Friday 24 February 2017

RICH Mavoko Atoa Povu Kwa Wanaosema Amekosea Kujiunga na Lebo ya Diamond WCB.Fahamu zaidi hapa.

Muimbaji wa Kokoro, Rich Mavoko amedai kuwa kama bado kuna watu wanaona uamuzi wake wa kusainishwa na label ya Diamond, WCB ni kujishusha sababu yeye ni msanii mkubwa, hawaijui biashara yake.


“Mimi nakutana vitu vingi, mtu mwingine nyuma ya pazia haoni,” muimbaji huyo alikiambia kipindi cha Ngaz Kwa Ngaz cha Salama Jabir.
“Tunashoot, tunatoa video, tunarelease ngoma inahit, mimi ndo nakuwa napata tabu.Mtu anayesema nimejishusha kimuziki kujiunga WCB anakuwa hajui biashara yangu,” aliongeza.

Rich alisainishwa na WCB mwaka jana na kuachia wimbo wake wa kwanza, Ibaki Story.

Kwa upande mwingine, Rich alidai kuwa asipofanya muziki atakuwa akiwaandikia watu wengine mashairi na kwamba Tanzania ina upungufu mkubwa wa waandishi wa Bongo Flava.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa


0 comments:

Post a Comment