Friday 31 March 2017

MAJERAHA YA NGOMA, SASA NI HOFU KWA YANGA MAANA HAKUNA UHAKIKA KESHO.FAHAMU ZAIDI HAPA.

Yanga wamekuwa na hofu kubwa kutokana na suala la majeruha kuwaandama.


Mshambuliaji Donald Ngoma bado anaonekana hana nafasi ya kuisaidia Yanga katika mechi dhidi ya Azam FC, kesho.

Ngoma anaonekana hajapona vizuri hali inayosababisha hofu kubwa kwa Yanga ambayo italazimika kuwategemea Obrey Chirwa na Simon Msuva.

Mshambuliaji mwingine, Amissi Tambwe naye ni majeruhi, hivyo kumfanya Kocha George Lwandamina kuwa na wakati mgumu.

Katika mazoezi ya leo, Ngoma alionekana hakuwa vizuri hali inayoashiria kama hakufanya kitu leo, basi kesho ana nafasi ya asilimia chache kucheza.

Kama Yanga itapoteza mechi ya kesho dhidi ya Azam FC itakuwa imejiweka katika wakati mgumu sana.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment