Tuesday 31 May 2016

Kurasa ya bet_africa ilivyokiki baada ya post ya mtoto wa Diamond Platnumz.Fahamu zaidi hapa.

Kurasa ya bet_africa ilivyokiki baada ya post ya mtoto wa Diamond Platnumz ‘Tifah‘ amabyo ilikuwa post kwenye kipengele chao cha Cute Day Selection.
Post yao ilisema “Our #CuteDay selection today is @diamondplatnumz‘ s daughter Princess Tifah ❤️” na baad aya hapo imekuwa post iliyopata comment nyingi zaidi kuliko post yoyote waliyowahi kuweka kwenye kurasa hii ya instagram ya kituo cha BET kwenye tawi lao la Afrika.

#YALIYOJIRI>>>>Mbowe#Tupo Tayari Kutimuliwa Wote Bungeni.Fahamu zaidi hapa.

Naibu Spika wa Bunge, Dk Tulia Ackson sasa amesababisha makubwa zaidi; wabunge kutoka vyama vya upinzani wako radhi kutimuliwa wote iwapo kiongozi huyo ataongoza vikao vyote vilivyosalia na wao kuendelea na msimamo wao wa kumsusia. 

Jana, Dk Ackson aliingia kuongoza kipindi cha maswali na majibu na wabunge wote wa vyama vya upinzani wakatoka ndani ya ukumbi na alipomuachia mwenyekiti wa Bunge, Andrew Chenge kuendelea na shughuli zilizosalia, walirejea ukumbini. 

“Kama Naibu Spika atakuwepo kwenye kile kiti, hatatuona bungeni, hata kama ni leo, ni kesho hata Bunge lote. Tuko tayari kuchukua gharama hiyo,” alisema kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani, Freeman Mbowe akiwa nje ya ukumbi wa Bunge baada ya kuongoza wabunge wenzake kutoka ukumbini wakati wa kipindi cha maswali na majibu. 

Kauli hiyo ya Mbowe imekuja siku moja baada ya Dk Ackson kukataa Bunge kujadili sakata la wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom) waliotimuliwa kwa maelezo kuwa hawafundishwi kwa muda mrefu kutokana na walimu wao kugoma wakidai malimbikizo yao. 

Kitendo cha Dk Ackson kukataa hoja hiyo ijadiliwe, kilisababisha vurugu bungeni kiasi cha kuita askari kuingia kuwatoa wabunge waliokuwa wakipiga kelele na baadaye kuwaamuru waliokataa kukaa waondoke ukumbini. 

Wakiwa nje, walifikia uamuzi wa kususia vikao vyote vitakavyoongozwa na Naibu Spika na wakaanza kutekeleza uamuzi huo jana asubuhi. 

Kauli ya Mbowe pia imekuja siku moja baada ya Kamati ya Maadili, Kinga na Haki za Bunge kuwasimamisha wabunge saba kutoka vyama vya upinzani kuhudhuria vikao vya kuanzia mkutano huu hadi ujao kwa maelezo kuwa walifanya fujo wakati wakipinga hoja ya Serikali ya kusimamisha matangazo ya moja kwa moja ya baadhi ya shughuli za Bunge. 

Jana, Mbowe alisema wako tayari kutimuliwa wote kama uamuzi huo utawapendeza viongozi wa Bunge kwa kuwa siasa inaweza kufanywa ndani na nje ya Bunge. 

Mbowe alisema kuwa hali ilishafika hatua nzuri ya kujenga demokrasia nchini na kwamba pamoja na matatizo yaliyokuwepo, hali ilikuwa ikienda vizuri. 

“Lakini tangu kuingia kwa Serikali ya Awamu ya Tano mnaweza kuona Bunge limegeuka kituko. Bunge limegeuka mahali pa kukomoana. Bunge limekuwa mahali pa kutishana,” alisema Mbowe. 
“Naibu Spika anaamua kusitisha mjadala wa maana ili apate muda wa kuwadhibiti na kuwafukuza wabunge bungeni na anaona sifa. 

Tunaacha kujadili hoja ya msingi kama mambo ya Udom. Watoto wadogo wanalala nje haoni ni muhimu, anaona muhimu ni kuwafukuza wabunge wa upinzani.” 
Mbowe, ambaye pia ni mbunge wa Hai, alisema hawezi kukaa, kumsikiliza na kumheshimu Dk Ackson, bali wapinzani wataheshimu anayewaheshimu bila kujali anatoka chama gani na hawatamuheshimu asiyewaheshimu bila kujali cheo chake. 

“Sasa leo (jana) tumekataa kushiriki kipindi cha maswali na majibu kwa sababu yeye (Dk Ackson) anasimamia kipindi hicho na akitoka tutarudi bungeni. 

Akija mwenyekiti, akija Spika mwenyewe tutarudi bungeni. Lakini kama Naibu Spika atakuwepo kwenye kile kiti hatatuona bungeni, hata kama ni leo, ni kesho hata Bunge lote. Tuko tayari kuchukua gharama hiyo,” alisema Mbowe.
Dk Ackson alikuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuanzia Septemba mwaka 2015 hadi Novemba 2015 alipochukua fomu za kugombea uspika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano kwa tiketi ya CCM. 

Siku moja kabla ya CCM kuchagua mgombea wake, Dk Ackson alijitoa, hatua iliyoonekana ni kumpisha kada mwenye uzoefu zaidi, Job Ndugai. 

Wakati CCM wakisubiri uchaguzi wa mgombea wao, Rais John Magufuli alimteua Dk Ackson kuwa mbunge na baadaye akachukua fomu za kuwania unaibu spika, akiwa mgombea pekee wa chama hicho. 

Tangu aanze kuongoza Bunge, Dk Ackson amekuwa akikwaruzana na wabunge wa upinzani, ambao walishawahi kuhusisha kuteuliwa kwake na Rais kuwa mbunge ili apate mwanya wa kugombea unaibu spika, na mpango wa Serikali kutaka kulidhibiti Bunge. 

Akizungumzia mkakati wao jana, Mbowe alisema kwa kuwa siasa haifanywi bungeni tu, watakwenda kwa wananchi kuwashitaki viongozi wa Bunge. 

Alisema watafanya hivyo kwa kuwa kitendo cha kuwafungia wabunge wa upinzani kuwatetea wananchi ndani ya Bunge, kinaweza kufanywa pia nje ya chombo hicho. 

“Tutawaamsha wananchi nje ya Bunge kwa kuwa ni fursa hivyo tunakutana na wabunge wote waliotimuliwa na tutaungana wote bila kujali chama cha siasa kwa kuwa tumekubaliana kusimamia ajenda ya nchi na si ya chama chochote,” alisema Mbowe. 

LHRC yataka wabunge warudishwe 
Wakati wabunge saba wakianza kutumikia adhabu ya kufungiwa kuhudhuria vikao, Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kimelitaka Bunge kuwarejesha ili kuendelea na majukumu yao. 

Mkurugenzi mtendaji wa kituo hicho, Dk Helen Kijo Bisimba alisema hoja ya kuwafukuza wabunge hao kwa sababu ya kudai haki ya kurushwa bunge ‘live’ ni kuwapokonya haki Watanzania waliowachagua kwenda kuwawakilisha bungeni. 

“Wabunge hao wamechaguliwa na wananchi na wanatetea bunge hilo kurushwa ‘live’ kwa maslahi ya wananchi waliowatuma, halafu kiti cha Spika kinaamua kuwafukuza bungeni. 

"Endapo ningepewa nafasi ya kuwashauri wapiga kura, ningewaambia kwenda kushiriki vikao vya Bunge wenyewe kwa sababu wabunge wao wameondolewa bungeni, hata mimi mbunge wangu wa Kawe ameondolewa,”alisema.

#YALIYOJIRI>>>Wahadhiri UDOM Wataja Kiini cha Mgomo Kilichosababisha Wanafunzi 7802 Warudishwe Nyumbani.Fahamu zaidi hapa.

JUMUIYA ya Wanataaluma ya Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOMASA) imesema kilichotokea si walimu kugoma kufundisha programu ya Stashahada Maalumu ya Elimu, Sayansi, Hisabati na Tehama, bali tatizo ni kutoelewana na Menejimenti ya chuo kutokana na mazingira mabovu ya uendeshaji wa programu hiyo chuoni hapo.

Aidha, imelaani kitendo cha wanafunzi 7,802 wa Programu Maalumu ya Ualimu wa Msingi na Sekondari, waliorudishwa nyumbani bila kupewa muda wa kutosha kujiandaa kwa kuzingatia umri wao na mazingira waliyokuwa wanaishi, hali inayofanya wazagae mitaani huku wakiwa hawana pa kwenda.

Hayo yako kwenye tamko lililotolewa jana na Katibu wa jumuiya hiyo, Lameck Thomas, ambalo lilieleza kuwa lawama zimekuwa zikitupwa kwa walimu kutokana na taarifa hizo kutolewa na upande mmoja, ambao ni Menejimenti ya chuo kwenda serikalini bila kuwepo na taarifa yoyote kutoka kwa walimu kupitia jumuiya yao.

Thomas alisema si kweli kama walimu waligoma kufundisha lakini tatizo kubwa ni kutoelewana kati ya walimu na Menejimenti ya chuo kutokana na mazingira mabovu ya uendeshaji wa programu hiyo chuoni hapo.

"Hatuzungumzii fedha zaidi tunazungumzia suala la kuboresha elimu ili taifa lipate walimu wa baadaye katika kufundisha Sayansi, Hisabati na Tehama, vifaa vya kufundishia navyo ni changamoto kubwa,” alisema.

Katibu huyo alisema kama Jumuiya ya Wanataaluma wanapata hisia kwamba Wizara ya Elimu, imeamua kwa makusudi kushirikiana na uongozi wa chuo kupotosha uhalisia wa jambo hilo kwani hakuna hata wakati moja ambao wamefanya mawasiliano na walimu wenyewe kupata ukweli kutoka upande wao.

“Alichosema waziri bungeni juzi ni taarifa ya upande mmoja ambayo haitatupeleka kwenye utatuzi wa kudumu wa suala hili kutokana na ukweli kwamba walimu nao wana mengi ya kuzungumza,” alisema katibu huyo.

Alisema serikali imejenga desturi ya kuonana na menejimenti za vyuo pindi yanapotokea matatizo bila kupata taarifa kutoka vyanzo vingine hali ambayo imekuwa inasababisha vyanzo sahihi vya matatizo kutojulikana kwa uwazi.

Alisema changamoto za ufundishaji kutokana na uhaba na walimu kulingana na idadi ya wanafunzi waliopo. Akitoa mfano alisema kwa sasa Chuo cha Sayansi Asilia na Hesabu, kina upungufu wa walimu 128 waliokuwa wanahitajika kufundisha programu hiyo kwa ufanisi; na kwa muhula uliopita walimu 72 tu ndio walibeba mzigo wa upungufu huo na muhula huu hali ilikuwa inaelekea kuwa mbaya zaidi.

“Wingi wa wanafunzi na uhaba huu wa walimu ulisababisha upangaji wa ratiba na kufundisha kutokana na ukweli kwamba kozi ziligawanywa katika mikondo mingi ambayo walimu walilazimishwa kuifundisha huku wakiwa na majukumu ya kufundisha kozi za shahada na majukumu mengine,” alifafanua.

Alisema chuo kimekuwa na desturi ya kupokea wanafunzi wengi bila kuzingatia idadi ya walimu waliopo na miundombinu ya kufundishia na kujifunzia na hiyo si mara ya kwanza kwa chuo kufanya hivyo, kwani mwaka 2008 walileta wanafunzi wengi ambao matokeo yake walimu kufundisha masomo mengi kuliko uwezo wao wa kazi.

Alisema taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Taaluma ilipotoshwa, kwani haijaeleza ukweli wa madai uliowasilishwa na chuo husika. 

Alisema katika Chuo cha Sayansi Asilia na Hesabu taarifa inasema yaliyowasilishwa ni madai ya Sh milioni 367.8 na kupungua mpaka Sh milioni 90 wakati uhalisia ni kwamba madai hayo hata yangebanwa namna gani yasingepungua mpaka chini ya Sh milioni 223.7.

Alisema mfano mwingine ni Chuo cha Elimu Masafa na Sayansi za Kompyuta ambao taarifa inasema waliwasilisha madai yanayozidi Sh milioni 100 wakati taarifa ya chuo inasema ni madai ya Sh milioni 53.7 tu.

Mwenyekiti wa jumuiya hiyo, Edson Baradyana alisikitishwa na yaliyotokea na kuitaka serikali kufanya jitihada za makusudi ili kumaliza mgogoro huo na hilo litawezekana kama walimu, wanafunzi na Menejimenti kukaa pamoja.

Baradyana alisema wanafunzi hawakutendewa haki kwani ilitolewa notisi ya ghafla ya kuondoka chuoni huku wengine wakiwa hawana nauli na hawakujua pa kwenda hali inayofanya waendelee kuzurura mitaani.

Alisema wanaamini kama Menejimenti ya chuo ingeonesha ushirikiano wa karibu kwa walimu wanaofundisha programu hiyo na kushirikiana, hayo yasingetokea au yasingekuwa makubwa kiasi hicho.

“Lazima kuangaliwa na kutatuliwa kwa changamoto nyingine zilizoibuliwa na wanataaluma na wanafunzi katika uendeshaji wa programu hiyo badala ya kujikita kwenye suala la malipo tu, serikali iwe na utaratibu wa kuwasiliana na walimu na wanafunzi mara kunapotokea matatizo vyuoni ili kupata taarifa toshelezi kutoka pande zote,” alisema Mwenyekiti wa Udomasa.

Aidha, wakati wa kurejeshwa nyumbani kwa wanafunzi hao wa Udom kukibebwa kisiasa na vyama vya upinzani, taarifa ya serikali imeeleza kuwa wahadhiri waliogoma, walitaka kulipwa posho ya zaidi ya Sh milioni 900.

Akitoa taarifa ya pili bungeni juzi usiku, Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako  alisema wanafunzi hao si sehemu ya kazi zilizoko katika mikataba ya ajira ya wahadhiri hao, ila ni sehemu ya kazi ya ziada.

Kwa kuwa kazi hiyo ni ya ziada, Profesa Ndalichako alisema walikubaliana walipwe posho ya kazi ya nyongeza ambayo uongozi wa Chuo Kikuu cha Dodoma ulikuwa tayari kutoa zaidi ya Sh milioni 200.

Kwa mujibu wa Profesa Ndalichako, wahadhiri hao walisisitiza kuwa wanataka posho hiyo iwe zaidi ya Sh milioni 900, jambo lililokataliwa na Mkaguzi wa Ndani wa Mahesabu wa Udom aliyesema kuwa kiwango hicho ni kikubwa kuliko uhalisia wa kazi yenyewe.

Kutokana na kutokubaliana kati ya wahadhiri hao na uongozi wa Udom, wahadhiri hao ndio wakaitisha mgomo wa kufundisha wanafunzi hao huku wakiendelea na kazi za kufundisha walio katika programu za shahada ya kwanza na kuendelea.

Profesa Ndalichako alisema kwa uamuzi huo wa wahadhiri, serikali isingeweza kuwachukulia hatua kwa kuwa wamegomea kazi ya ziada na si kazi waliyoajiriwa na kuingia mkataba na chuo.

Kwa hali hiyo, Profesa Ndalichako alisema serikali ililazimika kuingilia kati ambapo Mei 10, mwaka huu Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Stella Manyanya alikwenda chuoni hapo kutafuta suluhu.

Mbali na Naibu Waziri, alisema hata makatibu wakuu wa wizara hiyo nao walikwenda kuzungumza na wahadhiri hao bila mafanikio, huku wanafunzi hao wakikaa chuoni bila kuingia darasani kwa wiki ya tatu.

Profesa Ndalichako alisema mbali na madai ya wahadhiri hao, pia wakati wa kutafuta suluhu ya jambo hilo, walitazama suala la tija kwa wanafunzi hao wa diploma maalumu ambao ni zaidi ya 7,800 na pia kwa wanafunzi wa shahada ya kwanza ambao pia wanapaswa kufundishwa na wahadhiri hao.

Kutokana na kukosa masomo kwa wiki tatu mfululizo na kuwepo kwa uwezekano wa kukosekana tija katika ufundishaji, Profesa Ndalichako alisema ndio uamuzi wa kuwarudisha nyumbani wanafunzi hao ukafanyika ili serikali iangalie upya utaratibu wenye tija zaidi wa kuwaendeleza wanafunzi hao.

Aidha, Profesa Ndalichako alisema wakati wanafunzi hao wakitakiwa kurudi nyumbani, walizingatia hali yao ya kipato, kwa kuwa tayari walikuwa wameshapewa fedha za kujikimu za siku 60 tangu Aprili 21, mwaka huu. 

Profesa Ndalichako aliwataka wanafunzi hao kuvuta subira wakati serikali inatafuta namna bora ya kuwapatia elimu hiyo kwa kuzingatia tija kwao.

#YALIYOJIRI>>>> Rais Magufuli Awatangazia Vita Wafanyabiashara ‘Wajanja’.Fahamu zaidi hapa.

Rais John Magufuli amesema Serikali yake itaendelea kupambana na wanaoingiza bidhaa zilizochini ya kiwango na wale wanaokwepa kodi.

Amesema kwa kufanya hivyo, wanachangia kuviua viwanda vya ndani ya nchi.

Rais Magufuli ameyasema hayo jana kwenye hafla ya utaoji wa Tuzo ya Rais ya wazalishaji bora wa viwandani kwa mwaka 2015 zilizofanyika jijini Dar es Salaam.

Tuzo hizo zimeandaliwa na Shirika la Wenye Viwanda Nchini (CTI).

Rais amesema pia hatawavumilia watendaji wote watakao wakwamisha wafanyabiashara wenye nia ya kuanzisha viwanda nchini kwa sababu zisizo za msingi na kuwaahidi kuwasaidia waweze kufanikisha ndoto zao.

Pia, amesema ni vizuri wafanyabiashara wote nchini wakatumia fursa zipatikanazo katika awamu hii ya uongozi wake, ili wasije kuzijutia baadaye.

“Nasema kwa dhati kutoka moyoni, you have my support, mkishindwa katika kipindi cha awamu ya tano basi hamtaweza tena,” alisema.

Rais Magufuli alisema nchi inapokuwa na viwanda vingi vitatoa ajira kwa Watanzania, vitaongeza mapato kwa Serikali na kuingiza fedha za kigeni kwa kuuza bidhaa nje ya nchi.

“Nina dhamira ya dhati ndani ya moyo wangu kuwasaidia wenye nia ya kuanzisha ya viwanda, siwachukii matajiri nawapenda matajiri,” alisema.

Rais Magufuli aliwapa moyo wafanyabiashara wenye viwanda kuanzisha vingine ili Serikali iweze kunufaika zaidi.

Alisema Tanzania ina rasilimali nyingi kama maliasili na madini na akawahakikishia wawekezaji kuwa lipo soko kubwa la bidhaa watakazozitengeza lenye watu milioni 160 katika nchi za Afrika Mashariki na Kati.

Magufuli alisema sekta ya viwanda ni muhimili mkubwa wa uchumi katika nchi huku akitolea mfano wa nchi za China, India, Korea Kusini, Malaysia, Thailand na Vietnam  ambazo zimekuwa kwa kasi kwa sababu ya uwepo wa viwanda.

Alisema viwanda vinapoanzishwa nchini badala ya kuuza mali ghafi kwa bei ndogo zitatengenezwa bidhaa ambazo zitauzwa nje ya nchi na kutoa ajira kwa Watanzania.

“Badala ya kuuza ngozi tutengeneze viatu hapa hapa nchini au badala ya kuuza ng’ombe Comoro tumepeke nyama iliyosindikwa,” alisema.

Alisema nchi kama ya Sudan Kusini ina mahitaji makubwa ya unga wa mahindi.

“Lakini wanaofaidika na soko hilo ni Wakenya ambao wanakuja nchini wananunua mahindi, wanasaga na kuyapeleka huko,hivi wafanyabiashara tunashindwa hata kuanzisha viwanda vya kusaga mahindi,” alisema

Alisema Mkoa wa Arusha una ng’ombe wa  maziwa lakini yananunuliwa na Wakenya ambao wanayasindika kwenye viwanda vyao na kuja kuyauza hapa nchini.

Hata hivyo, alisema Serikali inaangalia uwezekano wa kuanzisha benki ya maendeleo ya viwanda kwa lengo la kutoa mikopo yenye masharti nafuu na riba ndogo.

Kuhusu kuondoa kwa changamoto mbalimbali zinazokwamisha maendeleo ya viwanda nchini, Magufuli alisema Serikali imeshatenga Sh1trilioni katika mwaka wa fedha ujao kwa ajili ya ujenzi wa reli ya kati kwa ajili ya kurahisisha usafirishaji wa bidhaa mbalimbali.

Pia, Serikali imeunda kamati maalumu itakayoangalia mazingira ya ufanyaji biashara nchini ikiwamo kodi na tozo mbalimbali.

“Nchi yetu inakuwa na kodi za ajabu ajabu, mfano zao la kahawa kulikua na zaidi ya kodi 30. Haya ndiyo tunayoyaangalia,” alisema.

 Kuhusu upatikanaji wa mitaji na riba kubwa zinazotozwa na benki, alisema katika kukabiliana na matatizo hayo Serikali inajiandaa kuanzisha benki ya viwanda itakayowasaidia wenye wawekezaji.

Kwa upande wake  Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage alisema Serikali imejikita katika kuhamasisha ujenzi wa viwanda vingi zaidi nchini.

“Tumeandaa mkakati wa pamba hadi inakuwa nguo, alizeti hadi mafuta na tunaendelea kufufua viwanda vilivyokufa,” alisema.

Akizungumzia changamoto zinazowakabiri wenye viwanda nchini, mwenyekiti wa Shirikisho la Wenye Viwanda (CTI), Samuel Nyantahe alisema uchakavu wa miundombinu ya umeme na miundombinu ya barabara imekuwa ikiongeza gharama za uzalishaji.

Pia, alilalamikia uwapo wa utitiri wa kodi, mamlaka za usimamiaji biashara na uwapo wa bidhaa bandia zinazotishia bidhaa za ndani

Jacqueline Wolper afunguka kuwa alifilisiwa na ‘Mkongo’ hadi hana gari wala pakulala.Fahamu zaidi hapa.

Msanii wa filamu, Jacqueline Wolper baada ya kukiri kwamba anatoka kimapenzi na Harmonize, amefunguka na kueleza madai ya kufilisiwa na Mkongo ambaye alikuwa mpenzi wake wa zamani. Akiongea katika promo ya kipindi kipya cha Take One ambacho kinatarajiwa kuruka Jumanne hii, Wolper amedai yeye ndiye aliyetendwa na Mkongo ambaye alikuwa mpenzi wake, kwani wakati anaanza naye mahusiano alikuwa ana gari na nyumba lakini baadae akijikuta hana hata sehemu yakulala.
 
Jacqueline Wolper na Mkongo 

Muigizaji huyo ambaye amekuwa akionyesha uwezo mkubwa katika filamu zake, amedai alikuwa anajilipia nyumba kwa dola, lakini ulifikia wakati akafilisika na kuanza kulala hoteli.

Wolper amedai mahusiano hayo yalimsababishia kugombana na baadhi ya watu wake wa karibu ambao walikuwa wakimshauri vizuri, lakini yeye alikuwa akiwaaona kama wanamfitini.

Muigizaji huyo ambaye amewahi kutamba na filamu yake Tom Boy, kwa sasa anatoka kimapenzi na hit maker wa wimbo ‘Bado’, Harmonize kutoka WCB.

Habari Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya June 1 yako hapa.



#MICHEZO>>>SERIKALI YAPIGA MKWARA MZITO UCHAGUZI WA YANGA.Fahamu zaidi hapa.

Kizingumkuti cha uchaguzi mkuu wa yanga chaendelea baada ya zoezi la uchukuaji fomu za kugombea nafasi mbalimbali katika klabu ya Yanga kuwa na sintofahamu kubwa.

Serikali ilitoa maelekezo ya kuelekea uchaguzi huo lakini kunaonekana kuwepo kwa vikwazo mbalimbali ili zoezi hilo lisifanikiwe.

huyu hapa kaimu katibu mkuu wa BARAZA LA MICHEZO LA TAIFA
akielezea.

Nyongeza Ya Majina ya Vijana Waliomaliza Kidato cha 6 Wanaotakiwa Kujiunga na JKT Kabla ya Tarehe 10 Mwezi wa 6.

Vijana wafuatao wameongezwa kuhudhuria mafunzo ya jkt katika makambi mbalimbali kama inavyoonekana hapo chini.

Pia baadhi ya vijana wamehamishwa makambi kutokana na sababu mbalimbali.Waripoti kwenye makambi kama inavyoonekana  hapa chini kabla ya tarehe 10 juni 2016.

S/NO    JINA                                                        KIKOSI
1     ABDILLAH RAMADHANI HAJI         MGAMBO JKT
2     ABDUL M. MTEKETA         MGAMBO JKT

3     ABDULAZIZ SALUM AHMAD         MARAMBA JKT

4     AGNES PETER MAGANGA         RUVU JKT

5     AGNESS EMMANUEL KITANDU         RUVU JKT

6     AGNESS PETER MAGANGA         MARAMBA JKT

7     AJUAE DAVIS AMINIELI         KANEMBWA JKT

8     ALEX MLOSO         MARAMBA JKT

9     ALFRED AIDAN MBANO         RUVU JKT

10     ALLY KAFERA ALLY         KANEMBWA JKT

11     ALVIN ISMAEL MAKUNDI         RUVU JKT

12     AMBWENE FRANK MWAKANEMA         MARAMBA JKT

13     AMOS ASEGE         RUVU JKT

14     AMOS KINGU         MARAMBA JKT

15     ANNA JORAM TIMBA         RUVU JKT

16     ANNA M. JANUARY         MSANGE JKT

17     ANTIA PANCRAS KAKWERA         RUVU JKT

18     AVITUS MUSHABI         RUVU JKT

19     BEATRICE BONFACE         MARAMBA JKT

20     BEAUTNESS JOHN NJAU         RUVU JKT

21     BENJAMIN STEPHEN NYANDA         RUVU JKT

22     BERNADINAH T. MAYOMBYA         RUVU JKT

23     BIBIANA CLETUS NJOKHA         RUVU JKT

24     BONIFACE DEOGRATIUS         RUVU JKT

25     BONIFACE JOHN         RUVU JKT

26     BRENDA JOHN BABU         MARAMBA JKT

27     BUNURI JUMA         RUVU JKT

28     CALISTER MKOLO         RUVU JKT

29     CAROLINE HENRY KABOGO         MARAMBA JKT

30     CAROLINE SOSTHENES MAHERI         RUVU JKT

31     CECILIA MPEMBA         RUVU JKT

32     CLEMENCE GWINO         RUVU JKT

33     COSTANTINE PETER         RUVU JKT

34     DANIEL BENEDICT MASHIKU         MAKUTOPORA JKT

35     DAVID L. MARIBA         RUVU JKT

36     DAVID R. MKUMBO         RUVU JKT

37     DENIS G SADALA         MARAMBA JKT

38     DEOUS SILIVESTA LUBINGA         RUVU JKT

39     DIALO MNYUKI         MAFINGA JKT

40     DICKSON JOCTAN MATOGO         MARAMBA JKT

41     DONAT ERENEST MAJALA         MAKUTOPORA JKT

42     DONATH ERNEST MAJALA         MAKUTOPORA JKT

43     DORCUS DEOGRATIUS         RUVU JKT

44     EDDAH SAUL ASWILE         RUVU JKT

45     EDWARD MMBARA MKIZU         MARAMBA JKT

46     ELAIN DIDAS MUTABINGWA         RUVU JKT

47     ELIAN E. NGONDO         RUVU JKT

48     ELINAZI YOAZ MSUYA         RUVU JKT

49     ELIZABETH DANIEL KIYABO         MGAMBO JKT

50     ELIZABETH MWAKITEGA         RUVU JKT

51     ELVIS MAHENGE SIMON         RUVU JKT

52     EMMA A. KILONZO         RUVU JKT

53     EMMANUEL PHILIPO         MGAMBO JKT

54     EVELYNE SCARION         RUVU JKT

55     EZEKIEL KWAKA MSESE         RUVU JKT

56     FABE MAGNUS NGONYANI         MAKUTOPORA JKT

57     FANUEL VICTOR KISIRI         RUVU JKT

58     FELICIAN PASCHAL ULAYA         RUVU JKT

59     FESTO MWAKAYO         RUVU JKT

60     FRANCES MASHAKA LUJAJI         RUVU JKT

61     FRODIANUS FIDERI         RUVU JKT

62     GABRIEL PATRICK LWESYA         MLALE JKT

63     GAUDENSIA MOHAMED MWALUNGWE         MAKUTOPORA JKT

64     GEORGE STANSLAUS SHAYO         RUVU JKT

65     GEORGIA ISHENGOMA         RUVU JKT

66     GERVAS PASCHAL KIHANGA         RUVU JKT

67     GETRUDE J. MASIMBANI         RUVU JKT

68     GIFTI A. LUGOME         MARAMBA JKT

69     GLORIA ALBERT MARINGO         RUVU JKT

70     GODFREY CHRISTIAN ROEBERT         RUVU JKT

71     GOODLUCK JOHN WILLSON         MGAMBO JKT

72     GREEN EUSTAD         RUVU JKT

73     GROLIA GODWIN KAHWA         MAFINGA JKT

74     HAJI SHEMHILU         RUVU JKT

75     HAPPINESS MGURU         RUVU JKT

76     HARRISON DAVID MRANGO         RUVU JKT

77     HASSAN RAJABU NJAU         RUVU JKT

78     HAWA ISSA MDENG'O         MARAMBA JKT

79     HAWA ISSA MDENG'O         MARAMBA JKT

80     HERI MOHAMED MKUMBEGE         RUVU JKT

81     HERIETH MAHENGE         RUVU JKT

82     HINDU HAMIS MRISHO         RUVU JKT

83     IBRAHIM ABDALLAH         RUVU JKT

84     IELEEN DIDAS MUTABINGWA         RUVU JKT

85     IMELDA IGNAS MBUNDA         MAKUTOPORA JKT

86     INZARI CHARLES LUGUTU         BULOMBORA JKT

87     IRENE KYENKUNGU         RUVU JKT

88     JACKLINE ADAM LEYNA         MGAMBO JKT

89     JACKLINE HERBET STEWARTH         MARAMBA JKT

90     JACKSON LUPAKISYO MWAIPUNGU         RUVU JKT

91     JAFARI S. JAFARI         RUVU JKT

92     JANE MGINJA MTIMBA         RUVU JKT

93     JANETH FORTUNATUS WAMBURA         RUVU JKT

94     JANETH V. KILONZO         RUVU JKT

95     JAPHET MASOTA         MARAMBA JKT

96     JASMIN MARTIN         RUVU JKT

97     JASMIN MARTIN SHAYO         MARAMBA JKT

98     JASMINE RASULI         RUVU JKT

99     JASON STEVEN         RUVU JKT

100     JIDIRU IZADINI KALOKOLA         RUVU JKT

101     JOHANITHA JOHN         MAFINGA JKT

102     JOHNSON JONATHAN JOHN         RUVU JKT
103     JORAM MBOMA JONATHAN         RUVU JKT
104     JOSEPH E. JOHNSON         MARAMBA JKT
105     JOSEPH REGNALD TUNGALAZA         RUVU JKT
106     JOSEPH TARIMO         RUVU JKT
107     JOSEPHINE BONIFACE MHANDO         RUVU JKT
108     JUENI MALIJANI         RUVU JKT
109     JUSTINE REGNALD MAKENE         RUVU JKT
110     KELVIN GEDION LEMNGE         MARAMBA JKT
111     KHADIJA E. KALONGA         RUVU JKT
112     KIBIBI HASAN JAMBIA         MARAMBA JKT
113     LAULENCIA ENGITRAUDA         842KJ
114     LEAH THOMAS MTWEVE         RUVU JKT
115     LILAN HENRY CASTORY         MAKUTOPORA JKT
116     LILIAN KANG'WA MASANJA         RUVU JKT
117     LUCIA JORAM TIMBA         RUVU JKT
118     LUGENDO LUCAS CHAPUGA         RUVU JKT
119     MARIAM M. JUMA         RUVU JKT
120     MARIAM WAMBURA         MSANGE JKT
121     MARIAMU S LIPENDE         MAKUTOPORA JKT
122     MARKO MICHAEL KASONI         RUVU JKT
123     MARTIN EWALD MALYAWERE         RUVU JKT
124     MARTINA GEORGE MWAILUSI         RUVU JKT
125     MARY ANTHONY MASSAWE         RUVU JKT
126     MARY I MREMA         MAKUTOPORA JKT
127     MASTERBETTER JOHN         RUVU JKT
128     MATHIAS BAHATI ORESTI         MAKUTOPORA JKT
129     MESHACK MARTIN LYIMU         MARAMBA JKT
130     MESHACK MARTIN LYIMU         RUVU JKT
131     MICHAEL DEOGRATIUS NJAU         MGAMBO JKT
132     MIRIAM M. JUMA         RUVU JKT
133     MUSSA KALUME AGUSTINE         RWAMKOMA JKT
134     MUSSA S. MAIGE         RUVU JKT
135     MWAMINI KADUMA         RUVU JKT
136     NAISHOOKI WILBERT OLE-MBILE         RUVU JKT
137     NAOMI ENMANUEL LEKASHINGO         MARAMBA JKT
138     NASRA NURDIN YUSSUPH         RUVU JKT
139     NEEMA JAMES MANYAMA         RUVU JKT
140     NEEMA MAIKO MASAGASI         RUVU JKT
141     NEEMA MSUYA         RUVU JKT
142     NESTARY AGATHON NDUNGURU         MAFINGA JKT
143     NESTARY AGATON NDUNGURU         MAFINGA JKT
144     NICODEMO JACOB         RUVU JKT
145     NOEL JAMES MWAKISOMBE         RUVU JKT
146     NORBERT NOEL         KANEMBWA JKT
147     NUSRAT ZAKARIA         RUVU JKT
148     OCTAVIAN BUBERWA         RUVU JKT
149     OMARI DIWANI OMARI         RUVU JKT
150     OMARY MAKOTA ALLY         KANEMBWA JKT
151     PAUL KATUNZI         MSANGE JKT
152     PRISCILA WENDE MGANA         MAKUTOPORA JKT
153     PROJESTUS H.CHAMAHANGA         RUVU JKT
154     RACHEL DAVID ISSAME         RUVU JKT
155     RACHEL DAVID ISSAME         RUVU JKT
156     RACHEL RAYMOS FOYA         RUVU JKT
157     RAHEL FESTUS ISOKOZA         RUVU JKT
158     RAMADHANI ALLY NJERA         RUVU JKT

159     RAMADHANI MBWAMBO         MARAMBA JKT

160     RAMADHANI RAJABU RAMADHANI         RUVU JKT

161     RAMADHANI RAJABU RAMADHANI         RUVU JKT

162     RECHO DANIEL MWALIMU         MAKUTOPORA JKT

163     REHEMA DEUS RUBALE         RUVU JKT

164     REHEMA SHAWARI IKAJI         MARAMBA JKT
165     REMIDIUS REYMOND MUTA         RUVU JKT

166     RETISIA SAANANE         RUVU JKT

167     RIDHIWANI SHABANI MAKUMBI         MGAMBO JKT

168     RISHAD KIHOMO MLELWA         RUVU JKT

169     ROGERS JOHN EZEKIEL         RUVU JKT

170     ROMAN CASTORY         RUVU JKT

171     ROSEMARY T. MASIAGA         MSANGE JKT

172     SADICK HASHIM MWAISAKA         RUVU JKT

173     SAIMON P. SOZIGWA         MARAMBA JKT

174     SALA A. MWAKAJWANGA         RUVU JKT

175     SALEHE MACHIBYA JONIOR         MGAMBO JKT

176     SALMIN AMRI         MARAMBA JKT

177     SALOME AMOS         RUVU JKT

178     SALOME SHITUNGURU         RUVU JKT

179     SHUKRANI MWAIPWISI         MAFINGA JKT

180     SIMON P. SOZIGWA         RUVU JKT

181     SOLINA SABAS         RUVU JKT

182     SOPHIA DEUS RUBALE         RUVU JKT

183     SOPHIA S. MATHIAS         MARAMBA JKT
184     STEPHEN F. NDALUSE         RUVU JKT

185     STIVEN NDALUSO         RUVU JKT

186     SUSAN PATRICK MNASIZU         RUVU JKT

187     SWEED IDD         RUVU JKT

188     TATU HAMAD HATIBU         RUVU JKT

189     TATU JUMA MYOVELA         MARAMBA JKT

190     TOMESTECLES H.CHAMAHANGA         RUVU JKT

191     TUMAINI JOHN MAKUNENGE         BULOMBORA JKT

192     TUMPALE JAPHET         RUVU JKT

193     VAILET GEORGE SIMBA         RUVU JKT

194     VALERIAN VEREMUND CHARLE         MAFINGA JKT

195     VERONICA CASMIR NDAMBARIKA         MAKUTOPORA JKT

196     VERUS THOBIAS KASONSO         RUVU JKT

197     VERUS TOBIAS KASONSO         RUVU JKT

198     VICTOR DAUDI ANYASIME         RUVU JKT

199     VICTOR L. AMBELE         RUVU JKT

200     VICTORY HENRY         RUVU JKT
201     WALTER FRUGENCE SAMKY         RUVU JKT

202     WILLIAM OSIAS MWANYIKA         RUVU JKT

203     WILLIAM PATRICK ASSEY         MGAMBO JKT

204     YASSER HAMAD MALESA         MARAMBA JKT

205     ZAMDA MWALIMU         MAKUTOPORA JKT