Saturday 19 November 2016

#YALIYOJIRI>>>>Alichokizungumza Ester Bulaya Baada ya Mahakama Kuu Kumpa Ushindi dhidi ya Wasira.Fahamu zaidi hapa.

November 19, 2016 Kesi ya kupinga matokeo ya Ubunge wa Ester Bulaya iliyofunguliwa na wapiga kura wa jimbo la Bunda dhidi ya aliyekua mgombea wa CCM Stephen Wasira ilitolewa hukumu yake ambapo Mahakamu Kuu ilimpa ushindi na kumthibitisha Ester Bulaya kuwa Mbunge halali.

Mshindi wa Ubunge wa jimbo hilo Ester Bulaya amezungumza kuelezea jinsi alivyoyapokea maamuzi ya Mahakama Kuu chini ya Jaji Noel Chocha juu ya kesi ya kupinga matokeo iliyofunguliwa na wapiga kura wanne wa mgombea Stephen Wasira.


“Kiukweli namshukuru sana Mungu, na wananchi wa jimbo la Bunda Mjini kwasababu walishaamua na mahakama imeamua lakini kwa uvumilivu wao na hivi ninavyozungumza kuna watu wametoka Musoma kwa miguu mpaka Bunda wakishangilia ushindi wa Mbunge wao” – Ester Bullaya


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi


Bonyeza Hapa CLICK HERE

 

0 comments:

Post a Comment