Thursday 22 February 2018

Vilio, Simanzi Vyatanda Muhimbili Wakati wa Kuchukuliwa Mwili wa Akwilina.

VILIO na simanzi vimetawala wakati wa kuchukua mwili wa aliyekuwa mwanafunzi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), Akwilina Akwilini aliyeuawa kwa kupigwa risasi Feb 16, 2018.

Mwili wa Akwilina umechukuliwa leo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili na kupelekwa NIT k wa ajili ya kuagwa kabla ya kupelekwa nyumbani kwao Rombo kwa mazishi.

Jeneza lenye mwili wa mwanafunzi huo liko katika gari maalumu la kubebea maiti.

Baada ya kuaga mwili wa mwanafunzi huyo, saa 10 jioni safari kuelekea wilayani Rombo mkoani Kilimanjaro kwa mazishi itaanza. Akwilina atazikwa kesho.
Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment