Friday 29 September 2017

LEMA: MWIGULU AONDOKE NDANI YA MASAA 12.



Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

BREAKING: Ofisi ya Bunge kuhusu Mbowe kunyang'anywa gari Nairobi.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Majambazi Wapora Msikitini, Wamjeruhi Mlinzi kwa Panga.

WATU wanaosadikiwa kuwa ni majambazi, wamevamia Msikiti Mkuu wa Ijumaa ulioko Kata ya Igunga Mjini wilayani hapa mkoani Tabora, kisha kumjeruhi mlinzi na kupora baadhi ya vitu ikiwemo vitabu vya dini ya Kiislamu.

Mlinzi aliyejeruhiwa ni Juma Mussa (55), mkazi wa Mtaa wa Nkokoto kata ya Igunga ambaye amelazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Igunga na hali yake bado ni mbaya. Mkuu wa Wilaya ya Igunga ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya, John Mwaipopo alithibitisha kutokea kwa uhalifu huo na mtuhumiwa mmoja amekamatwa pamoja na vitu vilivyoibwa.

Alimtaja mtuhumia huyo kuwa ni Juma Mponi (45) ambaye ni mkazi wa Mtaa wa Stendi ya Mabasi mjini Igunga, na kutamba kuwa hakuna jambazi atakayetoka salama Igunga kwa kuwa polisi wamejipanga kikamilifu kukabiliana na matukio kama hayo.

Akizungumza kwa shida akiwa wodini, mlinzi huyo alisema shambulio hilo limetokea Septemba 25, mwaka huu saa 8 usiku, ambako watu hao walifika msikitini hapo kisha kurusha jiwe kwenye eneo alilokuwa amekaa.

Alisema baada ya kuona jiwe hilo, aliamua kusimama na mara jambazi mmoja aliruka uzio wa msikiti kisha akaingia na kuanza kumshambulia kwa mapanga kichwani. Alibainisha kuwa wakati akishambuliwa, aliona majambazi wengine wakifungua milango ya msikiti na mmoja wao akimweleza mwingine “wewe maliza kabisa huyo mlinzi.”

Hata hivyo, mlinzi huyo aliendelea kuuomba msaada kwa kupiga kelele ili asaidiwe, hali iliyowafanya majambazi kukimbia kusikojulikana wakiondoka na baadhi ya mali za msikiti. Mhasibu wa Msikiti Mkuu wa Ijumaa, Issa Said Feruzi alitaja vitu vilivyoibiwa na majambazi hao kuwa kuwa ni misahafu minne, feni moja, saa kubwa, vitabu vya hitima 30, kitabu cha mapato na matumizi, daftari za Tabligh nne, maikrofoni na stendi yake, miswala miwili; vyote vikiwa na thamani ya Sh 374,000.

Hata hivyo, alisema vitu vyote vimepatikana na viko Kituo cha Polisi Igunga; huku Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya ya Igunga, Melchades Magongo amekiri kumpokea Juma Mussa, akieleza kuwa alimpokea hospitalini hapo akiwa na majeraha kichwani ambayo yanaonesha alikatwa na kitu chenye ncha kali. Dk Magongo alisema hali ya mlinzi huyo bado si nzuri akiendelea kupatiwa matibabu zaidi katika wodi namba nane hospitalini hapo.



Tupe Maoni Yako

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Ujumbe wa Ancelotti Baada ya Kufukuzwa.

Baada ya kufutwa kazi aliyekuwa kocha wa Bayern Munich Carlo Ancelotti ameishukuru bodi ya timu hiyo kwa kumwamini pamoja na ushirikiano waliompa katika kipindi chote alichofundisha timu hiyo.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Ancelotti ameandika “Imekuwa heshima kubwa kuwa sehemu ya historia ya Bayern Munich. Napenda kuishukuru Klabu, Wachezaji na zaidi mashabiki wa kushangaza ambao sijawahi kukutana nao tangu nianze kufundisha soka”.
Mtalaam huyo wa ufundi mwenye miaka 58 alipoteza kibarua chake jana mchana baada ya bodi ya Bayern Munich kuketi na kocha huyo na kuazimia kutoendelea na mkataba wake uliokuwa unamalizika 2019.
Baadhi ya wachezaji wa Bayern Munich Thiago Alcantala, Frank Ribery, Robert Lewandowski na Arturo Vidal wamemshukuru Ancelotti kila mmoja akieleza kwa namna ambavyo amefaidika kuwa chini ya kocha huyo kwa msimu mmoja


Tupe Maoni Yako

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Serikali Yaifungia Gazeti la Raia Mwema kwa Siku 90.

 Serikali imesitisha uchapishaji na usambazaji wa gazeti la kila wiki la Raia Mwema kwa muda wa siku 90 kuanzia leo.

Mkurugenzi wa Idara ya Habari (Maelezo) na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dk Hassan Abbasi amesema leo Alhamisi kuwa agizo hilo pia linahusu toleo la mtandaoni.

Dk Abbasi amesema adhabu hiyo inatokana na toleo namba 529 la Septemba 27 hadi  Oktoba 3 lililochapisha habari ya uchambuzi inayosomeka “Urais utamshinda John  Magufuli.”

Mwenyekiti wa Bodi ya Raia Mwema, Jenerali Ulimwengu amesema wameambiwa sababu ya kusitishwa kwa gazeti hilo ni habari hiyo.

Ulimwengu amesema kwa sasa wanashauriana kuona ni nini cha kufanya.



Dk Abbasi amesema katika taarifa kwa vyombo vya habari kuwa, Serikali inasisitiza uchambuzi huo ni maoni ya Raia Mwema  ya haki (fair comment), hata hivyo, kwa bahati mbaya, na nia ovu, makala hiyo ilisheheni nukuu za kutunga na zisizo za kweli zikimsingizia Rais John Magufuli.

Amesema gazeti hilo pia limewahi kuonywa kwa makosa mbalimbali.



Amesema nukuu za uongo, kutungwa na zenye nia mbaya zikidai Rais alipata kusema ni, “Suruali za zamani msizitupe, mtazihitaji baadae,” na “Watakaobaki  Dar es Salaam baada ya mwezi wa saba watakuwa wanaume kwelikweli.”



Dk Abbasi amesema walipotakiwa kuthibitisha wapi iwe ndani au nje ya nchi Rais alipata kutoa kauli hizo, wahariri wa Raia Mwema waliomba muda ambao walipewa. “Wakarejea na kuthibitisha kuwa hawana ushahidi huo, wakakiri kosa na kuomba radhi.”



Mkurugenzi huyo amesema bado Serikali inaamini Watanzania wakiufanyia mzaha upotoshaji wa taarifa na uchochezi katika zama hizi za Tehama amani na utulivu uliopo kwa miaka mingi utapotea na kukaribisha maafa kama ilivyotokea kwingineko duniani.



“Serikali, katika uamuzi huu, uliochukuliwa kwa mujibu wa mamlaka aliyonayo Waziri wa Habari katika kifungu cha 59 cha Sheria ya Huduma za Habari Na. 12, 2016, imetoa adhabu ndogo tofauti na ukubwa wa kosa kwa kuwa wahariri wa gazeti hili hawakufanya tashtiti, wamekiri kosa,” amesema.

Dk Abbasi amesema kupitia hilo, wamejifunza mambo kadhaa kuhusu changamoto za kiwango cha weledi wa uandishi wa habari nchini kiasi cha kuwalazimu kutoa ufafanuzi wa kina kwa faida ya umma na tasnia yenyewe; kwamba uandishi ni taaluma adhimu na yenye haki na wajibu vinavyopaswa kufuatwa na si kufanyiwa dhihaka.


Tupe Maoni Yako
Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

VIDEO:WAZIRI MBARAWA: 'Watanzania wengi wanafikiri treni inajengwa siku 3'.



Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Shilole Hausiki Kuvunja Ndoa Yangu Bali ni Wazazi wa Nawal- Nuhu Mziwanda.

Mwanamuziki Nuh Mziwanda amekanusha suala linaloongelewa na watu kuwa kuvunjika kwa mapenzi kati yake na mzazi mwenzie chanzo chake siyo Shilole bali ni wazazi wa binti huyo.

“Unajua watanzania ukiwapa picha tu, basi wao wataandika maneno wataandika wenyewe Shilole hausiki hata kidogo kuvunjika kwa mahusiano yangu.”

“Wahusika ni wazazi wake ambae yeye aliamua kuwasikiliza wazazi wake kwa kuolewa na mtu mwingine na hatukuwa na ugomvi wowote ila ndio hivyo wazazi walikuwa na nguvu sana kunizidi mimi,” aliongeza.

Aidha Nuh Mziwanda aliongeza kuwa mahusiano yake ameyaweka kando na yupo kupambana na hali yake, lakini anashukuru Mungu mtoto wake bado anaendelea vizuri na anapata taarifa zote muhimu kumuhusu mtoto wake lakini mengine imebaki stori.


Tupe Maoni Yako

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Upinzani Kenya Waitisha Maandamano Makubwa Wiki Ijayo.

Muungano wa upinzani nchini Kenya umeitisha maandamano ya umma kupinga mapendekezo ya kuifanyia mabadiliko sheria ya uchaguzi.

Wabunge wanaoegemea upande wa serikali wanafanya hima kupitisha mswada ambao utamwezesha Uhuru Kenyatta kutangazwa rais bila ya kufanyika uchaguzi ikiwa upinzani utasusia marudio ya uchaguzi tarehe 26 mwezi Oktoba.

Wanachama wa upinzani walitoka nje wakati upande wa serikali ukitumia wingi wake bungeni kuharakisha mabadiko ambayo yatasababisha mswada huo kuwa sheria kabla ya marudio ya uchaguzi.

Kati ya yale yaliyo kwenye mswada huo ni kuruhusu mgombea kutangazwa rais bila ya kufanyika uchaguzi ikiwa mgombea mwingine atasusia uchaguzi.

Viongozi wa upinzani Kenya wazuiwa kwenye uwanja wa ndege Nairobi
Upinzani kuandamana Kenya
''Zaidi ya 100 walifariki'' katika maandamano Ethiopia
Marudio hayo ya uchaguzi yana wagombea wawili, Rais Uhuru Kenyatta na Raila Odinga.
Mswada huo pia unasema kuwa mahakama ya juu haiwezi kufuta matokeo ikiwa mfumo wa eletroniki utafeli
Kufeli kwa mfumo wa kupiga kura kwa njia ya eletroniki ndio ilikuwa sababu kuu ya kufutwa kwa matokeo ya urais.

Mgombea wa Upinzani Raia Odinga amekashifu hatua hizo kama jaribio la kuiba kura na kumpendela rais Uhuru Kenyatta.
Ametisha maandamano ya kote nchini kila Jumatatu na Ijumaa kuanzia wiki ijayo.


Tupe Maoni Yako

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

VIDEO:MEYA BONIFACE: MAKONDA AMENITISHIA, ANATAKA NIONDOE KESI YAKE YA KUFOJI CHETI.



Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Lijualikali Aachiwa Ahojiwa na Polisa Kwa Saa Nne.

Mbunge wa Kilombero mkoani Morogoro, Peter Lijualikali ameshikiliwa na kuhojiwa na polisi wilayani Malinyi kwa saa nne.

Pamoja naye, viongozi wengine watatu wa Chadema walishikiliwa jana Alhamisi wakidaiwa kufanya mkusanyiko bila kuwa na kibali cha polisi.

Akizungumza leo Ijumaa baada ya kuachiwa mbunge huyo amesema aliamriwa na polisi  kusimama alipokuwa akitoka kwenye kikao cha ndani cha viongozi na baadhi ya wanachama wa Chadema katika Kijiji cha Makerere wilayani Malinyi.

“Nilipoamriwa kushuka kwenye gari nilitii na kuongozana na polisi hadi kituo cha i Malinyi ambako nilihojiwa kwa nini nifanye kikao bila kibali. Nikawaambia kilikuwa ni kikao cha ndani wakasisitiza kuwa ni lazima tuwe na kibali,” amesema Lijualikali.

Amesema hakuna sheria inayowataka kuwa na kibali wanapofanya vikao vya ndani kwa kuwa hawahitaji ulinzi wa polisi katika vikao hivyo na hapakuwa na uwezekano wa kutokea vurugu.

Mbunge huyo amesema alipoona anahojiwa muda mrefu aliamua kumpigia simu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Ulrich Matei aliyemweleza yupo likizo.

Amesema aliamua kumpigia Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba na kumweleza kilichotokea ambaye aliahidi kushughulikia suala hilo.

“Nashukuru baada ya kuongea na Mwigulu niliachiwa. Niliondoka kituoni hapo saa nne usiku tangu wanishikilie saa 12:00 jioni. Walinitaka kuripoti kesho yake (leo) saa mbili asubuhi na niliripoti wakaniambia niripoti tena Oktoba 5,” amesema.

Wengine waliokamatwa pamoja na mbunge huyo ni Mwenyekiti wa Chadema Malinyi, Emmanuel Lukindo; Katibu wake, Sadi Lyampawe na Katibu Mwenezi wa wilaya, Lucas Lyambalimu ambao wote wameachiwa kwa dhamana.


Tupe Maoni Yako

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Yanga Kumkosa Tshishimbi Mechi ya Kesho.

Klabu ya Yanga imeeleza kuwa imejiandaa vyema kuelekea mchezo wa ligi kuu ya soka Tanznaia Bara kesho dhidi ya Mtibwa Sugar kwenye uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam.

Akiongea na Wanahabari leo kwenye makao makuu ya klabu msemaji wa Yanga, Dismass Ten amesema timu hiyo imejiandaa vya kutosha na inahitaji pointi tatu muhimu kwenye mchezo huo.
“Timu imejiandaa vizuri, sisi ni mabingwa watetezi kwahiyo tunahakikisha tunachukua pointi tatu muhimu na hatutadharau mechi”, amesema Ten.

Aidha kocha msaidizi wa timu hiyo Shadrack Nsajigwa amesema wachezaji wote wapo vizuri isipokuwa Amis Tambwe ambaye alikuwa majeruhi lakini tayari ameshapata kibali cha daktari na anaendelea vizuri na mazoezi.

Yanga ambayo ipo nafasi ya sita ikiwa na alama 8 itamkosa nyota wake wa Kimataifa kiungo Tshishimbi Kabamba ambaye anatumikia adhabu ya kukosa mechi moja baada ya kupata kadi 3 za njano katika mechi 3 zilizopita.


Tupe Maoni Yako

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Tanzia: CUF Yapata Pigo Kiongozi Wao Afariki.

Kiongozi wa CUF Mheshimiwa Ali Juma Suleiman ambaye alikuwa Kaimu Mwenyekiti wa (CUF) Jimbo la Mto Pepo na Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa (CUF) Wilaya ya Magharibi A. Zanzibar amefariki dunia usiku wa kuamkia leo katika hospitali ya Mnazi Mmoja.

Baadhi ya viongozi wa (CUF) na wanachama pamoja na wananchi wakiwa katika hospitali ya Mnazi Mmoja kufuatilia mwili wa Marehemu Ali Juma Suleyman.

Naibu Katibu Mkuu (CUF) Zanzibar, Nassor Ahmed Mazrui amethibitisha kutokea kwa kifo hicho na kusema kuwa Mheshimiwa Ali Juma alikuwa amelazwa hospitali ya Mnazi Mmoja kufuatia kuvamiwa nyumbani kwake na kupigwa kisha baadaye kutupwa katika maeneo ya Masingini na makundi ya watu yanayoendesha vurugu Zanzibar.

"Nasikitika kutangaza kifo cha Mheshimiwa Ali Juma Suleiman, Kaimu Mwenyekiti wa CUF Jimbo la Mto Pepo na Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa CUF Wilaya ya Magharibi A. Amefariki dunia majira ya saa 4 usiku hapa jana hapa Mnazi Mmoja Hospital baada ya kupigwa vibaya na Mazombi juzi usiku" alisema Naibu Katibu Mkuu CUF Nassor Mazrui

Viongozi wa CUF wamesema kuwa mwili wa marehemu umeshafanyiwa uchunguzi tayari na sasa wamekabidhiwa kwa ajili ya kufanya mazishi ambayo yatafanyika leo katika makaburi ya Mwanakwereke, nje kidogo ya mji wa Unguja. 


Tupe Maoni Yako

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Mwanaume Aliyeshauriwa na Mganga Kufanya Mapenzi na Punda Atupwa Jela.

Mwanamme mmoja nchini Afrika Kusini aliyetambulika kwa jina la Ntando Mankungwini ametupwa jela mwaka mmoja baada ya kukutwa akifanya mapenzi na Punda.

Ntando (23) alikutwa usiku wa Jumatano ya septemba 20 mwaka huu kwenye zizi la nyumba jirani na nyumbani kwao mjini Mount Fletcher, Afrika Kusini akiwa nyuma ya punda usiku wa manane, kitendo ambacho wamiliki wa punda huyo walijua kuwa ni mwizi ila walikuja kustuka baada ya kumlika tochi na kumkuta akiwa utupu.

Wamiliki hao wa punda walimkamata na kumpeleka polisi na ndipo mtuhumiwa alikutwa na makosa ya unyanyasaji wa wanyama.

Mtuhumiwa akiwa Mahakamani alikiri kosa hilo la kufanya mapenzi na punda huyo huku akieleza kuwa alitekeleza sharti alilopewa na mganga wa kienyeji.

Ntando amesema alienda kwa Mganga wa Kienyeji kusaka dawa ya kuongeza nguvu za kiume na ukakamavu, ndipo aliposhauriwa kutembea na Punda.

Tayari mahakama ya mwanzo wilayani Mount Fletcher, Cape Town imetoa hukumu jana kwa kumfunga mwaka mmoja jela kwa kosa la unyanyasaji wa wanyama.




Tupe Maoni Yako

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Pendeza na Dar Empire Products: Badili Muonekano Wako na Kuweka Mwili Wako Sawa Bila Madhara yoyote.

PENDEZA NA DAR EMPIRE PRODUCTS: BADILI MUONEKANO WAKO NA KUWEKA MWILI WAKO SAWA KWA PRODUCT ZISIZO NA MADHARA YEYOTE WALA KEMIKALI, MATOKEO NI KWAARAKA.


  1)ONDOA NYAMA UZEMBE MIKONONI, KIUNONI KUPAK
2)TOA  KITAMBI KABISA
 3) PUNGUZA MWILI MZIMA KUANZIA KILO UNAZOITAJI WEWE
4) ONDOA MICHIRIZI ILIYO SHINDIKANA
 5) TOA MAKOVU, CHUNUSI, WEUSI KWENY MAPAJA KIKWAPAN
 6) KUWA MWEUPE WAKUPENDEZA
7) ONGEZA NGUVU ZA KIUME
  8) RUDISHA HAMU YA TENDO NA KUCHELEWA KUFIKA KILELE
9)ONDOA MAFUTA USONI
 10) ONDOA MIKUNJO USON

 TUNAPATIKAN DAR ES SALAAM:  PIGA CM

+255658 440 707

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Soma Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo.

Job Opportunity at Info-Consultancy Ltd, Sales Representative

Job Opportunity at Bluebay Hotels, General Manager

Job Opportunity at World Vision, ICT-Officer

Job Opportunity at Mamujee Products Ltd, Quality Inspector

Job Opportunity at ESAMI, Maintanance Officer

Job Opportunity at Mobisol, Head of Human Resources



Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

TID Atangaza Nia ya Kugombea Ubunge wa Kinondoni 2020 Je Atamng'oa Mtuli?

Msanii wa muziki wa kizazi kipya Khalid Mohamed maarufu kama T.I.D, ametangaza nia ya kugombea ubunge jimbo la Kinondoni, kwenye uchaguzi ujao unaotarajiwa kufanyika mwaka 2020, na kumng'oa mbunge wa sasa wa jimbo hilo Maulid Mtulia.

Akizungumza kwenye kipindi cha East Africa Breakfast kinachorushwa na East Africa Radio, TID amesema sababu inayomsukuma kugombea nafasi hiyo ni kutokana na mbunge wa sasa kushindwa kulitimizia mahitaji yake jimbo hilo, hivyo atatumia nafasi hiyo kuhakikisha anamng'oa ifikapo 2020, kwa kuwa yeye anafahamu vizuri matatizo ya Kinondoni kutokana na kuwa mzawa wa mahali hapo.

Akiendelea kuzungumzia suala hilo, TID amesema iwapo atapewa dhamana ya kuliongoza jimbo hilo, atahakikisha anatatua matatizo yote yanayowakabili watu wa Kinondoni, likiwemo janga la madawa ya kulevya.


Tupe Maoni Yako

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

TFF Yaanika Viingilio Mechi ya Tanzania Dhidi ya NIigeria.

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limeweka wazi viingilio vya mchezo wa marejeano kuwania kufuzu fainali za Kombe la Dunia dhidi ya Nigeria itakayopigwa, Jumapili Oktoba mosi, mwaka huu.

Mashabiki wataingia kwenye uwanja wa Azam Complex kwa viingilio vya kawaida kushuhudia mechi hiyo timu ya taifa ya wanawake wenye umri wa chini ya miaka 20 ‘Tanzanite’ itakayocheza dhidi ya Falconets ya Nigeria.

Viingilio vitakuwa ni Sh. 500 tu kwa mashabiki watakaoketi eneo la mzunguko huku kwa wale watakaokaa jukwaa kuu (VIP) watalipia Sh. 1,000 tu katika mchezo utakaofanyika Uwanja wa Azam, Chamazi ulioko nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.

Kocha wa Tanzanite, Sebastian Nkoma, amesema kwa namna alivyokiandaa kikosi chake ana imani kitaweza kupindua matokeo ya awali ambayo Tanzanite ililala mabao 3-0 katika mchezo uliofanyika Uwanja wa Samuel Ogbemudian, ulioko Jimbo la Benin nchini Nigeria, wiki mbili zilizopita.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Thursday 28 September 2017

Mwakyembe Akabidhiwa Ripoti ya Maandalizi ya Mashindano ya Afcon Mwaka 2019.

Kuelekea katika mashindano ya Afcon U-17 mwaka 2019 ambapo Tanzania ndiyo wenyeji, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na michezo Dkt. Harrison Mwakyembe amesema atahakikisha mashindano hayo yanaenda vizuri bila ya kuwa na tatizo lolote.

Dkt. Mwakyembe amesema hayo katika kikao cha ufunguzi wa mashindano hayo yaliyofanyika leo Jijini Dar es Salaam na kuahidi kufuatilia kwa ukaribu ukarabati wa viwanja pamoja na timu ili kujihakikishia kuwa hakuna tatizo kwa upande wa maandalizi.

"Uenyeji wa mashindano haya hatuja yapokea kwa gafla hivyo tutahakikisha tunafanya maandalizi mazuri kwa timu yetu na miundombinu ili kuhakikisha nchi yetu ya Tanzania inafanya vizuri katika mashindano hayo", amesema Dkt. Mwakyembe.

Naye Makamu wa Rais wa Kamati ya ufundi ya maendeleo ya shirikisho la soka Barani Afrika (CAF) ambaye pia ni mwakilishi wa ukanda wa Afrika Mashariki, Leodgar Chilla Tenga amesema anaendelea kuhamasisha zaidi ili kuhakikisha heshima ya Tanzania katika maandalizi inafanikiwa kwa kiwango kikubwa.

"Heshima ya nchi katika soka ni uwezo wa kuandaa mashindano pamoja na kuyafanikisha kwa kiasi kikubwa. CAF wanamatumaini makubwa na Tanzania juu ya uenyeji wa mashindano haya japo kuna mahitaji mengi lakini yanawezekana kufanikishwa", amesema Tenga.

Kwa upande wake,  Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Wallace Karia amesema licha ya maandalizi ya miundombinu lakini watahakikisha wanaiandaa timu vizuri kwani mashindano hayo ni sehemu ya kufuzu kushiriki mashindano ya kombe la dunia la vijana.



TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Team Wema Wamfanyia Wema 'Suprise' Kubwa Kwenye Siku Yake ya Kuzaliwa.

Ikiwa leo Septemba 28, 2017, mwigizaji mahiri Bongo, Wema Isaac Sepetu almaarufu Keki ya Taifa, anasheherekea birthday yake, mashabiki wake wameungana kwa pamoja na kumfanyia surprise akiwa saluni kwa kumpelekea keki na shampeni wakiwa na matarumbeta.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Download wimbo mpya wa Chemical Ft Fid Q & Cliff Mitindo unaoitwa "HERO".

https://my.notjustok.com/track/download/id/274998



Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Muziki wa Ali Kiba ni Mzuri Zaidi ya wa Diamond- Faiza.

Muigizaji wa Filamu Bongo, Faiza Ally amefunguka kuupa zaidi muziki wa Alikiba kuliko ule wa Diamond.
Faiza amesema hayo katika mahojihano na TBC Fm kwa kueleza kuwa Diamond ni mburudishaji wa jumla aliyeleta mapinduzi ya kimuziki lakini Alikiba muziki wake ni bora zaidi.

“Kwanza kati ya muziki wa Diamond na Alikiba, naupenda sana muziki wa Kiba, muziki wake ni mzuri kuliko wa Diamond,” amesema Faiza na kuendelea.

“Diamond ni ile full Entertainment ukimwalia tu unatabasamu lakini Kiba ana muziki mzuri. Nikizungumzia mtu aliyeutoa muziki akaupa heshima mpaka akampa changamoto Kiba na yeye akasimama mpaka tukaanza kumuona kwenye hali ya tofauti ni Diamond,” amesema.

Ikumbukwe kuwa September 3 mwaka huu Faiza aliandika ujumbe katika mtandao wa Instagram na kueleza  kuwa kumpenda Diamond ni jambo la lazima na sio ombi kutokana na mengi mazuri aliyofayanya katika muziki wa Bongo Flava.

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Download wimbo mpya wa Dullayo Ft. Beka Flavour unaoitwa "Caro".

https://my.notjustok.com/track/download/id/274999


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Download wimbo mpya wa Amber LULU Ft. Ice Boy unaoitwa "KUMOYO".

https://my.notjustok.com/track/download/id/275000


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Omog Ndiye Aliyeishikisha Adabu Yanga, Bado Anahitajika Simba Kuliko Yeye KulikoHata Anavyoihitaji Yeye- Manara.

Haji Manara amefunguka na kusema Kocha Mkuu wa Simba, Joseph Omog anahitajika zaidi na Simba kuliko hata yeye anavyohitaji Simba na kudai ni kocha pekee aliyeweza kuipa Simba vikombe viwili na kuifunga Yanga mara tatu katika mechi nne walizokutana.

Manara amesema hayo jana wakati akielezea mambo mbalimbali kuelekea mchezo wao na Stand United ambao unatarajiwa kupigwa katika uwanja wa Kambarage Shinyanga ambapo amedai wanaiheshimu timu hiyo lakini wao wanakwenda kwa lengo la kutafuta pointi tatu.

"Makocha watano wamekaa hapa Simba wameshindwa kutupa nafasi ya pili, wameshindwa kutupa kikombe lakini Omog katupa vikombe viwili na vyote kamnyang'anya Yanga kakutana na Yanga mara nne kampiga mara tatu, halafu kuna mtu mtaani anasema Omog hafai, Simba sasa hivi inamuhitaji zaidi Omoh kuliko Omog anavyoihitaji Simba kwa sasa" alisema Haji Manara

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Msigwa Afikishwa Mahakamani kwa Tuhuma za Kutishia Kuua.

Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa amepandishwa kizimbani leo Alhamisi katika Mahakama ya Mwanzo Mjini Iringa kwa madai ya kumtusi na kutishia kumuua aliyekuwa Diwani wa Kata ya Kitwiru, Baraka Kimata.

Mbali na Msigwa pia Diwani wa Viti Maalum, Selestina Johanes na dereva wa mbunge huyo, Godi Mwaluka wamepandishwa kizimbani kwa kosa hilo.

Akisoma shtaka hilo Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo, Rehema Mayagilo amesema kuwa mbunge huyo na washtakiwa hao wawili wanashtakiwa kwa madai ya kumtusi na kutishia kumuua diwani huyo.

Hakimu Mayagilo amesema kuwa Msigwa na wenzake walitenda kosa hilo jana saa nane mchana katika viunga vya Ofisi za Halimashauri ya Manispaa ya Iringa.

Baada ya kusomewa shtaka hilo Msigwa na wenzake wamepata dhamana na kesi hiyo imeahirishwa hadi Oktober 9 mwaka huu itakapotajwa tena.

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Download wimbo mpya wa Nikki Wa II unaoitwa "Kihasara".


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Chadema Wapingana na Mwigulu Yasimamia Msimamo Wake wa Uchunguzi Kutoka Nje Shambulio la Lissu.

Chadema imesema haitabadili msimamo wake wa kutaka wataalamu kutoka nje kuchunguza shambulio dhidi ya mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu.

Juzi, Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba alisema hakuna haja ya kuhangaika kutafuta wachunguzi kutoka nje kwa kuwa mazingira watakayofanyia kazi ni yaleyale na hivyo kuitaka Chadema kuviamini vyombo vya ndani vya uchunguzi.

Lakini jana, Chadema imeeleza kuwa haioni kinachoendelea na hata kama ni mazingira yaleyale, wachunguzi kutoka nje ndiyo muafaka.

Lissu, mmoja wa wabunge wa upinzani asiye na woga wa kusema anachokiamini, alishambuliwa kwa risasi mchana wa Septemba 7 akiwa katika gari nje ya makazi yake mjini Dodoma akitokea bungeni.

Pamoja na washambuliaji kufyatua risasi zipatazo 32, Lissu alinusurika kifo na kupelekwa Hospitali ya Mkoa wa Dodoma na baadaye alipelekwa Nairobi, Kenya kwa matibabu zaidi, safari ambayo iligubikwa na mabishano baina ya Chadema, uongozi wa Bunge na Serikali, iliyotaka ahamishiwe Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH).

Chadema imekuwa ikihusisha shambulio hilo na tofauti za kisiasa na hivi karibuni ilisema pamoja na kuwa na imani na vyombo vya usalama, inataka wachunguzi kutoka nje kwa kuwa vyombo vya dola vimetuhumiwa.

Mkurugenzi wa itikadi na mambo ya nje wa Chadema, John Mrema aliiambia Mwananchi jana kuwa ikiwa Serikali haina hofu, iruhusu wachunguzi hao ili yapatikane majibu ya nani alihusika.

Mrema alisema hakuna haja ya kuzuia wachunguzi hao kwa kuwa wana uwezo wa ziada.

“Kwa nini Serikali haitaki wachunguzi huru? Ni kweli kwamba wakija watafanya kazi kwa mujibu wa sheria za nchi, lakini hii haibadili msimamo wetu, hawa wana vifaa na wanaweza kusaidia kupata majibu,” alisema Mrema.

Alisema tangu kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Dodoma, Gilles Muroto alipotoa taarifa za awali za tukio hilo, hakuna taarifa nyingine zozote zilizopatikana, jambo ambalo alisema linaendelea kuwatia hofu.

Mrema alisema yapo mauaji mengi kama ya Kibiti ambayo wananchi hawajui matokeo ya uchunguzi wala hakuna waliofikishwa mahakamani.

Kiongozi huyo wa Chadema alisema hata suala la mauaji ya Kibiti halijatolewa taarifa wala watuhumiwa kufikishwa mahakamani, huku kada wa chama hicho, Ben Saanane akiwa hajulikani alipo na mauaji ya mwenyekiti wa Chadema mkoani Geita, Alphonce Mawazo yakiwa hayajatolewa ripoti.

Alisema wataalamu hao kutoka nje wapo tayari kuja kufanya kazi ya kuchunguza tukio hilo na kwamba kitendo cha kuwakataa kinaongeza shaka kwao.

“Tunakaribia mwezi hatujui chochote,” alisema Mrema.

“Kwa hiyo muafaka ni wachunguzi huru. Mtu hawezi kupigwa risasi mchana kweupe tena Dodoma Mjini...” alisema.

Mbunge wa Iringa Mjini, Peter Msigwa alisema kuzuia wachunguzi hao kunawafanya wafikirie kuwa kuna watu ambao hawataki kuumbuka na kuongeza kuwa kama nia ipo, iwaruhusu.

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Uganda Yafuata Nyayo za Tanzania Yapiga Stop Bunge Kuonyeshwa Live.

Vyombo vya habari nchini Uganda vimezuiwa kuonyesha moja kwa moja matangazo ya Bunge ambalo linaendelea na vikao.

Mkurugenzi wa Tume ya Utangazaji nchini humo, Godfrey Mutabuzi amesema redio na runinga zote haziruhusiwi kurusha matangazo ya Bunge moja kwa moja kuanzia leo Alhamisi.

Amesema sababu ya Bunge kutoonyeshwa moja kwa moja ni za kiusalama.

Wabunge nchini Uganda walipigana jana Jumatano ndani ya ukumbi wa Bunge wakiwa katika siku ya pili ya kikao cha kujadili muswada wa kuondoa ukomo wa miaka ya kugombea nafasi ya Urais kwa mujibu wa Katiba ya Taifa hilo.

Katika ugomvi huo, wabunge walirushiana viti na kuharibu vipaza sauti. Kikao hicho kiliongozwa na Spika wa Bunge, Rebecca Kadaga.

Ugomvi huo ulianza pale Spika alipochukua hatua ya kuwafukuza wabunge wapatao 25, wengi wao wakiwa ni wa upinzani kwa madai ya utovu wa nidhamu.

Mwingine aliyetolewa ndani ya ukumbi ni waziri wa Serikali aliyeshtakiwa kwa kufyatua risasi bungeni Jumanne.

Wabunge wanadai kama kikomo cha umri wa miaka 75 kitaondolewa, basi Rais aliye madarakani sasa atapata mwanya wa kugombea tena mwaka 2021.

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Soma Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Siku ya Leo.

Job Opportunity at Mobisol, Head of Human Resources

Job at Shinyanga Urban Water Supply and Sanitation Authority (SHUWASA)

Job Opportunity at Save The Children Tanzania

Job Opportunity at VSO, Programme Manager Youth

Job Opportunity at KP Recruiters, Sales Coordinator

Job Opportunity at KP Recruiters, Sales Manager

Nafasi zingine ingia www.ajirayako.co.tz

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Pendeza na Dar Empire Products: Badili Muonekano Wako na Kuweka Mwili Wako Sawa Bila Madhara yoyote.

PENDEZA NA DAR EMPIRE PRODUCTS: BADILI MUONEKANO WAKO NA KUWEKA MWILI WAKO SAWA KWA PRODUCT ZISIZO NA MADHARA YEYOTE WALA KEMIKALI, MATOKEO NI KWAARAKA.


  1)ONDOA NYAMA UZEMBE MIKONONI, KIUNONI KUPAK
2)TOA  KITAMBI KABISA
 3) PUNGUZA MWILI MZIMA KUANZIA KILO UNAZOITAJI WEWE
4) ONDOA MICHIRIZI ILIYO SHINDIKANA
 5) TOA MAKOVU, CHUNUSI, WEUSI KWENY MAPAJA KIKWAPAN
 6) KUWA MWEUPE WAKUPENDEZA
7) ONGEZA NGUVU ZA KIUME
  8) RUDISHA HAMU YA TENDO NA KUCHELEWA KUFIKA KILELE
9)ONDOA MAFUTA USONI
 10) ONDOA MIKUNJO USON

 TUNAPATIKAN DAR ES SALAAM:  PIGA CM

+255658 440 707
"Dar Empire" inakukaribisha kwa wale wenye mchunusi usoni na kuona tatizo kwako "Dar Empire" Suluhisho linafanya uso kuwa safi na kuondoa chunusi.
Kwa mawasiliano zaidi call:+255658440707.




"Dar Empire" Inawapa habari mpya ya kutoa "MICHILIZI" inayokusumbua wai sasa upate tiba.
Kwa mawasiliano zaidi call:+255659994437.

"Dar Empire" inawakaribisha kwa wale wote ambao wanataka kupunguza kitambi na uzito wai sasa hii nafasi ni yako.
Kwa mawasiliano zaidi call:+255658440707


"Dar Empire" inawakaribisha kwa wale wote ambao wanataka kupunguza kitambi na uzito wai sasa hii nafasi ni yako.
Kwa mawasiliano zaidi call:+255658440707
 "Dar Empire" Inatoa uduma ya kutoa sumu mwilini kwa hasa wale wagonjwa wenye uitaji 
 Kwa mawasiliano zaidi call:+255658440707.
"Dar Empire" kutoa vipodozi na Inakuletea Dawa za meno kung'alisha kutoa gesi.
Kwa mawasiliano zaidi call:+255658440707.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa