Wednesday 29 November 2017

Uwoya Amnyima Penzi Dogo Janja Tangu Ndiku Afariki.

Kwa habari za kunyapia nyapia ni kwamba Irene Pancras Uwoya (Sheila Abdul) aanza kumchukia dogo janja kiasi cha kuyumbisha penzi lao na mbaya zaidi amekuwa akimnyima penzi dogo janja na mara nyingi hupenda kumkwepa kwepa janjaro na kiasi fulani anahisi kama janjaro ndo chanzo cha mumewe kipenzi Hamadi Kataut.

Dogo janja mara kwa mara akitafutwa kujibu suala hili la kunyimwa penzi na uwoya amekuwa akibabaika sana na muda mwengine hupenda kujibu nje ya mada ili asiendelee kuulizwa. 

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Alikiba na Abdukiba Kwenye Kolabo ya Pamoja Kuachia Nyimbo Mpya Kesho.

Baada ya kimya cha muda mrefu wakali kutokea Bongoflevani Alikiba na Abdukiba ambao ni ndugu wa damu wameamua kurudi tena kwenye headlines za bongofleva baada ya kujiandaa kuachia wimbo wao mpya.

Uthibitisho wa kuachia wimbo huo umepatikana baada ya Alikiba na Abdukiba kupost kupitia mitandao yao ya Instagram kwa kuahidi kuwa wataachia Audio na Video kwa pamoja siku ya Alhamisi hii, ambapo Abdukiba ameandika…>>>“The long wait is almost over!!!!King’s Music presents @officialabdukibaanew single featuring @officialalikiba – Audio & Video zinadondoka Alhamisi hii. Subscribe to AbduKiba youtube channel uwe wa kwanza kuiona video ya #Singledirected by @hanscana_#SupportedByKiba#KingKiba..” – Abdukiba


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

TANESCO Wataja Chanzo cha Kukatika kwa Umeme Dar, Pwani.

Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) limetoa taarifa kwa wateja katika mikoa ya Dar es Salaam na Pwani kuwa baadhi ya maeneo hayana umeme kutokana na hitilafu iliyojitokeza.

Taarifa ya Tanesco imesema baadhi ya maeneo ya mikoa hiyo hayana umeme kuanzia saa 3:20 asubuhi ya leo Jumatano Novemba 29,2017 kutokana na mashine namba tatu ya kuzalisha umeme kwa njia ya gesi asilia kituo cha Ubungo II kupata hitilafu.

“Mafundi wa shirika wanaendelea na jitihada za kutatua hitilafu hiyo kwa haraka ili kurejesha umeme katika hali yake ya kawaida,” imesema taarifa ya Tanesco.

Shirika hilo limesema litaendelea kutoa taarifa za maendeleo ya kazi hiyo.

Pia, Tanesco imetoa tahadhari kwa wananchi kutosogelea, kushika wala kukanyaga waya uliokatika au kuanguka.

Uongozi wa shirika hilo umewaomba radhi wateja kwa usumbufu uliojitokeza.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Inasikitisha Baba Amtoa Kafara Mwanaye Amkata Sehemu za Siri kwa Shoka.

MTU mmoja huko mwenye umri wa miaka 39 huko Chhattisgarh, India, amemtoa kafara mwanaye mdogo katika kitendo cha ushirikiana kwa kumkata uume na sehemu za kichwa kwa shoka hadi kusababisha kifo chake, kwa madai ya kufukuza mapepo mabaya ‘mashetani’.

Watuhumiwa wakiwa chini ya ulinzi.
Kitendo hicho kilifanyika huko Balodabazar wilayani Chhattisgarh, polisi walisema jana. Ramgopal Patel, na mganga wa kienyeji, Rajesh Yadav (19) walikamatwa leo, ikiwa ni siku mbili baada ya kufanya kitendo hicho kijijini Amera.
Polisi walisema mwili wa mtoto huyo mwenye umri wa miaka 13 ulikutwa ukiwa katika dimbwi la damu ambapo baada ya polisi kufanya uchunguzi, Patel alikiri kumwua mwanaye huyo ili kuondoa mapepo mabaya na hivyo wamemfungulia mashitaka. 

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Mabasi ya Mwendokasi Kupanua Wigo Sasa Hadi Sinza, Masaki.

WAKALA wa  Mabasi Yaendayo Haraka (DART) unatarajia kupanua wigo wa usafiri huo kwa kuongeza ruti za Sinza, masaki na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Sambamba na ruti hizo, DART pia inatrajia kuongeza mabasi katika mfumo wake kutoka 140 yaliyopo sasa hadi mabasi 305 pindi awamu ya kwanza ya mfumo huo itakapokamilika.

Mtendaji Mkuu wa DART, Mhandisi Ronald Lwakatare, alisema hayo jana wakati akizungumza na waandishi wa habari, baada ya kupokea wageni sita kutoka serikali ya Rwanda ambao wako nchini kwa ziara ya siku tano ya kujifunza mradi huo unavyofanya kazi nchini.

“Tunatarajia kuwa hatua ya kukamilika kwa awamu ya kwanza ya mradi huu, itaongeza idadi ya watumiaji wa mabasi ya mfumo huo kutoka 200,000 kwa siku   kufikia watumiaji 400,000 hadi 500,000 kwa siku,” alisema.

Mhandisi Lwakatare alisema mradi huo utaongeza njia  kutoka mbili zilizopo sasa hadi njia  tisa, hivyo kupanua huduma ya usafiri katika maeneo mbalimbali yaliyomo ndani ya mfumo wa DART katika awamu ya kwanza ya mradi.

“Awamu ikikamilika tutakuwa na njia tisa, kuna nyingine zitakuwa zinaenda Masaki, Sinza, Chuo Kikuu na maeneo mengine ambayo yako jirani,” alisema.

Kuhusu athari zilizotokana na mvua zilizonyesha Oktoba 26,  mwaka huu, Mhandisi Lwakatare alisema mfumo wa mabasi uliathiriwa na mvua hizo na mabasi 40  yaliharibika na kati ya hayo 20  yaliharibika zaidi.

Hata hivyo, alisema mabasi hayo  yameshatengenezwa na yameanza kutoa huduma na kwamba wamejipana kuhakikisha mitaro yote inayozunguka karakana ya Jangwani inasafishwa ili kuepuka eneo hilo kukumbwa tena na mafuriko.

“Tumefarijika kupokea ugeni kutoka serikali ya Rwanda kuja kutembelea mradi kwa lengo la kujifunza hatua tuliyofikia ukizingatia kuwa jiji la Kigali nalo lina mpango wa kuwa na mfumo kama huu,” alisema.

Timu hiyo inaongozwa na Rwagatore Etienne kutoka Mamlaka ya Jiji la Kigali akiwa na wataalamu washauri ambao ndio waliopewa kazi ya usanifu wa jiji la Kigali kuwa na mfumo wake wa mabasi yaendayo haraka.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Uchambuzi wa Wimbo Mpya wa Diamond Platnumz Unaitwa Sikomi.

UCHAMBUZI WA WIMBO
JINA LA WIMBO: SIKOMI
MSANII : DIAMOND PLATNUMZ

UTANGULIZI

Diamond Platnumz ni msanii wa muziki wa kizazi kipya (bongofleva) kutoka Tanzania. Anaiwakilisha nchi yake na fasihi ya kiswahili nje na ndani ya nchi kwa ufanisi. Wimbo wake mpya wa Sikomi ni mojawapo ya nyimbo zake nyingi ambazo amepata kuziimba tangu alipoanza mziki wake. Ufuatao ni uchambuzi wa wimbo wa Sikomi. Angalizo uchambuzi huu utajikita zaidi kwenye vipengele vya maudhui na wala mhakiki hajagusa vipengele vya fani.

DHAMIRA KUU
Dhamira kuu katika wimbo wa Sikomi ni mapenzi. Msanii anaeleza historia yake ya kimahusiano toka alipotoka kimuziki mpaka hapa alipofika. Amegusia visa na mikasa aliyopitia katika mahusiano yake ya kimapenzi. Msanii amepitia katika mengi katika mapenzi lakini bado haachi kujihusisha na mapenzi huu ndiyo msingi wa jina la wimbo "Sikomi". Msanii anasema kila anapoumizwa na mwanamke mmoja anatafuta mwanamke mwingine wa kumfuta machozi.

DHAMIRA NDOGO NDOGO

USALITI KATIKA MAPENZI

Msanii anaeleza jinsi alivyosalitiwa na wanawake aliowapitia msanii anasema " aliyonifanyia wa sentro siwezi Sema... ndiyo maana sikushangaa ile ghafla toka CCM kwenda CHADEMA"
Msanii anaeleza jinsi alivyoumizwa na usaliti katika mapenzi. Msanii anasema mara baada ya kutoka kimuziki alivamia tasnia ya bongo movie ambapo alisalitiwa sana.

Msanii anaeleza jinsi alivyosalitiwa na Penny aliyedai ana ujauzito wake hali iliyompelekea kumhonga gari mpenzi wake huyo ambaye mwisho wa siku alikuja kumsaliti. Msanii anasema ameshafumania na kufumaniwa pia katika mapenzi hii ni kielelezo cha usaliti katika mapenzi kwenye kazi ya msanii.

MIGOGORO
Msanii amesadifu yale yanayotokea katika jamii kwa kuonesha migogoro mbalimbali kwa kutumia wahusika katika wimbo wake baadhi ya migogoro ni hii ifuatayo;

Mgogoro wa msanii na mama yake

Mgogoro wa nafsi wa msanii kuhusu kuachana na mapenzi au kuendelea.

Mgogoro wa msanii na Esma kuhusu kuachana na mapenzi ni baada ya Esma kumwambia msanii mapenzi basi msanii hakutaka kusikia.

Mgogoro wa msanii na Zari. Msanii anasema richa ya Zari kumzalia watoto wawili wa kiume na wa kike lakini bado alimsaliti.

Mgogoro wa Msanii na wa Sentro na mgogoro wa msanii na wa sentro.

NAFASI YA MWANAMKE KATIKA JAMII

Msanii amemchora mwanamke kama mzazi na mlezi mfano ni mama yake na msanii na Zari.

Msanii amemchora mwanamke kama mshauri mzuri mfano ni mama yake na msanii na Esma.

Mwanamke kama mtu mwenye mapenzi ya dhati mfano Zari aliyempenda msanii mpaka kumzalia watoto wawili, mama yake msanii na Esma.

Msanii amemchora mwanamke kama mtu aliyekosa msimamo na msaliti, mfano wa Sentro na Penny.

KUFANIKIWA KWA MSANII KIMAUDHUI

Msanii ameweza kusawiri ipasavyo mambo yanayotokea katika jamii ya kitanzania na hasa katika ulimwengu wa mapenzi.

UDHAIFU WA MSANII
Msanii amekuja na hitimisho jumuishi kuwa wasanii wa sinema (bongo movie) siyo wa kuaminiwa jambo ambalo siyo la kweli kwenye uhalisia kwani kuna wasanii wengi wa tasnia ya filamu wanajiheshimu na wengine ni watu wazima wenye kujiheshimu pia na kuaminika na jamii. 
Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Korea Kaskazini: Tunaweza Kushambulia Eneo Lolote Marekani.

Korea Kaskazini imesema kuwa imefanikiwa kulifanyia majaribio kombora lake la masafa marefu ambalo linaweza kufika eneo lolote la Marekani.
Runinga ya kitaifa nchini humo imesema kuwa Pyongyang sasa imefanikiwa kuafikia azimio lake la kuwa taifa lenye nguvu za kinyuklia.
Kombora hilo kwa jina Hwasong-15 ambalo imesema ndio kombora lenye uwezo mkubwa lilirushwa katika giza mapema siku ya Jumatano.
Lilianguka katika maji ya Japan lakini liliweza kuruka juu zaidi ya kombora jingine lolote la taifa hilo .
Marekani yatishia kuiadhibu Korea Kaskazini
Kombora la Korea Kaskazini lashindwa kupaa
Marekani: Korea Kaskazini ilikusudia uchokozi
Kitengo cha habari cha taifa hilo KCNA kilisema kuwa kombora hilo liliruka katika kimo cha kilomita 4,475 na kusafiri kwa umbali wa kilomita 950 katika dakika 53.
Kombora hilo lililofyatuliwa kwa mwinuko halikupitia katika anga ya Japan kama makombora mengine hapo awali na lilianguka kilomita 250 karibu na pwani yake ya kaskazini , kulingana na maafisa wa Japan.
KCNA imeongezea kuwa kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un ambaye alishuhudia kufyatuliwa kwa kombora hilo alitangaza 'kwa majivuno' kwamba sasa tumekamilisha lengo letu la miaka mingi la kuwa taifa lenye nguvu za kinyuklia.
Ripoti hiyo imesema kuwa kama taifa lenye nguvu za kinyuklia na linalopenda amani, Korea Kaskazini itafanya kila iwezalo kutekeleza lengo lake la kuleta amani na udhabiti duniani.
Imesema kuwa, silaha zake za ulinzi dhidi ya sera ya kibepari ya Marekani, hazitatishia taifa lolote duniani iwapo maslahi ya Korea Kaskazini hayatakiukwa.''Hilo ndio tangazo letu''

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Lulu Diva, Rich Mavoko Wanaswa Kwenye Mahaba Mazito.

MWANAMUZIKI Lulu Diva amenaswa na msanii mwenziye Rich Mavoko wakiwa katika pozi za kimahaba usiku mnene katika viwanja vya Leaders Club jijini Dar es Salaam kwenye shoo ya Fiesta hivi karibuni.

Rich Mavoko alitumia udhaifu wa Lulu na kuanza kumshikashika maeneo mbalimbali ya mwili wake ambaye aliona raha na vicheko kedekede.  Mrembohuyo  hakujali kamera zilizokuwa zikimmulika ndani ya usiku huo mnene, kwani muda wote alikuwa bize akisikilizia mapapaso hayo bila woga.

Naye Mavoko aliyekuwa akimpapasa,  hakuwa nyuma katika kuhakikisha nafasi hiyo haipotei bila kutumika ipasavyo.

Huko nyuma wawili hao waliripotiwa kuwa wapenzi, jambo ambalo walilikanusha kila mara. 

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Breaking News: Waziri Majaliwa Anasa Semi Trailer 44 Zilizokua Zinataka Kutolewa Kinyemela Bandalini Amuagiza IGP Sirro Kukamata Wamiliki.

WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa leo Novemba 29, 2017 amemtaka Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Simo Sirro kuwakamata Bw. Bahman wa Kampuni ya NAS na Wakala wa Kampuni wa Wallmark Bw. Samwel kwa kutaka kutoa Bandarini magari makubwa 44 aina ya Semi Trailer bila ya kulipa kodi kwa kutumia jina la Waziri Mkuu.
Aidha, Majaliwa ameitaka Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) kufanya kazi kwa mujibu wa sheria na kutowasikiliza wafanyabiashara wanaotaka kukwepa kodi kwa madai ya kupewa vibali vya msamaha wa kodi kutoka viongozi wa juu serikalini.
“Mtu asije hapa aseme amepewa kibali na Rais Magufuli, Makamu wa Rais Mama Samia au Waziri Mkuu cha kuruhusu kutoa mzigo wake bila kufuata taratibu, akija mtu na taarifa hizo akamatwe mara moja na achukuliwe hatua kwa mujibu wa sheria,” alisema Waziri Mkuu.
Waziri Mkuu ametoa agizo hilo leo Jumatano alipofanya ziara ya kushtukiza Bandarini baada ya kupata taarifa za mfanyabiashara huyo aliyetaka kutapeli kutoa magari hayo yaliyoingizwa nchini mwaka 2015 kutoka nchini Uturuki.
Hatua hiyo imekuja baada ya Bw. Bahman wa kampuni ya NAS kutaka msamaha wa kodi kwa kuidanganya TPA kwamba amewasiliana ana Waziri Mkuu na wasipotekeleza agizo hilo watapata matatizo. 

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Natamani Kufanya Kazi na Ali Kiba Katika Ujio Wangu Mpya- Sister P.

Msanii mkongwe kwenye bongo fleva, Sister P ambaye amewahi kutamba kwa ngoma kama, Anakuja,  Hey Dj na zingine amefunguka na kusema kuwa katika ujio wake mpya kwenye muziki anatamani kufanya kazi na mfalme Alikiba kwani anaamini watafanya kazi kubwa.

Sister P amesema hayo leo alipokuwa akipiga stori na mwandishi wa tovuti ya EATV na kudai kuwa akifanya kazi na Alikiba lazima itakuwa kazi kubwa na bora zaidi sababu watakuwa wamekutana wanamuziki na si wasanii.
"Kwa sasa nimejipanga vya kutosha kwa ajili ya kuanza mashambulizi mwakani mwezi wa kwanza, kuna ngoma nyingi ndani nimefanya na mtayarishaji mpya kwenye muziki anaitwa Banny Music chini ya Big Sound studio, lakini kiu yangu kubwa kufanya kazi moja na Alikiba kwani naamini itakuwa kazi kubwa zaidi sababu tutakuwa tumekutana wanamuziki na siyo wasanii" alisisitiza Sister P

Sister P ambaye hivi sasa muonekano wake umebadilika tofauti na zamani ameahidi kuwashangaza Watanzania kwa kazi zake mpya na kusema anaamini kuwa atarudi kwenye nafasi yake licha ya kukaa kimya kitambo kwenye muziki. 
Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Thursday 2 November 2017

Mama Mzazi wa Dogo Janja Ampa Baraka Zote Mwanaye Kwenye Ndoa Yake Asema 'Nimelidhika Hata Mtume Mohamad Alioa Mwanamke Mkubwa'.

Mama mzazi wa msanii Dogo Janja Bi. Zaituni Omari, amesema habari za mtoto wake kuoa ni za kweli na yeye kama mzazi alimpa baraka zote, vinginevyo asingeweza kuoa.

Mama yake Dogo Janja ameyasema hayo alipokuwa akiongea na mwandishi wa habari na kusema kwamba yeye kama mzazi ameridhika kwani pia ametimiza matakwa ya dini.
“Alishawahi kuniambia kuwa anataka kuoa na mimi nikampa baraka zote, alivyokuwa tayari alinijulisha akaniambia kama kuna uwezekano niende isipokuwa kuna mambo yakaingilia kati, ila kwa vile Madee ni kama baba yake na ninamuamini sana nikawaruhusu waendelee, kila anachofanya hafanyi yeye kama yeye lazima kiko nyuma yangu, sio stori za kiki ni kweli kaoa na hawezi kuoa bila kuwasiliana na familia yake”, amesema mama yake Dogo Janja.
Kuhusu suala la tofauti ya umri kati yake na Irene Uwoya, mama yake Dogo Janja amesema kwamba suala la umri halijalishi sana isipokuwa kikubwa ni maelewano.
“Nimeridhika kwa sababu hata dini yetu ya Kiislam Mtume Mohamad alioa mwanamke mkubwa, kwa hiyo umri haujalishi, kikubwa na maelewano”, amesema Mama yake Dogo Janja.
Ijumaa ya wiki iliyopita kulianza kuonekana kwa picha mtandaoni zinazoonyesha Irene Uwoya na Dogo Janja 

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Nyarandu Akanusha Taarifa Zinazosambazwa Kwenye Mitandao ya Kijamii.

WAKATI Bunge likimtema rasmi aliyekuwa Mbunge wa Singida Mashariki (CCM), Lazaro Nyalandu, mwenyewe amejitokeza na kuponda habari zinazosambazwa kueleza ubaya akisema ni uzushi.

Jana Nyalandu alisema taarifa zinazosambazwa kwenye mitandao ya kijamii, ikiwamo WhatsApp na Facebook kuelezea kasoro za kiutendaji akiwa Waziri wa Maliasili na Utalii ni uzushi ambao Watanzania wanapaswa kuupuuza.

Nyalandu alitangaza kujivua gamba CCM, kuandika barua ya kuachia kiti cha ubunge na kueleza nia yake ya kujiunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Jumatatu iliyopita.

Chadema, kupitia Katibu Mkuu wake, Dk. Vicent Mashinji, kilitangaza kumpokea awe mwanachama na kwamba alichelewa kutoa uamuzi huo.

Lakini jana taarifa ya Spika wa Bunge, Job Ndugai, ilieleza kuwa hajapokea barua ya Nyalandu kujiuzulu nafasi yake.

Aidha, Ndugai alisema alichopokea ni barua kutoka kwa Katibu Mkuu wa CCM ya Oktoba 30, kimsingi, ikimtaarifu kuwa Nyalandu amepoteza sifa ya kuwa mwanachama wa chama hicho na ubunge kwa mujibu wa ibara ya 13 ya katiba yao.

Katika ujumbe alioandika katika akaunti yake ya mtandao wa Tweeter jana, Nyalandu alisema ni uzushi, uongo wa kupuuzwa na aibu kubwa.

"Fake news alert! (Tahadhari habari za uzushi!) Habari hii ni ya kutungwa na kufikirika. Kibaya zaidi ni ya uongo. Siasa za aina hii ni za kizamani. Aibu tupu!" Aliandika Nyalandu katika akaunti yake hiyo.

Katika ukurasa huo, Nyalandu ambaye amekuwa Mbunge wa CCM tangu mwaka 2000, aliambatanisha na majadiliano ya watu wanne kwenye kundi la WhatsApp liitwalo 'Chadema Taifa' yakionyesha washirikia wake ni Mchungaji Peter Msigwa, Nyalandu na muundaji wa kundi.

Katika kundi hilo, ilidaiwa Nyalandu ameandika kuwa yuko katika wakati mgumu kwa kuwa serikali inataka kumshtaki kwa kuhusika kuuza vitalu na wanyama, na kwamba anaomba ushauri.

Katika majadiliano hayo, muundaji wa kundi, anayedaiwa kuwa Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, anaonekana kumpa pole Nyalandu na kumshauri kuhama chama hicho.

Mbali na chapisho hilo la Nyalandu, maandiko mbalimbali yamesambaa kwenye mitandao ya kijamii tangu tamko la Nyalandu la Jumatatu, yakieleza jinsi alivyogawa vitalu vya uwindaji na wanyamapori.

Mwaka 2012, aliyekuwa Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa, Itikadi na Uenezi ya CCM, Nape Nnauye, alitangaza operesheni ya kuvua magamba, akiwataka wanachama wa CCM wote ambao hawatakiwi, kukihama chama hicho haraka kabla ya kuvuliwa magamba.

Kutokana na operesheni hiyo ya CCM, Chadema kiliibuka na operesheni 'Vua Gamba Vaa Gwanda', ikiwa na lengo la kuvuna wanachama wengi waliokataliwa CCM na kuwataka kuvaa sare za chama hicho na kuungana nao.

Katika taarifa yake ya kujitoa CCM Nyalandu aliyochapisha katika akaunti yake ya mtandao wa kijamii wa Instagram, Nyalandu aliomba kutua Chadema ili aungane nao kuleta mabadiliko ya kisiasa na kiuchumi nchini.

"Nitaomba kama itawapendeza wanachama wa Chadema, basi waniruhusu kuingia malangoni mwao, niwe mwanachama, ili kuungana na Chadema na Watanzania wote wanaopenda kuleta mabadiliko ya kisiasa na kiuchumi nchini kwa kupitia mfumo wa kidemokrasia na uhuru wa mawazo."

Nyalandu (45) alisema amejiuzulu ubunge kuruhusu kufanyika kwa uchaguzi mwingine ili wananchi wapate fursa ya kuchagua itikadi wanayoona inawafaa kwa majira na changamoto lukuki.

Mwanasiasa huyo aliyewahi kuwa Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Singida na Mjumbe wa Kamati za Siasa Wilaya na Mkoa, alisema: "Ni imani yangu, kamwe hayatakuwa ya bure maneno haya, wala uamuzi huu niufanyao mbele ya Watanzania leo ili kwamba, sote kama taifa tuingie kwenye mjadala wa kuijenga upya misingi ya nchi yetu."

Aliandika zaidi: "Ni maombi yangu kwa Mungu kuwa haki itamalaki Tanzania, upendo, amani na mshikamano wa watu wa imani zote za dini, mitazamo yote ya kiitikadi za kisiasa na makabila yote nchini uimarike. Tushindane kisera na kuruhusu tofauti za mawazo, lakini tubaki kama ndugu na taifa lililo imara na nchi yenye adili."

Nyalandu alitangaza nia kuwania urais Desemba 28, 2014 katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Uwanja wa Ilongero jimboni kwake, wakati akihutubia mamia ya wananchi.

Katika mkutano huo, Nyalandu alisisitiza "sasa ni zamu ya vijana kuongoza nchi" huku akiwaambia wananchi kuwa safari yake ya ubunge kwa miaka 15 inaanzisha safari nyingine bila kuwaeleza ikiwa bado ana nia na ubunge au la. Siku hiyo, aliambatana na mkewe, watoto na wazazi wake.

Ingawa alikuwa mmoja kati ya wanaCCM 38 waliojitokeza kuwania urais mwaka 2015, jina lake lilikatwa pamoja na kina Lowassa na Sumaye na kuteuliwa Rais Magufuli kupeperusha bendera ya chama hicho.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Yanga Kuwakosa Ngoma, Tambwe, Kamusoko na Juma Abduli Katika Mechi Dhidi ya Singida United.

Kikosi cha Yanga kitaondoka kesho mapema kwa basi lake kwenda Singida kwa ajili ya mchezo wa Ligi Kuu ya soka Tanzania Bara dhidi ya wenyeji, Singida United Jumamosi Uwanja wa Namfua.

Lakini wachezaji wanne tegemeo hawatakuwepo kwenye msafara huo ambao ni beki Juma Abdul, kiungo Thabani Kamusoko, Donald Ngoma na Mrundi, Amissi Tambwe.
Abdul hatakuwemo kwa sababu anatumikia adhabu ya kadi tatu za njano, wakati Kamusoko, Ngoma na Tambwe wote ni majeruhi wa muda mrefu.
Yanga inaendelea na mazoezi asubuhi ya leo Uwanja wa Uhuru mjini Dar es Salaam kabla ya safari ya kesho kwenda kupambana na timu inayofundishwa na kocha wao wa zamani, Mholanzi, Hans van der Pluijm.
Yanga inakwenda kwenye mchezo huo, ikitoka kutoa sare na wapinzani wa jadi, Simba kwa kufungana 1-1 Jumamosi iliyopita Uwanja wa Uhuru. Sare hiyo imefanya timu hizo ziendelee kufungana kwa pointi 16 kileleni mwa Ligi Kuu.
Ligi Kuu itaendelea Ijumaa, Maji Maji FC wakiikaribisha Stand United Uwanja wa Maji Maji mjini Songea, wakati Jumamosi Singida watakuwa wenyeji wa Yanga Uwanja wa Namfua, Singida na Ndanda FC wataikaribisha Mtibwa Sugar Uwanja wa Nangwanda Sijaona, Mtwara.
Mechi nyingine za Jumamosi, Kagera Sugar wataikaribisha Tanzania Prisons Uwanja wa Kaitaba, Bukoba, Njombe Mji FC wataikaribisha Mbao FC Uwanja wa Saba Saba na Azam FC watakuwa wenyeji wa Ruvu Shooting Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.
Jumapili kutakuwa na mechi mbili ambapo Mbeya City watakipiga na Simba, Lipuli FC nao wataikaribisha Mwadui FC Uwanja wa Samora mjini Iringa.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Wednesday 1 November 2017

SOMA Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo.

Job Opportunity at Halotel Tanzania

Job Opportunities at Shugulika Recruitment

Job Opportunity at Mwananchi Communications Limited, Reporter

Job Opportunity at Kibo Poultry Products, Senior Accountant

Job Opportunity at CVPeople Africa, Delivery Manager

Job Opportunities at African Minerals and Geosciences Centre, Volunteer Trainees

Job Opportunity at One Acre Fund, Program Partnership Specialist

NAFASI ZINGINE INGIA WWW.AJIRAYAKO.CO.TZ 

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Babu Aliyemfanyia Tohara Dogo Janja Afunguka, Asema Irene Uwoya ni Size yake.

Babu mmoja Arusha amewatoa hofu mashabiki waliodai dogo janja huenda akawa anachapiwa mzigo na vijana wabemba nondo mjini,amedai kwa jinsi anavyomfahamu dogo janja alivyo lazima Uwoya atulie kabisa,pia ameongeza hata kama wangekuwa Wolper,Uwoya ,Wema na Aunt Ezekiel pamoja lazima wote wangetulia tu. 

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa