Monday 30 May 2016

#YALIYOJIRI>>>Serikali imeanza kutengeneza sheria ya kutambulisha Dodoma kama Makao Makuu ya nchi.Fahamu zaidi hapa.

Serikali imeanza kutengeneza sheria ya kutambulisha Dodoma kama Makao Makuu ya nchi na inatarajiwa kupelekwa bungeni ili kuondoa changamoto ya migogoro baina ya Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu (CDA) na wananchi.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira na Watu wenye Ulemavu), Jenista Mhagama alisema hayo bungeni hivi karibuni.Alisema kuanzishwa kwa sheria hiyo kutarahisisha katika kuhamia Dodoma pamoja na kuondoa migongano ya kisheria kati ya taasisi mbalimbali inayosimamia masuala ya ardhi mkoani Dodoma, ikiwa ni pamoja na kueleza mipaka ya CDA.


“Nataka wananchi wa Dodoma waamini kuwa serikali ina lengo la kuhakikisha azma hii ya serikali kuhamia Dodoma inatekelezeka, ikiwa ni pamoja na kuondoa migogoro yote kwa kufuata sheria na taratibu na kunapokuwa na matatizo kwa ushirikiano wetu na wao inaisha,” alisema.Alisema.


watahakikisha migogoro yote inaisha, lakini kwa kufuata sheria ikiwa wananchi wana haki watapata na pale sheria inapowataka wao waipe haki serikali waoneshe ushirikiano.Waziri huyo alisema mji wa Dodoma utajengwa kisasa na kuonesha kweli ni makao makuu kama ilivyo miji mingine duniani kwa kuwa kioo cha nchi ilivyo.Alisema katika kuonesha nia ya serikali ya kuhamishia makao makuu Dodoma kabla ya kumalizika kwa mkutano wa Bunge watakutana na wabunge wa mkoa huo na wizara kujadiliana namna bora ya kuondoa changamoto hiyo.

0 comments:

Post a Comment