Wednesday 21 March 2018

Mahakama Kuu Iimetoa Amri kwa Serikali Kupeleka Majibu Juu ya Abdul Nondo.

Mahakama Kuu leo imetoa amri kwa serikali kuweza kupeleka majibu ya maombi yaliyofunguliwa na Mawakili wa Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi nchini Abdul Nondo kujibu kesi ya kutompeleka Mahakamani kwa zaidi ya siku 10 tangu kukamatwa kwake.


Amri hiyo imetolewa leo Jumatano ya Machi 21 ambapo Mahakama kuu mbele ya Jaji Sameji  iliwataka DCI,IGP na AG kufika mahakamani kwa ajili ya kujibu mashtka juu ya Nondo ambapo leo majibu ya maombi hayo wyametakiwa yapelekwe Machi  26 na walalamikaji  kupeleka majibu yao ya nyongeza yapelekwe Machi 27.

Aidha  mahakama inatarajiwa kusikiliza maombi ya pande zote mbili 04/08/18 kutoa hatma ya Abdu Nondo.

Kwa upande mwengine kesi ya mwanafunzi huyo (Nondo)  iliyosikilizwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Iringa imeahirishwa mpaka Jumatatu ya tarehe 26 March 2018 ambapo Hakimu atatoa uamuzi kwamba mshitakiwa apewe dhamana ama asipewe dhamana, mshitakiwa amerudishwa rumande.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment