Tuesday 13 February 2018

Karani Adai Nyoka Alikula Mamilioni ya Pesa.

Karani mmoja nchini Nigeria amefukuzwa kazi baada ya kuwaambia wakaguzi wa hesabu kuwa nyoka alikula naira milioni 36.

Pesa hizo ni sawa na dola 100,000 za kimarekani.

Karani Philomena Chieshe alikuwa akifanya kazi katika ofisi ya bodi ya mtihani ya Nigeria inayokusanya pesa za mtihani.

Bodi hiyo ya mtihania iliiambia BBC kuwa ilitupilia mbali madai yake na imeanisha kumchukulia hatua za kinidhamu.,

Kisa hicho kimezua shutuma na dhihaka kwenye mitandao ya kijamio nchini Nigeria.

Nayo tume ya kupambana na rushwa nchini Nigeria iliandika ujumbe huu katika Twitter ambayo nembo yake ni mwewe.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment