Wednesday 28 February 2018

YANGA YAANDIKA HISTORIA MTWARA, YAICHARAZA NDANDA MABAO 2-1.

Young Africans imeandika historia ya kwanza katika Uwanja wa Nangwanda Sijaona baada ya kuifunga Ndanda FC kwa mabao 2-1, mchezo wa Ligi Kuu Bara.

Walikuwa Yanga walioanza kucheka na nyavu za Ndanda mapema kabisa kwenye dakika ya 6 ya mchezo, baada ya Pius Buswita kutumia vema madhaifu ya mabeki wa Ndanda kwa kfunga bao la kwanza.

Na katika dakika ya 29, Hassan Kessy, alifunga bao la pili kwa mguu wa kushoto katika eneo la hatari la wapinzani wao, na kuufanya mchezo uende mapumziko kwa mabao 2-0.

Kipindi cha pili, Ndanda walikuja na uhai wakipambana kupata mabao ya kusawazisha japo ammbo hayakuwa rahisi, lakini jitihada zao ziliwasaidia kupata bao la kufutia machozi katika dakika ya 83 kupitia kwa Nassor Kapama.

Mpaka dakika 90 zinamalizika, Ndanda FC 1-2 Young Africans.

Matokeo haya sasa yanaifanya Yanga kuwa na alama 40, nyuma ya Simba iliyo na 45.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Mwimbaji Misri Afungwa kwa Kuikashifu Mto Nile.

Mwimbaji wa Misri Sherine Abdel Wahab amehukumiwa miezi sita gerezani kwa kutania juu ya hali ya usafi wa mto Nile.

Sherine, ni mmoja wa waimbaji maarufu nchini humo pia ni jaji katika kipindi cha mashindano ya waimbaji, The Voice- alimwambia mashabiki wake kuwa kunywa maji kutoka mto huo kunaweza kumpatia vijidudu.

"Kunywa Evian badala yake." akatania
Mwimbaji mwingine, Laila Amer, pia alihukumiwa siku ya Jummane kifungo cha miaka miwili kutokana na video ya muziki.

Bi Amer - ambaye hana umaarufu kama Sherine - alipatwa na hatia ya 'kuchochea ufitini na uovu". Muongozaji wa kipindi na muigizaji walihukumiwa kwa vipindi vifupi.

Sherine, amehukumiwa na mahakama moja Cairo kwa kusambaza habari zisizo za kweli. Chombo cha habari Misri, Ahram kimesema aliagizwa kulipa paundi 5,000 za Misri.

Mzaha
Mashtaka dhidi ya Sherine yalifunguliwa mwezi Novemba, baada ya kuonekana video mtandaoni ikimuonesha akiombwa kuimba wimbo uitwao Mashrebtesh Men Nilha (umewahi kunywa maji ya mto Nile?).akajibu ''Nikinywa maji ya mto Nile nitapata kichocho''. Kichocho ni ugonjwa unaojitokeza maeneo ya vijijini nchini Misri.

Mbali na kesi dhidi yake, Chama cha wanamuziki nchini humo kimetangaza kuwa kimempiga maruguku kuuimba wimbo huo kuhusu Misri.

Abdel Wahab baadae aliomba radhi kutokana na tukio hilo akiwa kwenye tamasha lililofanyika huko Jumuia ya falme za kiarabu zaidi ya mwaka mmoja uliopita.

Another singer, Shyma alihukumiwa kwa kucheza video ya maadili mabovu


Maamuzi ya mahakama yaliyotolewa siku ya Jumanne inafanya idadi ya wanamuziki kuhukumiwa kifungo kufikia watatu miezi ya hivi karibuni

Mwezi Desemba, Shaimaa Ahmed ajulikanaye kifupi Shyma alihukumiwa kifungo cha miaka miwili baada ya kuonekana kwenye Video ya muziki akiwa amevalia nguo za ndani huku akila ndizi kwa mbwembwe.

alikutwa na hatia ya kuweka video yenye maadili mabaya akahukumiwa sambamba na muongozaji wa video hiyo.Baadae hukumu ilipunguzwa na kuwa ya mwaka mmoja baada ya kukata rufaa.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

EXCLUSIVE:Video ambayo inayoonyesha Hoteli aliyojenga Mr. II SUGU Mbeya.




Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

CCM na Polisi Wapangua Tuhuma za Freeman Mbowe.

Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe ameibua tuhuma mpya dhidi ya baadhi ya idara za Serikali ikiwamo polisi akidai kuna mkakati wa kuwafungulia kesi ya uhaini, mauaji na ugaidi viongozi wa chama chake.

Pia, ameinyooshea kidole CCM akidai kwamba inatafuta umaarufu kwa nguvu kwa kununua madiwani.

Hata hivyo, polisi na CCM wamekana tuhuma hizo na kumtaka Mbowe aache siasa za malumbano.

Mbowe alitoa kauli hiyo jana katika mkutano na waandishi wa habari, muda mfupi kabla ya kuwaongoza viongozi wa chama hicho kuripoti Kituo Kikuu cha Polisi jijini Dar es Salaam kuhojiwa kwa madai ya kufanya maandamano kinyume cha sheria na kuachiwa kwa dhamana.

Wakati Mbowe akieleza hayo, Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa alisema tuhuma dhidi ya polisi si za kweli na ndio maana viongozi hao walifika kituoni hapo kwa ajili ya kuhojiwa.

“Tutaendelea kuwahoji hawa viongozi kwa kufanya maandamano bila ya kuwa na kibali jambo ambalo ni kosa,” alisema Mambosasa.

Mbali ya Mambosasa, katibu wa itikadi na uenezi wa CCM, Humphrey Polepole pia alimjibu akisema, “Mbowe na viongozi wenzake wa upinzani wafanye siasa safi na watoe uongozi bora. Waache siasa za matukio na uchochezi kwa sababu hazibadilishi maisha ya watu. CCM tumeamua, hasa Awamu ya Tano kushughulika na shida za watu na kuwaletea maendeleo.”

Alichokisema Mbowe

Mbowe alidai kwamba mkakati wa kuwafungulia kesi hizo unatokana na matukio mbalimbali yaliyotokea ya mauaji na utekaji huku akidai vyombo vya dola vinashindwa kutimiza wajibu wake hivyo kujenga chuki miongoni mwa jamii.

Alisema kuna matukio yaliyojitokeza katika uchaguzi mdogo wa ubunge wa Kinondoni uliofanyika Februari 17 yalisababisha kifo cha mwanafunzi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), Akwilina Akwilini (22) na wanachama watano wa Chadema kupigwa risasi za moto.

Akwilina aliuawa kwa kupigwa risasi na polisi Februari 16 akiwa ndani ya daladala eneo la Mkwajuni, Kinondoni wakati polisi wakiwazuia wafuasi na viongozi wa Chadema waliokuwa wakiambatana kwenda ofisi ya msimamizi wa uchaguzi wa Kinondoni kushinikiza kupewa viapo vya mawakala wao.

Siku nne baadaye, Mambosasa aliwataka viongozi saba wa Chadema kufika polisi kwa mahojiano.

Mbowe alisema, “Wanatafuta namna ya kutubambika kesi za kigaidi, mauaji au za kihaini... ni mkakati wa kweli na tunamweleza Rais, hatutarudi nyuma katika kutetea demokrasia ya kweli. Mpaka sasa wanachama wetu watano kati yao wawili ni wanawake waliopigwa risasi za moto hawataki kuwapatia dhamana, wanajua wakitoka wataongea yaliyowasibu ndio maana hawataki kuwaachia wala kuwapeleka mahakamani.”

Mbowe aliendelea kutuhumu, “Risasi hizo zilielekezwa kwetu, sitaki kusema mimi ila hii si Tanzania tunayoitambua... Tumeanza kuzoea kuuana, kuumizana na wanasababisha machafuko na haya ni maonevu na haya mambo hayakuwapo zamani, tujiulize kwa nini yanatokea sasa?

“Hizi chaguzi zitaendelea kuzaa majeraha na maumivu kwani wanaosababisha wanalindwa na viongozi wa juu. Haiwezekani mawakala wetu hadi siku ya mwisho walikuwa hawajapata hati ili waibe kura na ndicho walichokifanya.”

Kuhusu madai ya kuwapo kwa mkakati wa kuifuta Chadema, Mbowe alisema unaweza kufanikiwa lakini athari zake zitakuwa ni kubwa kwa Taifa, “Wataiua Chadema lakini si mioyo ya watu, utaiua CUF na vyama vingine si hisia za watu na unapoziua taasisi kama hizi zinazowasemea watu wanatengeneza magenge huko na wataunda vikundi vya kigaidi ambavyo ni hatari zaidi.

“Chama hiki si cha kigaidi ni chama cha mikusanyiko ya watu wengi na CCM kama wanataka kurudisha imani kwa wananchi wasifanye hivyo kwa kununua madiwani, wafanye mambo yanayoeleweka na watakubalika.”

Alikuwa akizungumzia barua ya Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi aliyoiandikia Chadema akitaka ijieleze kutokana na madai ya uvunjifu wa Sheria ya Vyama vya Siasa na ile ya maadili kwa kufanya maandamano Februari 16.

Barua hiyo ya Februari 21, iliyokuwa ikitakiwa kujibiwa kabla ya Februari 25, Jaji Mutungi katika sehemu ya barua hiyo alisema licha ya tuhuma hizo kuwa zinafanyiwa kazi na taasisi zingine za Serikali, hata ofisi yake kwa namna moja au nyingine anaweza kulishughulikia.

“Hivyo, kwa barua hii, nakitaka chama chenu kuwasilisha maelezo ya kwa nini kisichukuliwe hatua za kisheria, kwa kukiuka Sheria ya Vyama vya Siasa na Kanuni za Maadili ya Vyama vya Siasa, kwa kuchochea wananchi kuandamana bila kufuata utaratibu wa sheria na kufanya vurugu,” ilieleza sehemu ya barua hiyo ambayo tayari Chadema ilishasema kuwa imeijibu.

Hukumu ya Sugu

Mbowe alizungumzia hukumu ya mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema) Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ na Katibu wa Chadema Kanda ya Nyasa, Emmanuel Masonga iliyotolewa juzi ya kuhukumiwa miezi mitano jela akidai ni mkakati ovu uliopagwa.

“Tunaheshimu sana Mahakama na Mahakama inapaswa kuheshimiwa lakini mawakili mmojammoja wanapofanya makosa wanaichafua Mahakama. Jaji Mkuu (Profesa Ibrahim Juma) alisema wanasiasa tusiingilie Mahakama, hatutaisema vibaya au kuihukumu hapana, tunawahukumu watendaji wa mahakama,” alisema Mbowe.

“Hukumu hii tuliijua siku nne kabla na mtakumbuka hakimu (Michael Mteite) tulimkataa toka mwanzo na sisi kama Chadema hatutaki kusema hatuna imani na Mahakama, lakini Jaji Mkuu kama alivyosema tusiingilie Mahakama na Jaji Mkuu anapaswa kujua hili na kama anataka kuanza, basi aanze na kesi hii ya Mbeya.”

Mbowe alisema amekuwa akiombwa na wanachama na wananchi kutoa kauli ya kulipiza kisasi kwa yanayowakuta lakini alisisitiza kwamba hatafanya hivyo akisema kutofautiana kiitikadi si kigezo cha kusababisha uvunjifu wa amani.

“Tupambane na watawala waovu na si wananchi kwa wananchi na wanaostahili kulaumiwa ni Serikali. Wanachama wa Chadema waendelee kuwa makini, tuchukue kila tahadhari kwani vyombo vinavyopaswa kutupa ulinzi havifanyi hivyo,” alisema Mbowe.

Majibu ya Mambosasa

Hata hivyo, Kamanda Mambosasa alisema tuhuma za Chadema dhidi ya jeshi hilo hazina mashiko huku akisisitiza kuwa polisi wanafanya kazi yao kwa weledi na ndiyo maana viongozi hao walikuwa wakihojiwa kituoni hapo.

“Muwaulize hao Chadema kwa nini tuhuma wazielekeze jeshi la polisi? Wao wenyewe wanajua ndiyo maana leo (jana) hii tunaendelea kuwahoji kwa kufanya maandamano bila ya kuwa na kibali jambo ambalo ni kosa,” alisema Mambosasa.

Polepole amjibu Mbowe

Polepole alipotafutwa kutoa maoni yake juu ya kauli hizo za Mbowe alisema, “Hatuna muda wa kulumbana siasa za madaraka. Mbowe asitafute mchawi nje ya chama chake na yeye mwenyewe. Anayetuharibia wigo wa demokrasia sasa hivi ni mtu ambaye anazungumza masuala ya kuhamasisha na kuleta taharuki. Anazungumzia kubeba majeneza ya Watanzania, mbona hajazungumza kubeba majeneza ya watoto wake. Mbona hasemi watoto wake wako wapi? Anapiga mawe polisi na kuandamanisha watu lakini watoto wake wako salama.”

Alisema siasa za namna hiyo hazileti maendeleo katika Taifa na kwamba CCM sasa inafuatilia kazi ambayo iliwaahidi Watanzania katika Uchaguzi Mkuu wa 2015.

Polepole pia alizungumzia madai ya Mbowe kuhusu hukumu ya Sugu na kusema, “Mtu kigeugeu ni mbaya sana. Mahakama ikiamua yeye mbunge wake halali, mahakama nzuri. Mahakama ikimhukumu mbunge wake Sugu na wengine wanaotoa lugha ya uchochezi na uongo na wanashindwa kuthibitisha, mahakama mbaya. Huo si ustaarabu wa uongozi ni ukigeugeu wa kisiasa.”

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Tuesday 27 February 2018

Ngorongoro heroes kucheza na Dr congo fainali za africa.

Timu ya Taifa ya Vijana chini ya miaka 20(Ngorongoro Heroes) imepangwa kucheza na DR Congo kwenye mchezo wa kutafuta tiketi ya kucheza fainali za Vijana za Africa zitakazochezwa Niger mwezi Novemba.

Mchezo wa kwanza utachezwa Tanzania kati ya Machi 30,31 na April 1,2018 na ule wa marudiano utachezwa Congo kati ya Machi 20,21 na 22.

Mshindi katika mchezo huo atacheza na Mali katika raundi ya pili itakayochezwa kati ya Mei 11,12 na 13,2018.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Mbowe,Viongozi wa Chadema waachiwa baada ya kuhojiwa kwa saa tano.

Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na viongozi wengine wac hama hicho wameachiwa kwa dhamana baada ya kuhojiwa Kituo Kikuu cha Polisi tangu saa 6:50 mchana

Viongozi hao walifika kituoni hapo leo Jumanne Februari 27, 2018 na kuachiwa saa 1:02 usiku, kuitikia wito wa polisi.

Walikwenda kituoni hapo baada ya Mbowe kumaliza mkutano wake na waandishi wa habari makao makuu ya chama hicho yaliyopo mtaa wa Ufipa, Kinondoni.

Mmoja wa mawakili wa viongozi hao, Frederick Kihwelo ameileza MCL Digital leo kuwa wote wameachiwa kwa dhamana kwa kutakiwa kuwa na mdhamini mmoja na kutakiwa kuripoti tena kituoni hapo Machi 5, 2018 saa 1 asubuhi.

Amesema viongozi hao walianza kuhojiwa saa 8:30 mchana, baada ya kufanya mazungumzo ya tuhuma zinazowakabili.

Februari 20, 2018 Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam iliagiza kukamatwa viongozi saba waandamizi wa Chadema akiwamo Mbowe.

Wito huo ulikuja siku chache baada ya tukio la kuuawa kwa mwanafunzi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), Akwilina Akwilini.

Akwilina aliuawa kwa kupigwa risasi akiwa ndani ya daladala eneo la Mkwajuni, Kinondoni jijini Dar es Salaam wakati polisi wakiwatawanya wafuasi wa Chadema waliokuwa wakienda ofisi za mkurugenzi wa Halmashauri ya Kinondoni kudai viapo kwa mawakala wao.

Viongozi wengine waliohojiwa sambamba na Mbowe ni  naibu makatibu wakuu, John Mnyika (Bara) na Salum Mwalimu (Zanzibar).

Pia, wamo mwenyekiti wa Baraza la Wanawake Chadema (Bawacha), Halima Mdee; mwenyekiti wa Kanda ya Serengeti, John Heche na Esther Matiko ambaye ni mweka hazina wa Bawacha.

Mdee, Matiko, Heche na Mnyika walisharipoti awali na walitakiwa kurejea kituoni leo. Viongozi wengine waliwakilishwa na wanasheria.

Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk Vicent Mashinji  hakwenda polisi kwa kuwa yupo nje ya nchi.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Hizi Hapa Sababu Kuu za Wanaume Kupenda Wake za Watu.

ASSALAM aleikum mpenzi msomaji wangu, umzima? Unaendeleaje na mishughuliko yako? Mimi mzima, namshukuru Mungu kwa kunijaalia kuwa miongoni mwa wale wanaopendwa. Yes, mimi napendwa na hiyo ni bahati sana.

Wapo watu wanatafuta watu wa kuwapenda lakini mpaka sasa hawajawapata. Ndiyo maana nilishawahi kusema kwamba, ukibahatika kumpata mtu anayekupenda na kwa bahati nzuri na wewe ukawa na chembechembe za mapenzi kwake, shukuru Mungu na mshikilie.

Kumbuka mapenzi ndiyo yanachukua nafasi kubwa kwenye maisha yetu. Hata kama umzuri, una pesa nyingi na mali za kumwaga kiasi gani, kama huna mtu wa ‘kuinjoi’ naye, maisha yako lazima yatakuwa ni yenye upungufu mkubwa.

Ndiyo maana wapo ambao ni matajiri lakini kwa kuwa mapenzi yanawachanganya, wanafikia hatua ya kujiua. Hapo ndipo unathibitisha kwamba, mapenzi yanachukua asilimia kubwa katika maisha yetu ya furaha ya kila siku.

Mpenzi msomaji wangu, wiki hii nataka kuzungumzia sababu tano za kwa nini baadhi ya wanaume wanapenda sana kuwa na uhusiano na wapenzi wa watu.

Nimefikia hatua ya kuandika makala haya kwa kuwa, kila siku tunasikia fulani kafumaniwa na mke wa mtu au fulani anatembea na mpenzi wa mtu. Pia wapo wanawake ambao wameingia kwenye ndoa lakini bado wanasumbuliwa sana na wanaume.

Mbaya zaidi wanaume hao wanaelezwa kabisa kuwa, wameingia sehemu ambayo tayari mwingine kashajiweka lakini hawakubali, wanang’ang’ania.

 Achilia wapenzi tu, wapo pia wake za watu ambao wanatokewa na wanaume. Yaani mwanaume anajua kabisa huyu ni mke wa mtu na anampenda sana mumewe lakini jamaa linang’ang’ania lipewe nafasi kwa kuwa lishapenda.

Katika hili naomba niseme kwamba, si kila anayemtongoza mke wa mtu au mpenzi wa mtu ni kiwembe. Wapo ambao wana mapenzi ya kweli na wameshindwa kujizuia. Mwanamke anaweza kuwa ndani ya ndoa lakini akawa ameolewa na mwanaume ambaye siye aliyepangiwa na Mungu.

Katika mazingira hayo ndiyo unamkuta mtu anakomaa na mke wa mtu, kila siku anaimbisha akiomba apewe nafasi. Akiambiwa, ‘si unajua mimi mke wa mtu’ anasema, ‘sasa mimi nifanyeje wakati nahisi wewe ndiye mke wangu niliyepangiwa na Mungu?’

 Kwa bahati mbaya zaidi unaweza kukuta na mwanamke naye licha ya kwamba ameolewa lakini naye anajihisi kumpenda mwanaume huyo na wakati huohuo hapati kile ambacho alikitarajia kwenye ndoa yake. Hapo ndipo unamkuta mwanamke anakuwa njia panda.

Anyway, hiyo ni mitihani katika maisha, sasa nirudi kwenye zile sababu za baadhi ya wanaume kuwatokea wake/wapenzi wa watu.

 PENZI LA DHATI

Kama nilivyosema, baadhi ya wanaume si kwamba wanaonyesha kuwa wao hawajatulia kwa kuwatokea wake za watu. Baadhi yao penzi la dhati walilonalo dhidi ya wale ambao wameshaingia kwenye ndoa ndilo huwasukuma kufanya hivyo.

Wanachokifanya wao ni kueleza hisia zao bila kujali kuwa, mlengwa ana mtu au laa. Ndiyo maana mtu huyo anaweza kuwa anajua ukweli kwamba fulani ni mke wa mtu lakini kwa kuwa anaamini huyo ndiye wake, analazimika kujaribu zali.

Mimi niseme tu kwamba, kwenye hili siyo dhambi kueleza hisia zako lakini ndugu yangu kama unajua kabisa huyo uliyempenda yuko ndani ya ndoa yake au ana mpenzi wake, pambana na hisia zako. Jizuie kwani kumpa usumbufu mke wa mtu ni kujitafutia matatizo bure.

HAKUNA GHARAMA

Baadhi ya wanaume wanawatokea wake za watu kwa kuwa hawatapata usumbufu wa pesa za matumizi, vocha, mavazi na vitu vingine. Wao wanaamini watakuwa wanatoa penzi tu lakini mambo mengine mwenye mke atahudumia.

Lakini wengine wanataka kuanzisha uhusiano na wake za watu kimaslahi. Kwamba mwanaume anaweza kuona mwanamke flani ameolewa na mwanaume mwenye nazo lakini mke anaonekana kutopata penzi analolihitaji. Yeye anatupa ndoano, akiamini akimridhisha kimapenzi, atakuwa anahongwa yeye na maisha yake yatakuwa poa.

Hata kwenye hili nikupe tahadhari. Kama unatokea kumpenda mke wa mtu ili umchune au ili kukwepa kugharamia, tamaa yako hiyo itakuponza. Acha utegemezi, mwanaume aliyekamilika ni yule mwenye uwezo wa kumtunza mtu anayempenda, usikimbie majukumu na kutaka vya mteremko. Kumbuka wengi walioingia kwenye uhusiano na wake za watu kwa tamaa za pesa na mali, yamewakuta makubwa.

 USUMBUFU HAKUNA

Kuna wanaume ambao hawapendi kusumbuliwa kwa mambo ya wivuwivu na wapenzi wao, mara nyingi mwanaume anapoanzisha uhusiano na mtu ambaye ana mtu wake anahisi hatasumbuliwa.

Yale mambo ya; ‘uko wapi baby’, uko na nani, nataka tuonane leo’ yanakuwa si kwa kiwango kile ambacho kinakuwepo kwa mtu ambaye hana mtu.

 HAKUNA KUGANDANA

Wapo wanaume ambao wao wanataka kila mwanamke mzuri bila kujali ameolewa au yuko singo. Lakini pia wapo ambao hawataki kuingia kwenye uhusiano na mwanamke ambaye atagusia future. Kwa kifupi wanaume wa staili hii wanaamini wakiwa na wake za watu, hawawezi kugandwa wala kuulizwa juu ya ‘future’.

 SIFA TU

Kama ulikuwa hujui wapo wanaume ambao wakitembea na mke wa mtu wanaona sifa sana. Akimtongoza mke wa mtu, akakubaliwa, roho yake inakuwa fresh. Na wengine hawawezi kubaki na siri, kila atakayekutana naye atamwambia; ‘yule mbona nishampitia’.

Hiyo yote sifa. Mtu yuko tayari kutumia gharama yoyote ili mradi atembee na mke/ mpenzi wa mtu, aandike historia kwamba fulani licha ya kwamba ni mke wa mtu lakini ameshatembea naye.

Mpenzi msomaji wangu, leo niishie hapo lakini nilichotaka ni kueleza tu sababu za kwa nini baadhi ya wanaume wanakuwa wasumbufu kwa wake za watu bila kujali hatari iliyo mbele yao. Nasema hatari kwa sababu kumpenda mke wa mtu, ukawa unamsumbua kila wakati hatari yake ni pale taarifa zitakapomfikia mwenye mali. Yatakayokukuta hapo ni aidha kuuawa au kufanyiwa vitendo vya kudhalilishwa. Ndiyo maana hapo kati nimesema kwamba, pambana na hisia zako. Kumbuka ule usemi usemao, mke wa mtu ni sumu!

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Monday 26 February 2018

VIDEO: 'Serikali Inafurahia Viongozi Wa Upinzani Wanavyouwa?' Mtatiro Afunguka.

Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi ya Chama cha Wananchi CUF,  Julius Mtatiro amesema kukaa kimya kwa Serikali pindi wanapouawa Viongozi wa Vyama vya Upinzani kunaashiria kuwa Serikali inafurahia vifo hivyo hali ambayo inawafanya wauaji waendelee kufanya mauaji hayo kwa kuwa hawakemewi na Serikali.

TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI:

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Maneno ya Izzo B, Rama Dee na Niki wa Pili Muda Mchache Baada ya Sugu Kuhukumiwa Miezi 5.

Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi na mwenzake Emmanuel Masonga wamehukumiwa kwenda jela miezi mitano na Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Mbeya leo Februari 26, 2018 baada ya kukutwa na hatia kutumia lugha ya fedhea dhidi ya Rais Magufuli.


Baada ya kuhukumiwa kwenda jela baadhi ya wasanii wa muziki wa bongo fleva wamefunguka yao ya moyoni kuhusu tukio hilo huku wengine wakimtia moyo kuwa gerezani siyo kaburini hivyo atamaliza muda wake na kurudi uraiani kuwapigania wananchi wa Mbeya.

"Nguvu ya Mungu ikapate kuwa nawe pamoja na familia yako, gerezani sio kaburini 'stay strong' Jongwe" aliandika Niki wa Pili

Kwa upande wake msanii Rama Dee yeye amesema kuwa ameumizwa sana na bahari ya Sugu kufungwa jela miezi mitano na kudai si picha nzuri katika nchi yetu kwa mambo kama haya.

"Nasikitika sana kwa hii habari kama msanii pia kama rafiki wa Sugu, hii si picha nzuri" Rama Dee

Aidha msanii Izzo Bizness ambaye anaiwakilisha Mbeya vizuri katika muziki wa Hip hop pia ameonyesha hisia zake na kumtaka Mbunge huyo kuwa mvumilivu na kusimama imara katika kipindi hiki.

Mbali na huyo Rapa Roma Mkatoliki alikuwa na haya ya kusema juu ya kifungo cha Sugu "Hata hili lipatita' stay strong Joseph Zaburi 35: 1-28 " 

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

SIMBA HII ACHA KABISA, YATOA DOZI NZITO KWA MBAO, OKWI AZIDI KUCHEKA NA NYAVU.

Simba imeendeleza ubabe katika michezo ya Ligi Kuu Tanzania Bara baada ya kuipa dozi nene Mbao FC jioni ya leo kwa mabao 5-0, mchezo ukipigwa kwenye Dimba la Taifa, Dar es Salaam.

Mchezo huo ambao Simba waliutawala kwa asilimia kubwa, ulianza kutikisa nyavu zake katika dakika ya 37 kupitia Shiza Kichuya, na dakika chache baadaye Emmanuel Okwi alifunga bao la pili kwa njia ya penati, baada ya kuchezewa faulo ikiwa ni dakika ya 41.

Mpaka dakika 45 za awali zinamalizika, Simba walikuwa kifua mbele kwa mabao 2-0.

Kipindi cha pili kilianza huku Simba wakionesha uchu wa kufunga zaidi, ambapo 69, Emmanuel Okwi alifunga tena bao, na kufikisha mabao mawili kwenye mchezo huo.

Na katika dakika ya 82, Erasto Nyoni aliongeza bao la 3, na baadaye kuelekea mwishoni mwa mchezaji, Nicoulous Gyan akapigilia msumari wa mwisho, kwa kufunga bao la 5.

Mpaka dakika 90 zinamaliza, Simba SC 5-0 Mbao FC.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Mbao Yaitumia Salamu za Maaangamizi Simba Katika Mechi ya Leo.

Kikosi cha Mbao kimeamua kupeleka salamu kwa wapinzani wao Simba kuelekea mchezo wao wa leo Jumatatu utakaopigwa katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kwa kusema kuwa wamekuja jijini Dar es Salaam kupata ushindi na si vinginevyo.

Mwenyekiti wa timu hiyo, Solly Zephania Njashi, alisema kuwa maandalizi yao ya mchezo wa leo yapo vizuri na wamejiandaa vya kutosha na wamekuja kwa ajili ya kupata ushindi.

“Sisi tumejiandaa vizuri kwa ajili ya mchezo wetu wa kesho (leo) na mashabiki wafike kwa wingi kwani tuna uhakika tutaibuka na ushindi, tumejipanga kuhusu hilo.
“Sisi tumekuja kupata ushindi, siyo kupoteza, sema tatizo huwezi jua naye mpinzani wako amejipanga vipi kwenye mchezo huo, lakini sisi tupo vizuri na kikosi hakina majeruhi, bali kuna mmoja tu ambaye tulimpandisha kutoka kwenye academia, ila mwalimu atatoa ripoti kama atacheza au la,” alisema Njashi. 

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Baada ya kutajwa katika orodha ya watu hatari nchini, Zitto Kabwe afunguka.

Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe amemjibu Mkurugenzi wa kampuni ya CZI, Cyprian Musiba na kusema kuwa taarifa aliyoitoa haimtishi bali analitaka taifa kushughulika na watu wanaomfadhili ili kuharibu mahusiano ya taifa la Tanzania na nchi nyingine duniani.

Zitto Kabwe aliandika hayo katika ukurasa wake wa mtandao wa Twitter, baada ya Musiba kuitisha mkutano na vyombo vya habari ili kutangaza orodha ya watu hatari na wanaotishia usalama wa nchi, ambapo naye (Zitto) alitajwa kuwa miongoni mwa watu kwenye orodha hiyo.

Aidha alitaka watu kumpuuza na kutoshughulika naye na badala yake washughulike na Idara ya usalama ambayo aliitaja kuwa ndiyo inayomfadhili katika kufanya yote hayo.

Katika mkutano aliofanya na waandishi wa habari, Cyprian Musiba alitaja orodha ya watu ambao aliwataja kuwa ni hatari kwa usalama, na taifa linapaswa kuchukua hatua za haraka dhidi yao ili taifa lisije likaingia kwenye matatizo.

Katika orodha yake, Musiba aliwataja Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe kuwa ni mtu hatari kwa taifa na chama hicho kimepeleka vijana kupata mafunzo nchini ujerumani, ambao wana kazi ya kuratibu mipango ya kiharifu.

Musiba alimtaja pia mwanadada Mange Kimambi na kusema kuwa yeye anatumiwa na Shirika la Kijasusi la nchini Marekani (FBI), ili kuhamasisha watu wafanye uasi ndani ya serikali yao. Alieleza kuwa hii ni kutokana na serikali iliyopo madarakani kutokuendana na sera za Marekani na hivyo FBI kupitia Mange Kimambi imeamua kuingilia kati.

Aliendelea na kumtaja mjasiriamali Maria Sarungi kuwa ni hatari kwa taifa kwani yeye hutumia mitamdao ya kijamii kujadili mambo ya kuikashifu serikali iliyoko madarakani.

Vilevile alimtaja pia Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe kuwa ni mtu wa kuangaliwa, kwani anahamasisha maandamano

Aliendelea kuwataja pia Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu, Mbunge wa Tarime Vijijini John Heche, Musa Tesha, John Marwa  pamoja na Evarist Chahali.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Kada wa CCM, Shyrose Bhanji Aukana Ujumbe Ulioandikwa Katika Instagram yake Kuhusu JPM.

Kada wa CCM, Shyrose Bhanji amuomba radhi Rais Magufuli kwa ujumbe uliosambaa ukitokea katika ukurasa wake wa Instagram. Amesema alidukuliwa

Kupitia akaunti yake ya Instagram ulisambaa ujumbe unaosema ''Sikubaliani na utawala wa Rais JPM, niko tayari kwenda jela"

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Breaking News: Mahakama Yawahukumu kwenda Jela Sugu, Masonga Baada ya Kukutwa na Hatia.

MBUNGE wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi na Katibu wa Chadema Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Emmanuel Masonga wahukumiwa kifungo cha miezi mitano jela baada ya kutiwa hatiani kwa kosa la kutumia lugha ya fedheha dhidi ya Rais 
Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Sugu Awasili Mahakamani kwa Hajili ya Kusomewa Hukumu Ulinzi Wahimarishwa.

Ulinzi umeimarishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mbeya ambako itatolewa hukumu ya kesi inayomkabili mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi maarufu Sugu na Katibu wa Chadema Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Emmanuel Masonga.

Katika eneo la mahakama wapo askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) wakiimarisha ulinzi nje ya jengo. Tayari washtakiwa wameshafika mahakamani.

Mahakama leo Februari 26,2018 inatoa hukumu ya kesi ambayo Sugu na Masonga wanashtakiwa kwa kosa la kutumia lugha ya fedheha dhidi ya Rais John Magufuli.

Wawili hao wanadaiwa kutenda kosa hilo kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Desemba 30,2017 eneo la Uwanja wa Shule ya Msingi Mwenge jijini Mbeya.

Hukumu inatarajiwa kutolewa na Hakimu Mkazi Mfawidhi, Michael Mteite aliyesikiliza kesi hiyo. Upande wa mashtaka na wa utetezi ulikamilisha ushahidi Februari 9,2018.

Jamhuri iliwasilisha mashahidi watano na kielelezo kimoja cha sauti iliyodaiwa kurekodiwa na shahidi wa tano, Inspekta Joram Magova.

Upande wa utetezi uliwasilisha mashahidi sita wakiwamo Sugu na Masonga waliokana kutamka maneno wanayoshtakiwa kuyatoa.

Washtakiwa walitetewa na mawakili Sabina Yongo, Boniface Mwabukusi na Hekima Mwasipu kabla ya kujitoa, hivyo sasa wanawakilishwa na Peter Kibatala.

Kwa mara ya kwanza, Sugu na Masonga  walifikishwa mahakamani Januari 16 na kusomewa mashtaka na Wakili wa Serikali Mkuu, Joseph Pande aliyeeleza upelelezi ulikuwa umekamilika na walikuwa tayari kuendelea na usikilizaji. 

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa