Friday 31 March 2017

Bombardier Zaingiza Faida ya Bilioni 9 kwa Miezi Minne Toka Zianze Kufanya Kazi Rasmi.Fahamu zaidi hapa.

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Ndege la ATCL, Lasislaus Matindi amesema wamefanikiwa kukusanya shilingi Bilioni 9 kwa miezi minne tu kwa kutumia ndege hmbili zilizonunuliwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli.
Kipindi ndege hizo zinanunuliwa baadhi ya watu walikosoa kuwa hazikuwa na tija kwa Taifa.
Kampuni ya Ndege ya Tanzania (ATCL) ilianzishwa mwezi Novemba 2002 baada ya Serikali kubinafsisha lililokuwa Shirika la Ndege la Tanzania (Air Tanzania Corporation, ATC). katika Shirika hilo, Shirika la Ndege la Afrika Kusini (SAA) lilinunua hisa asilimia 49 ndani ya ATC.
Hata hivyo ubia kati ya ATCL na SAA ulikabiliwa na matatizo ya kiuendeshaji na kulazimika kusitishwa mwezi Agosti 2006 na ATCL kurejeshwa tena serikalini kwa asilimia 100.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

Baada ya Harmorapa..Sasa Kuna Wemarapa..Adai Wema Anajipendekeza Kwake Ila Hana Mpango Nae.Fahamu zaidi hapa.

Kuna imani kuwa duniani wawiliwawili! Hii inajidhihirisha kwa mwanadada Lisa Deedee `Tuerny’ ambaye amejipatia umaarufu mitandaoni kutokana na kufananishwa na staa wa sinema za Kibongo, Wema Sepetu.
Kupitia gazeti hili, mrembo huyo anafunguka mambo mbalimbali usiyoyajua kuhusu yeye; Ijumaa: Hivi Tuerny ulijuaje kuwa unafanana na Wema?
Tuerny: Nakumbuka mwaka 2012 niliweka picha mtandaoni, mama akanitumia sms kwamba ninafanana na Wema, nilishtuka lakini tangu hapo akawa kama amebariki hicho kitu. Nilishangaa kila sehemu niliyokwenda watu wananiambia nafanana na Wema.
Ijumaa: Ulijisikiaje kufananishwa naye na ni changamoto zipi unazokutana nazo?
Tuerny: Sikuona kama ni kero, nilichukulia kawaida tu, haikuwa chanzo cha mimi kufanya vitu vya kufanana naye, mimi siyo mtu wa shobo kama hao wengine na sijawahi kuwa shabiki wake, changamoto ni kwamba wengi wanajua Wema ni ndugu yangu wakati si kweli.
Ijumaa: Je, umeshawahi kuwa na ukaribu na Wema?
Tuerny: Sijawahi na sifikirii, ila kipindi watu wanaanza kunifananisha naye alifurahi akawa ana-comment kwenye picha zangu Instagram, akawa ananisifia na mimi ninamjibu, lakini kutokana na maneno ya watu akachukia na kunipotezea.
Ijumaa: Kwa nini hupendi awe rafiki yako?
Tuerny: Yeye ana marafiki wengi na kwenye maisha yangu sipendi kuwa na mtu mwenye marafiki wengi, kwani majungu yatakuwa mengi.
Ijumaa: Nilisikia kuna kipindi uliwahi kukutana na Wema lakini ukampotezea hata salamu hukumpa, kwa nini?
Tuerny: Ni kweli, mwaka 2015 nikiwa kwenye mishe zangu nilimuona pale Klabu Cafee, akatabasamu na mimi pia, tatizo mimi sijui kujipendekeza ndiyo maana sikumfuata.
Ijumaa: Vigogo wangapi ambao wamewahi kukuomba penzi, kwa kutaka kuonja ladha ya copy ya Wema?
Tuerny: Inawezekana watu wanaumiza kichwa kwa sababu hiyo, lakini wanashindwa kunifuata kutokana muonekano wangu, mimi ni kauzu zaidi ya dagaa.
Ijumaa: Uliwahi kukumbwa na kashfa ya kutoka kimapenzi na Romy Jones, ilikuwaje?
Tuerny: Sijawahi kuwa naye, watu walizusha kwa sababu zao binafsi.
Ijumaa: Mfano Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ sukari ya warembo, akikutokea utakubali?
Tuerny: Hahaa siwezi, kuwa na mwanaume mpaka nimpende siyo tu kwa sababu yeye ni f’lani.
Ijumaa: Ni mwanaume wa aina gani anakidhi vigezo kuingia naye kwenye uhusiano?
Tuerny: (anacheka) awe mrefu, mwenye bodi na anajielewa, yaani asiwe mtu wa kuongea sana, maana sipendi mtu muongo.
Ijumaa: Kuna mastaa ambao wameshawahi kukuomba penzi na ulishawahi kutoka na wangapi?
Tuerny: Wapo wengi wanaoshoboka, huwa nawapotezea na siwezi kuwataja kwa sababu sipendi kujikweza.
Ijumaa: Je, una ndoto ya kuwa msanii wa filamu au muziki au video queen?
Tuerny: Mmh, kuwa video queen hapana labda mtu anilipe si chini ya milioni saba, kuhusu filamu labda niwe dairekta, ila ndoto yangu kubwa ni kuwa mwanamuziki, naamini itatimia ‘soon’.
Ijumaa: Unajishughulisha na nini, kinachoweza kukukwamua kimaisha?
Tuerny: Nina saluni yangu inaitwa T flawless ipo Magomeni-Mikumi ninapoishi, yaani make up studio, napamba maharusi na watu wa kawaida.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

Amini Usiamini..Makonda na Mchungaji Gwajima Kupatanishwa!..Fahamu zaidi hapa.

Kuna habari zilizoko chini ya viunga vya watawala zinasema watu wa ‘’kitengo’’ wameamua kulifanyia kazi suala la Mchungaji Gwajima, Clouds Media International na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kwa sababu halitoi afya njema kisiasa.
Kwa kifupi, ‘’kitengo’’ ni neno ambalo kwa kiingereza ni ‘’The ruling class/The Establishment’’. Hawa ni watu ambao moja ya kazi zao ni kutathmini kwa kina hali ya kisiasa, kiuchumi na kiulinzi nchini halafu baadaye hutoa mwelekeo kwa taasisi zinazohusika.
Kwa hiyo kuna uwezekano mkubwa hatutaweza kumsikia tena Mchungaji Gwajima akimzodoa Makonda katika mahubiri yake kanisani.
Ieleweke kuwa baada ya Uchaguzi Mkuu 2015 kumalizika, watu wa ‘’kitengo’’ walifanya tathmini na kubainisha watu ambayo wataweza kufanikisha mikakati ya kisiasa kwa CCM na kiuchumi kwa serikali katika mikoa ambayo inaonekana ni muhimu sana kisiasa na kiuchumi. Mikoa hiyo muhimu sana ilipelekewa viongozi ambao watafanikisha mikakati hiyo na mojawapo ni Mkoa wa Dar es Salaam.
Kwa wale wanadhani Makonda ataondolewa hivi karibuni katika Mkoa wa Dar es Salaam, nadhani wataendelea kusubiri sana mpaka pale watu wa ‘’kitengo’’ watakapo jiridhisha kuwa kazi waliyomtuma ameshindwa kuifanya au makosa anayofanya ni makubwa kiasi kwamba yanaondoa hata madhumuni makuu ya uwepo wake kama Mkuu wa Mkoa.
Nimalizie kwa kusema, Mkuu wa taasisi ya watu wenye ‘’suti nyeusi’’ ametoa onyo kali kwa vijana wake kwa yaliyotokea Clouds Media International na kwa Nape Nnauye kwa sababu kazi waliyopewa ni kumlinda Mkuu wa Mkoa na sio yeye Mkuu wa Mkoa awape kazi za kufanya nje ya misingi yao ya kazi. Ieleweke kuwa baada ya kufanyika uchunguzi wa kina kiulinzi ilibainika Makonda anatakiwa kuboreshewa ulinzi.
Msishangae sana kwa nini Nape Nnauye ameamua kuwa kimya kuhusiana na kadhia ya kutishiwa bastola. Ameelezwa ukweli wa hali halisi iliyopelekea kitendo hicho kutokea.
Mjumbe hauwawi! Naiwakilisha jinsi ilivyo!

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

SIMBA WAKO KAMILI KWA AJILI YA KAGERA, WASEMA WANACHOTAKA NI USHINDI.FAHAMU ZAIDI HAPA.

Kikosi cha Simba wako vizuri kwa ajili ya mechi ya Ligi Kuu Bara dhidi ya Kagera Sugar, keshokutwa.


Simba wako tayari kwa mechi hiyo na kesho watafanya mazoezi ya mwisho kwenye Uwanja wa Kaitaba mjini humo.


Kocha Msaidizi wa Simba, Jackson Mayanja amesema kikosi chao kipo tayari kwa ajili ya mechi.



“Mechi ni ngumu tena sana na Kagera ni timu nzuri, tunalitambua hilo. Lakini tumejiandaa na tupo tayari. Sasa ni maandalizi ya mwisho na wachezaji, makocha na wengine tunataka kushinda,” alisema.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

MAJERAHA YA NGOMA, SASA NI HOFU KWA YANGA MAANA HAKUNA UHAKIKA KESHO.FAHAMU ZAIDI HAPA.

Yanga wamekuwa na hofu kubwa kutokana na suala la majeruha kuwaandama.


Mshambuliaji Donald Ngoma bado anaonekana hana nafasi ya kuisaidia Yanga katika mechi dhidi ya Azam FC, kesho.

Ngoma anaonekana hajapona vizuri hali inayosababisha hofu kubwa kwa Yanga ambayo italazimika kuwategemea Obrey Chirwa na Simon Msuva.

Mshambuliaji mwingine, Amissi Tambwe naye ni majeruhi, hivyo kumfanya Kocha George Lwandamina kuwa na wakati mgumu.

Katika mazoezi ya leo, Ngoma alionekana hakuwa vizuri hali inayoashiria kama hakufanya kitu leo, basi kesho ana nafasi ya asilimia chache kucheza.

Kama Yanga itapoteza mechi ya kesho dhidi ya Azam FC itakuwa imejiweka katika wakati mgumu sana.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

Tanzania na Ethiopia zasaini mikataba 3.Fahamu zaidi hapa.

IKULU, DAR: Tanzania na Ethiopia zasaini mikataba 3. Rais Magufuli na Waziri Mkuu wa taifa hilo wakubaliana kushirikiana katika Ulinzi, Riadha, Mafunzo ya Kiswahili na Bandari.

Kiongozi huyo wa Ethipia ameahidi na kufungua Ubalozi wa Ethiopia hapa Tanzania.
Aidha rais Magufuli ameahidi kutoa eneo la bure kwaajili ya kujengwa kwa ofisi za ubalozi huo.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

Skendo Zampa Stress Davido, Alazwa Hospitali.Fahamu zaidi hapa.

MKURUGENZI wa Lebo ya HKN, David Adeleke ‘Davido’ amekimbizwa hospitali na kulazwa huku chanzo kikidaiwa kuwa ni ‘stress’. Tukio hilo limejiri juzikati ambapo inaelezwa kuwa, Davido amekuwa akisumbuliwa na skendo inayozidi kuenea kwa kasi kuhusiana na kuzaa na mwanamke anayefahamika kama Ayomide Labinjo.

Haikuelezwa hasa hospitali ipi amelazwa lakini kupitia Mtandao wa Snaptchat, Davido liweka kipande cha video akiwa ametundukiwa dripu na kuwaambia mashabiki wake wamuombee.

Hivi karibuni, Ayomide alizungumza na Jarida la Punch na kuanika kila kitu kuwa, amezaa na Davido baada ya kulazimishwa wasitumie kinga.

“Kama Davido unanisikiliza ulijue hili kuwa uligoma kutumia kinga,” Ayomide aliliambia Punch. Tayari, Ayomide kwa kushirikiana na mama yake wameshafungua mashtaka yakumtaka Davido ashiriki katika malezi ya mtoto huyo.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

Mahakama Kenya Imeizuia Serikali Kuajiri Madaktari Kutoka Tanzania.Fahamu zaidi hapa.

KENYA: Mahakama imeizuia Serikali kuajiri Madaktari kutoka Tanzania kwa sababu ndani ya nchi hiyo kuna Madaktari 1,400 wasioajiriwa.

Mpaka sasa takribani watanzania 400 wenye taaluma ya Utabibu wameomba kazi hiyo.

Rais Magufuli alikubali ombi la kupeleka Madaktari 500 ili kupunguza uhaba wa Madaktari nchini Kenya kutokana na mgomo unaoendelea nchini humo.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

Hali Mbaya CCM Yawaliza Makatibu Wakuu.Fahamu zaidi hapa.

Viongozi wa CCM mkoa wa Morogoro wamewataka makatibu wa matawi na mashina wa chama hicho kuachana na mpango wa kususia uchaguzi wa viongozi wa ngazi hiyo kwa madai ya kutokulipwa posho za kusimamia Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.
Akizungumza kwa niaba ya wenzake jana, Katibu wa Tawi la Luleni, Kata ya Tomondo, Salumu Waziri alisema kutokana na kudai posho hizo kwa muda mrefu ameamua kususia uchaguzi huo na tayari amekabidhi fomu za wagombea kwenye ofisi ya kata.
Waziri alisema chama hicho kilitoa fedha za posho na kumkabidhi kiongozi mmoja wa wilaya ambaye hakuwalipa.
Katibu wa CCM Mkoa wa Morogoro, Kulwa Milonge alisema chama hicho kilishatoa fedha za kuwalipa viongozi wa matawi na mashina kupitia kwa katibu wa wilaya hiyo.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

TANZIA Mbunge Viti Maalum CHADEMA afariki dunia.Fahamu zaidi hapa.

Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Viti Maalum (CHADEMA) akiwakilisha walemavu Dkt. Elly Macha amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Dkt Elly Macha (Enzi za uhai wake)

Msemaji wa CHADEMA Tumaini Makene amethibitisha kutokea kwa kifo hicho, ambapo amesema mbunge huyo alikuwa akipatiwa matibabu mkoani Arusha.

"Taarifa ni za kweli, mbunge Viti Maalum Dkt. Elly Macha amefariki, lakini sijapata bado taarifa za kina, lakini ninachojua ni kwamba amekuwa akipatiwa matibabu kwa muda mrefu Arusha" Amesema Makene


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

Kudadeki..Hivi Ndivyo Tundu Lissu Alivyopambana Kisheria Mahakamani Hadi Mbunge wa Chadema Lijualikali Akaachiwa Huru.Fahamu zaidi hapa.

MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam jana ilitengua hukumu ya kifungo cha miezi sita jela iliyotolewa na Mahakama ya Wilaya ya Kilombero Januari 11 dhidi ya Mbunge wa jimbo hilo, Peter Lijualikali.
Jaji Ama-Isaria Munisi alitengua hukumu hiyo dhidi ya Lijualikali wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) baada ya kukubaliana na warufani kwamba hati ya mashtaka iliyomtia hatiani ilikuwa na upungufu.
Lijualikali na dereva wake ambaye alihukumiwa kifungo cha nje waliwakilishwa mahakamani hapo na mawakili Tundu Lissu ambaye ni Rais wa Chama cha Wanasheria (TLS), Fred Kiwelo na Enock Edwin.
Upande wa wajibu rufani - Jamhuri - uliwakilishwa na Wakili wa Serikali, Faraja Nchimbi.
Adhabu ya dereva wa Lijualikali aliyehukumiwa kifungo cha nje, Stephani Mgatta pia imetenguliwa.
“Mahakama hii imeona maelezo ya hati ya mashtaka na vifungu vilivyotumika vina mapungufu na kwamba washtakiwa walishtakiwa pasipo kuwepo na hati ya mashtaka dhidi yao… mahakama hii inawaachia huru washtakiwa na inatengua adhabu ya kifungo” alisema Jaji Munisi.
Akifafanua zaidi alisema ushahidi uliotolewa na upande wa jamhuri katika mahakama ya chini ulikuwa haujitoshelezi kuweza kuwatia hatiani washitakiwa hao.
Alisema kutokana na mapungufu hayo makubwa mahakama hiyo inatengua adhabu za vifungo walizopewa washitakiwa hao na kuwaachia huru.
Baada ya kutolewa hukumu hiyo, Mkurugenzi wa Mashitaka nchini (DPP), Biswalo Mganga, alisema anasubiri kupitia hukumu hiyo ili aamue kama anakata rufani au la.
Mahakama ya Wilaya ya Kilombero ilimuhukumu Lijualikali (30) kwenda jela miezi sita licha ya kosa lake kuwa na adhabu ya faini, baada ya upande wa mashtaka kudai kuwa ni mkosaji mzoefu.
Alidaiwa kufanya fujo na kusababisha taharuki katika maeneo ya ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.
Mwendesha mashtaka, Inspekta wa Polisi, Dotto Ngimbwa aliiambia Mahakama hiyo kuwa Lijualikali aliyekuwa mshtakiwa namba moja na Mgata (35) walitenda kosa hilo Machi mosi, 2016 kwenye kikao cha Baraza la Madiwani katika eneo la Kibaoni; ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.
Hakimu Mkazi, Timothy Lyon aliwatia hatiani washtakiwa hao baada ya kuridhika kuwa ushahidi wa upande wa mashtaka haukuacha shaka.
Hakimu huyo alisema mshtakiwa wa kwanza Mbunge ambaye alikuwa na kesi tatu huko nyuma, atatumika kifungo cha miezi sita jela.
GEREZA LA UKONGA
Mgata alihukumiwa kifungo cha nje cha miezi sita baada ya hakimu kuona hilo lilikuwa kosa lake la kwanza.
Baada ya kuhukumiwa kifungo hicho, Lijualikali alipelekwa katika Gereza la Ukonga jijini Dar es Salaam, kwa mujibu wa Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Lissu, alipozungumza na Nipashe kwa simu miezi miwili iliyopita.
Lissu aliiambia Nipashe siku hiyo kuwa alimtembelea mbunge huyo kwenye Gereza la Ukonga.
"Baada ya kuhukumiwa, walimpeleka Gereza la Ukonga," Lissu alisema. "Jumapili nilikwenda kumtembelea na kumweleza kuhusu mipango ya chama kumuombea dhamana na kukatia rufani hukumu iliyotolewa dhidi yake.
"Aliniambia hatayumba, ataendelea kupambana kutetea haki za wananchi wa jimbo lake na Watanzania kwa ujumla."


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

Kimenuka South Africa..Rais Jacob Zuma Afikiria Kujiuzulu.Fahamu zaidi hapa.

Kutokana na migogoro inayoendelea South Africa ndani ya chama tawala cha African National Congress (ANC), Rais Jacob Zuma anajifikiria kujiuzulu nafasi hiyo mwakani japokuwa muda wake haujaishia.

Nini maoni yako


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

Waziri Mkuu Ataka Mkataba Uvunjwe....Ni wa Mkandarasi aliyenyang’anywa pasipoti na Rais Magufuli.Fahamu zaidi hapa.

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali haitavumilia wakandarasi wasio na uwezo na ambao wanapewa kazi lakini wanashindwa kuzimaliza katika muda uliopangwa.

Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo, jana (Alhamisi, Machi 30, 2017) wakati akizungumza na watumishi wa Halmamshauri ya Chalinze na wale wa Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira (CHALIWASA) katika ofisi zao, karibu na daraja la mto Wami, wilayani Bagamoyo, mkoani Pwani.

Alikuwa ameenda kukagua mradi wa upanuzi wa mtambo wa maji Chalinze na ujenzi wa mfumo wa kusafirisha na kusambaza majisafi pamoja na matenki ya kuhifadhia maji ambao umechukua muda mrefu lakini haujakamilika. Awamu ya kwanza ilianza mwaka Septemba mosi 2001 na kukamilika Desemba mosi 2003.

Alimuagiza Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Gerson Lwenge ahakikishe kuwa kazi ya ujenzi wa mradi huo inaimarika na kufikia asilimia 80 la sivyo, wakamilishe taratibu za kukatisha mkataba na kutafuta mkandarasi mwingine.

Agizo la Waziri Mkuu linafuatia taarifa aliyopewa kwamba mkandarasi wa mradi huo, Overseas Infrastructure Alliance (OIA) Pvt Ltd ya India alipaswa kumaliza kazi hiyo Februari 22, mwaka huu lakini hadi sasa mradi huo umekamilika kwa asilimia 23 tu.

“Nimeelezwa kwamba mmempatia nyongeza ya siku 100 ambayo inaisha tarehe 31 Mei 2017, kama kazi yake haitakuwa ya kuridhisha na kufikia walau asilimia 80, itabidi Mheshimiwa Waziri uendelee na taratibu zako za kukatisha mkataba, tuanze kutafuta mkandarasi mwingine,” alisema.

“Hii kampuni niliikuta Lindi kwenye mradi mwingine wa maji kama huu. Nilitoa maagizo ya kuharakisha ujenzi ukamilike lakini hawakufanya hivyo hadi Mheshimiwa Rais alipoenda na kuagiza mkandarasi anyang’anywe pasi yake ya kusafiria mpaka atakapomalizia kazi.”

“Kwa kifupi ni kwamba hii kampuni haina uwezo wa kufanya hizi kazi, na ndiyo maana hadi sasa wamekamilisha asilimia 23 tu ya mradi wakati walipaswa kuwa wamemaliza hivi sasa,” amesema Waziri Mkuu na kuongeza: “Mheshimiwa Waziri endelea na utaratibu wa kuwaondoa kisheria sababu hata tukiwaongezea muda bado hawatakamilisha kazi.”

“Nimesikitika sana kukuta mkandarasi hajafikia malengo. Mtu akipewa kazi anapaswa awe na uwezo wa kifedha wa kuifanya ile kazi ili hata Serikali ikichelewesha malipo yake, yeye aendelee na kazi,” aliongeza Waziri Mkuu.

Akizungumzia kuhusu ufanisi wa mradi huo, Waziri Mkuu alimtaka Mkurugenzi Mtendaji wa CHALIWASA, Eng. Christer Mchomba, ahakikishe kuwa wanapeleka maji hadi majumbani mwa wateja na kuweka mita ili wananchi waweze kulipa bili zao badala kuishia kutoa huduma hiyo kwenye vioski (viula).

“Kazi ya kupeleka maji majumbani ni yenu CHALIWASA na siyo ya Wizara. Pelekeni maji na mfunge mita ili watumiaji waweze kulipa bili zao. Pia toeni elimu kwa wananchi kupitia mikutano ya hadhara, waelezeni mipango yenu na wapi mlipofikia. Kazi yenu siyo kutandika mabomba tu, bali kutekeleza majukumu mliyopewa kwa niaba ya Serikali,” alisema.

Kuhusu mitambo inayotumika, Waziri Mkuu alisema mashine zilizopo ni za siku nyingi tangu 2003; hivyo amemuagiza Waziri Lwenge afuatilie upatikanaji wa mashine za kisasa kwani hilo suala ni kubwa na haliwezi kubebwa na CHALIWASA. “Bora mngeanza kuagiza mashine mpya hivi sasa, badala ya kusubiri zichakae kabisa, ndipo muanze kufikiria kuagiza.”

Mapema, akitoa taarifa ya mradi huo, Eng. Mchomba alisema awamu ya tatu ya ujenzi wa mradi huo ilisainiwa Mei 18, 2015 kati ya DAWASA na OIA yenye ubia na kampuni ya Pratibha Industries kutoka India kwa gharama ya dola za Marekani milioni 41.36 ambazo zilikuwa ni fedha za mkopo nafuu kutoka benki ya Exim ya India.

“Kazi zilizopangwa kufanyika ni upanuzi wa mtambo wa maji ili kuongeza uzalishaji wa maji kutoka mita za ujazo 500 hadi 900 kwa siku; ujenzi wa mfumo wa mabomba ya kusambaza maji wenye kilometa 1,022; ujenzi wa matenki makubwa 19 ya kuhifadhia maji; vituo tisa (9) vya kusukumia maji (booster stations) na vioski (viula) vya kuchotea maji 351.”

Alisema hadi sasa mkandarasi huyo amekwishalipwa dola za Marekani milioni 15.81 sawa na asilimia 38 na anaendelea na ulazaji mabomba ambapo hadi sasa amekwishalaza mabomba yenye urefu wa km.141 sawa na asilimia 12.4.

Alisema mradi huo umelenga kuvinufaisha vijiji 68 ambavyo 19 kati ya hivyo viko Kaskazini mwa mto Wami na 49 viko Kusini mwa mto huo.

Akizungumzia utendaji kazi wa mkandarasi huyo, Eng. Mchomba alisema Serikali imechukua hatua za kimkataba dhidi yake kwa kumtoza gharama ya kuchelewa kumaliza mradi (liquidated damages) kuanzia Februari 23, 2017.

“Pia mkandarasi amepewa notisi ya siku 100 ya kumtaka aongeze kasi ya kazi, vinginevyo tutasitisha mkataba ifikapo terehe 31 Mei, 2017 kulingana na kipengele namba 8.7 cha mkataba,” alisema.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
ALHAMISI, MACHI 30, 2017.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

SOKA LINALIPA MWANANGU, LINGARD MIEZI 18 MAN UNITED, SASA ANA GARI LA SH MILIONI 500.FAHAMU ZAIDI HAPA.

Jesse Lingard sasa ana miezi 18 tu ndani ya kikosi cha Manchester United na mafanikio ya kimaisha yameanza kuonekana.
Umri wake ni miaka 24 tu, tayari sasa anamiliki gari la kifahari aina ya Bentley Continental GT lenye thamani ya pauni 200,000 (zaidi ya Sh milioni 545.2)
Hii inaonyesha kiasi gain mchezo wa soka unavyoweza kulipa. Kama una kipaji ni vizuri kukitumia kwa ajili ya mafanikio.
Kwa wachezaji wa nyumbani Tanzania, inawezekana vigumu kufikia kununua gari la Lingard, lakini soka ni mchezo unaoweza kuwa ajira itakayobadilisha maisha yako. Inategemea kiasi gani uko makini katika kazi yako.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

Waziri Mkuu wa Ethiopia kutua nchini Leo.Fahamu zaidi hapa.

Waziri Mkuu wa Ethiopia, Hailemariam Dessalegn anatarajiwa kuwasili nchini kesho, Machi 31 kwa ziara ya kitaifa ya siku mbili kufuatia mwaliko wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli.

Hayo yalisemwa jana  na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano Afrika Masharika, Dkt. Suzan Kolimba alipokuwa Akizungumza na waandishi wa habari.
Alisema kuwa ziara ya Waziri Mkuu wa Ethiopia, Dessalegn imetokana na mkutano kati yake na Rais Dkt. Magufuli uliofanyika baada ya mkutano wa kawaida wa 28 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika uliofanyika hivi karibuni huko nchini Ethiopia.

Alisema kuwa madhumuni ya ziara hiyo ni pamoja na kukuza mahusiano mazuri yaliyopo baina ya Tanzania na Ethiopia pamoja ‎na kujadili fursa zaidi za ushirikiano katika maeneo mbalimbali ikiwemo uwekezaji na biashara.

“Mahusiano ya Tanzania na Ethiopia ni mazuri, Ethiopia imeonesha nia ya kufungua Ubalozi wake hapa nchini hivi karibuni. Kwa sasa Ethiopia inawakilishwa nchini na Balozi wake aliyepo Nairobi nchini Kenya” alisema Naibu Waziri Kolimba.

Wakati wa ziara hiyo,Waziri Mkuu wa Ethiopia, Dessalegn atakutana na Rais Dkt. John Magufuli kwa mazungumzo, watashuhudia uwekwaji saini wa mikataba ya ushirikiano kwenye maeneo mbalimbali kabla ya kuzungumza na Waandishi wa Habari.

Aprili 01 mwaka huu, Waziri mkuu huyo wa Ethiopia atatembelea Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) na kujionea shughuli mbalimbali zinazofanywa Bandarini hapo, Dessalegn na ujumbe wake wataondoka siku hiyo hiyo kurejea Ethiopia.

Hata hivyo, Mwaka 2015 Waziri Mkuu wa Ethiopia, Dessalegn alitembelea Tanzania na kushiriki uzinduzi wa Kiwanda cha kutengeneza dawa za kuua viluwi luwi vya mbu wanaoeneza Malaria kilichojengwa Kibaha, Pwani kwa ufadhili wa Serikali ya Cuba.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

Huyu Ndiye Mwakyembe Bwana..Soma Hapa Maneno Aliyompokea Nayo Nay a Mitego Baada ya Kufika Dodoma…Lazima Ucheke Aisee.Fahamu zaidi hapa.

Rapper Nay wa Mitego, Alhamis hii aliitikia wito wa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt Harrison Mwakyembe kukutana naye mjini Dodoma kwaajili ya kuzungumza namna ya kuuboresha wimbo wake Wapo ambao licha ya kuikosoa vikali serikali pamoja na Rais Dkt John Magufuli umepokelewa kwa mikono miwili.
Hatua hiyo ilikuja baada ya Rais Magufuli kuamuru kuachiwa huru kwa Nay ambaye alikuwa amekamatwa na polisi na wimbo wake kufungiwa na BASATA. Akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma, Dkt Mwakyembe alisema wasanii wana nafasi kubwa katika kuisaidia serikali kukemea mambo maovu.
Amewataka vijana kutambua kuwa Tanzania ni nchi inayozingatia utawala wa sheria na kwamba wana uhuru wa kukosoa bila kutukana au kwenda nje ya maadili. “Na ndio maana tukasema kwa wimbo wa Nay hapana, hebu ngoja tuusikie, mbona ni wimbo mzuri tu,” alisema Mwakyembe.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

Bajeti ya Kenya ya mwaka 2017/2018 Yasomwa.....Ajira Sekta ya Umma Zasimamishwa.Fahamu zaidi hapa.

Bajeti ya Kenya ya mwaka 2017/2018, imesomwa jana kinyume na inavyosomwa kawaida mwezi Juni, kutokana na uchaguzi mkuu utakaofanyika Agosti mwaka huu, huku ikitangaza kusimamisha ajira katika sekta ya umma.

Katika bajeti hiyo ya shilingi za Kenya trilioni 2.6 (Takriban shilingi trilioni 52 za Tanzania) Waziri wa Fedha, wa nchi hiyo, Henry Rotich ameondoa kodi kwenye mahindi yanayoagizwa kutoka nje kwa kipindi cha miezi minne ijayo,

Aidha kodi imeondolewa kwenye dawa za kuulia wadudu za nchini humo pamoja na magari ya utalii yanayoundwa nchini Kenya.

Katika bajeti hiyo ambayo ni ya mwisho kwa serikali ya Jubilee katika muhula wake wa kwanza, serikali imeongeza kodi kwenye kamari hadi 50% kutoka 7.5% ya awali kama njia ya kukomesha uchezaji kamari.

Serikali pia imetangaza kusimamisha ajira katika sekta za umma isipokuwa sekta ya elimu kama njia ya kupunguza matumizi.

Jumla ya Shilingi bilioni 524.6 za kenya katika bajeti hiyo zitatokana na mikopo kutoka nje na ndani ya nchi.

Shilingi bilioni 2 za Kenya  zimetengwa kuwaajiri walimu, na zingine bilioni 4 kuwalipia mtihani wanafunzi wa darasa la nane na kidato cha nnemwaka 2017 na 2018 huku serikali za kaunti zikipata jumla la shilingi bilioni 329.

Ili kuhakikisha kuwa vijana wana ajira, serikali imetenga shilingi milioni 450 Ksh kwa kuboresha kiwanda cha Rivatex, na zingine milioni 250 kuboresha kiwanda cha maziwa cha New KCC.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

Hatarii..Siwema Amvua Nguo Hadharani Nay wa Mitego ,Aanika Siri Zake Zote.Fahamu zaidi hapa.

MZAZI mwenziye na Mwanamuziki Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’,  Siwema Hudson amesema kitendo cha serikali kumpa kashikashi kutokana na wimbo wake wa Wapo hakikumshangaza kwani alitarajia hayo yatokee kwa kuwa zilipendwa wake huyo ni mtu wa kukurupuka.
Akizungumza na gazeti hili juzi baada ya Nay kutoka polisi, Siwema alisema yeye amekaa na Nay kwa muda mrefu na mara nyingi akiamua jambo ndiyo hivyo wala hakuna mtu anayeweza kumshauri.
“Unajua Nay anapenda kukurupuka na wala hataki mtu apinge wazo lake, kama ameamua kufanya kitu anafanya tu na nilifahamu kuwa ipo siku hilo lingemtokea, sasa kama limepita anatakiwa kujitathmini upya,” alisema Siwema


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

Sakata la Vyeti Feki ..Ikulu Yatupa Mpira kwa Waziri Huyu..Kuhusu Vyeti vya Makonda Amefunguka Haya Mazito.Fahamu zaidi hapa.

WAKATI uhakiki wa vyeti vya watumishi wa umma unakamilika leo, Ikulu imemtwisha mzigo Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), George Simbachawene, kuwa ndiye mhusika mkuu wa suala hilo.
Kwa mujibu wa tangazo lililotolewa Machi 20, mwaka huu na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dk. Laurian Ndumbaro, uhakiki wa vyeti vya elimu na taaluma pamoja na namba za mitihani kwa watumishi wa umma ulioanza Machi 12, mwaka jana, utakamilika rasmi leo.
Katika tangazo hilo, Dk. Ndumbaro anaeleza kuwa uhakiki huo haujalenga kumkoma mtumishi wa umma bali kuhakikisha kunakuwa na watumishi wenye sifa stahiki na kitaaluma na kitaalamu ili kutoa huduma zilizo bora na kwa weledi kwa wananchi.
"Serikali inasisitiza kuwa mtumishi wa umma atakayeshindwa kutumia muda uliotolewa kuwasilisha nakala za vyeti au namba za mitihani kwa wale waliopoteza, atakuwa amejiondoa mwenyewe katika ajira serikalini," linaeleza tangazo hilo ambalo Florence Temba, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Ofisi ya Rais, Utumishi, aliithibitishia Nipashe kuwa ni lao.
Alipoulizwa na Nipashe kama uhakiki huo unawahusu pia wateule wa Rais, Temba alisema ni kwa watumishi wote wa umma, lakini akadai kuwa vyeti vya wateule wa Rais vinahakikiwa na Ofisi ya Rais Tamisemi.
Nipashe ilipomtafuta Simbachawene kuzungumzia suala hilo, alidai masuala ya uhakiki wa vyeti kwa watumishi wote wakiwamo wateuliwa unafanywa na Wizara Nchi, Ofisi ya Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.
"Utumishi ndiyo wanaofanya hiyo kazi ya uhakiki na utunzaji wa taarifa zote za watumishi na wateuliwa, hivyo siwezi kujibu hilo suala," alisema Simbachawene.
Kutokana na majibu hayo ya Simbachawene, Nipashe ilimtafuta tena Temba ambaye alisisitiza kuwa wanaohakikiwa na wizara yao ni watumishi wa umma na kwamba vyeti vya elimu na kitaalamu vya wateule huwa wanavipeleka kwenye mamlaka husika za uteuzi.
Akizungumza na Nipashe kwa simu jana mchana kuhusu uhakiki wa vyeti vya elimu na kitaalamu vya wateule wa Rais, Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano Ofisi ya Rais, Ikulu, Gerson Msigwa, alisema Simbachawene ndiye anayepaswa kuzungumzia uhakiki huo.
"Muulize huyo huyo Simbachawene. Vyeti vinahakikiwa huko huko Tamisemi. Simbachawene yuko Ofisi ya Rais Tamisemi ambako mambo ya uhakiki (kwa wateule) yanafanyikia huko," alisema Msigwa.
Jitihada za Nipashe kutaka kuzungumza na Simbachawene jana hazikuzaa matunda baada ya simu yake ya mkononi kutopokewa na hakujibu ujumbe mfupi wa maandishi tuliomtumia kuhusu suala hilo.
Kwa miaka mingi, ripoti za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) zimekuwa zikionyesha upotevu wa mabilioni ya shilingi kutokana na malipo ya watumishi hewa.
Kutokana na changamoto hiyo, Machi 12, mwaka jana, serikali ya awamu ya tano ilielekeza kufanyika kwa uhakiki wa watumishi hewa kwa kukagua vyeti vya kazi wanavyotumia ili kuwe na usimamizi na uwajibikaji.
Juni 22, mwaka jana, Rais John Magufuli akatangaza kusitisha ajira serikalini ili kuhakiki watumishi wote wa umma.
Kutokana na uamuzi huo, nyongeza ya mishahara kwa watumishi wa serikali na wakala zake pamoja na utoaji wa vibali vya likizo ya bila malipo vilisitishwa kwa muda hadi uhakiki utakapokamilika.
Kwa mujibu wa Dk. Ndumbaro, baada ya kusitishwa kwa ajira, taarifa zilisambazwa katika halmashauri zote na idara za serikali kutekeleza maelekezo yaliyotolewa na wizara Juni 13, jana kusitisha ajira hadi pale uhakiki utakapokamilika.
Kutokana na uamuzi huo, ajira 71,496 zilizokuwa zimepangwa kutolewa mwaka huu wa fedha na serikali kwenye sekta mbalimbali ikiwamo elimu, afya na viwandani hazijatolewa, huku zikiwa zimebaki siku 91 kabla ya kumalizika kwa mwaka wa bajeti.
Kwa mujibu wa Temba, sekta ya elimu mwaka huu ilitarajiwa kuwa na ajira mpya 28,957, afya 10,870, kilimo 1,791, mifugo 1,130, huku maeneo mengine ambayo hayakutajwa, yakitarajiwa kuwa na ajira 28,748.
Ofisa huyo wa serikali aliiambia Nipashe kuwa hadi kufikia Agosti 2016, watumishi 839 walikuwa wamefikishwa kwenye mamlaka za kiuchunguzi likiwamo Jeshi la Polisi na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana Rushwa (Takukuru) kwa ajili ya kutoa maelezo kabla ya kufikishwa mahakamani kutokana na kunufaika kwa kujipatia fedha kupitia watumishi hewa.
Tangu Rais Magufuli aingie madarakani Novemba 5, 2015, serikali yake imekuwa ikifanya kazi kubwa ya kukomesha vitendo vya ufisadi vikiwamo hivyo vya kuwapo kwa malipo ya kila mwezi yanayokwenda mifukoni mwa maofisa wachache wasio waaminifu badala ya fedha hizo kuelekezwa katika shughuli nyingine za maendeleo.
Credit - Nipashe


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

Dk Slaa: Mvumilieni Magufuli.Fahamu zaidi hapa.

BAADA ya kuishi nchini Canada kwa zaidi miaka miwili sasa, aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Willbrod Slaa amesema anakuna kichwa ili kupima mazingira yaliyomfanya aondoke nchini na familia yake kama yapo au laa.
Septemba,2015 wakati wa Uchaguzi Mkuu Dk. Slaa alijiweka kando na siasa, kwa kile alichokieleza kutofautiana na chama chake juu ya masharti ya kumpokea aliyekuwa mgombea urais wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa),Edward Lowassa.
Hata hivyo Dk. Slaa ambaye amekuwa mbunge wa Karatu kwa vipindi vitatu mfululizo, hakuweza kuainisha mazingira yaliyomfanya aondokea nchini na kwenda kuishi ughaibuni.
“Sina tabia ya kuyumbishwa…sina chuki na mtu yeyote, sipendi siasa za udanganyifu na propaganda. Nimeachana na siasa tangu Julai 28,2015, baada ya kuona misingi ya chama nilichoshiriki kukijenga imepotoshwa,”alisema Dk. Slaa siku alipotangaza kuachana na siasa.
Pamoja na mambo mengine, alisema sharti la kwanza ambalo alitaka Chadema izingatie ni kiongozi huyo wa zamani ndani ya serikali ya CCM, kujisafisha dhidi ya tuhuma ya kashfa ya sakata la Kampuni ya Kufua Umeme ya Richmond aliyohusishwa nayo akiwa Waziri Mkuu.
Kurudi nchini
Akizungumza na MTANZANIA akiwa nchini Canada jana, Dk. Slaa alisema amemaliza masomo yake na baada ya kufanya tafakari atarejea nchini wakati wowote.
“Ni kweli nimemaliza masomo yangu. Bado napima mazingira yaliyonifanya niondoke na familia yangu. Baada ya hapo tutaangalia uwezekano wa kurejea,”alisema.
Alisema kuhusu matarajio yake ya kisiasa, watu wameshindwa kumwelewa siku ambayo alitangaza kustaafu siasa za vyama.
Alisema alichomaanisha ni kwamba, pamoja na kuachana na siasa za vyama,atakuwa tayari kupiga kelele pale anapoona masilahi ya Taifa yanaumia.
“Hadi sasa sijapiga kelele kwa kuwa sijaona masilahi ya Taifa yakiangamizwa, hatua mbalimbali zinazochukuliwa ni kweli zinawaumiza wasiohusika.
“Ndio maana nilitumia katika makala mojawapo mtego wa panya huwakamata wanaohusika na wasiohusika. Hivyo, makosa madogo mimi hayanisumbui kwa kuwa hakuna binadamu kamilifu ,”alisema.
Rais Magufuli
Akizungumzia utendaji wa Rais Dk. John Magufuli, alisema watu waelewe hakuna nchi hata moja ambapo kiongozi atakubalika na watu wote kwa asilimia 100.
Alisema wako watu ambao masilahi yao yataguswa kwa namna moja au nyingine hivyo lazima watapiga kelele.
Kutokana hilo, alisema Rais Dk. Magufuli katika kundi ambalo halihitaji fedha ameyatekeleza yote kwa asilimia 99.9, ikiwa ni pamoja na uwajibikaji serikalini, kuchukua hatua kali dhidi ya rushwa, uwizi wa mali za umma, uwindaji haramu na kudhibiti dawa za kulevya.
“Hatua zote zimechukuliwa,zinapaswa kuwa endelevu. Kwa bahati mbaya mchwa wengine waliopenya mpaka ndani ya Ikulu na Serikali na huwezi kufagia Serikali nzima kwa siku mmoja.
“Kwa jinsi Rais ambavyo hayumbi na wala hayumbishwi, nina hakika atafikia malengo na kurudisha Taifa kwenye misingi ya tunu za Taifa ya uwazi, ukweli, uadilifu, kuheshimiana na kuthaminiana na hasa kujali utu.
“Hii ndiyo hali ambayo JPM kila siku anaiita ‘Transition’ (kipindi cha mpito). Tutafika tu, tunatakiwa kuwa wavumilivu na wenye uzalendo wa kweli ana nia njema ya kufikisha Taifa mahali pazuri. Hii inahitaji kuweka pembeni maslahi yetu binafsi kama mtu mmoja mmoja, viongozi wa Serikali au hata wa kisiasa,”alisema Dk. Slaa.
Upinzani
Kuhusu mwenendo huo endapo utasaidia upinzani kuingia Ikulu 2020, Dk. Slaa alisema wakija na ajenda mbadala na makini yenye kuwalenga wananchi moja kwa moja itawasaidia.
Dk. Slaa ambaye pia alipata kugombea urais kupitia Chadema mwaka 2010, alisema endapo wataendelea kurukia kauli za Rais, basi upinzani utafutika kabla ya 2020.
“Kama nilivyorejea mara kadhaa, upinzani makini utaingia Ikulu kwa ajenda mbadala. Ajenda makini yenye kuwalenga wananchi moja kwa moja katika kuwatoa kwenye kero zao mbalimbali.
“Hadi sasa ninachoona ni ‘kurukia’ kauli za JPM, lakini kauli si ajenda na hatupeani maksi kwa kuzungumzia usahihi wa lugha. Wako wanaotazama usahihi wa lugha na mahali pa kutazama usahihi huo. Kimsingi hayo ni masuala ya darasani au kwenye uandishi wa vitabu.
“Aidha kumtuhumu JPM kukiuka Katiba na sheria nayo haina tija. Wote wanaomtuhumu wanajua kuwa wakiambiwa waonyeshe kifungu mahususi alichokiuka yeye mwenyewe katika utendaji wake hawana majibu ya kuridhisha.
“Hivyo mimi sijaona mwenendo wa JPM unaosaidia kuingiza upinzani Ikulu. Isitoshe kama hawatakuja na ajenda makini na mkakati ulioandaliwa unaowatoa wananchi hapa walipo kwenda kwenye raha, upinzani unaweza kufutika kabla ya 2020,”alisema Dk. Slaa.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

Thursday 30 March 2017

Download wimbo mpya wa Weusi unaoitwa "Ya Kulevya".




Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

Mbinu 5 Kali za Jinsi ya Kutongoza Msichana Yoyote Mrembo na Akubali.Fahamu zaidi hapa.

Je , unamtamani msichana mrembo ambae kwa sasa ni kama marafiki ? au unavutiwa na yule demu unayemuona kila siku mtaani na unashidwa kujizuia sema hujui uanzaje ? Haijalishi kama unamjua au hamjuani , ila inapokuja kwenye kumtongoza mwanamke unachotakiwa kujua ni uelewa wa vitu kadhaa kuhusu jinsi kutamani kunavyokua na jinsi ya kufanyia kazi ili ufanikiwe .
Kumtongoza demu na vitu unavyotakiwa kujua
kwanza kabisa kama unataka kumtongoza msichana au kumfanya tu akupende tu , inabidi uwe mtu poa ambae anaweza kuvuta macho ya wasichana.
Kama hautaweza kua mtu anayeweza kumvutia msichana kirahisi , utakua bado unauwezo wa kumtongoza mwanamke unayempenda lakini itakua ngumu kuwezesha yeye akukubali .
Kiufupi fatisha njia hizi 11 rahisi na kiukweli kabisa utakua vizuri katika kutongoza na hata kwa mambo mengine yatakayofuata baada ya hapo.
Tumia njia hizi moja baada ya nyingine na ijapokua utacheza karata zako vizuri basi lazima umpate mrembo yoyote unayemtaka hata kama kuna watu wengine kibao wanamfukuzia .
1 . Kua karibu nae
Siku zote , kama unataka kumtokea msichana njia muhimu kabisa ni kuweza kumjua kwa undani .Usikurupuke kurupuke tu ukaanza kutongoza , msichana ataogopa au atakuona mtu rahisi kua nae na mwisho wa siku utaishia kumboa tu .
Ongea nae na upate kumjua vizuri . Mtumie message na usiwe na mzuka , mfanye awe kama rafiki kwanza . Usimtokee kwanza sema pia usisubiri sana maana ataanza kukuchukulia poa .
2 . Kua mtu unayependeka
Hii ni hatua muhimu sana . Na huu ndio wakati utagundua kama anahisia na wewe kweli au anakuchezea akili . Pia unapoongea nae mara kwa mara jaribu kugundua vitu anavyovipenda. Jaribu kuweka ukaribu nae kwenye kitu ambacho wote mnakipenda.
3 . Usilale Usiku
Ndio maana mitandao mingi ya simu ikawapa ofa za usiku watu kama nyie muongee usiku kucha . Usiku ndio muda sahihi wa kuweza kutoa ya moyoni na kueleza hisia zako kwa msichana . Anza kwa kuweka maongezi ya kawaida na kadiri unavyoendelea weka vionjo fulani vitakavyomfanya aanze kuingia line bila kugundua kama unamtokea.
4 . Ishi Maisha mawili
Unapoongea nae usiku , mwaga sera zako na funguka kuhusu mambo ya mapenzi sema mkikutana ana kwa ana mchana usiongelee mambo ya mapenzi kabisa labda aanze yeye na hivyo kumaanisha ashaingia line na anapenda maongezi hayo .
Pia epuka kuongelea kuhusu mambo yenu ya kimapenzi mnapokua na marafiki wengine bali fanyeni hivyo mkiwa wawili . Kwa kufanya hivyo unamfanya aamini kuna uhusiano motomoto wa siri unapikika kati yenu.
5 . Usimfanye ajue unampenda
Wanaume wengi ufanyaga kosa hili kubwa . Wanawaambia wanawake wanawapenda au wanahisia za kimapenzi kwao . Ni kweli unampenda , anajua hivyo tayari . Au hajui ? Unampigia simu kila saa , mnataniani kimapenzi na anaona uhusiano wenu kabisa .
Kwahiyo japokua anahisi unampenda , usije kuonyesha hivyo kwani anahitaji kusikia kutoka kwako ili ajihakikishia hisia zake . Chukulia poa na usifunguke kuhusu hisia zako kwake , kitendawili alichonacho ndicho kitamfanya azidi kukunata na kutaka kujua mwisho wa mambo .


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

Lissu - Nikikutana na Rais Magufuli Nitamsimanga na Kumpa Vidonge Vyake.Fahamu zaidi hapa.

Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Tundu Lissu amesema uongozi wa chama hicho umemwandikia Rais John Magufuli kutaka kukutana naye Ikulu ya Dar es Salaam kwa ajili ya kujitambulisha rasmi na kufanya mazungumzo.
“Ni mkutano baina ya Rais na rais,” alisema Lissu katika mahojiano na gazeti hili alipotembelea ofisi za Mwananchi Communications Limited (MCL) inayozalisha magazeti ya Mwananchi, The Citizen na Mwanaspoti.
Lissu, ambaye pia ni mbunge wa Singida Mashariki, alichaguliwa kuwa rais wa chama hicho mapema mwezi huu, na Rais ni mmoja kati ya viongozi kadhaa waliowaandikia kuomba kukutana nao.
Aliwataja wengine kuwa ni Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Jaji Mkuu, Mkuu wa Jeshi la Polisi na marais wawili wastaafu, Benjamin Mkapa na Jakaya Kikwete.
Alisema tayari Jaji Mkuu ameshakubali ombi lao.
Kuhusu ombi lao kwa Rais Magufuli, Lissu alisema atatumia fursa hiyo vizuri, iwapo watakubaliwa.
“Nikifika nitaanza kwa kumshukuru Rais kwa kuwafundisha Watanzania maana ya utawala wa sheria, uhuru wa mawazo, uhuru wa vyombo vya habari na uhuru wa Mahakama na Bunge,” alisema Tundu Lissu.
Lissu alifafanua baadaye kuwa Rais Magufuli amefumbua wengi macho kujua vitu hivyo kutokana na jinsi anavyoendesha nchi, ndio maana atamshukuru.
“Tumeomba appointment na Rais Magufuli tuzungumzie utawala wa sheria,” alisema Lissu.
“Leo ni Jumatano? Barua tulimpelekea Jumatatu. Tutaenda kujitambulisha na kuzungumzia utawala wa sheria na mwelekeo wa taifa hili. Ni between presidents. Tuna imani kwamba atatukaribisha. Tutamweleza maoni yetu, pale tunapoona amekosea tutamweleza na pale anapoona tuna matatizo atatueleza.”
Alisema wanajua kuwa Rais ana shughuli nyingi, lakini wanatarajia atatenga muda kwa ajili yao.
“Tunafahamu yuko busy, lakini kama anaweza kuangalia Shilawadu, atakuwa na muda hata nusu saa au saa nzima ya kuongea na kiongozi wa chama cha mawakili wa Tanganyika,” alisema.
Lakini akaonyesha jinsi alivyopania kueleza matatizo anayoyaona katika utawala wa sasa.
“Nakwenda kumpa vidonge vyake, kabisa! Wala sitammezea. Nitamwambia kwa heshima zote kwamba Mheshimiwa Rais, sisi kama mawakili wa Tanganyika tuna wasiwasi mkubwa na mwelekeo wa Serikali yako,” alisema.
“Wamenituma nikueleze mwelekeo na matendo ya Serikali yako. Unatawala vibaya, nje ya Katiba, wameniambia nije nikwambie ujirekebishe. Nakwenda kumsimanga tu. Halafu tukitoka pale namwambia Mheshimiwa Rais tupige picha, wajue nilikuja.”
Alisema iwapo Rais hatakubali kuwaalika, ataueleza umma.
“Atakuwa amenirahisishia, nawaita waandishi wa habari nawaambia. Tulimwambia Bwana mkubwa tumsalimie na tumweleze kwamba haturidhiki na utawala wake, yeye amekataa amekimbia,” alisema Lissu.
Hata hivyo, mkuu wa Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Gerson Msigwa amemtaka Lissu kusubiri taratibu za kiutawala.
Msigwa alimshangaa Lissu kwa kitendo chake cha kuzungumza katika vyombo vya habari ilhali anajua utaratibu wa kiutawala.
“Yeye kama ameandika barua barua si asubiri majibu? Muulizeni inakuwaje kabla hajapewa majibu anaenda kutangaza katika vyombo vya habari? Si asubiri utaratibu wa kiutawala,” alisema Msigwa.
Lissu alisema ofisi nyingine walizopeleka maombi kama hayo ni ya Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Jaji Mkuu, Mkuu wa Jeshi la Polisi na marais wastaafu, Benjamin Mkapa na Jakaya Kikwete.
Kwa upande wake, Waziri wa Katiba na Sheria Profesa Paramagamba Kabudi alisema hana taarifa juu ya barua hiyo kwa kuwa tangu ateuliwe hajaingia ofisini.
“Nimekuwa katika vikao vya Kamati za Bunge vinavyoendelea mjini Dodoma, hivyo sina habari hiyo,” alisema.
Hata hivyo, Profesa Kabudi alisema inawezekana ni kweli rais huyo wa TLS amewasilisha barua hiyo ofisini kwake lakini yeye bado haijamfikia.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa