Tuesday 6 March 2018

Gazeti Lililomuandika Mange Vibaya Lapewa Onyo Kali na Serikali.

Serikali imelionya Gazeti la Tanzanite kwa kuchapisha picha za utupu kitu ambacho ni kinyume na maadili ya kazi hiyo.

Hatua hiyo imekuja baada msemaji wa serikali Dkt. Hassan Abbas kuahidi kulichukulia hatua gazeti hilo baada ya kupokea malalamiko mengi kutoka kwa wananchi kutokana na ukakasi wa habari zake pamoja na picha wanazochapisha.


Onyo hilo limetolewa hii leo mjini Dodoma na Msemaji wa Serikali, Dkt. Hassan Abbas alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari.

Amesema kuwa wametoa onyo kwa Gazeti hilo kwakua ni jipya pia ni mara yake ya kwanza kutenda kosa kama hilo hivyo ni bora kujirekebisha.

Amesema kuwa Gazeti hilo halikuwa na kosa katika maudhui ya kuandika ila kosa kubwa ni kutumia picha za utupu, hivyo kwenda kinyume na maadili.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment