Tuesday 27 March 2018

Augustine Mrema Akunwa na Muziki wa Daimond "Nampenda sana Daimond Huyu Mtoto Anajua Kuimba".

Mwenyekiti wa Chama cha TLP, Augustine Mrema amesema yeye ni miongoni kwa watu ambao wamekuwa wakifuatilia muziki wa wasanii wa hapa nchini na kati ya watu ambao wanamkuna ni Naseeb Abdul maarufu kama Diamond.

Mrema amesema kwamba anapenda sana nyimbo za mwanamuzi huyo na kwa muda mrefu amekuwa akizifuatilia.

“Nampenda sana Diamond si ndiyo yule aliyeimba ‘zilipendwa huku akitutaja mimi na Lipumba? Huyu mtoto anajua kuimba,”anasisitiza.

Mrema amesema kuwa wimbo huo ametokea kuupenda kwa kwa sababu unaonyesha hali halisi ya maisha yake sasa kwa kuwa ni ukweli usiopingika kwamba yeye na Lipumba sasa ni zilipendwa.

“Kweli tumekuwa wazeee, wakati wetu umefika na sasa tunatakiwa kuwapisha vijana waendeleze gurudumu lakini usifikirie mimi mzee ukajua sisikilizi muziki wa kizazi kipya nasikiliza zote na ninafurahi sana wanafanya kazi nzuri,”ameongeza. 

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment