Tuesday 31 May 2016

#MICHEZO>>>CAF YARUDISHA HATUA YA MTOANO MICHUANO YA KLABU.Fahamu zaidi hapa.

Shirikisho la Soka Afrika limetaja mfumo mpya wa mashindano kuanzia mwakani, na sasa limerudisha mfumo wa mechi za mtoano kuanzia hatua ya Robo Fainali.

Katika kikao cha Jumanne ya Mei 24, mwaka 2016 mjini Cairo, Misri; Kamati ya Mashindano ya Klabu ya CAF ilikubaliana juu ya mfumo mpya wa Ligi ya Mabingwa na Kombe la Shirikisho. Mabadiliko katika mashindano hayo mawili yalitangazwa na Rais wa CAF, Issa Hayatou katika Mkutano Mkuu wa 38 wa shirikisho hilo uliofanyika mjini Mexico City, kwamba kuanzia mwakani kutakuwan na timu 16.

0 comments:

Post a Comment