Tuesday 27 March 2018

Breaking News: Freeman Mbowe na Viongozi Wengine wa Chadema Wafikishwa Mahakamani.

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe na viongozi wengine wa chama hicho, wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa ajili ya kusomewa mashtaka yanayowakabili.

Viongozi wa CHADEMA wengine waliofikishwa Mahakamani ni Katibu Mkuu Dr. Vincent Mashinji, Mbunge wa Kibamba John Mnyika, Naibu Katibu Mkuu Zanzibar Salum Mwalim, Mbunge wa Iringa Mjini Peter Msigwa na Ester Matiko Mbunge. 

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Mwenyekiti UVCCM Amvaa Waziri Shonza "Mnawafungia Kina Roma, Daimond Mtaimba Nyie".

Kufuatia sakata la kufungiwa kwa baadhi ya wasanii na nyimbo zao, akiwemo Roma Mkatoliki, Diamond Platnumz, Snura na wengine, Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Kheri James, amekerwa na maamuzi hayo yaliyofanywa na Basata na Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, kupitia kwa Naibu wake, Juliana Shonza.



Akizungumza jana Mjini Dodoma, Kheri James alieleza masikitiko yake na kusema kuwa wizara hiyo inarudisha nyuma maendeleo ya wasanii ambao wengi wao ni vijana wanaojitafutia kipato kupitia tasnia hiyo.



“Mmemfungia Roma, mmemfungia Diamond na wengine, kila anaenyanyuka mamkata mguu, hivi mnavyowafungia mtaimba nyie?



“Kama wizara itendelea na tabia hiyo ya kuwafungia wasanii, na wao ndio viongozi wa sanaa je watamsimamia nani wakishawafungia wote?” alihoji Kheri. 

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Augustine Mrema Akunwa na Muziki wa Daimond "Nampenda sana Daimond Huyu Mtoto Anajua Kuimba".

Mwenyekiti wa Chama cha TLP, Augustine Mrema amesema yeye ni miongoni kwa watu ambao wamekuwa wakifuatilia muziki wa wasanii wa hapa nchini na kati ya watu ambao wanamkuna ni Naseeb Abdul maarufu kama Diamond.

Mrema amesema kwamba anapenda sana nyimbo za mwanamuzi huyo na kwa muda mrefu amekuwa akizifuatilia.

“Nampenda sana Diamond si ndiyo yule aliyeimba ‘zilipendwa huku akitutaja mimi na Lipumba? Huyu mtoto anajua kuimba,”anasisitiza.

Mrema amesema kuwa wimbo huo ametokea kuupenda kwa kwa sababu unaonyesha hali halisi ya maisha yake sasa kwa kuwa ni ukweli usiopingika kwamba yeye na Lipumba sasa ni zilipendwa.

“Kweli tumekuwa wazeee, wakati wetu umefika na sasa tunatakiwa kuwapisha vijana waendeleze gurudumu lakini usifikirie mimi mzee ukajua sisikilizi muziki wa kizazi kipya nasikiliza zote na ninafurahi sana wanafanya kazi nzuri,”ameongeza. 

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Breaking News: Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Chamsimamisha Masomo Abdul Nondo.

Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Profesa William Anangisye, amemsimamisha masomo Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi (TSNP), Abdul Nondo hadi kesi yake ya kutoa taarifa za uongo mitandaoni na kudanganya kutekwa itakapomalizika.

Nondo alipewa dhamana na mahakama ya Iringa, jana Jumatatu,Machi 2018 baada ya kusota rumande kwa wiki kadhaa


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Baada ya Kuumia Mazoezini Jana Jonas Mkude Haya Hapa Majibu ya Daktari.

Kiungo mchezaji wa Simba, Jonas Mkude, aliumia jana wakati kikosi hicho kikijiandaa na mazoezi kuelekea mchezo ujao wa ligi dhidi ya Njombe.

Mkude aliumia wakati akiwania mpira na kiungo mshambuliaji, Mzamiru Yassin na kuepelekea kuanguka chini kisha kutolewa nje ya Uwanja wa Boko Vetarani.

Kufuatia kuumia huko, kwa mujibu wa Afisa Habari wa Simba, Haji Manara, Daktari wa timu hiyo, Yassin Gembe, alisema Mkude hajapata maumivu makali, na anaweza akarejea baada ya siku mbili mpaka tatu.

Wakati Simba inajiandaa kuivaa Njombe Mji, Aprili 3 2018, kumekuwa na hofu kubwa kwa mashabiki kama ataweza kurejea mapema, japo majibu ya Daktrari yameeleza hatachukua muda mrefu. 

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Monday 26 March 2018

MBONGO ASHINDA UBINGWA WA DUNIA NGUMI ZA KULIPWA, AMTWANGA MZUNGU.

Bondia wa ngumi za Kulipwa nchini, Bruno Tarimo 'Vifuaviwili' amewasili nchini leo mchana akitokea Australia baada ya  kufanikiwa  kushinda mkanda wa ubingwa wa WBA Oceania kumtwanga kwa pointi mpinzani wake, Billel Dib 'Baby Face' raia wa Australia.

 Pambano hilo la raundi kumi ambalo lilifanyika  wikiendi iliopita  kwenye Ukumbi wa Seagulls Rugby League Club, uliopo katika Mji wa  Tweed Heads kwenye Mkoa wa  New South Wales, Australia.
Bruno nakuwa ni bondia wa pili kutoka katika Gym ya Sharif, Bagamoyo Pwani kufanikiwa kushinda ubingwa nje ya ardhi ya Tanzania baada ya hivi karibuni, bondia Maoni Ally kushinda ubingwa wa WBC nchini Afrika Kusini.

Mara baada ya kutua nchini, Vifuaviwili alisema kuwa ushindi wake umetokana na kufanya mazoezi kwa juhudi kabla  pambano hilo huku akisisitiza hakutaka kuwaangusha Watanzania ndiyo maana amefanya kweli.
"Nashukuru nimerejea nyumbani na ubingwa ambao Watanzania walinituma huko nilipotoka kwa sababu sikutaka kuwaangusha licha mpinzani wangu kuwa bora ndani ya ulingo kwa kuwa alinisumbua lakini sikutaka kuwaangusha mlionitunma ubingwa huu," alisema  Bruno Vifua Viwili.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

MOURINHO AGEUKA KUWA MBOGO, HAMTAKI POGBA KIKOSINI.

Kocha wa Manchester United, Jose Mourinho, ameshindwa kuvumulia kelele zinazoendelea mitandaoni baada ya kusema rasmi hamuhitaji mchezaji Paul Pogba kwenye kikosi chake.

Kauli hiyo imekuja kutokana na wawili hao kuteka vichwa vya habari kwa muda mrefu kuwa hawana mahusiano mazuri.

Taarifa zinaeleza kuwa Mourinho ameitaka klabu yoyote inayomuhitaji mchezaji huyo iweke ofa mezani ili wakubaliane maana hana mpango naye.

Toni Kroos ametajwa kama mbadala anaywezeka kurithi nafasi ya Pogba kwenye kikosi cha United endapo ataondoka klabuni hapo.

Pogba alijiunga na mashetani hao wekundu mwaka 2016 kwa dau la uhamisho wa dunia wa £89m.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Mange Kimambi Atabiri Roma Mkatoliki Kuhamia CCM Kama Alivyotabiri Wema Kuhama na Ikawa.

ANAYO ENDELEA MTANDAONI :
Unakumbuka kabla ya wema sepetu kurudi ccm Mange Kimambi aliandika kwenye page yake ya instagram na kutoa sababu mbili nzito zilizomfanya Wema kurudi CCM?

Awamu hii kamuibukia Roma Mkatoliki, anadai mda wowote anajiunga CCM

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

MAREKANI: Rais Trump ametoa amri ya kufukuzwa kwa wanadiplomasia 60 wa Kirusi.

MAREKANI: Rais Trump ametoa amri ya kufukuzwa kwa wanadiplomasia 60 wa Kirusi, kufuatia Urusi kuhusishwa na shambulio la sumu kwa Jasusi wa zamani raia wa Urusi nchini Uingereza

Tayari nchi za kadhaa za Ulaya zikiwemo Ujerumani, Ufaransa na Ukraine zimetangaza kuwafukuza wanadiplomasia wa Kirusi katika nchi zao

Viongozi wa EU walikubaliana wiki iliyopita kuwa inawezekana sana Urusi ilihusika katika shambulio la sumu la Sergei Skripal(Jasusi) na binti yake kusini mwa Uingereza

Hata hivyo, Urusi imepinga kuhusika na shambulio hilo

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

TCRA Kutoa Hatima ya Times Fm Maojiano na Diamond Wiki Hii.

Hatima ya Kituo cha Redio Times cha jijini Dar es Salaam kilichotakiwa kuwasilisha kipindi cha mahojiano waliyoyafanya na mwanamuziki Diamond Platinumz kwa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kwa ajili ya uchunguzi zaidi, itajulikana wiki hii.

Taarifa zilizoifikia MCL Digital leo Jumatatu Machi 26, 2018 zinaeleza kuwa kamati ya maudhui ya TCRA iliyokuwa ikifanya uchunguzi huo inakaribia kumaliza kazi hiyo.

Machi 22, 2018, Times ilipokea barua ya kuwataka wawasilishe kipindi hicho kilichorushwa Machi 19, 2018 na kutii agizo hilo.

Mwanamuzi Diamond alizua mjadala baada ya kuzungumzia suala la nyimbo za wasanii hao kufungiwa akimlalamikia Naibu Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Juliana Shonza kutowatendea haki wasanii.

Ofisa Mkuu Idara ya Utangazaji wa mamlaka hiyo, Andrew Kisaka ameieleza MCL Digital leo kwamba tayari kamati ya maudhui inakaribia kumaliza kazi yake ya kupitia maudhui ya kipindi hicho.
chanzo: Mwananchi 

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Irene Amvaa Wema Sepetu Amtupia Dongo Zito Kisa ni Diamond.

Video vixen aliye jizolea umaarufu baada ya kuonekana kwenye video ya ‘Kwetu’ ya msanii Rayvanny Irene, amemtolea povu zito staa wa Bongo movie Wema Sepetu huku ikidaiwa kisa ni penzi la Diamond.

Tangu Zari aweke wazi kuwa kaachana na Diamond na kuwa single Kumekuwa na tetesi nyingi sana kwenye social media juu ya nani hasa anayechukua nafasi ya Zari na moja kati ya Wanawake waliotajwa kuwa na uhusiano na Diamond kwa sasa ni Irene na Wema.

Kuna stori ili trend sana kwenye mitandao ya kijamii siku za nyuma kidogo ambapo ilisemekana kuwa Irene na Wema wamepeana kichapo cha maana baada ya kugongana Madale nyumbani kwa Diamond.

Stori hiyo ilidai kuwa Diamond anatoka na Irene na Wema kwa wakati mmoja na wikiendi hii Irene kamtupia dongo Wema ambapo amemcheka kuwa anajiita African beauty wakati hata kiwanja hana!.

African beauty ni wimbo mpya wa Diamond na siku wimbo huo ulipotoka wasanii mbali mbali wa WCB akiwemo Harmonize alimtunuku Wema jina la African beauty jambo ambalo lilimfanya Wema ajitambe kuwa ni African beauty.

Fununu za Irene kuwa na Mahusiano na Diamond zilianza siku nyingi sana wakati bado Diamond yuko na Zari ingawa Diamond alikuwa anakataa kuwa hana Mahusiano naye.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Saturday 24 March 2018

Diamond amtaka Lulu Diva kumzalia mtoto Rich Mavoko.

Baada ya kukanusha kwa muda mrefu, hatimaye imebainika kuwa Rich Mavoko na Lulu Diva ni wapenzi.

Aliyeweka wazi hilo ni Diamond Platnumz ambaye anafanya kazi na Rich Mavoko kupitia label yake ya WCB. Katika kumtakia kheri ya siku ya kuzaliwa Lulu Diva, Diamond amemwandika haya mrembo huyo.

We @luludivatz nae Utulete Mtoto sasa, Tushachoka picha zenu za Kuviziwa kwenye ma Parties😏👌🏼#AfricanBeauty

Utakumbuka Fiesta ya Dar es Salaam iliyofanyika November, 2017 kuna picha zilisambaa mtaandaoni zikiwaonyesha Rich Mavoko na Lulu Diva katika mapozi ya kimahaba ingawa wenyewe walikanusha na hilo pia ila kwa kauli hii ya Diamond ni wazi lilokuwa likisema lipo. 

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Okwi,Bocco Waahidi Kupata Ubingwa wa Ligi Kuu.

BAADA ya Simba kutolewa katika Kombe la Shirikisho Afrika, mastraika wa timu hiyo John Bocco na Emmanuel Okwi kwa pamoja wameapa kufia uwanjani ili Wekundu wa Msimbazi wabebe ubingwa wa Ligi Kuu Bara msimu huu.

Simba iliondolewa na Al Masry ya Misri katika Kombe la Shirikisho baada ya awali kutoka sare ya mabao 2-2 jijini Dar es Salaam halafu ugenini wakatoka suluhu.

Kutokana na hali hiyo, Okwi na Bocco wamesema lengo lao sasa ni kuhakikisha wanapambana kufa na kupona kwenye Ligi Kuu Bara ili waweze kuiwezesha Simba kutwaa ubingwa.

Simba inaongoza katika ligi kuu ikiwa na pointi 46 sawa na Yanga, inayoshika nafasi ya pili, lakini wenyewe wana tofauti kubwa ya mabao ya kufunga na kufungwa.

Akizungumza na Championi Jumamosi, Okwi alisema, mipango yao ya kuiwezesha Simba kutwaa ubingwa wa Kombe la Shirikisho imekwama, sasa wanaelekeza nguvu zao kwenye ligi kuu.

“Tunarudi kujipanga kwenye ligi kuu, kwani ndiyo sehemu pekee tunapotakiwa tupambane kufa na kupona ili mwakani tuweze kushiriki tena michuano ya kimataifa, tutapambana tuwe mabingwa,” alisema Okwi.

Kwa upande wake, Bocco ambaye pia ni nahodha wa Simba, yeye alisema; “Kiu yangu na wachezaji wenzangu ni kuhakikisha tunatwaa taji la Ligi Kuu Bara, maana ndiyo silaha pekee tuliyonayo kwa sasa, hiyo ndiyo tiketi ya sisi kucheza mechi za CAF mwakani.

“Pia tunajua furaha ya mashabiki wa Simba kwa sasa ni kuona tunatwaa ubingwa na siyo kitu kingine, hivyo tumejipanga kuhakikisha hilo linatokea bila tatizo.”

Simba leo Jumamosi inatarajiwa kuanza mazoezi kujiandaa na mchezo dhidi ya Njombe Mji, Aprili 3, mwaka huu. 

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Wednesday 21 March 2018

Mahakama Kuu Iimetoa Amri kwa Serikali Kupeleka Majibu Juu ya Abdul Nondo.

Mahakama Kuu leo imetoa amri kwa serikali kuweza kupeleka majibu ya maombi yaliyofunguliwa na Mawakili wa Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi nchini Abdul Nondo kujibu kesi ya kutompeleka Mahakamani kwa zaidi ya siku 10 tangu kukamatwa kwake.


Amri hiyo imetolewa leo Jumatano ya Machi 21 ambapo Mahakama kuu mbele ya Jaji Sameji  iliwataka DCI,IGP na AG kufika mahakamani kwa ajili ya kujibu mashtka juu ya Nondo ambapo leo majibu ya maombi hayo wyametakiwa yapelekwe Machi  26 na walalamikaji  kupeleka majibu yao ya nyongeza yapelekwe Machi 27.

Aidha  mahakama inatarajiwa kusikiliza maombi ya pande zote mbili 04/08/18 kutoa hatma ya Abdu Nondo.

Kwa upande mwengine kesi ya mwanafunzi huyo (Nondo)  iliyosikilizwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Iringa imeahirishwa mpaka Jumatatu ya tarehe 26 March 2018 ambapo Hakimu atatoa uamuzi kwamba mshitakiwa apewe dhamana ama asipewe dhamana, mshitakiwa amerudishwa rumande.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Khadija Khopa Achoka Kuwa Single Ataka Mwanaume wa Kumuoa "Nataka Mume Sipendi Dhambi".

Malkia wa Mipasho nchini Tanzania asiyekuwa na mshindani, Khadija Kopa ametangaza rasmi kuhitaji mume wa kumuoa ili aweze kuishi naye huku akiweka vigezo vyake kuwa hataki aliyechini ya miaka 40 kwa madai hawezi kufundisha tution.


Khadija Kopa ametoa kauli hiyo wakati alipokuwa anazungumza kwenye kipindi cha KIKAANGONI kinachorushwa mubashara kupitia kurasa za EATV kila siku ya Jumatano kuanzia saa 8:00 mchana hadi 10:00 alasiri.

"Sijaolewa ila sitaki kusomesha tuition, nataka mwanaume aliyekuwa na umri mkubwa kuanzia 40 kwenda juu, mwenye mapenzi ya dhati na huba, mwenye kujali na kujua ninataka nini, atakayeweza kuijali familia yangu pamoja na watoto wangu, awe mnene kidogo na sio mwembamba, awe na rangi yeyote na kabila lolote lile kwasababu mimi sina ubaguzi katika vitu hivyo", amesema Khadija Kopa.

Pamoja na hayo, Khadija Kopa ameendelea kwa kusema "napenda mwanaume mfanyakazi maana kupata pesa ni majaliwa ila asiwe mwanaume wa kulala nyumbani akanitegemea mimi nikafanye kazi ili yeye aje kula maana maisha ni kusaidia nasio kuegemea upande mmoja tena wa mwanamke".

Aidha, Khadija Kopa amesema sababu kubwa iliyompelekea mpaka sasa kutoolewa ndoa nyingine baada ya aliyekuwa mume wake kufariki ni kutokana na kuwa na wasiwasi na wanaume wa sasa.

"Nina wasiwasi kwa mwanaume atakayekuja kunioa kwa sasa, maana najiuliza mengi je atakuwa na huba kama marehemu mume wangu ndio maana mpaka sasa sijaolewa kwa kuwa nafikiria sana. Mume wangu aliyefariki alikuwa ni mwenye huba, mwenye kunijali, nimekaa naye miaka yote sijawahi kugombana naye, nilikuwa natamani kumuona akinuna ananuna vipi, alikuwa na vigezo vyote", amesisitiza Khadija Kopa.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Necta Yafanya Mabadiliko Mtihani Darasa la Saba.

Wanafunzi wa darasa la saba ambao watafanya mtihani mwaka huu watakutana na mabadiliko ya mfumo wa utungaji  wa mtihani wa kuhitimu elimu ya msingi .

Mabadiliko hayo yamefanywa na Baraza la Mitihani la Taifa  (Necta) jana na kutangazwa na Katibu Mtendaji wa baraza hilo, Dk Charles Msonde.

Ofisa Habari wa Necta, John Nchimbi amesema mabadiliko hayo aliyatangaza Dk Msonde katika mkutano mkuu wa tano wa maofisa elimu mkoa na wilaya unaofanyika Dodoma.

Nchimbi amesema katika muundo huo mpya kila somo litakuwa na maswali 45, kati ya hayo, maswali 40 yatakuwa ya kuchagua jibu sahihi na matano yasiyo ya kuchagua (yatakuwa ya kujieleza/kuonyesha njia na jibu nk).

Amesema maswali 40 kila swali litakuwa na alama moja na maswali matano kila swali litakuwa na alama mbili huku majibu ya maswali 40 yatajibiwa kwenye OMR FORM na maswali matano yatajibiwa kwenye karatasi maalum itakayoandaliwa.

Kutokana na muundo huo mpya, Necta imetoa wito kwa walimu wakuu kuanza kuwapima wanafunzi kwa kutumia mabadiliko hayo ili kuwajengea uzoefu.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Mwakyembe Amshukia Diamond, Asema Umarufu Utamkosti, Awezi Bishana na Shonza na Atapotea Kubishana na Serikali.

Waziri wa Habari Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe ameeleza kukerwa na mwanamuziki Diamond Platnumz kutokana na kumdharirisha naibu wake Juliana Shonza wakati akihojiwa katika kipindi cha The Play List cha Times FM na mitandaoni.

Katika maelezo yake Mwakyembe amesema inaelekea sasa Diamond ameanza kulewa umaarufu sasa. Kuhusu hoja ya vikao anavyodai mwanamuziki huyo Mwakyembe amesema kuwa “kama ni vikao na wasanii, tumefanya vingi sana, lakini Diamond hahudhurii vikao hivyo na si wajibu wa Serikali kumfanyia kikao chake mwenyewe, haijalishi nibmaarufu kiasi gani."

