Monday 14 November 2016

#YALIYOJIRI>>>>Martin Kadinda Afunguka Asema Wema Sepetu Anaangushwa na Marafiki zake.Fahamu zaidi hapa.

Mbunifu wa mavazi kutoka Bongo, Martini Kadinda amesema hawezi kumchagulia Wema Sepetu marafiki wa kuwa nao karibu na hawezi kujiingiza kwa lolote katika ugomvi wao.

Akipiga story ndani ya eNewz, Kadinda amesema ugomvi ambao unatokana na marafiki zake Wema unamshusha Wema kwa kuwa Wema ni mtu maarufu na ana jina kubwa hivyo alichokifanya ni kumzuia Wema kuweka ugomvi wake katika mitandao ya kijamii.

Pia Martin ameendelea kuwasihi mashabiki zake kuendelea kumpenda Wema na kazi zake ambazo anazifanya na siyo vinginevyo na pia wasimuhukumu Wema kwa mambo yanayoandikwa mitandaoni kwa kuwa hawajui chanzo chake.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi

Bonyeza Hapa CLICK HERE
 

0 comments:

Post a Comment