Monday 14 November 2016

#MICHEZO>>>>KIUNGO MKABAJI AITWAYE CHAILA, AKUBALI KUTUA YANGA KUMFUATA LWANDAMINA.FAHAMU ZAIDI HAPA.

CHAILA (KULIA)...

Baada ya kocha George Lwandamina kumalizana na Yanga, mchezaji wa kwanza ambaye ataungana naye anaonekana kuwa ni Meshack Chaila kutoka Zesco ya Zambia.
Taarifa zinaeleza, Yanga tayari wamefanya mazungumzo ya awali na kukubaliana na Chaila raia wa Zambia ambaye hiyo karibuni ametoka kwenye fungate baada ya kufunga ndoa.
Imeelezwa kiungo huyo, kakubali kusaini mkataba wa miaka miwili ili aungane na Lwandamina.
Chaila ni kiungo mkabaji na mtu wa kazi, sehemu ya kiungo ambayo Yanga wamekuwa na tatizo nayo kwa kipindi sasa.
Lwandamina aliyekuwa kocha mkuu wa Zesco, akiwa bosi wa Chaila, tayari amemalizana na Yanga na hivi karibuni ataanza kazi.
 Chaila amethibitisha kufanya mazungumzo na Yanga: “Wamezungumza na meneja wangu, mambo yako katika hatua nzuri na ikiwezekana Novemba 15 nitajiunga nao. Hapa Zesco hawana shida kumuachia mchezaji.”

Chaila ambaye alizungumza na mtandao wa Soka25 East, ameonyesha yuko tayari kujiunga na Yanga na kufanya kazi na Lwandamina.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi

Bonyeza Hapa CLICK HERE
 

0 comments:

Post a Comment