Monday 21 November 2016

#BURUDANI>>>HATIMAYE TAMASHA LA FIESTA LAPATA MPINZANI….DIAMOND AANZISHA TAMASHA LAKE..KUMLETA STAR HUYU WA MAREKANI.FAHAMU ZAIDI HAPA.

 Katika kusherehekea Christmas mwaka huu, WCB wanatarajia kufanya show yao ya kwanza wakiwa pamoja, December 24 iliyopewa jina Wasafi Beach Party jijini Dar es Salaam.
Wasanii wote wa label hiyo wakiongozwa na Diamond watatumbuiza. Lakini huenda kukawa na ugeni mkubwa wa staa wa nje na tayari meneja wa Diamond, Sallam ametease jina.

Akiweka picha ya mrembo wa Marekani, Amber Rose, Sallam ameandika kwenye Instagram, “Wangapi watu wanataka huyu dada ashuke bongo siku akinukishe watu wale nae Bata???”
Naye Diamond alichombeza kwenye post yake: Eti Manager @sallam_sk anauliza wangapi wangependa huyu dada @amberrose siku ashuke Bongo watu wale nae Bata???”

Huenda label hiyo ikawa imepanga kumleta mrembo huyo kuwa host wa tamasha lenyewe.

Hiyo haitakuwa mara ya kwanza kwa ex huyo wa Wiz Khalifa kuja Afrika. Mwaka jana alienda Lagos, Nigeria kwa mwaliko wa D’Banj ambako hata hivyo alikaa jukwaani kwa dakika 7 tu.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi


Bonyeza Hapa CLICK HERE

 

0 comments:

Post a Comment