"Hatuwezi kuwa na sheria kwa wasanii wengine na sheria maalum kwake, nadhani hizi ni dalili za kuanza kulewa umaarufu kwani Diamond si Kiongozi wa Shirikisho la Muziki wala msemaji wa Chama cha Muziki wa kizazi kipya kuwasemea wenzake," amesema Mwakyembe.

Aidha Waziri Mwakuembe amemalizia kwa kumshauri mwanamuziki huyo kuwa "si busara kwake kushindana na Serikali, na kama ana ushauri basi autoe kistaarabu utazingatiwa lakini si kwa kumshambulia Naibu Waziri kwa dharau na kejeli jinsi alivyofanya. Sijafurahishwa hata kidogo." 

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Tuesday 20 March 2018

Mkurugenzi wa TBC, Dkt. Ayub Rioba apata Ajali Kigoma.

Watu wawili wamefariki Dunia wilayani Kasulu mkoani Kigoma kufuatia ajali ya gari la Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utangazaji Tanzania TBC Dkt. Ayub Rioba, lililokuwa likitokea wilayani Kibondo kwenda Kigoma Mjini.

Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Kigoma, Kamishna Msaidizi Martin Otieno amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kusema kuwa chanzo cha ajali hiyo ni utelezi uliosababisha gari kuacha njia na kuwagonga waenda kwa miguu watatu.

Kamanda  Otieno aliwataja waliofariki katika ajali hiyo kuwa ni watembea kwa miguu wawili, waliofahamika kwa majina ya Teresia Mpoma (55) mkulima na Mkazi wa Nyakitonto, Yuster Masharubu (55) mkazi wa Nyakitonto na Majeruhi mmoja aliefahamika kwa jina la Diana Shedrack (10) mwanafunzi shule ya Msingi Nyakitonto, ambae hali yake ilielezwa kuwa mbaya huku akiendelea na matibabu katika Hospitali ya Wilaya ya Kasulu.

Amesmea Gari la Mkurugenzi Mkuu wa TBC lililopata ajali lenye namba za usajili STK 8769 lilikuwa na abiria wawili akiwemo mkurugenzi mkuu wa TBC, Dkt. Ayub Rioba na Mkuu wa kanda ya magharibi TBC Mhandisi Zebron Mafuru ambao wote wametoka salama na hali zao ni nzuri.

Kamanda Otieno aliongeza kwwa kutoa tahadhari kufuatia  Chanzo cha ajali hiyo kuwa ni utelezi unaotokana na Mvua zinazoendelea kunyesha Katika Mkoa huo,hivyo amewaomba madereva kuendesha magari kwa umakini kutokana na ubovu wa barabara hiyo na kuzingatia sheria za barabarani.

Dkt. Rioba yuko katika ziara ya kukagua vituo vipya vya matangazo vilivyojengwa katika maeneo ya mipakani.

Pichani kushoto ni Mkurugenzi mkuu wa TBC, Dkt. Ayub Rioba baada ya kunusurika kifo akiwa eneo la tukio pamoja na Polisi waliofika .
Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Monday 19 March 2018

Zitto Kabwe Alishitaki Jeshi La Polisi Mahakamani.

Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi wa Chama, ACT Wazalendo, Kabwe Ruyagwa Zitto amefunguka na kusema kuwa chama chake tayari kimefungua kesi ya Kikatiba katika mahakama Kuu Dar es Salaam kulishtaki jeshi la polisi.

Zitto Kabwe amesema hayo leo Machi 13, 2018 wakati akitoa tathmini ya ziara alizofanya kutembelea Madiwani katika kata mbalimbali nchini zinazoongozwa na ACT Wazalendo ambapo amedai katika ziara hiyo wamebaini mambo mengi ikiwa pamoja na hali ya maisha kuwa ngumu sana, migogoro ya ardhi, kukosekana kwa huduma ya Maji safi na salama, ukosefu wa huduma bora za afya, tatizo la Miundombinu ya Usafirishaji.

Kiongozi huyo aliendelea kuweka wazi mambo mbalimbali ambayo wamefanikiwa kuyaona katika ziara hizo kuwa ni pamoja na  ukosefu wa pembejeo za Kilimo, ukosefu wa masoko ya mazao ya wavuvi, wakulima na wafugaji, kushuka kwa bei ya mazao yao, kupanda kwa gharama za maisha ya watu, kupanda kwa gharama za vifaa vya ujenzi, upungufu mkubwa wa vyumba vya madarasa, vyoo pamoja na walimu, na kuzorota kwa hali ya usalama wa wananchi pamoja na mali zao, hali mbaya ya ajira kwa vijana pamoja na uminywaji mkubwa wa demokrasia na uhuru wa watu kukusanyika na kujieleza.

"Tumefungua Kesi ya Madai Na. 8/2018 Mahakama Kuu hapa Dar Es Salaam, kulishtaki Jeshi la Polisi, kutokana na Jeshi hilo kuingilia, visivyo halali shughuli, ziara yetu ya kuhamasisha maendeleo katika Kata tunazoziongoza. Tunaamini Mahakama itatenda haki kwenye suala hili" alisema kiongozi huyo

Aidha Zitto Kabwe ametoa ushauri kwa serikali kuhusu suala la Demokrasia nchini na kusema kuwa mazungumzo ya kitaifa ndiyo yanaweza kuwa na jibu kuhusu masuala haya na kuleta utatuzi juu ya jambo hili.

"Demokrasia na Ustawi wa Taifa tunaendelea kusisitiza rai yetu kuhusu umuhimu wa kuitisha Mkutano wa Kitaifa wa maridhiano ya kisiasa kama jukwaa la kuzijadili changamoto za uendeshaji wa siasa nchini. Jambo hilo litaondoa uadui unaoendelea kukua sasa kati ya serikali na wananchi, viongozi wa dini, mashiriki yasiyo ya Kiserikali, taasisi za wanafunzi, pamoja na vyama vya Upinzani. Tunaamini mazungumzo ya Kitaifa ndio jambo sahihi la utatuzi wa suala hili" alisisitiza Zitto Kabwe

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Friday 16 March 2018

Baada ya Magari ya Mwendokasi Kusitisha Huduma ya Usafiri Daladala, Bodaboda Zatumia Njia ya Mwendokasi.

Baada ya Mradi wa Mabasi yaendayo haraka (Dart) kusitisha huduma za usafiri wa mwendokasi leo, baadhi ya magari madogo, daladala na bodaboda wametumia fursa hiyo kupitisha magari yao katika barabara zinazotumika na magari hayo.

Mwananchi limeshuhudia daladala zikipita katika vituo hivyo huku zikishusha na kupakiza abiria katika kila kituo cha mwendokasi, huku trafiki wakielekeza baadhi ya magari kutoka kwenye barabara hizo.

Hata hivyo vituo vingi vya mwendokasi vimefungwa isipokuwa kituo cha Ubungo ambacho wahudumu wameonekana wamelala huku kukiwa hakuna abiria  wanaoingia katika kituo hicho.

Dereva wa daladala linalofanya safari zake Mbagala Rangitatu - Simu 2000 Jafari Himid amesema kutokana na foleni iliyopo katika barabara hiyo, wameamua kutumia barabara za mwendokasi ili kuokoa muda.

"Bila kufanya hivi hatuwezi kuwahisha abiria na hizi barabara leo hazina matumizi, hata trafiki wanatuachia hawajatukamata," amesema Jafari.

Hata hivyo barabara ya Morogoro Road ina foleni kubwa inayosababishwa na kipande cha barabara ya jangwani kujaa tope. 

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Thursday 15 March 2018

Download wimbo mpya wa Rockygazim unaoitwa "Nipokee".

https://my.notjustok.com/track/download/id/313584


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Video: Uzinduzi wa Diamond Watikisa Kenya Awaliza Wakenya Jukwaani na Historia ya Maisha Yake.

MSANII wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz amezindua rasmi albamu yake mpya ‘A Boy From Tandale’ jijini Nairobi na kufanya bonge la shoo akiwa na timu nzima ya WCB.

Mbali na WCB, wasanii wengine waliopada jukwaani na kutikisa katika shoo hiyo, ni msanii wa Marekani, Omario.


Albamu mpya ya Diamond imesheheni ngoma 20 kali zikiwemo alizowahi kuzitoa kipindi cha nyuma na nyingine mpya.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa