Tuesday 19 December 2017

Gdbless Lema atoa kauli Takukuru kutupa ushahidi wa Flashi ya Nassari.

Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema amesema kutupwa ushahidi wao na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) ni kupoteza sifa na imani kwa wananchi.

Amesema uamuzi huo unatoa sura ya matabaka kwamba kuna watu ambao wanafikishwa mbele ya vyombo vya sheria na wengine hawastahili.

Takukuru kupitia msemaji wake, Musa Misalaba jana Jumapili Desemba 17,2017 alisema taasisi hiyo imeshindwa kuendelea na uchunguzi wa tuhuma za rushwa zilizowasilishwa na Lema pamoja na mwenzake Joshua Nassari wa Arumeru Mashariki.

Imesema uamuzi huo unatokana na wabunge hao kuingilia uchunguzi na kuuvuruga licha ya kutahadharishwa kuhusu suala hilo.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumatatu Desemba 18,2017 mjini Arusha, Lema amesema uamuzi wa Takukuru umepoteza imani kwa wananchi ambao walikuwa na imani na chombo hicho.

Amesema kitendo cha mamlaka ya uteuzi kumteua waliyemtuhumu, Alexander Mnyeti kuwa Mkuu wa Mkoa wa Manyara kinatoa ujumbe kwa Takukuru.

Akizungumzia hilo, katibu wa Chadema kanda ya kaskazini, Aman Gorugwa amesema Takukuru ilipaswa kutafuta ushahidi.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Rose Muhando Atangaza Kujiunga na Chama cha Mapinduzi CCM.

Msanii wa nyimbo za Injili aliyetamba kwa vibao vyake murua na vyenye kuburudisha Rose Muhando, ametangaza kujunga rasmi na Chama cha Mapinduzi.

Msanii huyo ambaye aliomba kujiunga na chama hicho amekabidhiwa kadi ya Chama cha Mapinduzi leo yeye pamoja na kikundi chake, katika Mkutano Mkuu Maalum wa Tisa wa CCM Taifa, unaofanyika katika ukumbi wa Jakaya Kikwete, mjini Dodoma.

Rose Muhando kabla ya kukabidhiwa kadi ya chama cha CCM alitumbuiza kwa kibao maalumu alichokiandaa kwa ajili ya Rais John Pombe Magufuli ambacho amekipa jina la “Magufuli Tubebe”.

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey polepole alitangaza kuwa Rose Muhando pamoja na Kundi lake wameomba kupewa nafasi ya kutumbuiza kwa wimbo huo maalumu pamoja na kukabidhiwa kadi za CCM.

“Kundi la Ndugu Rose Muhando na yeye mwenyewe niwakaribishe Jukwani kwa wimbo ambao wameutunga maalumu kwa Ndugu Magufuli. Kundi hili walipokuwa wanakuja walikuwa na maombi mawili, ombi la kwanza ni kupewa nafasi ya kuimba wimbo huu maalumu na pili kujiunga rasmi na CCM,” amesema katibu wa Itikadi na Uenezi, Humphrey Polepole.

Hata hivyo Polepole amesema kuwa Rose Muhando na kundi lake watakabidhiwa kwa makatibu wa mikoa husika kwa ajili ya michakato ya kuwaandikisha kama wanachama wapya wa CCM.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Ambe Lulu Awatolea Povu Wanaomsema Prezzo "Usimfananishe Mume Wangu (Prezzo) na Young Dee".

Msanii wa muziki Bongo, Amber Lulu amedai mpenzi wake Prezzo asifananishwe na Young Dee.

Amber Lulu amesema hao ni watu wawili tofauti hivyo kuwafaninisha ni kumkosea heshima Prezzo.

“Usimfananishe mume wangu na watu wengine kwa sababu unakuwa unamkosea adabu, kwa hiyo Young Dee ni Prezzo usiwakee kabisa pamoja kwa sababu ni watu wawili ambao hawezi kuendana hata kidogo,” Amber Lulu ameiambia Bongo5.

Pia Amber Lulu ameongeza kuwa mara baada ya kuachana na Young Dee hata tattoo yake aliyokuwa ameichora mkononi aliifuta kwani aliiweka kwa muda tu. 

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Zari na Hamissa Mobetto Wakutana Uso kwa Uso Uganda.

Kama ulifikiri kuwa baby Mama wa Diamond Platnumz, Zari The Boss Lady na Hamisa Mobetto bifu lao limetulia au kuisha kabisa utakuwa umekosea.

Zari na Hamisa wamekuwa wakiripotiwa kutoelewana na kurushiana vijembe katika mtandao tangu Hamisa alipozaa na Diamond wakati akijua fika Zari na muimbaji huyo wa WCB bado ni wapenzi.

Sasa Hamisa na Zari si kwamba wanaviambiana tu kwenye mitandao, bifu lao limeenda mbali zaidi lakini katika njia ambayo ni nzuri.

Wakati Zari akitarajia kufanya event yake ya Zari All White Party nchini Uganda nyumbani kwao December 21 mwaka huu, siku hiyo hiyo Hamisa naye ameenda event yake.

Hata hivyo utakumbuka si mara ya kwanza kwa Zari kufanya party kama hiyo nchini Uganda na hata Tanzania ameshafanya hivyo lakini kwa Hamisa ni tofauti kitu ambacho ninatafsiriwa kama bado wanazidizi kuonyeshana umwamba. 

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Abiria wamiminika Ubungo Daradara Zaruhusiwa Kwenda Moshi, Arusha.

Magari ya abiria (daladala) yameanza kutumika kupakia abiria wanaosafiri kwenda mikoa ya Arusha na Kilimanjaro  ili kupunguza adha ya usafiri kwa abiria wanaosafiri msimu huu wa sikukuu za mwisho wa mwaka.

Akizungumza na Mwananchi, leo Jumanne Desemba 19, Mkuu wa Usalama Barabarani Kituo cha Mabasi yaendayo mikoani Ubungo (UBT),Inspekta Swamix Ibrahimu amesema gari hizo zimeanza kubeba abiria na asubuhi ya leo daladala nne zimeondoka kuelekea Moshi na Arusha.

"Daladala unazoziona hapa, tunazikagua na zipo kwaajili  ya dharura  endapo itatokea abiria wakawa wengi basi tunaruhusu zinapakia "amesema.

Si kwamba zinapakia muda wowote, hapana tutakuwa na daladala tano kwa siku ambazo zinakuwepo ikitokea abiria wameongezeka na basi kubwa hakuna basi tunaruhusu" amesema

 Ibrahimu amesema abiria bado hawajawa wengi  kiasi cha kuruhusu daladala nyingi kupakia. Mmoja wa wasimamizi wa daladala ambazo zimekutwa zikikaguliwa, Ignas Swai amesema gari zake ni imara na tayari zimekaguliwa na Askari na kupewa kibali na Sumatra.

"Nauli tunatumia IleIle iliyowekwa na Sumatra na tunapakia abiria wanaoenda Moshi na Arusha "amesema. 

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Soma Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Siku ya Leo.

Bonyeza Links zifuatazo Kusoma zaidi na Kuapply;

6 Job Opportunities at TANAPA, Tourism Promotion Assistant

7 Job Opportunities at TANAPA, Office Secretaries

Job Opportunity at Projects Abroad Tanzania, Medical Coordinator

14 Job Opportunities at TANAPA, Civil Technicians

Job Opportunity at Exact Manpower Consulting, Credit Officer

2 Job Opportunities at TANAPA, Assistant Internal Auditors

15 Job Opportunities at TANAPA, Accounts Technicians

Job Opportunities at TANAPA, Multimedia Projectionists

Nafasi zingine za ajira Ingia www.ajirayako.co.tz 

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Mbunge Sadifa Aachiwa kwa Dhamana Apewa Masharti Magumu.

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Dodoma iemwachia kwa dhamana aliyekuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), Sadifa Juma Khamis (Mbunge) anayekabiliwa na mashtaka ya kutoa rushwa wakati wa uchaguzi mkuu wa viongozi wa UVCCM Taifa.

Sadifa ameachiwa leo Desemba 19, 2017 baada ya mahakama kutupilia mbali pingamizi la upande wa mashtaka ambao waliliwasilisha mahakamani hapo kuweka zuio la kupewa dhamana.

Mtuhumiwa huyo ametakiwa kudhaminiwa na watu watatu pamoja na kusaini bondi ya Tsh. Milioni 1, huku akipewa masharti ya kutosafiri nje ya nchi.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Baada ya Kupitia Changamoto Vanessa Mdee Ashuhudia Maajabu.

Malkia wa Bongo Fleva anayefanya vizuri ndani na nje ya nchi, Vanessa Mdee amekiri kushuhudia maajabu ya Mungu baada ya kupitia changamoto miezi ya mwanzo wa mwaka na hatimaye kumaliza mwaka kwa kusaini mkataba mnene na Kampuni ya usambazaji wa


muziki 'Univesal Music Group'.

Kupitia ukurasa wake wa Istagram Vanessa ameweka furaha yake na kushangilia na mashabiki wake ambapo amewaambia kwamba huo ni mwanzo tu na kwamba mambo mengine makubwa yapo njiani.

"Nimeona niitumie siku na fursa hii kuwajulisha wapendwa mashabiki zangu mwanzoni mwa mwaka huu. Nilipitia changamoto nyingi Sana. Lakini kwa neema za Mungu. Nilitoka mahali pale na sio kuona baraka tu bali na maajabu mengi yaliyotokea kwenye maisha yangu i kiwemo kuwa mmoja wa familia ya Universal Music Group in a unique joint signing between Universal Music Germany, Airforce1 na Universal Music Group. Vanessa Mdee.



Ameongeza "hii ni mara ya kwanza kwa msanii wa kiafrika kupata deal ya aina hii yenye mkwanja mrefuu sana...Hii ni habari njema kwa mashabiki wangu na ndiyo kwanza tumeanza. Mambo makubwa zaidi yanakuja. Kumbuka kila mwisho wa Jumapili ndiyo mwanzo wa Jumatatu, usiogope kuanza upya"

Vanessa amewashukuru mashabiki zake, ndugu jamaa na marafiki ambao walikuwa pamoja na yeye kuanzia mwaka kuanza japo ulikuwa na changamoto mpaka sasa anbapo mwaka unaelekea kuisha.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Wolper Awatolea Povu Wanaomuandama Kuhusu Jino Lake la Silver.

MWANADADA mwenye mvuto kwenye tasnia ya Filamu za Bongo, Jacquiline Wolper amewafungukia wanaochukua picha zake na kuzi-edit huku wakimchafua kuhusu jino lake analodai kuwa limetengenezwa kwa madini ya Silver.

Staa huyo ambaye ni maarufu pia kwa kutupia pamba za maana amedai kuwa alitumia gharama zake kupanda ndege kwenda Sauzi kuweka jino la silver huku akiwaita ‘Kunguni’ wanaomfanyia mchezo huo mchafu.

Ngoja niwaeleze kitu kimoja ambacho amkijui kuhusiana na hili pengo…hli pengo nimelipandia ndege kwenda south kulitoa nakuweka ma slver kwa meno yangu kwa mahaba yangu mwenyewe ya kuwa na mwanya wa pembeni 😂😂sasa we kunguni unayetokea pasipojulikana unakuja kuchukua pcha naku edt unavyojua wewe ukizani nitakasirika au nitaumia am soleeee 🙄…unapoteza muda wako me najipenda nilivyo naikitokea nimechoka nitanyanyua makalio yangu hapa nitajilipia nauli nakwenda kuweka jino niwe na jino so plz usitokwe na damu juu ya hlo pengo langu ndilo nalodangia kwa tarfa yako kma ulikua ujui😂😂😂🔫#Pengodanga💃🥂🍾


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Ramsey Awapa Makavu Wema Sepetu na Ray.

STAA wa sinema za Nigeria (Nollywood), Ramsey Nouah amewalipua waigizaji wa filamu za Kibongo kwa kushindwa kuendeleza sanaa hiyo kwa kiwango alichoishia marehemu Steven Kanumba huku akilizungumzia kaburi la staa huyo, Ijumaa Wikienda lina mkada kamili.

Unapozungumzia Bongo Movies unawagusa vinara wake, Vincet Kigosi ‘Ray’, Wema Isaac Sepetu, Kajala Masanja, Aunt Ezekiel, Jacob Steven ‘JB’, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ na wengine wengi waliofanya kazi na Kanumba.

Katika Makaburi ya Kinondoni, Dar alikozikwa Kanumba miaka mitano iliyopita, Ramsey ambaye kwa mara ya kwanza alifika kaburini hapo wikiendi iliyopita alionekana mwenye huzuni kubwa na kushindwa kujizuia ambapo alimwaga machozi mfululizo kabla ya kutamka maneno mazito yaliyosisimua wengi waliofika kaburini hapo.


Mama Kanumba akilia kaburini kwa mwanaye.

MAMA KANUMBA

Muda mfupi baada ya kuwasili makaburini hapo, Ramsey alimshika mkono mama mzazi wa Kanumba, Flora Mtegoa na kumkumbatia na ndipo vilio vikashika nafasi hususan kwa mama huyo.
MAOMBI

Ramsey, alitumia dakika chache akiwa kimya huku uso wake ukionesha maumivu na ghafla alianza kushusha maombi akimuombea marehemu Kanumba huku watu wote wakimsikiliza.

“Baba, utukufu wako ni wa kipekee tazama tumesimama hapa leo tukiwa na huzuni mioyoni mwetu, machozi yakighubika mboni za macho yetu tukimkabidhi kwako mja wako, Steven (Kanumba) aliyelala hapa kwa mapenzi yako, mpokee mwanao baba na kumsamehe dhambi zake ili siku moja tuonane naye kwa mapenzi yako yakitimizwa, baba tazama moyo wangu ulivyokwazwa na kifo hiki, hakika sitaki kukufuru, lakini ulimchukua Steven wakati dunia ikimhitaji zaidi, lakini jina lako lihimidiwe kwa kila jambo,” aliomba Ramsey.
Baada ya kumaliza maombi hayo, Ramsey alianza kuzungumza maneno ambayo yaliashiria alikuwa akimwambia Kanumba, jambo lililoshangaza na kuvutia watu waliokuwepo.

“Steve, nimesimama mbele yako leo ukiwa hujitambui. Tuliachana ukiwa na pumzi yako, lakini leo (Jumamosi iliyopita) niko kando ya mahali ulipolala na huwezi kuamka japo kunipa mkono, lakini kibaya zaidi hukuniambia maneno ya kwaheri, kwa nini hukuniaga Steven? Kuna mahali nilikukosea?

Aaah nashindwa kuhimili maumivu haya, ninalo kaa la moto kifuani mwangu, lakini kinachoniumiza zaidi ni kwamba mahali ulipolala hapaendani na hadhi yako, hukupewa kabisa thamani yako kulingana na ulichokifanya kwenye tasnia ya filamu na bila kuficha ni kwamba filamu za Kitanzania zinakufa, najua huko uliko unaumia na kinachoendelea kwenye filamu zanu,” alisema Ramsey katika ‘mazungumzo’ yake na Kanumba.
Baada ya kumalizana na ibada ya kaburini kwa Kanumba, Ramsey alizungumza na waandishi wa habari na kulipuka maneno ambayo yalilenga kuwananga waigizaji wa filamu za Kibongo.

“Ni ukweli ulio wazi kwamba filamu za hapa (Bongo) zimekosa msisimko, lakini wanayo nafasi ya kurekebisha, nimesimama hapa na maumivu makali, lakini yote ninamshukuru Mungu na wito wangu kwa wasanii wamsaidie mama huyu (mama Kanumba) kwani mwanaye alitoa ajira kwa wasanii, lakini leo wanamuona mama huyo kama si chochote, wameshindwa kumuenzi Steven kulingana na thamani yake, waangalie mahali walipokosea ili laana ya Steven isizidishe makali yake, lakini kubwa wamsaidie mama huyu,” alisema Ramsey akipeleka ujumbe huo kwa wasanii wa Bongo Movies.
KUHUSU LULU

Katika mazungumzo hayo, Ramsey hakutaka kuingia kwa undani kuhusiana na msanii Elizabeth Michael ‘Lulu’ ambaye kwa sasa yuko jela akitumikia kifungo cha miaka 2 baada ya kupatikana na hatia ya kumuua bila kukusudia Kanumba, April 7, 2012 nyumbani kwa jamaa huyo, Sinza- Vatican, Dar.
Chanzo: Global Publishers 

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Chadema Waijia Juu CCM "Hatutaki Yajirudie ya Idi Amin".

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimekosoa kitendo cha CCM kuweka mgombea wake kwenye nafasi ya Spika wa Bunge la Afrika Mashariki wakati haikutakiwa kufanywa hivyo, na kusema kwamba kitendo hicho kitasababisha mgogoro wa kidiplomasia.


Kwenye taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari kutoka kwa chama hiko, imesema CCM imekiuka utaratibu wa Bunge hilo la kumtafuta Spika la kuliongoza kwa kumuweka mtu wao kwenye kinyang'anyiro, wakati kiutaratibu ilitakiwa Spika wa awamu hii atoke nchi ya Rwanda kulingana na mzunguko ambao ulikuwa unafuatwa, na kwamba kitendo hicho kinaweza kuleta migogoro itakayoathiri Jumuiya hiyo kama kipindi cha Idi Amin.

"Awamu hii Spika alipaswa kutoka Rwanda, lakini Tanzania kwa kuwa CCM imezoea kutokuheshimu sheria na kanuni zilizopo imemteua mbunge wake Adam Kimbisa kugombea nafasi ya Spika kinyume kabisa na kanuni za Bunge hilo, na huu ukiwa ni mwendelezo wa utamaduni wao wa kutokuheshimu sheria na kanuni, kitendo ambacho kinatishia ustawi na uwepo wa Jumuiya ya Afrika Mashariki", imeandika Taarifa hiyo.

Taarifa hiyo iliendelea kueleza kuwa .."CHADEMA tunalaani kitendo hiki, CCM wajue kuwa watabeba lawama zote kama kutakuwa na mgogoro ndani ya Bunge la Afrika Mashariki ambayo unaweza kupelekea mgogoro wa kidiplomasia katika Jumuiya nzima kutokana na tabia yao ya kutoheshimu taratibu zilizowekwa. Ttunataka kanuni za EAC ziheshimiwe, kwani tunakumbuka matendo ya Idd Amin mwaka 1977 yalivyovunja

 Jumuiya hii, hatutaki yajirudie kamwe".

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Tuesday 12 December 2017

Majonzi miili 14 ya Wanajeshi wa Jeshi la Wananchi (JWTZ) ikipokelewa.

Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam jana ulikuwa eneo la majonzi makubwa baada ya miili ya askari 14 wa Jeshi la Wananchi (JWTZ), waliouawa na waasi wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC), kufika nchini hatimaye.

Miili hiyo ilirejeshwa majira ya jioni na kupokelewa na umati wa askari wa JWTZ wakiongozwa na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk. Hussein Mwinyi pamoja na Mkuu wa Majeshi, Jenerali Venance Mabeyo.

Ni mara ya kwanza kwa wanajeshi wengi kiasi hicho wa JWTZ kuuawa katika misheni ya kulinda amani, kwa mujibu wa Jenerali Mabeyo aliyekuwa akijibu maswali ya waandishi wa habari uwanjani hapo.

Miili hiyo ililetwa na ndege maalum ya Umoja wa Mataifa huku ikiwa imefunikwa bendera ya UN.

Baada ya kuwasili, kwa huzuni wanajeshi walianza kuchukua mwili mmoja baada ya mwingine na kuhamishia katika magari maalum yaliyokuwa yameandaliwa.

Kila mwili ulibebwa na wanajeshi nane wakati wa kuhamishia katika magari hayo kwa ajili ya kusafirisha kwenda kuilaza katika Hospitali Kuu ya Jeshi ya Lugalo, jijini.

Jumla ya magari saba yalitumika kubebea miili hiyo, kila moja ikibeba miili miwili na kusindikizwa na kundi la wanajeshi.

Akizungumza kabla ya kuanza safari hiyo ya kwenda Hospitali ya Lugalo, Dk. Mwinyi alisema miili hiyo inatarajiwa kuagwa Alhamisi katika viwanja vya Wizara ya Ulinzi, eneo la Upanga.

Pia alisema tukio la kuuawa kwa wanajeshi hao wamelipokea kwa masikitiko makubwa na kwamba wataendelea kuchukua tahadhari ili kuzuia kutokea kwa tukio kama hilo tena.

Kwa upande wake, Jenerali Mabeyo alisema tukio kama hilo ni la kwanza kutokea na kwamba hawajatetereka.

“Unavyolinda amani, lazima utegemee lolote, na tukio hili ni la kwanza katika kipindi cha miaka mitano," alisema Jenerali Mabeyo. "Hatuna hofu."

"Isipokuwa unaposhambuliwa, unajitazama umekosea wapi halafu unajirekebisha."

Aidha, mkuu wa majeshi alisema hali ya wanajeshi waliojeruhiwa ambao wako Kinshansa, DRC na nchini Uganda inaendelea vizuri na kwamba mmoja aliyepotea kati ya wawili amepatikana.

Kufuatia vifo hivyo, Rais John Magufuli ambaye pia ni Amiri Jeshi Mkuu alituma salamu za rambirambi kwa Waziri Mwinyi, Jenerali Mabeyo, maofisa wote wa Jeshi na kwa familia zote za marehemu mwishoni mwa wiki iliyopita.

Katika salamu hizo Rais Magufuli alisema: “Nimepokea kwa mshtuko mkubwa taarifa za kuuawa askari wetu kumi na wanne na wengine arobaini na wanne kujeruhiwa, na wawili hawajapatikana huko DRC wakati wakitekeleza majukumu ya ulinzi wa amani.

"Natoa pole sana kwa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania na familia, (na) wakati tukisubiri taarifa kamili kutoka DRC niwaombe Watanzania tuwe na subira."Mungu wetu yuko pamoja nasi."

Taarifa ya Umoja wa Mataifa iliyotolewa na Katibu Mkuu wa UN, Antonio Guterres Ijumaa ilisema shambulio hilo ndilo baya zaidi kuwahi kutekelezwa dhidi ya walinda amani wa umoja huo katika historia yake miaka ya karibuni.Pia alielezea kusikitishwa na tukio hilo.

“Ningependa kueleza kusikitishwa kwangu na shambulio hilo lililotekelezwa usiku wa jana (Alhamisi) dhidi ya walinda amani wa Umoja wa Mataifa nchini DRC," alisema katika taarifa hiyo.

"Shambulio hilo lilitekelezwa kwenye kambi ya jeshi ya Semuliki, eneo la Beni katika mkoa wa Kivu Kaskazini.Taarifa ya UN ilisema pia wanajeshi watano wa Jeshi la DRC (FARDC) waliuawa kwenye shambulio hilo.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Msagasumu Awakata Ngebe Wanawake Wanaomshobokea " Nina Mke Wangu Acheni Shobo".

NGULI wa Muziki wa Singeli, Selemani Jabir ‘Msaga Sumu’, amewakata ngebe wanawake ambao wamekuwa wakimshobokea wakati yeye ana mke na watoto wawili.

Akizungumza na Full Shangwe, Msaga Sumu anayebamba na Ngoma ya Mwanaume Mashine alisema kuwa hana mpango na wanawake wanaomshobokea na haitakuja kutokea kwani ana ndoa yake anayoipenda.

“Imekuwa kero sasa, ninachoweza kuwaambia ni kwamba wanawake waache kunishobokea, Kwanza watambue kuwa ninaipenda familia yangu na kwa sasa ninatimiza miaka nane ya ndoa yangu, na nina watoto wawili, inshallah Mungu kanijalia,”alisema Msaga Sumu na kuongeza;

“Kwa sasa najipanga kuzindua rasmi Mwanaume Mashine ndani ya Dar Live hivyo soon nitatangaza.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Dully Sykse Atokwa Povu Kisa Bomberdier Atangaza Vita kwa Wasanii Wenzake.

ETI kisa Bombardier! Mkongwe wa Bongo Fleva nchini, Dully Sykse ametoa povu ikiwemo kutangaza vita na wasanii wa kizazi kipya kwa sababu ya kushindwa kumsapoti kwenye wimbo wake mpya.

Dully Sykes ambaye ameachia wimbo mpya wa Bombardier, alisema wasanii wa sasa ambao wengi ni wapya wana roho mbaya na yeye yuko tayari kupambana nao.

“Wasanii wa sasa wana roho mbaya, hawasapotiani kama wasanii wa zamani, ndiyo maana Bombadier yangu hawajanisaidia kuitangaz, hiyo inaonesha muziki ni vita na mimi niko tayari kupambana nao,” alisema Dully 

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Shamsa Ford Amfunda Shilole "Kuwa Mke Bora kwa Mumeo Ustar Weka Pembeni".

STAA wa Filamu nchini, Shamsa Ford amefungukia uamuzi wa msanii mwenzake wa Muziki, Zuwena Mohammed maarufu kama Shilole kwa kuamua kufunga ndoa tena ya Kidini na mpenzi wake, Uchebe ndoa iliyoshuhudiwa hivi karibuni na kutikisa kwenye mitandao na vyombo vya habari huku ikiwaacha midomo wazi kwa wale walidhani kuwa angerudiana na mpenzi wake wa zamani, Nuh Mziwanda.
Shamsa ambaye pia alifunga ndoa mwaka huu na mpenzi wake, Chidi Mapenzi ametumia ukurasa wake wa Instagram kumsihi Shilole atulie, aweke umaarufu pembeni, aitunze ndoa yake na hatimaye atafaidi matunda ya ndoa iliyo bora.
Shamsa ameandika;
“Hongera sana mamy. Umefanya maamuzi sahihi ya kumpendeza Mwenyezi Mungu.Cha muhimu uwe mke bora wa Kitanzania kwa mumeo na ustar uweke pembeni.
“Mumuweke Mungu mbele, uvumilivu na kuheshimiana inshaallah mtazikana.Karibu kwenye Chama mama….Sasa nyie mnao subili matajiri wawaoe wakati hao matajiri wana wake zao wameanza nao moja mtasubili sana mpaka uso uote sugu.Uzuri na Ustar una mwisho wake. Iitafika muda hata inzi hakusogelei……HONGERA MAMA @shilolekiuno_badgirlshishi,” ameadika Shamsa.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa