Friday 17 February 2017

Watumishi Wawili Wa Tra Wakamatwa Kwa Tuhuma Za Kujihusisha Na Biashara Haramu Ya Dawa Za Kulevya.Fahamu zaidi hapa.

Oparesheni za kuwakamata watuhumiwa wanaojihusisha na dawa za kulevya nchini imefanikiwa kukamata watuhumiwa wawili waliohusika kupitisha kemikali bashirifu za dawa hizo aina ya ephedrine huku wengine wawili wakiwa bado wanasakwa na polisi

Akitoa taarifa hiyo leo Jijini Dar es Salaam Kamishna wa Oparesheni wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya Bw. Mihayo Msikhela amesema watuhumiwa hao ni wafanyakazi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na wamegundulika baada ya kufanya uchunguzi wa ripoti ya majina iliyokabidhiwa kwao na uongozi wa mkoa wa Dar es Salaam.

Kamishan Msikhela amesema taratibu zinazotumika kwa sasa za kuwakamata watuhumiwa wa madawa ya kulevya ni za kiusalama zaidi ili kuzuia watuhumiwa wasipoteze ushahidi.

Aidha, Kamishna Msikhela amesema katika operesheni ya kupambana na dawa za kulevya inayoendelea nchini mikoa ya Simiyu, Mara na Lindi inaongoza katika uteketezaji wa madawa ya kulevya ya bangi na mirungi kwa kipindi cha siku nne.




Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment