Wednesday 29 March 2017

Facebook Nayo Yaja na Mtindo wa Snapchat.Fahamu zaidi hapa.

Baada ya Instagram kuanzisha Insta Stories, mtindo ulioipandisha chat Snapchat, Facebook nayo imekuja na mtindo huo kwenye app yake.
Kupitia app ya Facebook, sasa unaweza kushare matukio/stories na kuona kile marafiki zako wamekifanya kwa saa 24. Juu ya Facebook app, utaona picha za duara zinazowakilisha story walizoziweka marafiki zako na ukibonyeza, utaona picha, video ama michoro waliyoweka.
Baada ya saa 24, post hizo zitapotea na hazitaonekana tena.
Kwa maana hiyo Facebook sasa imeanzisha stories kwenye app zake zote, Facebook, Messenger, Instagram na Whatsapp. Hadi sasa Instagram stories zimekuwa na mafanikio makubwa.



Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment