Tuesday 28 February 2017

DOWNLOAD WIMBO WA ISHA MASHAUZI UNAOITWA "MWANAMKE MPANGO MZIMA".

DOWNLOAD WIMBO WA ISHA MASHAUZI MWANAMKE MPANGO MZIMA.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

DOWNLOAD WIMBO MPYA WA ROSE MUHANDO UNAOITWA "TAWALA".

DOWNLOAD WIMBO WA ROSE MUHANDO - TAWALA.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

HEKAHEKA: Mtoto mchanga aliyeibwa Tegeta apatikana Makaburini Ununio.Fahamu zaidi hapa.

February 22 2017 kupitia Leo Tena ya Clouds FM Heka Heka ilitokea Tegeta Kibaoni Dar es salaam ambapo Mtoto mchanga aliibwa na watu ambao hawakufaamika..Sasa Leo February 28 zikiwa zimepita siku sita mtoto huyo amepatikana makaburini.
Mtoto huyo apatikana akiwa ametelekezwa makaburini akiwa kwenye mfuko maeneo ya Ununio ambapo watu waliokitelekeza mfuko huu walikuwa ni Boda Boda na abiria aliye kuwa amebeba Mfuko huo.
Bonyeza play hapa chini kusikiliza full Stori

ULIPITWA NA HEKAHEKA YA MTOTO MCHANGA ALIVYOIBWA TEGETA DAR ES SALAAM



Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

Waziri Nape: Sikupinga vita dhidi ya biashara ya dawa za kulevya bali nilishauri busara itumike.Fahamu zaidi hapa.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye ametoa ufafanuzi juu ya kauli iliyonukuliwa ikionyesha kuwa alipinga vita dhidi ya dawa za kulevya iliyoanzishwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda. Amedai kuwa hakupinga vita hiyo bali alitaka busara itumike kwa washukiwa.

Waziri Nape alitoa ufafanuzi huo katika kipindi cha dakika 45 cha ITV, alipoulizwa swali na mtangazaji wa kipindi hicho kutaka kujua kuhusu kauli yake iliyoonesha kupinga utaratibu uliotumika wa kuwakamata au kuwapata watuhumiwa wa dawa za kulevya.

“Niseme kwanza ilitokea nilikuwa na mkutano na waandishi wa habari, ukienda leo ukanitaja Nape ukaniambia baada ya siku mbili njoo kituoni, hata kama nilikuwa na madawa ya kulevya nyumbani kwangu hivi unayakutaje? 
'Kwasababu kwa vyovyote vile nitayachukua, ntayaficha, ntakuja kituoni ntaripoti utanibana ntakwambia twende nyumbani kwangu ukakague mnaenda mnakagua mnakuta hamna, si basi! 
"Kwahiyo nikawa na wasiwasi kwamba inawezekana kabisa nia ilikuwa njema lakini nilidhani pangeweza kutengenezwa utaratibu bora zaidi ya namna ya kuwapata, kwasababu hapa kuna watumiaji, kuna wauzaji na wale ambao wanaleta sasa madawa ya kulevya,” alisema Nape.

Aliendelea, “Ukishughulika na mtumiaji huyu ukadhani ndiye mhalifu wako unakosea, kwasababu huyu ni muathirika na muathirika anahitaji dawa anahitaji huduma ameshaathirika, hapa wahalifu wetu nikuanzia huyu anayemletea halafu kuna huyu anayempa yule aliyemletea, sasa ili uwapate hawa wawili lazima umtumie huyu vizuri ili akupeleke kwa hawa wawili. Lakini ukimkamata huyu ukamtia ndani sasa hawa wawili watakimbia.”

“Kwahiyo mimi nikaona kwamba tunaivuruga vita yenyewe, anayeingiza madawa ya kulevya na anayesambaza kwa maana ya kuyauza, hawa ndiyo tatizo letu. Na ndio maana nikasema hebu tutumieni busara, watu wakadhani nimepinga. 
"Tena mimi nilisema mara nyingi sana tumieni busara namna ya kuiendesha vita hii. Madhara ya kutotumia busara katika vita hii ni makubwa sana, kwasababu ukimweka huyu mtu mmoja ndani hawa wengine wataendelea kuwaathiri wengine na ndiyo maana nasema hii vita tutumieni busara. 
"Hii vita ni ya kupigana kimya kimya kwasababu wanaofanya biashara hii hawaifanyi hadharani wanafanya kwa kificho. Shughulika nao kwa kificho, hii vita hakuna mahali ambapo wameshawahi pigana hadharani, tukitajana hadharani hata wenye chuki watatajana humo humo,” alisisitiza.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

Chadema yaweka ulinzi mkali nyumba ya mama Wema......Ni Baada ya Nyumba Hiyo Kupigwa Mawe Usiku.Fahamu zaidi hapa.

Nyumba ya mama Wema Sepetu, Mariam Sepetu, iliyopo Sinza Mori jijini Dar es salaam usiku wa kuamkia jana imepigwa mawe juu ya bati kwa muda wa saa moja na nusu.

Kutokana na tukio hilo viongozi wa Chadema wamechukua hatua ya kuweka ulinzi mkali nyumbani hapo na kuzungumza kuwa wamegundua kitu ambacho hawatakiweka wazi kwa sasa.


Baada ya tukio hilo kutokea mama Sepetu aliwasiliana na mwanae Wema Sepetu pamoja na viongozi wa Chadema, ambapo Meya wa Ubungo, Boniface Jacob alifika na kuangalia hali ya mama huyo na kuamua kuweka ulinzi.


”Tumeshaangalia mazingira yote tumegundua kitu ambacho hatuta kiweka wazi kwa sasa ila tutaweka ulinzi mkali na atakaye jaribu shauri yake hatuta kubali suala hili liendelee kumkuta kamanda wetu na mimi mara kwa mara nitafika kuangalia mazingira” amezungumza hayo Meya wa Ubungo, Boniface Jacob.


Meya alifafanua kuwa ulinzi huo hautaishia nyumbani kwa mama Wema bali hata nyumbani kwa Wema Sepetu ulinzi utaimarishwa kwani amegundua wanachama hao wapya wamekuwa wakiwindwa na watu wasiojulikana.


Wema alipohojiwa amesema, ” Mama yangu ameteseka usiku kucha kwa kukosa amani, amelia na kukosa hata hamu ya kula tumefika tumemkuta katika hali mbaya, najua yana mwisho ila tutazidi kufanya dua ya kumwomba Mungu atuepushie na mabaya yote,”.


Mama nae alihojiwa na kusema, ” sikuweza kutoka nje kwa kuwa najua mbaya wangu amekaa wapi na amekusudia kufanya nini,”.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

Steve Nyerere sio staa kwangu, ni panya – TID.Fahamu zaidi hapa.

Huu ni mwezi mbaya kwa mchekeshaji Steve Nyerere. Ni kwasababu kauli zake zimeendelea kumponza.

Hivi karibuni, kwenye mazungumzo yaliyovuja kati yake na mama yake na Wema Sepetu, alidai kuwa hitmaker wa Siamini, TID alipewa fedha na mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ili atoe hotuba kuhusu kuwa mtumiaji wa dawa za kulevya.

Mnyama alimind mbaya na kutishia kumshtaki mchekeshaji huyo. Na sasa mkali huyo ameibuka na kumwelezea Steve kuwa si staa kwake, bali ni kama panya tu.

“Steve Nyerere sio staa kwangu, he is a mouse,” ameiambia E-News ya EATV.

“Ukimuangalia kwanza he is a mouse, to me, me I have been doing this talent na nimejijengea umaarufu kupitia kipaji changu, sio kupitia uongo uongo, udananda sijui umbea umbea, sijafanya hivyo,” ameongeza.

“I have been working very hard to make this name. Huwezi kuniambia mimi eti nimepewa milioni mbili sijui, unanidhalilisha, kwanza unanihatarishia maisha yangu mtaani mimi nionekane snitch, nimewasnitch wananchi, nimepewa milioni 3 kuconfess pale, why? Milioni mbili na maisha yangu?

TID amemtaka Steve afike mbele ya mahakama athibitishe kuwa alichukua shilingi milioni 2, lasivyo patachimbika

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa afungua mkutano wa watendaji Wakuu wa Mashirika ya umma,Ikulu.Fahamu zaidi hapa.

Waziri  Mkuu, Kassim Majaliwa  mapema leo 28 Februari 2017, ameongoza mkutano wa siku moja wa watendaji wakuu na wenyeviti wa bodi za mashirika ya umma, unaojadili nafasi za mashirika ya Umma katika utekelezaji wa Mpango wa Pili ya Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano (2016/17-2020/21), Unaofanyika Ikulu Jijini Dar e Salaam.

Mkutano huo ulioandaliwa na Taasisi ya Uongozi kwa kushirikiana na Ofisi ya Msajili wa Hazina,Waziri Majaliwa amewapongeza wakuu hao ambapo amewataka kuhakikisha wanaongeza juhudi na maarifa katika mashirika yao ili kusonga mbele.

Akisoma hotuba ya ufunguzi wa mkutano huo, Waziri Mkuu Majaliwa amewataka wakuu hao kuongeza ubunifu zaidi ili kuongeza maarifa katika mashirika yao hii ni pamoja na kujiendesha kwa faida ili kuipunguzia Serikali mzigo wa kujiendesha.

Majaliwa amelipongeza Shirika la Nyumba NHC ambalo kwa miaka ya nyuma lilikuwa likiendeshwa kwa hasara, hata hivyo baada ya kuongeza ubunifu na kuingia kijana mzawa, wameweza kupiga hatua na sasa wamekuwa wa mfano wa kuigwa huku pia akipongeza baadhi ya mifuko ya Maendeleo ya Jamii pamoja na mabenki mengine kwa ikiongozwa na benki kuu, kutokana na kuwa na menejimenti nzuri, ubunifu na kutumia wataalamu waliobobea  katika fani zao, wameweza kufanya mambo makubwa.

“Kumekuwa na dhana potofu kwamba Mashirika ya Umma hayatakiwi kufanya biashara,  na kwamba yakifanya biashara lazima yapate hasara inaendelea kubaki kuwa ni dhana potofu. Ipo mifano mbalimbali” ameeleza Majaliwa huku akitolea mifano ya nchi zilizofanikiwa kwa mashirika ya Umma  kufanya vizuri  mfano

Mashirika kama Petrobras la Brazil, Statoil la Norway, CNOOC la China ambayo ni makubwa na yameweza kuwekeza nje  ya mipaka ya nchi zao.

Majaliwa amesema mpaka sasa Serikali imeweza kuwa na Mashirika ya umma 264 ambapo kati ya Mashirika hayo, Mashirika 65 ni Mashirika ya Kibiashara, Mashirika 187 ni mashirika ya  huduma wakati mashirika 12 ni udhibiti. Kati ya Mashirika 65 ya kibiashara, Mashirika 8 yanaendeshwa kwa ruzuku ya Serikali, wakati Mashirika 57 hayategemei ruzuku ya Serikali.

Awali akifungua mkutano huo, Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uongozi, Profesa Joseph Semboja amesema malengo ya mkutano ni kukusanya maoni ya viongozi kuhusu nafasi ya mashirika ya umma katika utekelezaji wa Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano, kuzungumzia changamoto tarajiwa katika utekelezaji wa majukumu haya na kutoa mapendekezo ya namna ya kukabiliana na changamoto hizo.

“Mashirika ya Umma yana nafasi na uwezo mkubwa wa kufanikisha utekelezaji wa Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Miaka Mitano, 2016/17–2020/21 wenye kaulimbiu ‘Maendeleo ya Viwanda kwa Mabadiliko ya Kiuchumi na Maendeleo ya Watu’,” amesema Profesa Semboja.

Profesa Semboja aliongeza, “Katika kuunga mkono jitihada za Serikali ya Rais John Magufuli, mkutano huu umewezakutanisha viongozi kutoka serikalini na mashirika ya umma kwa lengo la kubadilishana maarifa na uzoefu wa jinsi mashirika haya yatakavyoiwezesha Tanzania kuwa nchi ya viwanda kwa maendeleo endelevu.”

Mkutano huo unajadili namna ya kuboresha mifumo ya kiutendaji ndani ya mashirika na uhusiano miongoni mwa mashirika na taasisi za serikali, kufungamanisha mipango ya mashirika ya umma na Mpango wa Pili wa Maendeleo, kutathmini kiwango na aina ya rasilimali zinazohitajika kuwezesha utekelezaji wa mipango na; kufanya ufuatiliaji na tathmini ya mipango.

Jumla ya washiriki 100,  kutoka wizara, mashirika ya umma na mamlaka za udhibiti takribani 52 nchini.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

Wema Sepetu amchinjia baharini Batuli.Fahamu zaidi hapa.

Sasa Wema Sepetu na Batuli ni mbuzi na chui, urafiki ndio umefika mwisho. Tukio hilo limetokea baada ya Wema kukasirishwa na kitendo cha Batuli kusema kuwa yeye alishalipwa fedha zake za kampeni na CCM.

Kupitia mtandao wa Instagram, Wema Sepetu ameweka picha ya rafiki yake huyo wa zamani na kuandika ujumbe ambao umeashiria kuwa urafiki wao ndio basi tena.


“Neno Moja Kwake…! Temporary Post… Mimi naanza… Alikuwa Rafiki yangu na Tulipendana sana….,” ameandika Wema kwenye picha ya Batuli hiyo hapo juu aliyoiweka kwenye mtandao huo.

Baada ya ujumbe huo wa Wema, Nay wa Mitego amemchochea muigizaji huyo ambaye wote kwa sasa wanakisupport Chadema kwa kuandika, “ @wemasepetu #MudaWetu Wana Maneno Mengi Tatizo Hawa Action… Usi mwamini ndugu Ata Rafiki, wachukulie Wote wanafiki, ishi tu kivyako Binadamu awa aminiki..!

Bongo5


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

Ridhiwani Aanika uhusiano wa Jakaya Kikwete na Lowassa.....Asimulia Jinsi Aliyopigiwa Simu na Baba Yake Baada ya Kupiga Picha na Lowassa.Fahamu zaidi hapa.

Mbunge wa Chalinze, Ridhiwani Kikwete ambaye pia ni mtoto wa rais mstaafu, Dkt. Jakaya Kikwete ameeleza uhusiano uliopo kati ya baba yake na Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa kuwa bado ni maswahiba.

Ridhiwani ametoa ufafanuzi huo kutokana na imani iliyojengeka kuwa kuna uhasama kati ya Dkt. Kikwete na Lowassa ambao awali walikuwa maswahiba wakubwa kabla ya siasa kuingiza doa kwenye uhusiano huo.
 Uhasama huo uliaminika kuwepo na kuongezeka hasa baada ya Dkt. Kikwete kuongoza kamati ya maadili ya CCM iliyoliondoa jina la Lowassa katika orodha ya waliokuwa wakiwania nafasi ya kugombea urais, hali iliyopelekea mwanasiasa huyo kuhamia Chadema na kugombea nafasi hiyo.

Akizungumza wikendi hii na mtangazaji wa Clouds FM, Millard Ayo baada ya kuenea mitandaoni picha inayomuonesha akisalimiana na kuteta na Lowassa, Ridhiwani alieleza kuwa hakuna uhasama kati ya baba yake na mwanasiasa huyo mkongwe kama wengi wanavyoamini.

Aliongeza kuwa amewahi kuwashuhudia wakizungumza na kuwasiliana kama kawaida kwa njia ya simu mara kadhaa.

“Kwanza hakuna ugomvi kati ya watu hawa wawili. Unajua watu wanashindwa kuelewa kwamba hakuna urafiki katika masuala ya kazi. Kwa mfano suala lile la kumtafuta rais, jambo la kutafuta rais sio jambo la Jakaya peke yake,” alisema Ridhiwani.

“Ukweli wa mambo ni kwamba Bwana Lowassa na bwana Kikwete ni watu wanaosaidiana katika mambo mengi sana,” aliongeza.

Katika hatua nyingine, Ridhiwani alieleza kuwa baba yake alipoona picha yake na Lowassa wakisalimiana baada ya kukutana Jumamosi iliyopita Uwanja wa Taifa kwenye mechi ya watani wa jadi, Simba na Yanga alimpigia simu kutoka Ethiopia na kumtaka kuendelea na hali hiyo kwani siasa sio vita.

“Kwa mfano hata jana jioni alinipigia simu, of course alikuwa yuko Ethiopia, akaniambia ‘bwana nimeona kwenye picha uko na bwana Edward [Lowassa] ilikuwa wapi hapo?’, nikamwambia nimekutana nae uwanja wa Taifa tulikuwa tunaangalia mpira,” “[Akasema] ‘aah naye alikuja kuangalia mpira’ nikasema ndio. Akasema ‘okay hayo ndio mambo mnayotakiwa kufanya, msifike sehemu mkaona kama siasa ni vita’.

“Kwahiyo ndio maana mimi baada ya kuongea naye akaniambia siasa sio vita, na mimi niliposhika simu yangu Instagram yangu nikaandika kwamba ‘tunaendelea kujifunza…. Lakini basically najifunza kutoka kwa maneno ya mzee wangu ambaye ameniambia kwamba ‘siasa sio vita na kwamba na ninyi katika umri wenu inabidi muendelee kujifunza’ kwahiyo hata mimi comment yangu kwenye Instagram, actually sababu yake kubwa ni hiyo,” alifafanua.

Ridhiwani alieleza kuwa alimuona Lowassa baada ya kipindi kirefu kupita hivyo aliamua kumfuata na kumsalimia ambapo pamoja na mambo mengine, Lowassa alimuuliza alipo Dkt. Kikwete na akampa salamu zake amfikishie na familia kwa ujumla.

Lowassa alilazimika kujiuzulu nafasi ya uwaziri mkuu mwaka 2008 katika Serikali ya Awamu ya Nne iliyokuwa inaongozwa na Dkt. Kikwete kutokana na sakata la Richmond.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

Mwanamuziki Timbulo Aiponda Label ya QS Mhonda...Adai Haijui Muziki ndio Imempotezea Muda Q Chief.Fahamu zaidi hapa.

Timbulo amedai kuwa licha ya wimbo wake hivi karibuni kuvuja ikiwa na ID ya label ya QS Mhonda, haimaanishi kuwa amesainishwa na label hiyo.

Akiongea na Pride FM, Timbulo amedai kuwa wimbo huo ulirekodiwa kipindi ambacho walikuwa na makubaliano ya kufanya kazi pamoja na sio kusainishwa. “Siwezi kusaini na QS, sio label ya muziki ambayo mimi naiona inaweza kukuza muziki wangu,” Timbulo alimuambia mtangazaji wa redio hiyo, Eddy Msafi.

“Sio label ya muziki Tanzania ambayo inafanya hata muziki ambao unatakiwa Tanzania. Hawajui chochote kuhusu muziki, hiyo ni label ambayo labda wangekuwa wanafanya vitu vingine kama masuala ya ujenzi na vitu vingine kibao ambavyo mkurugenzi amesomea,” amesisitiza.

Hivi karibuni label hiyo ya QS Mhonda imeingia kwenye headlines kutokana na kuwa na ugomvi na Q-Chief aliyekuwa amesainishwa mkataba wa maisha. Chief amepigana hadi amefanikiwa kujitoa kwenye label hiyo kwa madai kuwa haikuwa ikimsaidia kwa lolote.

Yenyewe ilidai kuwa imetumia zaidi ya shilingi milioni 200 kwa Q-Chief lakini haijawahi kupata faida. Moja ya kitu kikubwa ambacho kampuni hiyo imefanya ni kumuanganishia collabo na msanii wa Nigeria, Patoranking ‘Koku’ ambayo inaonekana kama ilikuwa ni ya kupoteza muda. Wimbo huo ulivuja mtandaoni na kupotea ndani ya muda mfupi.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

Monday 27 February 2017

Download wimbo mpya wa Nombo unaoitwa "Nalia".

Download wimbo wa Nombo-Nalia.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

Download wimbo mpya wa JamboSquad unaoitwa "Mamiloo".

Download wimbo wa JamboSquad - Mamiloo.



Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

Download wimbo wa Barakah Da Prince & Alex B Wasong unaoitwa "Sijui Raha".

Download wimbo wa Barakah Da Prince & Alex B Wasong - Sijui Raha.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

Download wimbo mpya wa Tunda Man unaoitwa "Simba".

Download wimbo wa Tunda Man - Simba.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa
                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

Zitto Kabwe Aandika Ujumbee Huu Baada Ya Godbless Lema Kunyimwa Dhamana.Fahamu zaidi hapa.

Baada ya Mahakama ya Rufani ya Tanzania iliyokaa Arusha kutupa Rufaa zote mbili zilizofunguliwa na Serikali dhidi ya maamuzi ya Mahakama Kuu Kanda ya Arusha kuhusiana na dhamana ya mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema, Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe amezungumza.

Kiongozi huyo wa ACT ametumia Facebook kutoa malalamiko yake:
Mnamkamata mtu kwa kosa lenye dhamana. Mahakama Kuu inaruhusu dhamana. Serikali inakataa rufaa kuzuia dhamana. Mtu anakaa jela miezi 4, tena mwakilishi wa watu. Siku ya hukumu kuhusu dhamana Serikali inaondoa shauri mbele ya jopo la majaji 3. Lengo? Kumkomoa mtu. Siasa za ukomoaji zinajenga chuki kwenye jamii na chuki inazaa visasi. Haitoshi majaji kukemea Ofisi ya DPP. Mfumo wetu lazima uweke uwezo wa waendesha mashtaka wa aina ya kesi ya Mbunge wa Arusha Mjini kuwajibishwa. Wanasheria tazameni namna ya kuwajibisha ofisi ya DPP kwa uonevu wa makusudi dhidi ya wananchi.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

Steve Nyerere, Mama Wema Wafika Pabaya.Fahamu zaidi hapa.

DAR ES SALAAM: Hapatoshi na joto la ugomvi linazidi kupanda kila kukicha kufuatia mama wa mwigizaji Wema Isaac Sepetu, Mariam Sepetu kuingia kwenye mgogoro mzito na Mwigizaji Steven Mengere ‘Steve Nyerere’. Wawili hao wameingia kwenye mgogoro huo baada ya Steve kumtuhumu mama Wema kuvujisha mazungumzo yao ya siri yaliyoshusha tuhuma nyingi kwa viongozi mbalimbali wa serikali wakiwamo mawaziri.

MUVI ILIVYOANZA
Baada ya mazungumzo hayo ya siri kuvuja Alhamisi iliyopita, tathmini za wachangiaji mbalimbali mitandaoni, zilimmwagia lawama mama Wema kwa kuhusika na kusambaa kwa sauti hiyo kwani asilimia kubwa ya mazungumzo yaliyosikika katika ‘clip’ ya sauti hiyo, yalikuwa yakimuaibisha na kumfanya aonekane mmbeya mbele ya jamii hivyo isingekuwa rahisi Steve kuyavujisha.

STEVE NAYE ANENA
Siku hiyohiyo, Steve alizungumza na gazeti dugu na hili, Risasi Jumamosi  ambapo alieleza kwa kifupi kuwa, mama Wema amehusika katika kuvujisha sauti hiyo ili amharibie maisha yake kwani mazungumzo yake yatakuwa yamewachafua mawaziri hao kwa kitendo cha kuwahusisha na suala zima la kumtetea Wema bungeni katika msala wake wa madawa ya kulevya.

WAFIKA PABAYA
Kikizungumza na mwanahabari wetu, chanzo makini ambacho kipo karibu na Steve, kilisema kuwa kitendo cha kuaminika kwamba mama Wema ndiye aliyevujisha sauti hiyo, kilimsikitisha Steve ambapo aliapa kula naye sahani moja kwani bimkubwa huyo alionekana kudhamiria kumharibia maisha. “Steve alikasirika sana. Aliona kabisa mama Wema amemchezea mchezo kwani alipofanya tathmini ya harakaharaka, aligundua kabisa mama Wema alimpigia simu na kumuingiza kwenye mtego makusudi ili yeye aweze kuingia kingi.

“Ndiyo maana ukisikiliza ile sauti, mama Wema alikuwa anamkazania katika eneo lile Odemba aangua kilio Dar muhimu la kumtuhumu Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam (Paul Makonda) ndipo Steve naye akawa anajaa tu bila kujua dhamira ya mama Wema,” kilisema chanzo hicho.

STEVE AJIKOKI

Chanzo hicho kilizidi kuweka bayana kuwa, kitendo hicho cha Steve kuamini mama Wema amemwaga mboga, naye alianza kukusanya data zake ili amwage ugali maana ameona hakuna sababu ya kumtendea haki mtu ambaye amedhamiria kumharibia maisha. “Wewe si unajua Steve na mama Wema wemeshafanya mengi, walikuwa karibu, sasa Steve naye hawezi kukubali, atakuja na bonge moja la bomu ambalo akililipua, mama Wema hatakaa asahau maishani mwake,” kilisema chanzo.

MAMA WEMA HAJALI

Wakati chanzo hicho kikieleza kwamba Steve amejikoki kulipuka na jambo, Ijumaa iliyopita, mama Wema na mwanaye waliitisha mkutano wa vyombo vya habari nyumbani kwake na kueleza kwamba wameamua kuingia vitani kupigania ‘haki’ na alipoulizwa kuhusu kuvujisha sauti yake na Steve, hakuonekana kujali.

“Mimi sijashika simu, halafu kwanza Steve ni mwanangu tu…,” alisikika mama Wema ambaye pia alitumia mkutano huo na mwanaye kutangaza kukihama Chama cha Mapinduzi (CCM) na kuhamia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

WEMA NAYE ALIKINUKISHA

Katika mkutano huo, Wema alisema anatambua kuwa ana kesi lakini kilichomfanya afanye uamuzi huo ni kupigania haki kwa kile alichosema hata kama alikuwa mtuhumiwa, hakupaswa kuchukuliwa kama alivyochukuliwa wakati yeye ana heshima kwenye jamii na alikipigania Chama Cha Mapinduzi katika Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2015. Wema alienda mbali zaidi na kusema, yeye pamoja na wasanii wenzake, wanakidai chama hicho tawala na kwamba licha ya kuongoza dola, hakijamtendea haki hata kama alikuwa mtuhumiwa.


STEVE NAYE ATEMA CHECHE
Juzi Jumamosi, Steve naye aliandaa mkutano wa waandishi wa habari ambapo pamoja na mambo mengine ya ufafanuzi wa yale yaliyosikika katika ‘audio’ yake na mama Wema, alitumia mkutano huo kupinga mambo aliyoyazungumza Wema aliyoona ni ya uongo likiwemo la kudai hawakulipwa katika kampeni.

“Hakuna msanii ambaye anakidai chama katika Timu ya Mama Ongea na Mwanao ambayo mimi nilikuwa mwenyekiti na Wema akiwa makamu mwenyekiti, sijui labda timu nyingine. Kwanza jamani, ifike mahali tuseme ukweli. Wema ninaweza kusema ndiye msanii pekee ambaye alilipwa hela nyingi kuliko wasanii wengine wote,” alisema Steve katika mkutano huo.

MAMA WEMA KUBURUZWA MAHAKAMANI?
Hata hivyo, chanzo kilicho karibu na Steve, kimeeleza kuwa huenda Steve akamfungulia mashitaka mama Wema kwani Sheria ya Makosa ya Mtandao inamruhusu. “Sheria ya makosa ya mtandao imemkalia vibaya kweli mama Wema kwa sababu inaonesha dhahiri yeye ndiye kahusika kumchafua. Steve nilivyomuona, siku si nyingi atamburuza mahakamani,” kilisema chanzo hicho.

MDAU ANENA
Mdau mkubwa wa sinema za Kibongo ambaye hakupenda jina lake litajwe gazetini, alisema suala hilo anavyoliangalia limefika pabaya kwani sasa kila upande unajipanga kumtupia mwenzake mashambulizi na ukizingatia suala limeshakuwa la kivyama sasa.

“Wewe si unajua Wema na mama’ke wamehamia Chadema, watafanya kila linalowezekana ‘kumpiga’ Steve aonekane hafai na Steve naye hatakubali, ameandaa mashambulizi ya kila namna kuhakikisha anawabomoa Wema na mama’ke hivyo sasa hivi usitegemee tena Steve akawa na uhusiano mzuri na familia ya Wema,” alisema mdau huyo.

WALIKOTOKA!
Kabla ya kufikia hapo, Wema na Steve walikuwa marafiki wakubwa walioshibana hadi kufikia hatua ya kuwa kama ndugu kwani familia ya mama Wema iliamini Steve ni kama mtoto wao. Steve na Wema wameshirikiana katika dili nyingi mjini zilizowafanya waingize fedha pamoja serikalini na hata sekta binafsi lakini sasa wamegeuka chui na paka.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

NDANI YA DAKIKA 19, MADRID WAPIGA MABAO MATATU NA KUYAANGUSHA MANYAMBIZI 3-2 LA LIGA.FAHAMU ZAIDI HAPA.

Real Madrid ililazimika kupigana kijeshi na kufunga mabao matatu ndani ya dakina 19 ili kuepuka kipigo kutoka kwa Manyambizi wa Villarreal.

Tayari walikuwa nyumba kwa mabao 2-0, hali ambayo ilitishia “maisha” yao ndani ya La Liga. Mwisho wakashinda kwa mabao 3-2.

Wakalazimika kufanya kazi ya ziada na kufunga mabao hayo matatu kupitia kwa Gareth Bale, Cristiano Ronaldo na Alvaro Morata na haikuwa kazi rahisi. Cheki pichaaaaz


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa


Hali Ilivyo Corner Baa Sinza Baada ya Agizo la Kufungwa Kutokana na Biashara za Machangudoa Kushamiri.Fahamu zaidi hapa.

AGIZO la mkuu wa Wilaya ya Kinondini Mkoani Dar es salaam Ali Hapi, kuzitaka baa zote zilizopo ndani Wilaya ya Kinondoni zinazojihusisha na Biashara ya machangudoa kufungwa, Corner Baa ya Sinza Mori Jijini Dar es Salaam imefungwa kwa sasa.
Ametoa agizo hilo baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa wananchi wa kata ya Kijitonyama waliodai kuwa kuna baadhi ya baa zimekuwa zikiwahifadhi wanaouza miili, hali ambayo ni hatari kwa mazingira na makuzi ya watoto.


“Tutashughulika na changudoa na tutashughulika na wenye baa zinazowahifadhi machangudoa, kwa sababu hili ni suala lililo kinyume cha sheria, serikali inapambana na hili tatizo halafu mwingine analikumbatia, hilo haliwezekani, tutawachukulia hatua za kisheria,” amesema.
Awali, akitoa malalamiko yake kupitia mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya shule ya Sekondari ya Mama Salma Kikwete, mkazi mmoja wa Kijitonyama alidai kuna baa zilizogeuka kero kwao.

Salum Milongo/GPL

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa


LIGI KUU YA WANAWAKE, RATIBA YOTE HII HAPA.

Ligi Kuu ya Mpira wa Wanawake, hatua ya timu sita Bora (6), ilianza rasmi jana kwa Mlandizi Queens ya Pwani kuilaza JKT Queens ya Dar es Salaam mabao 3-2 katika mchezo wa awali mchana kabla ya ule wa jioni Sisterz ya Kigoma kuifunga Fair Play ya Tanga mabao 5-1.
Ligi hiyo inayochezwa Kituo kimoja cha Uwanja wa Karume, Ilala Dar es Salaam inakutanisha timu sita zinazowania ubingwa wa ligi hiyo ya wanawake ambayo inafanyika kwa mara ya kwanza nchini Tanzania. Pia ni ya kwanza kwa nchi za Afrika Mashariki.
Timu sita zilizofanikiwa kufika hatua ya Sita Bora ni JKT Queens ya Dar es Salaam, Mlandizi Queens ya Pwani na Fair Play ya Tanga kutoka Kundi “A” wakati kutoka Kundi “B” zimo Marsh Acedemy ya Mwanza, Sisterz ya Kigoma na Panama ya Iringa.
Mara baada ya mechi za jana Februari 26, 2017; ligi hiyo sasa itaendelea kesho Februari 28, mwaka huu ambako kwa michezo ifuatayo:   
Februari 28, mwaka huu kutakuwa na mchezo kati ya Marsh Academy na Panama saa 8.00 mchana wakati saa 10.00 jioni kutakuwa na mchezo kati ya Mlandizi na Fair Play.
Machi 2, mwaka huu kutakuwa na mchezo kati ya Sisterz na Marsh Academy saa 8.00 mchana wakati saa 10.00 jioni kutakuwa na mchezo kati ya Panama na JKT Queens.
Machi 4, mwaka huu kutakuwa na mchezo kati ya Fair Play na JKT Queens saa 8.00 mchana wakati saa 10.00 jioni kutakuwa na mchezo kati ya Marsh Academy na Mlandizi Queens.
Machi 6, mwaka huu kutakuwa na mchezo kati ya Panama na Sisters saa 8.00 mchana wakati saa 10.00 jioni kutakuwa na mchezo kati ya JKT Queens na Marsh Academy.
Machi 8, mwaka huu kutakuwa na mchezo kati ya Sisters na Mlandizi Queens saa 8.00 mchana wakati saa 10.00 jioni kutakuwa na mchezo kati ya Panama na Fair Play.
Machi 10, mwaka huu kutakuwa na mchezo kati ya Marsh Academy na Fair Play saa 8.00 mchana wakati saa 10.00 jioni kutakuwa na mchezo kati ya Mlandizi na Panama.
Machi 11, mwaka huu kutakuwa na mchezo mmoja tu saa 10.00 jioni ambako JKT Queens watamaliza na Sisterz.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa


BAO LA KICHUYA LILIVYOKATISHA UHAI WA SHABIKI SIMBA MFANYAKAZI WA HOTELI.FAHAMU ZAIDI HAPA.

Shabiki wa Simba, mfanyakazi wa Hoteli ya Protea alianguka na kupoteza maisha baada ya Shiza Kichuya kufunga bao la pili dhidi ya Yanga.

Simba ilitoka nyuma kwa bao moja, ikafunga mawili kupitia Laudit Mavugo na Kichuya na kuibuka na ushindi wa mabao 2-1.

Suleiman Victor alikuwa akisikiliza mpira kupitia redio ya EFM, alianguka na kupoteza maisha wakati akishangilia.

Wafanyakazi wenzake walijitahi kumuwahisha katika Hospitali ya Tumaini enero la Upanga, lakini tayari alipoteza maisha.

Msemaji wa TFF, Alfred Lucan naye alithibitisha hilo.

“Ni kweli tumepata taarifa za shabiki huyo, ni taarifa za masikitiko. Tumeelezwa baada ya kuanguka wakati anashangilia, aliuathiri ubongo wake,” alisema.


Bao la Kichuya lilifungwa katika dakika ya 81 baada ya kutokea pembeni mwa uwanja na kuachia mkwaju mkali.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa


Lema Yupo Gerezani Kwa Sababu Isiyo na Msingi..Ila Hawajui Wanazidi Kumkomaza Kisiasa-Rungwe.Fahamu zaidi hapa.

Mwenyekiti  wa Chama cha Ukombozi wa Umma (Chauma), Hashim Rungwe, amemtembelea Mbunge wa Arusha Mjini, Godbles Lema (Chadema), ambaye   bado yuko mahabusu katika Gereza la Kisongo mkoani Arusha.

Akizungumza na waandishi wa habari  mjini Arusha jana baada ya kuonana na mbunge huyo, Rungwe alisema baadhi ya matatizo yanayotokea kwenye jamii yanasababishwa na baadhi ya watawala.

Alisema hali hiyo imekuwa ikiibua chuki miongoni mwa wananchi   jambo ambalo si zuri na linahitaji kukemewa.

Kiongozi huyo alimtembelea Lema    akiwa  amefuatana  na viongozi mbalimbali akiwamo Makamu Mwenyekiti wa Chauma, Kayumbo Kabutali  na wabunge wa Bukoba Mjini, Wilfred Lwakatare na Moshi Vijijini, Antony Komu,  wote wa Chadema


“Historia ya zamani inatufunza matatizo yanayotokea katika jamii yanachangiwa na mambo yanayotendwa na baadhi ya watawala  ambayo yanaleta chuki.

“Na chuki siyo kitu kizuri kwa sababu inazidi kuwa kubwa kwenye mioyo ya watu hata kama wako kimya,”alisema na kuongeza:

“Hili limewahi kutokea enzi za mitume hata Nelson Mandela aliwekwa ndani na alipotoka dunia nzima iliamka hivyo tunaona kuna baadhi ya watu wanawekwa ndani bila sababu ya msingi, natoa wito kwa wenye mamlaka kuangalia suala hili.”

Mwenyekiti huyo alisema ni wakati wa watanzania wote kwa ujumla kupigia kelele suala hilo kwa vile  Mbunge ambaye ni mwakilishi wa wananchi, anazuiliwa kwa makosa yenye dhamana jambo la kukemewa.

“Tumekuja Arusha   kumuangalia Lema kwa sababu ni mwenzetu na tuna masikitiko na kama walifikiri wakimuweka Lema ndani wanamsimamisha au kumkomesha, wanamkomaza kisiasa.

“Anapata ujasiri wa aina Fulani kwa sababu  haelewi kwa nini yuko ndani, wangemkuta na malori matatu ya silaha sawa,” alisema.

Mbunge wa Bukoba Mjini alisema ameridhishwa na kupata matumaini na hali ya mbunge huyo kwa vile  ni yuleyule na ameongeza ujasiri wa kulisema lile analoamini.

Naye Mbunge wa Moshi Vijiji, Antony Komu,  alisema Lema ameomba wabunge wote bila kuangalia itikadi za vyama vyao wanapaswa kuwa makini wakati wa utungaji wa sheria.

Alisema   kutokana na baadhi ya upungufu wa sheria kuna watu wako gerezani kwa muda mrefu.

Alisema  katika gereza hilo asilimia kubwa wako gerezani kwa muda mrefu kutokana na upungufu wa sheria mbalimbali.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa


CHADEMA Wamwandalia Sherehe Wema Sepetu.......Wapambe Wake 500 Wanaomuunga Mkono Kumfuata.Fahamu zaidi hapa.

Chama cha Demokrasi na Maendeleo (Chadema), kimesema kipo kwenye maandalizi ya kumkabidhi kadi mrembo wa Tanzania mwaka 2006, Wema sepetu, pamoja na kundi lake lenye zaidi ya watu 500.

Wema alikuwa mmoja kati ya wanachama maarufu wa CCM katika kundi la wasanii wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25, mwaka juzi kwa kaulimbiu ya ‘mama ongea na mwanao’.

Akiwa kama kiongozi wa wasanii, alishiriki kumnadi Mgombea Mwenza wa CCM ambaye kwa sasa ni Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan.

Katika mkutano wake na wanahabari mwishoni mwa wiki,  Wema  alisema kwa sasa ameamua kuvaa magwanda na yupo tayari kwa mapambano.

Mkuu wa Idara ya Habari wa Chama cha Demokrasi na Maendeleo (Chadema), Tumaini Makene jana alisema   wapo kwenye maandalizi na kabla ya Machi 5, mwaka huu watamkabidhi Wema kadi ya uanachama   na kundi lake linalomuunga mkono.

“Wema atakabidhiwa kadi kwa utaratibu maalumu maana ameonyesha heshima na nia ya kujiunga kwenye mapambano ya kweli.

“Kwa kweli Chadema tunafarijika sana na kuja kwake maana kuna timu kubwa inayomuunga mkono pia wanataka kujiunga na chama.

“Tena na wengine wanatoka katika mashirikisho mbalimbali  ikiwamo TFF.  Kwa hiyo hapo unapata picha ya Wema ni mwanachama mpya wa Chadema mwenye mvuto wa aina yake na huwezi kubeza hata kidogo kuja kwake,” alisema Makene

Alisema   wakati wowote chama hicho kitatangaza lini mwanachama huyo atakabidhiwa kadi ya Chadema, tukio ambalo alisema litakuwa la aina yake.

Akizungumza nyumbani kwao Sinza, Dar es Salaam mwishoni mwa wiki, Wema alisema amechukua uamuzi wa kuhama CCM baada ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, kumtaja katika orodha ya watu wanaotumia dawa za kulevya.

Alisema kitendo hicho kilimdhalilisha kwa kiwango kikubwa.

“Nimeamua kufanya uamuzi wa kuhama CCM na sasa nahamia Chadema.  Sitaki nionekane labda nimepata hasira kulingana na tuhuma zinazonikabili, lakini nataka nionekane nimefanya uamuzi kama binadamu yeyote angeweza kufanya.

“Nimekubali na nimekiri kwamba nilisema nitakufa nikiwa CCM lakini ya Mungu mengi. Natamani ningejua awali, nasema sijachelewa, naamini uamuzi wangu nilioufanya ni sahihi na nimeingia kwenye vita.

“Nipo tayari kupigana, nina imani kwamba kutakuwa na watu wengine wapo nyuma yangu wengi watanifuata,” alisema.

Wema aliyekuwa na mama yake mzazi, Miriam Sepetu ambaye naye   alitangaza kuhama CCM na kuhamia Chadema, alisema alipokuwa kada wa CCM alikuwa mwaminifu na kwa kipindi chote alikipigania kwa uwezo wake wote.

“Nimetuhumiwa hivi karibuni na nilivyokuwa kama kada nilijitoa maisha yangu, utu wangu, nilipoteza muda wangu kupigania kile ambacho nilikiamini ni sahihi lakini siku moja kisinitupe na kinithamini kwa kile nilichokifanya lakini tofauti na nilivyokuwa natarajia havikutokea.

“Sisemi kama nilikuwa nafanya ili nije kubebwa kama princess (binti wa mfalme) ama queen (malkia) kwa sababu Wema ulikuwa unajitoa basi hata ukikosea usiadhibiwe au ukiwa unatuhumiwa usichukuliwe hatua, hapana, sijamaanisha hivyo,” alisema.

Alisema baada ya kushutumiwa aliamua kukaa kimya muda mrefu kwa kuwa alikuwa anatafakari alipokosea.

“Nimekaa kimya muda mrefu si kwamba nimefurahia kilichotokea, nilikuwa bado natafakari na kutathmini where did I go wrong (wapi nilikuwa nimekosea).

“Ni kitu gani ambacho nimekosa na kufanyiwa hichi nilichofanyiwa, nilichogundua ni kitu ambacho najua mwenyewe siwezi kusema nafurahia,” alisema.

Wema alisema kitendo cha kutuhumiwa bila wahusika kuwa na uhakika na tuhuma kimemnyong’onyeza na kumvunja moyo kwa kiasi kikubwa.

“Wanasema wenyewe ‘tenda wema nenda zako usingoje shukrani’, lakini siku ya mwisho siwezi kuwa mnyonge kwa sababu naamini there is something called democracy (kuna kitu kinaitwa demokrasia) katika nchi yangu na hicho ndicho nataka kukipigania,” alisema.

Alisema  uamuzi aliouchukua ni mgumu lakini hatarudi nyuma na anaamini kuna kundi kubwa la watu wasiopungua 500 watamfuata.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa


Serikali Yasema Makonda Aliingizwa 'Mkenge.Fahamu zaidi hapa.

Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imesema itamchukulia hatua muwekezaji aliyetoa ardhi kwa serikali ya mkoa wa dar es Salaam kwa ajili ya ujenzi wa viwanda, kwa madai kuwa ardhi aliyoitoa siyo yake.


Waziri wa wizara hiyo, William Lukuvi, ametoa kauli hiyo leo jijini Dar es Salaam na kufafanua kuwa muwekezaji huyo aliidanganya serikali pamoja na kumdanganya mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda, ambaye ndiye aliyekabidhiwa eneo hilo kwa niaba ya serikali.

Mbali na kosa la kuidanganya serikali, Lukuvi pia amesema atamchukulia hatua mfanyabiashara huyo kwa kumiliki ardhi kinyume cha sheria.

Kuhusu Mkuu wa Mkoa , Paul Makonda, Lukuvi amesema tayari amekwishafanya naye mawasiliano na kumuelewesha kuwa alidanganywa kwa kuambiwa kuwa anapewa eneo kwa ajili ya viwanda, huku eneo lenyewe likiwa ni mali ya serikali.

Siku ya Jumanne wiki iliyopita Makonda alikabidhiwa ekari 1500 za ardhi na Mkurugenzi wa Azimio Housing Estate Mohamed Iqbal kwa ajili ya ujenzi wa viwanda vidogo vigogo nchini, katika eneo la Kigamboni Dar es Salaam.

Akizungumza mara baada ya makabidhiano hayo eneo la Kisarawe II wilaya ya Kigamboni Mkurugenzi huyo alisema wameamua kumkabidhi eneo hilo ili kuunga mkono jitihada za Rais Magufuli za kuijenga Tanzania ya viwanda na kuwakomboa wananchi wenye uchumi wa kati.

Kwa upande wake Makonda aalieleza kuwa dhamira ya viwanda ya Rais Magufuli inabidi itafsiriwe kwa vitendo, hivyo eneo hilo litatumika kwa ajili ya ufugaji, kilimo, usindikaji, utengenezaji wa sabuni na eneo hilo litatumika na wilaya zote.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa


AUDIO: Askofu Gwajima aelezea sakata zima la Makonda kutumia vyeti vya mtu mwingine.Fahamu zaidi hapa.

Siku kadhaa baada ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kusema kuwa hawezi kujibu madai ya mitandao ya kijamii kuwa alitumia vyeti vya mtu cha kidato cha nne, Askofu Gwajima wa Kanisa la Ufufuo na Uzima ameibuka na kusema kuwa ni kweli alitumia vyeti hivyo.

Askofu Gwajima amesema kuwa anamfahamu sana Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam na kuwa jina lake halisi ni Daudi Bashite na kwamba hilo la Paul Makonda ni la mwenye vyeti hivyo.

Aidha, Askofu Gwajima amedai kuwa anavyovyeti vya Daudi Bashite vinavyoonyesha kuwa hakufaulu na kwamba atashangaa kama Waziri wa Elimu, Prof. Ndalichako atalifumbia macho jambo hili. 
Pia ametishia kuwa, kama mamlaka husika hazitachukua hatua haraka basi yeye atatoka hadharani na vyeti hivyo.

Hapa chini ni sauti ya Askofu Gwajima akihubiri kanisani kwake.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa