Monday 27 February 2017

Hali Ilivyo Corner Baa Sinza Baada ya Agizo la Kufungwa Kutokana na Biashara za Machangudoa Kushamiri.Fahamu zaidi hapa.

AGIZO la mkuu wa Wilaya ya Kinondini Mkoani Dar es salaam Ali Hapi, kuzitaka baa zote zilizopo ndani Wilaya ya Kinondoni zinazojihusisha na Biashara ya machangudoa kufungwa, Corner Baa ya Sinza Mori Jijini Dar es Salaam imefungwa kwa sasa.
Ametoa agizo hilo baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa wananchi wa kata ya Kijitonyama waliodai kuwa kuna baadhi ya baa zimekuwa zikiwahifadhi wanaouza miili, hali ambayo ni hatari kwa mazingira na makuzi ya watoto.


“Tutashughulika na changudoa na tutashughulika na wenye baa zinazowahifadhi machangudoa, kwa sababu hili ni suala lililo kinyume cha sheria, serikali inapambana na hili tatizo halafu mwingine analikumbatia, hilo haliwezekani, tutawachukulia hatua za kisheria,” amesema.
Awali, akitoa malalamiko yake kupitia mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya shule ya Sekondari ya Mama Salma Kikwete, mkazi mmoja wa Kijitonyama alidai kuna baa zilizogeuka kero kwao.

Salum Milongo/GPL

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa


0 comments:

Post a Comment