Saturday 14 April 2018

Video ya utupu ya Nandy na Bill Nass yawawekea uzibe Harmonize na Diamond Platnumz.

Kwa wafuatiliaji wa mitandao ya kijamii nchini Tanzania, hususani kwa wale ambao wanamfuatilia Diamond Platnumz utagundua kuwa jana Aprili 12, 2018 aliahidi kuachia video ya wimbo wa ‘Kwa ngwaru’ ambayo amemshirikishwa na Harmonize lakini mpaka sasa hivi hakuna chochote kile walichofanya.

Diamond kupitia kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii jana aliahidi kuachia video ya Kwa ngwaru kwa kuahidi kuwa endapo angepata maoni (Comments) 10,000 kwenye posti yake aliyochapisha kwenye mtandao wa instagram, basi wangeachia video ya wimbo huo ambao umetokea kupendwa sana na mashabiki wa wakali hao lakini posti hiyo hadi sasa imefikisha comments elfu 13 na video hiyo bado haija achiwa.

Hii haina ubishi kuwa video ya utupu ya Nandy na Bill Nass imepoteza attention kwa mashabiki wengi wa muziki nchini Tanzania kutokana na ukubwa wa wasanii hao ambao kila Mtanzania alikuwa anaamini kuwa ndio zao jipya la wasanii wa kizazi kipya.

Hata hivyo, mpaka sasa hivi si Diamond wala Harmonize aliyetoa kauli yoyote ile kuhusiana na kuachia video hiyo ingawaje mashabiki wengi walitazamia kuona video hiyo kwa siku ya jana.

Kwa mujibu wa maelezo ya Nandy na Bill Nass kuhusu video yao ya utupu iliyovuja siku ya jana hadi sasa bado haijajulikana ni nani aliyevujisha kwani wamekuwa wakitupiana lawama kila mmoja.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment