelezo yake Mwakyembe amesema inaelekea sasa Diamond ameanza kulewa umaarufu sasa. Kuhusu hoja ya vikao anavyodai mwanamuziki huyo Mwakyembe amesema kuwa “kama ni vikao na wasanii, tumefanya vingi sana, lakini Diamond hahudhurii vikao hivyo na si wajibu wa Serikali kumfanyia kikao chake mwenyewe, haijalishi nibmaarufu kiasi gani."

"Hatuwezi kuwa na sheria kwa wasanii wengine na sheria maalum kwake, nadhani hizi ni dalili za kuanza kulewa umaarufu kwani Diamond si Kiongozi wa Shirikisho la Muziki wala msemaji wa Chama cha Muziki wa kizazi kipya kuwasemea wenzake," amesema Mwakyembe.

Aidha Waziri Mwakuembe amemalizia kwa kumshauri mwanamuziki huyo kuwa "si busara kwake kushindana na Serikali, na kama ana ushauri basi autoe kistaarabu utazingatiwa lakini si kwa kumshambulia Naibu Waziri kwa dharau na kejeli jinsi alivyofanya. Sijafurahishwa hata kidogo." 

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Thursday, 15 March 2018

Video: Uzinduzi wa Diamond Watikisa Kenya Awaliza Wakenya Jukwaani na Historia ya Maisha Yake.

MSANII wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz amezindua rasmi albamu yake mpya ‘A Boy From Tandale’ jijini Nairobi na kufanya bonge la shoo akiwa na timu nzima ya WCB.

Mbali na WCB, wasanii wengine waliopada jukwaani na kutikisa katika shoo hiyo, ni msanii wa Marekani, Omario.


Albamu mpya ya Diamond imesheheni ngoma 20 kali zikiwemo alizowahi kuzitoa kipindi cha nyuma na nyingine mpya.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Zinaweza zikafungiwa nyimbo zetu zikachezwa za kina Nicki Minaj – Diamond.

Zinaweza zikafungiwa nyimbo zetu zikachezwa za kina Nicki Minaj – Diamond
Msanii Diamond Platnumz bado anaonekana kutokubaliana na uamuzi wa Mamlaka ya Mawasiliano Nchini (TCRA) wa kuzifungia nyimbo zake mbili ambazo ni Waka na Hallelujah.

Muimbaji huyo akizungumza na Classic FM nchini Kenya amesema serikali ni lazima iangalie maudhui ya wimbo husika na msanii husika nini hasa alilenga.

“Huwezi kuimba nyimbo za mapenzi usitaje maneno ya kimahaba, ni uongo kwa sababu utakuwa haufikishi ujumbe,” amesema.
“Nyimbo kama Waka na Hallelujah ni nyimbo ambazo nilifikiria kufanya kitu ili soko lingine watusikilize, serikali lazima ielewe. Na kinachouma zaidi zinaweza zikafungiwa nyimbo zetu zikachezwa za kina Nick Minaj, so ni lazima tuangalie,” amesisitiza Diamond.

February 28 mwaka huu Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ilipokea list ya nyimbo 15 zisizokuwa na maadili kutoka kwa Baraza la Sanaa Taifa (BASATA) na kuamuru kutopigwa katika vyombo vya habari. Katika list hiyo Nay wa Mitego alifungiwa nyimbo tatu na Diamond nyimbo mbili.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Wednesday, 14 March 2018

Irene Uwoya Ampa Onyo Kali Dogo Janja " Thubutu Uwone Tena Ndo Utanijua ".

Mke wa msanii wa muziki Dogo Janja, Irene Uwoya ametoa majibu juu ya habari zilizopo za mumuwe kutaka kuongeza mke wa pili hadi wanne.

Uwoya ametoa majibu hayo baada ya kukuta habari zimezagaa katika mitandao mbalimbali juu ya mpingo ya mumuwe aliyoweka ya kutaka kufikisha idadi ya wake wanne katika ndoa.

“Ndoutajua mim Kabila gani…thubutu uwone tena wasikudanganye @dogojanjatz,” ameandika mrembo huyo katika mtandao wake wa kijamii wa Instagram mapema leo baada ya kuona stori za mumuewe za kumuongezea mke zikitawala.

Katika kipindi cha The Playlist ya Times Fm kilichoruka juzi ( 12-03-2018) mkali huyo wa ‘Wayu Wayu’ alidai kuwa anampango wa kuongeza mke wa pili hadi wanne kila baada ya miaka 10. 
Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Tuesday, 6 March 2018

Kumbe Daxx Ndo Baba Kijacho wa Dayna Nyange..... Dayna Afunguka A-Z "Ujauzito Haujifichi".

Msanii Dayna Nyange amezungumza na kuelezea skendo zilizopo za yeye kuhusishwa kutoka na Daxx ambaye ni Fashion Model na ameonekana kwenye video mpya ya Dayna Nyange ya ‘Sale Sale’ ikiwa ni pamoja na kuhusishwa kuwa mjamzito.

Dayna Nyange amesema kwamba yeye anamahusiano na Daxx lakini siyo ya kimapenzi kwani yeye anaye mpenzi wake na ishu ya yeye kuwa na mimba kasema hajawahi kusema kama ni mjamzito lakini Mimba haijifichi na kama ipo watu wataona na waandae Pampas na maziwa ya mtoto.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Thursday, 1 March 2018

Bell 9 Aleta Kali Aifananisha Basata na Baba Asiyejua Jina la Mwanaye.

Msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Belle 9 amelishangaa Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) kwa kushindwa hata kuwajua wasanii japo hata kwa majina.


Belle 9 amesema hayo baada ya BASATA kuchanganya majina kwa kumtaja kwenye orodha ya wasanii waliofungiwa nyimbo zao jana Februari 28, 2018 badala ya kuweka jina la Roma Mkatoliki.

“Kwahiyo mimi ni Roma Mkatoliki haya basi tongwe record baby jei mada yo yo yo Roma!  Hii ni sawa na kua na baba ambaye akisikia umekosa ana kuhukumu lakini akiulizwa jina la mwanao anaitwa nani anajiuma uma halafu analitaja jina la mtoto wa jirani ambalo huwa analiskia akiwa anakuja kukuhukumu,“ameandika Belle 9 kwenye ukurasa wake wa Instagram.

Soma zaidi – TCRA yazifungia nyimbo 15, Diamond na Nay maumivu zaidi

BASATA walikosea kumtaja Belle 9 kwenye kipengele cha wimbo wa Kibamia ambapo waliandika Abemego Damiani a.k.a Roma Mkatoliki.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Wednesday, 28 February 2018

Mwimbaji Misri Afungwa kwa Kuikashifu Mto Nile.

Mwimbaji wa Misri Sherine Abdel Wahab amehukumiwa miezi sita gerezani kwa kutania juu ya hali ya usafi wa mto Nile.

Sherine, ni mmoja wa waimbaji maarufu nchini humo pia ni jaji katika kipindi cha mashindano ya waimbaji, The Voice- alimwambia mashabiki wake kuwa kunywa maji kutoka mto huo kunaweza kumpatia vijidudu.

"Kunywa Evian badala yake." akatania
Mwimbaji mwingine, Laila Amer, pia alihukumiwa siku ya Jummane kifungo cha miaka miwili kutokana na video ya muziki.

Bi Amer - ambaye hana umaarufu kama Sherine - alipatwa na hatia ya 'kuchochea ufitini na uovu". Muongozaji wa kipindi na muigizaji walihukumiwa kwa vipindi vifupi.

Sherine, amehukumiwa na mahakama moja Cairo kwa kusambaza habari zisizo za kweli. Chombo cha habari Misri, Ahram kimesema aliagizwa kulipa paundi 5,000 za Misri.

Mzaha
Mashtaka dhidi ya Sherine yalifunguliwa mwezi Novemba, baada ya kuonekana video mtandaoni ikimuonesha akiombwa kuimba wimbo uitwao Mashrebtesh Men Nilha (umewahi kunywa maji ya mto Nile?).akajibu ''Nikinywa maji ya mto Nile nitapata kichocho''. Kichocho ni ugonjwa unaojitokeza maeneo ya vijijini nchini Misri.

Mbali na kesi dhidi yake, Chama cha wanamuziki nchini humo kimetangaza kuwa kimempiga maruguku kuuimba wimbo huo kuhusu Misri.

Abdel Wahab baadae aliomba radhi kutokana na tukio hilo akiwa kwenye tamasha lililofanyika huko Jumuia ya falme za kiarabu zaidi ya mwaka mmoja uliopita.

Another singer, Shyma alihukumiwa kwa kucheza video ya maadili mabovu


Maamuzi ya mahakama yaliyotolewa siku ya Jumanne inafanya idadi ya wanamuziki kuhukumiwa kifungo kufikia watatu miezi ya hivi karibuni

Mwezi Desemba, Shaimaa Ahmed ajulikanaye kifupi Shyma alihukumiwa kifungo cha miaka miwili baada ya kuonekana kwenye Video ya muziki akiwa amevalia nguo za ndani huku akila ndizi kwa mbwembwe.

alikutwa na hatia ya kuweka video yenye maadili mabaya akahukumiwa sambamba na muongozaji wa video hiyo.Baadae hukumu ilipunguzwa na kuwa ya mwaka mmoja baada ya kukata rufaa.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

EXCLUSIVE:Video ambayo inayoonyesha Hoteli aliyojenga Mr. II SUGU Mbeya.




Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Monday, 26 February 2018

Maneno ya Izzo B, Rama Dee na Niki wa Pili Muda Mchache Baada ya Sugu Kuhukumiwa Miezi 5.

Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi na mwenzake Emmanuel Masonga wamehukumiwa kwenda jela miezi mitano na Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Mbeya leo Februari 26, 2018 baada ya kukutwa na hatia kutumia lugha ya fedhea dhidi ya Rais Magufuli.


Baada ya kuhukumiwa kwenda jela baadhi ya wasanii wa muziki wa bongo fleva wamefunguka yao ya moyoni kuhusu tukio hilo huku wengine wakimtia moyo kuwa gerezani siyo kaburini hivyo atamaliza muda wake na kurudi uraiani kuwapigania wananchi wa Mbeya.

"Nguvu ya Mungu ikapate kuwa nawe pamoja na familia yako, gerezani sio kaburini 'stay strong' Jongwe" aliandika Niki wa Pili

Kwa upande wake msanii Rama Dee yeye amesema kuwa ameumizwa sana na bahari ya Sugu kufungwa jela miezi mitano na kudai si picha nzuri katika nchi yetu kwa mambo kama haya.

"Nasikitika sana kwa hii habari kama msanii pia kama rafiki wa Sugu, hii si picha nzuri" Rama Dee

Aidha msanii Izzo Bizness ambaye anaiwakilisha Mbeya vizuri katika muziki wa Hip hop pia ameonyesha hisia zake na kumtaka Mbunge huyo kuwa mvumilivu na kusimama imara katika kipindi hiki.

Mbali na huyo Rapa Roma Mkatoliki alikuwa na haya ya kusema juu ya kifungo cha Sugu "Hata hili lipatita' stay strong Joseph Zaburi 35: 1-28 " 

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Sunday, 25 February 2018

Zamaradi Mketema Awa Mtangazaji wa Kwanza Kuingia Wasafi TV & Radio.

Kama mada inavyoonekana,aliyekuwa baby mama wa Ruge Mutahaba Zamaradi Mketema ajiunga rasmi na Wasafi TV inayomilikiwa na Diamond Platnumz.

Picha ni Zamaradi akiwa na Timu nzima ya WCB Wakiwa Zanzibar Kwa Ajili ya usaili wa Watangazaji Wengine.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa