Thursday 24 November 2016

#YALIYOJIRI>>>Wataalam wa afya kuanza kusajiliwa na kupewa leseni.Fahamu zaidi hapa.

Wataalamu mbalimbali wa sekta ya afya, sasa wataanza kusajiliwa na kupewa leseni zitakazowatambulisha na zitakuwa na masharti maalumu.

Hayo yamesema na Mganga Mkuu wa Serikali, Profesa Muhammad Kambi  jana Jumatano  jijini Dar es salaam, wakati akifungua mkutano wa mwaka wa Chama cha Wafiziotherapia (APTA).

Alisema serikali imeanza mchakato wa kuipitia upya Sheria ya Madaktari wa Tanganyika, ambayo itaongezwa sharti hilo pamoja na kuundwa kwa bodi maalumu itakayosimamia maadili ya watumishi hao.

“Lakini hivi sasa kuna taaluma nyingi ndani ya hii fani, kwa mfano ninyi wataalamu wa fiziotherapia. Mpo lakini sheria haiwatambui, kwa maana hiyo inakuwa vigumu hata kuwafuatilia. Ndiyo msingi wa kuipitia upya sheria hii,” alisema.

“Katika sheria mpya itakayoboreshwa, kila mtumishi atatakiwa kukata leseni. Kila mtumishi atatakiwa kujiendeleza kielimu, kuongeza ujuzi ili aendane na wakati uliopo kwa sababu mambo yanabadilika, kile ulichosoma jana unahitaji kujifunza zaidi,” alisema.

Aidha Kambi alisema tayari maboresho ya sheria hiyo yameshawasilishwa katika Kamati ya Baraza la Mawaziri ya Katiba na Sheria na imeshapitiwa.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi


Bonyeza Hapa CLICK HERE

 

#BURUDANI>>>Waziri Nape Nnauye Alitembelea Kundi la Wasafi Classic Linaloongozwa na Diamond Platinumz.Fahamu zaidi hapa.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mheshimiwa Nape Nnauye ametembelea ofisi za Kundi la musiki wa kizazi kipya la Wasafi.

Pamoja na mambo mengine uongozi wa kundi hilo umemuomba waziri huyo kushughulikia changamoto mbalimbali zinazowakabili ikiwa ni pamoja na kupunjwa mapato yatokanayo na miito ya simu (Caller tunes), wizi wa kazi za wasanii, kupata eneo (Ukumbi wa Kisasa) kwa ajili ya kufanyia maonesho makubwa ya musiki, wasanii kupata elimu juu ya kulipa kodi kwa kazi zao na kuongeza kiwango cha uwiyano kwa nyimbo za kitanzania zinazopigwa redioni dhidi ya nyimbo za kigeni.

Kwa upande wake Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye  amehaidi kuzifanyia kazi changamoto hizo na kuifanya tasnia ya muziki kuwa ajira kubwa kwa vijana wengi kwa kuongeza vipato vyao na pato la taifa kwa ujumla.

“Nimewaahidi kuzifanyia kazi changamoto hizi mapema iwezekanavyo ili kuongeza kipato kwa wasanii hapa nchini,” amesema Mheshimiwa Nnauye.

Wasafi Classic ni kundi la Muziki wa kizazi kipya(Bongo Flavour) Tanzania linalomilikiwa na Msanii Naseeb Abdul (Diamond Platinumz) na mpaka sasa lina wasanii wapatao 16 na linaongozwa na mameneja Babu Tale, Said Fella na Sallam SK.



Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi


Bonyeza Hapa CLICK HERE

 

#BURUDANI>>>>ALI KIBA Ashinda Tuzo za NAFCA na The Nol.Fahamu zaidi hapa.

Alikiba ashinda tuzo mbili za The Nollywood & African Film Critics (NAFCA)

Alikiba ameshinda vipengele viwili kwenye tuzo za heshima kubwa za The Nollywood & African Film Critics (NAFCA) ambazo hutolewa nchini Marekani.

Tuzo za mwaka huu zilitolewa wikiendi hii kwenye ukumbi wa Alex Theatre of Glendale, huko California. Zilikuwa ni tuzo za 6 na zilionekana katika nchi mbalimbali duniani.

Alikiba ameshinda kipengele cha Favorite Artist of The Year na Favorite Song of The Year



Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi


Bonyeza Hapa CLICK HERE

 

#YALIYOJIRI>>>HIFADHI YA TAIFA YA MSITU WA MKWENI UPO HATARINI KUTOWEKA KUTOKANA NA UHARIBIFU WA MAZINGIRA.FAHAMU ZAID HAPA.

Katikati Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina akishiriki katika kuteketeza tanuru la mkaaa katikati ya hifadhi ya m situ ya Mkwemu Wilayani Kahama.

Na Evelyn Mkokoi

Hifadhi ya Taifa ya Msitu wa Ukwemi uliyopo katika wilaya ya Kahama upo hatarini kutoweka kutokana na shughili za kibinadamu zinazofanywa ndani ya hifadhi hiyo zinazochangia kwa kiasi kikubwa uharibifu wa mazingira.
Hayo yameelezwa na Meneja kutoka wakala wa Taifa wa Misitu Bw. Mohamed Dosa wakati wa Ziara ya Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina alipotembelea HIfadhi hiyo iliyopo ndani ya Halmashauri ya Kahama inayopakana na Halmashauri ya Mbongwe Mmkoani geita.

Katika Ziara yake ya Ukaguzi wa Mazingira katika Hifadhi ya Msitu Huo, Naibu Waziri Mpina alielezwa kuwa shughuli kubwa zinazotegemewa na wakazi wa vijiji vya jirani na msitu huo ni, ukataji miti kwa uchomaji wa mikaa na ukataji wa magogo kwa shunghuli mbali mbali ikiwa ni pamoja na shughuli na ujenzi na utengenezaji wa samani za majumbani.
Meneja Dosa Amemuelezea Naiubu Waziri Mpina kuwa (generation) kizazi cha kwanza cha aina na miti ndani ya hifadhi hiyo kilishakwisha na miti inayoota na kuonekana sasa ni ya kizazi cha pili.
“changamoto kubwa tunayokumbana nayo katika kulinda hifadhi hii ni magari ya doria kuzunguka ndani ya msitu kwani ni mkubwa sana na hakuna skari wa kutosha kufanya doria. “ Alisisitiza Bw. Dosa.
Akiwa katikati ya Msitu huo Naibu Waziri Mpina alijionea Uharibifu mkubwa wa uchomaji mkaa na kushuhudia mhalifu Bw John Abdalah Sanga makazi wa kijiji cha jirani cha mwendakulima aliyekuwa akimaliza kuchoma mkaa katikati ya msitu huo na kueleza kuwa amekuwa akifanya kazi hiyo kwa takribani miaka mitatu sasa hali iliyompelekea Naibu Waziri Mpina na timu yake kutekekeza baadhi ya matanuru ya mkaa ndani yam situ huo.
Kwa upande wake Mratibu wa Baraza la Taifa la Hifadhi na usimamizi wa Mazingira NEMC kanda ya ziwa Bw. Jamal Baruti alieleza kuwa hali ya uharibifu wa misitu nchini bado ni kubwa na suala la mkaa bado ni changamoto, hivyo wanaanchi washiriki katika kuhifadhi misitu na kutafuta mbadala wa mkaa na misitu ni muhimu kwa kutunza baiyonuwai., wakati katibu tawala wa wilaya ya kahama Bw. Thomas Nganya akitoa Rai kwa wananchi waone kuwa suala la utunzaji wa mazingira ni jukumu la kila mmoja na siyo kuiachia seriali peke yake.
 Sehemu ya Hifadhi ya Msitu wa Mkwemu iliyoharibiwa vibaya na shughuli za binadamu ikiwa na pamoja na uchomaji wa mkaa, na baadhi ni magogo yanayoonekana pichani yaliyokuwa yamekatwa na wahalifu wa mazingira.
  Aliyeshika kiuno, Naibu Waziri Ofisi Ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina akiangalia Tanuru la Mkaa likitekea baada ya kushiriki kuteketeza ndani ya Msitu wa Mkwemu wilayani Kahama.



Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi


Bonyeza Hapa CLICK HERE

 

#YALIYOJIRI>>>Mawakili wa Lema wakata rufaa kudai dhamana.....Rufaa hiyo Itasikilizwa Jumatatu.Fahamu zaidi hapa.

Hatimaye  rufaa ya Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema iliyokatwa na mawakili wake itasikilizwa Jumatatu ijayo.

Rufaa hiyo itasikilizwa na Jaji Fatma Masengi ya kuomba mbunge huyo kupewa dhamana baada ya mawakili wanaomtetea jana kusajili maombi ya rufaa namba 112/113 ya mwaka 2016 Mahakama Kuu Kanda ya Arusha, ili kudai haki ya dhamana ya Lema aliyonyimwa kutokana na makosa ya kisheria yaliyofanywa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha.

Rufaa hiyo imepokewa Mahakama Kuu Kanda ya Arusha na kupangwa kwa Jaji Masengi ambaye ndiye atakayeamua hatma ya Lema kuwa nje kwa dhamana au la.

Mawakili wa Lema  ambao ni Sheck Mfinanga na Peter Kibatala jana walisema tayari wamesajili rufaa yao Mahakama Kuu na wanasubiri siku hiyo ili isikilizwe.

Mfinanga alisema wameamua kufungua maombi ya rufaa kwa ajili ya kujua ni kwa nini Lema amekosa dhamana ambayo awali Hakimu Desdery Kamugisha alisema ipo wazi.



Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi


Bonyeza Hapa CLICK HERE

 

#YALIYOJIRI>>>>Majaliwa awavaa waajiri wanaonyanyasa wafanyakazi, atoa kauli kuhusu viongozi wanaowaweka rumande watumishi.Fahamu zaidi hapa.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema Serikali haitawavumilia waajiri ambao hawatoi mikataba ya ajira kwa wafanyakazi wao na amewaonya waache tabia hiyo mara moja.

Ametoa agizo hilo jana (Jumatano, Novemba 23, 2016) wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Sita wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA) katika ukumbi wa Mwalimu Julius K. Nyerere ulioko Chuo cha Mipango, nje kidogo ya mji wa Dodoma.

Akijibu hoja ya waajiri kutokutoa mikataba ya ajira kwa wafanyakazi ambayo iliibuliwa kwenye risala yao, Waziri Mkuu alisema kifungu cha 14 cha Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini Na. 6 ya mwaka 2004  kinaelekeza aina mbalimbali za mikataba inayotakiwa kutumika kuajiri wafanyakazi. 
“Kisheria mwajiri anao wajibu wa kuhakikisha kila mtumishi wake ana mkataba wa kazi kwa maandishi,” alisisitiza.

Akijibu hoja kuhusu wafanyakazi kuwekwa ndani kiholela, kunyanyaswa, kushushwa vyeo na kusimamishwa kazi na wanasiasa, Waziri Mkuu alisema Serikali chini ya uongozi wa Dkt. John Pombe Magufuli itaendelea kuzingatia utawala wa sheria na kanuni za utawala bora ili kuhakikisha kuwa haki za wafanyakazi zinalindwa ipasavyo.

”Kimsingi watumishi wanasimamiwa na mamlaka za kinidhamu na sheria mbalimbali ambazo hazina budi kuangaliwa kwa pamoja kabla ya kuchukua hatua. Ninawaagiza viongozi wenzagu wa kisiasa na walioko katika wizara na taasisi zote za Serikali, mikoani, wilayani, kwenye idara za Serikali na Halmashauri wazingatie utawala wa sheria wakati wa kushughulikia masuala mbalimbali yanayohusu wajibu na haki za wafanyakazi,” alisema huku akishangiliwa.

Akijibu hoja kuhusu suala la watumishi kutopandishwa vyeo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala Bora), Bibi Angella Kairuki alisema kwa kipindi cha miaka mitano jumla ya watumishi 343,689 walipandishwa vyeo ikiwa ni kuanzia mwaka 2011 hadi 2016. Hata hivyo, alisema wanakabiliwa na changamoto ya watumishi wengine kutokidhi vigezo.

“Kuna baadhi ya watumishi hawakidhi vigezo vya maendeleo na masharti vya muundo wa masharti ya utumishi wa umma. Tumetoa maelekezo kuwa wale waliokosa vigezo na wamekaa muda mrefu bila kupandishwa vyeo, wapewe mafunzo na bajeti zitengwe ili waweze kutimiza vigezo vya muundo wa utumishi wa umma,” alisema.
Sauti ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akizungumza





Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi


Bonyeza Hapa CLICK HERE

 

#YALIYOJIRI>>>> RC Makonda apiga marufuku wauza mbogamboga na samaki.Fahamu zaidi hapa.

Mkuu  wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, amepiga marufuku wauzaji holela wa samaki na mboga mitaani badala yake wapeleke katika masoko maalumu.
 
Aidha ameliagiza jeshi la polisi na halmashauri zote mkoani humu kuwakamata wafanyabiashara watakaokiuka agizo hilo.
 
Makonda alitoa kauli hiyo jana, wakati alipotembelea Soko la Kimataifa la Samaki la Feri na kuzungumza na wafanyabiashara wa soko hilo, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya siku mbili katika Wilaya ya Ilala.
 
Wafanyabiashara hao walieleza kuwa, moja ya changamoto zinazowakabili ni pamoja na kuzagaa kwa wafanyabiashara huria wa samaki hususani katika vituo vya mabasi ya daladala na pembezoni mwa barabara mkoani humo.
 
Walidai kuwa, hali hiyo inahatarisha uhai wa soko hilo kwani watu wengi hawafiki kununua samaki katika soko hilo, badala yake huishia kununua katika vituo vya mabasi na mitaani.
 
Mfanyabiashara Said Ally alimueleza mkuu huyo wa mkoa kuwa, masoko huria ya mitaani yanaendelea kushamiri huku viongozi wa halmashauri na wananchi wakikaa kimya.
 
“Mkuu wa mkoa tusaidie sasa hivi kila kona kuna wauza samaki hasa katika vituo vya mabasi jambo linalosababisha feri tunakosa wateja wanaishia mtaani, soko litakufa kwa sababu watu hawaji tena tofauti na awali,” alisema Ngasa.
 
Mbali na hayo wafanyabiashara hao waliomba kuboreshwa kwa miundombinu ya soko hilo ambayo imechakaa licha ya soko kuwa la kimtaifa.
 
Kutokana na malalamiko hayo, Makonda alipiga marufuku biashara ya samaki na mboga mitaani na kumuagiza Kamanda wa Operesheni, Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lucas Mkondya kuwashughulikia wafanyabiashara wote watakao kiuka agizo hilo kuanzia sasa.
 
“Ni marufuku kufanya biashara ya samaki na mboga katika maeneo ambayo sio rasmi wafanyabiashara wapeleke katika maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya kufanyia biashara hizo,” alisema Makonda.




Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi


Bonyeza Hapa CLICK HERE

 

#YALIYOJIRI>>>>Mikoa inayoongoza kwa maambukizi ya virusi vya ukimwi nchini Tanzania.Fahamu zaidi hapa.

Mikoa ya Tabora, Katavi na Rukwa imetajwa kuwa ni miongoni  mwa mikoa  10 inayoongoza kwa maambukizi  ya virusi vya ukimwi.

Hiyo ni  kwa mujibu wa takwimu za mwaka 2011/2012 za Taasisi ya Mkapa.

Taarifa hiyo  ilitolewa na Meneja Mradi wa TB na Ukimwi kutoka Taasisi ya Mkapa, Dkt. Happenes  Wilbroad     katika mafunzo ya siku moja  ya viongozi wa dini  yaliyofanyika   Nzega.

Alisema  mkoa unaoongoza kwa maambukizi ya VVU kati ya mikoa hiyo mitatu ni  Rukwa wenyeasilimia  6.2 ukifuatiwa na Katavi asilimia  5.2 na Tabora asilimia 5.1.

Dk. Wilbroad alisema Taasisi ya Mkapa  imeanza kuendesha  mafunzo ya kuhakikisha wananchi wanatambua na kuepuka maambukizi mapya.

Alisema    jitiahada mbalimbali za kudhibiti maambukizi  hayo zinapaswa kufanyika  kunusuru maisha ya  wakazi wa maeneo hayo.

Alitaja sababu zinazochangia   maambukizi kuwa ni pamoja na ndoa za utotoni, tohara za jadi na baadhi ya wananchi kutozingatia elimu ya Ukimwi   na kukithiri  imani potofu za ushirikina.




Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi


Bonyeza Hapa CLICK HERE

 

Wednesday 23 November 2016

#MICHEZO>>>>SAFARI YA NDEMLA ULAYA YAANZA KUNUKIA, HII NI KAULI YA MENEJA WAKE.FAHAMU ZAIDI HAPA.

Kiungo kinda wa Simba, Said Ndemla, wakati wowote kuanzia sasa anaweza kuachana na timu hiyo na kwenda Ulaya kutafuta nafasi ya kucheza soka la kulipwa.

Meneja wa kiungo hiyo, Jamal Kisongo, amesema hivi sasa yupo katika harakati za mazungumzo na baadhi ya timu kutoka mataifa mbalimbali ya Ulaya ambayo yameonyesha nia ya kutaka kumchukua mchezaji huo.

Alisema endapo mipango hiyo itakaa sawa, muda wowote ataondoka nchini na kwenda huko kujaribu bahati yake ya kucheza soka la kulipwa kama ilivyo kwa mshambuliaji Mbwana Samatta anayekipiga katika timu ya KRC Genk ya Ubelgiji.

“Said Ndemla muda wowote kuanzia sasa anaweza kuondoka zake nchini na kwenda Ulaya kwa ajili ya kujaribu bahati yake ya kucheza soka la kulipwa kama alivyo Samatta.

“Hivi sasa nipo katika mazungumzo na baadhi ya timu ambazo zimeonyesha nia ya kumtaka na endapo mambo yatakaa sawa basi ataondoka nchini kwa sababu tayari ameshakomaa kiakili na kifikra, hivyo anaweza kupambana,” alisema Kisongo.

Alipoulizwa kama uongozi wa Simba unaujua mpango huo, alisema: “Simba wanaujua, hivyo mambo yakikaa sawa ataondoka, wala hawana shida."

SOURCE: CHAMPIONI



Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi


Bonyeza Hapa CLICK HERE

 

Download wimbo mpya wa Stamina Ft. Mr BLUE unaoitwa "Nitampigia".

Download wimbo wa Stamina Ft. Mr BLUE  unaoitwa "Nitampigia".




Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi


Bonyeza Hapa CLICK HERE

 

Download wimbo mpya wa Rich Mavoko Ft Diamond Platnumz unaoitwa "Kokoroko".

Download wimbo wa Rich Mavoko Ft Diamond Platnumz unaoitwa "Kokoroko".



Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi


Bonyeza Hapa CLICK HERE

 

#MICHEZO>>>>Arsenal yakubali sale ya kufungana Arsenal 2 - 2 Paris Saint Germain kwenye uwanja wake wa nyumbani Emirates Stadium.Fahamu zaidi hapa.




Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi


Bonyeza Hapa CLICK HERE

 

#YALIYOJIRI>>>GHARAMA ZA KUMLINDA RAIS MTEULE WA MAREKANI DONALD TRUMP.FAHAMU HAPA.

Tarehe 9, Novemba 2016 siku moja baada ya kufanyika uchaguzi mkuu wa Marekani, aliyekuwa mgombea wa Chama cha Republican Donald John Trump alitangazwa kuwa mshindi baada ya kumgaragaza mpinzani wake wa karibu na mgombea wa Chama cha Democratic, Hillary Clinton.
 
Baada ya kutangazwa kuwa Rais Mteule wa Marekani, vyombo vya ulinzi na usalama vya nchi hiyo vinawajibu wa kuhakikisha yeye (Donald Trump) na familia yake wanakuwa salama wakati wote.
 
Kwa mijibu wa taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Meya wa New York, Marekani gharama za kumlinda Trump na familia yake kwa siku moja ni zaidi ya dola milioni 1 (TZS bilioni 2.2).
 
Mke wa Donald Trump, Melania Trump pamoja na mtoto wao wa miaka 10, wao muda mwingi huwa nyumbani sababu ya shule kufungwa hivyo hutakiwa kulindwa muda wote huku Trump akiendelea na shughuli nyingine za serikali.
 
Mbali na hao bado kuna watoto wengine wa Trump na wajukuu zake ambapo wote hao wanatakiwa kulindwa na maafisa wa usalama wa Marekani.
 
Afisa wa Polisi katika Jimbo la New York aliwaeleza waandishi wa habari siku ya Ijumaa kuwa ulinzi wa Rais Mteule na familia yake ni suala namba moja wanalotakiwa kulishughulikia.
 
 Kazi kubwa polisi wanayotakiwa kufanya ni kutoa usaidizi kwa Maafisa Usalama wa Taifa ambao hasa ndio wana jukumu la kumlinda Rais Mteule


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi


Bonyeza Hapa CLICK HERE

 

Angalia Video mpya ya Rich Mavoko Ft Diamond Platnumz inayoitwa "Kokoroko".

New Video Rich Mavoko Ft Diamond Platnumz-Kokoroko.



Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi


Bonyeza Hapa CLICK HERE

 

#YALIYOJIRI>>>>RUNGU LA RC MAKONDA LAMVAA MWENYEKITI WA SERIKALI ZA MITAA KWA TUHUMA ZA KUHUJUMU MAPATO.FAHAMU ZAIDI HAPA.

MWENYEKITI WA MTAA WA GONGO LA MBOTO AKITIWA MBARONI NA JESHI LA [OLISI MARA BAADA YA AMRI YA RC MAKONDA 

Na Sosy

Mwenyekiti  wa Serikali ya Mtaa wa Gombo la Mboto Bakari Shingo atiwa mbaroni na jeshi la Polisi kwa amri ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda mara baada ya  kuhusishwa na tuhuma za kukusanya mapato kwa kutumia risiti anazozichapisha mwenyewe kinyume na Halmashauri inavyoagiza, kutoitisha mikutano ya hadhara kwa muda mrefu na kushirikina na wahalifu.

tuhuma  hizo zimempelekea Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda ambaye yupo kwenye ziara yake katika wilaya ya Ilala Pugu Kajiungeni, kumuagiza Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Ilala Salum Hamduni kumsweka rumande Mweyekiti huyo mpaka upelelezi utakapo kamilika.

Akitoa ushahidi kuhusu sakata hilo Mkazi wa Gongo la Mboto na Mjumbe wa Serikali ya Mtaa Pili Seif ameeleza kuwa hiyo imekuwa ni tabia ya mwenyekiti huyo kwa muda mrefu na taarifa zimefikishwa kwenye mamlaka husika ikiwemo kwa Mkuu wa Wilaya Sophia Mjema, Mkurugenzi Msongela Nitu na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa.



Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi


Bonyeza Hapa CLICK HERE

 

#BURUDANI>>>>Aunt Ezekiel: Achana na Mimi Wewe Wema Sepetu.Fahamu zaidi hapa.

MASTAA wawili waliokuwa mashosti siku za nyuma, Aunty Ezekiel na Wema Sepetu ‘Madam’ wameingia kwenye msuguano tena hivi karibuni huku hali ikionesha kuwa mastaa hao kwa sasa ndiyo basi tena.

Hali hiyo imetokea juzi baada ya Aunty kuweka picha ya kumtakia siku njema ya kuzaliwa rafiki na msanii mwenzake, Maimartha Jesse kwa kuandika, “Happy bday Kipenzi cha Roho yangu …..Unajua kama Nakupenda cha zaidi Naomba Yesu Akutunze milele.”

Katika post hiyo, followers kadhaa wa Aunty walikomenti akiwemo staa mwenzake kwenye tasnia hiyo, Wema Sepetu aliyekomenti “Yesu atamtunza…” Baada ya hapo, Aunty akaibuka na kumtolea povu Wema akimchana “Achana na mm ww @wemasepetu“ hali iliyoibua maswali na mijadala mingi mitandaoni, huku watu wakitaka kujua kwa nini Aunty amemshushua hivyo Wema.
Inasemekana kwamba, chanzo ni Miss Tanzania huyo wa mwaka 2006, Wema kumsema vibaya Aunty kwenye mitandao ya kijamii hasa Instagram. Kwa hali ilivyofikia mpaka sasa inaonesha sio rahisi tena kwa waigizaji hao kuelewana.

Tangu siku za hivi karibuni, Wema alipokosana na rafiki yake Muna Love na kumsema vibaya kwa kutumia video aliyojirekodi na kuisambaza mitandaoni, Wema kwa sasa amekuwa akijitahidi kuwa karibu na Aunty ili warudishe urafiki wao wa zamani japokuwa jitihada zake zinaonesha kugonga mwamba baada kuambulia maneno mazito kutoka kwa Mama Cookie.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi


Bonyeza Hapa CLICK HERE

 

#YALIYOJIRI>>>>YAMETIMIA...Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) Limetangaza Kupunguza Idadi ya Wafanyakazi Wake.Fahamu zaidi hapa.

Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) limetangaza kupunguza idadi ya wafanyakazi wake ikiwa ni njia ya shirika hilo kuweza kujiendesha kwa faida na kufikia malengo yake.

Mkurugenzi Mkuu wa shirikia hilo, Mhandisi Ladislaus Matindi alisema kuwa mchakato wa kupunguza asilimia 90 ya wafanyakazi wa shirika umekamilika na utaratibu wa kuanza kulisuka upya shirika utaanza hivi karibuni.

Mkurugenzi huyo alisema asilimia 10 ya wafanyakazi watakaobaki ndio waliokidhi vigezo vinne walivyovitoa ambavyo ni uaminifu, elimu, uzoefu na kujali wateja.

Kwa upande mwingine alisema kuwa wafanyakazi wengine wameenguliwa kwa sababu hawawezi kwendana na kasi inayotakiwa kwa sasa na shirika hilo.

Kwa sasa shirika hilo lina wafanyakazi 221 ambao wanaelezwa kuwa ni wengi kuliko mahitaji halisi. Katika mpango huu wa kupunguza wafanyakazi, wanatarajia kupunguza takribani wafanyakazi 200.

Kuna taarifa ambazo bado hazijathibitishwa na shirika hilo kuwa tayari limewasimamisha kazi takribani wafanyakazi wote katika kituo cha nchini Comoro na kile cha jijini Mwanza.




Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi


Bonyeza Hapa CLICK HERE

 

#YALIYOJIRI>>>Mwathirika wa UKIMWI Aliyewanajisi Watoto 100 Ahukumiwa Kifungo cha Miaka Miwil.Fahamu zaidi hapa.

Siku chache baada ya kuripotiwa taarifa za kukamatwa kwa mwanaume mmoja kutoka Malawi ambaye inadaiwa alikuwa akiwanajisi watoto wadogo wanaotajwa kufika 100 kwa maelezo kwamba anawasafisha na kufanya tambiko la kimila, Hatimaye amehukumiwa kwenda jela miaka miwili.

Hukumu hiyo imeonesha kutotenda haki kwa watoto hao kutokana na uchache wa miaka aliyofungwa mwanaume huyo. Tayari mashirika ya kutetea haki za binadamu na asasi za kupambana na maambukizi ya virusi vya HIV nchini Malawi zimekosoa hukumu hiyo

Michael Chipeta, wakili na mwanaharakati wa kutetea haki za binadamu nchini humo amekosoa hukumu hiyo na kusema kuwa kulikuwa na mapungufu mengi katika mchakato mzima wa kesi na hukumu dhidi ya mwathirika huyo wa virusi vya HIV, anayejulikana kama Eric Aniva mwenye umri wa miaka 45.

Eric Aniva alikiri kwamba amefanya ngono na wasichana wadogo kwa kulipwa fedha ambazo ni dola nne mpaka saba za Marekani kwa kuondoa usichana wa (kubikiri) kila mtoto mmoja, kwa imani kuwa ubikira ni mkosi na kwamba kitendo hicho kinawasafisha watoto hao pamoja na jamii hiyo.

Malawi ni katika nchi zenye maambukizi makubwa ya virusi vya Ukimwi duniani.





Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi


Bonyeza Hapa CLICK HERE

 

#MICHEZO>>>>Mbwana Samatta Atemwa Tano Bora ya Mchezaji Bora Afrika.Fahamu zaidi hapa.

Shirikisho la soka barani Africa (Caf) limetoa orodha ya majina ya wachezaji wanaowania tuzo ya mchezaji bora wa Afrika mwaka 2016, jina la mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania Mbwana Samatta halipo katika orodha ya wachezaji hao waliofanikiwa kuingia tano bora.


Samatta alikuwepo kwenye orodha ya awali safari hii alikuwa akiwania tuzo ya mchezaji bora Afrika kwa ujumla baada ya msimu uliopita kushinda tuzo ya mchezaji bora Afrika kwa wachezaji wa ndani wakati akiitumikia klabu ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.


Nahodha huyo wa Stars anaecheza klabu ya KRC Genk ya Ubelgiji amewaacha wachezaji wanaocheza kwenye vilabu vya Bundesliga, Premier League, na Serie A.


Orodha ya wachezaji watano wanaowania tuzo ya mchezaji bora Afrika


Pierre-Emerick Aubameyang of Gabon and Borrusia Dortmund

Riyad Mahrez of Algeria and Leicester

Sadio Mane of Senegal and Liverpool

Mohamed Salah of Egypt and Roma

Islam Slimani of Algeria and Leicester

Wachezaji wanaowania tuzo ya mchezaji bora Afrika kwa wachezaji wanaocheza ligi za ndani.


Khama Billiat of Mamelodi Sundowns and Zimbabwe

Keegan Dolly of Mamelodi Sundowns and South Africa

Rainford Kalaba of TP Mazembe and Zambia

Hlompho Kekana of Mamelodi Sundowns and South Africa

Denis Onyango of Mamelodi Sundowns and Uganda




Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi


Bonyeza Hapa CLICK HERE

 

#YALIYOJIRI>>>>Mamlaka ya Hali ya Hewa Nchini (TMA) Yataadharisha Kuhusu Uwezekano wa Kuja Kwa Mvua Kubwa.Fahamu zaidi hapa.

Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini (TMA) yataadharisha kuhusu uwezekano wa kuja kwa mvua kubwa yenye upepo, yawataka wananchi wachukue tahadhari.

Yasema mabadiliko ya hali ya hewa kwa sasa yanatokana na kuwepo kwa msimu unaotawaliwa na uwepo wa LANINA ambayo ni ongezeko la hali ya baridi katika eneo la Ikweta ya Bahari ya Pasifiki.

Bado matarajio ya vipindi vifupi vya mvua kubwa na upepo vitaendelea kuwepo katika msimu huu mpaka mwezi Disemba na mabadiliko kidogo yatajitokeza kwa baadhi ya mikoa ambapo mvua zitanyesha kwa wastani.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi


Bonyeza Hapa CLICK HERE

 

#YALIYOJIRI>>>Chadema Kukusanya Bilioni 13.9 Kwa Mwaka Kupitia Kadi Mpya za Wanachama Zitakazoanza Kutolewa Mwakani.Fahamu zaidi hapa.

Chadema imetangaza kuwa Januari itaanza kutumia kadi mpya za uanachama za kielektroniki, zitakazoiwezesha kukusanya Sh13.9 bilioni kwa mwaka na kupunguza utegemezi wa ruzuku ya Serikali.

Mkakati huo ulitangazwa jana na Mwenyekiti wa chama hicho Freeman Mbowe wakati wa mkutano wa ndani uliofanyika mkoani Morogoro. Tofauti na Mbowe, viongozi wengine wa chama hicho walioko mikaoni ni Edward Lowassa aliyeko Dodoma na Frederick Sumaye ambaye yupo Singida.

Mbowe alisema mfumo huo utasaidia pia kudhibiti baadhi ya viongozi wasio waaminifu, wanaotumia mwanya wa kuuza kadi na kushindwa kuwasilisha fedha kwenye hazina ya chama.

Alisema kwa mfumo huo mpya, kama Chadema itakuwa na wastani wa wanachama 100,000 katika wilaya moja na kila mmoja kulipa ada ya Sh1,000 kwa mwaka, maana yake itaingiza Sh100 milioni.

Kwa hoja hiyo ya Mbowe, ikiwa chama hicho kitakuwa na wastani wa wanachama 100,000 katika kila wilaya za Tanzania Bara ambazo ni 139, Chadema itakuwa na uwezo wa kukusanya Sh13.9  bilioni kila mwaka.

Vyama vya siasa vinapata ruzuku kwa mujibu wa sheria na ripoti ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ilibainisha kuwa jumla ya Sh67.7 bilioni zililipwa na Serikali kwa vyama vya siasa katika mwaka kipindi cha miaka minne, kuanzia mwaka wa fedha 2009/2010 mpaka 2012/2013. Fedha ambazo kwa mujibu wa CAG zilikuwa hazijakaguliwa kisheria.

Ikilinganishwa na mkakati mpya wa Chadema, fedha hizo ni ndogo katika kuhudumia shughuli za chama nchi nzima.

Mbowe alisema Chadema imeamua kuhakiki wanachama wake ili ifikapo Januari iwe tayari imemaliza kazi hiyo na kuingia rasmi katika mfumo mpya, utakaokisaidia kuondokana na dhana ya utegemezi wa ruzuku kutoka serikalini.

Alisema ili chama kipige hatua na kuondokana na utegemezi wa ruzuku serikalini, wamekusudia kuingia katika mfumo wa kupata mapato kutoka ndani ya wanachama kupitia ulipaji wa ada.

Mbowe alizungumza na wanachama hao kutoka ngazi za vitongoji, vijiji, kata na wilaya waliohudhuria mkutano mkuu maalumu wenye lengo la kuwakumbusha mambo mbalimbali ya kuimarisha chama hicho baada ya Serikali ya Rais Magufuli kuzuia mikutano ya hadhara.

“Katika kipindi cha miaka miwili ijayo, Chadema itakuwa tayari imefanya utambuzi wa wanachama wake kwa kuwatambua katika kila mtaa, kitongoji, kijiji, kata na jimbo kupitia mfumo mpya wa kadi za eleketroniki ifikapo Januari 2017,” alisema Mbowe.

Alisema katika baadhi ya maeneo ya mikoa hapa nchini, kadi za uanachama za Chadema ni lulu na zimekuwa zikiuzwa hadi Sh5,000 badala ya 500.

Alieleza kuwa mapato ya chama lazima yatokane na ada za wanachama na siyo ruzuku ya Serikali, kwa kuwa utegemezi wa ruzuku ni hatari kwa uhai wake.

“Hii ruzuku inayotolewa na Serikali inatolewa kwa sababu ya CCM na CCM bila ruzuku hakiwezi kujiendesha,” alidai.

Mbowe alisema kila jimbo linapata fedha za ruzuku kulingana na idadi ya kura ilizopata katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25 mwaka jana, akitolea mfano Jimbo la Mlimba kuwa Mbunge Suzan Kiwanga alishinda kwa kura 40,000 wakati urais Chadema ilipata kura 38,000 huku katika udiwani wakipata kata tisa kati 16.

“Kutokana na ruzuku, Mlimba itapata Sh163,688 kila mwezi. Unaweza kuona fedha za ruzuku kutoka ndani ya chama ni ndogo sana ambapo Mkoa wa Morogoro unapokea kiasi cha Sh2.2 milioni kila mwezi.

“Kufikia mwaka 2017 kupitia programu ya Chadema msingi, tumekusudia kukijikita zaidi kusaka wanachama kutoka ngazi ya mitaa, vitongoji na balozi na tutaanza uchaguzi ndani ya chama.

“Tumebaini kuwa baadhi ya maeneo Chadema tumeshindwa kupata wenyeviti wa Serikali ya vitongoji na vijiji, kukosa madiwani na wabunge kutokana na kukosa misingi imara wa wanachama,” alisema Mbowe.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi


Bonyeza Hapa CLICK HERE

 

#BURUDANI>>>>KAULI ya Basata Kuhusu Video Mpya ya Wimbo wa Rich Mavoko na Diamond Platnumz.Fahamu zaidi hapa.

Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) ambalo husimamia wasanii pamoja na kazi zao ikiwa ni wasanii wa filamu pamoja na wale wa muziki limesema kuwa linapitia video mpya ya mwanamuziki Rich Movoko aliyomshirikisha Diamond Platnumz kuona kama kuna vitendo vya udhalilishaji  wa kijinsia.

BASATA kupitia ukurasa wao wa Twitter wameandika kuwa wapo thabiti kusimamia maadili katika sanaa na udhalilishaji wa wanawake. Aidha wameeleza kuwa video hiyo iliyotoka jana usiku inayokwenda kwa jina la Kokoro ipo katika uhakiki kujionea kama picha za wanawake waliomo kwenye video hiyo zinakiuka maadili ya kitanzania na muda si mrefu watatoa taarifa.

BASATA wamekuwa wakiwafungia wasanii wengi wanaokiuka maadili ya sanaa ambapo miongoni mwa wasanii wengi waliofungiwa ni pamoja na Nay wa Mitego, Snura huku wengine wakipewa onyo na video nyingine kuzuiwa kuchezwa mchana kwa mfano Zigo Remix ya AY Ft. Diamond Platnumz na Asanteni Kwa Kuja ya Mwana FA.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi


Bonyeza Hapa CLICK HERE

 

Monday 21 November 2016

DOWNLOAD WIMBO MPYA WA MWANA FA FT VANESSA MDEE UNAOITWA "DUME SURUALI".

DOWNLOAD WIMBO WA MWANA FA FT VANESSA MDEE - DUME SURUALI.



Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi


Bonyeza Hapa CLICK HERE