Tuesday 31 May 2016

#YALIYOJIRI>>>>Wanafunzi wa chuo kikuu cha cha Dar es salaam Wagoma.Fahamu zaidi hapa.

Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam(UDSM) leo wamegoma wakiishinikiza Bodi ya Mikopo(HESLB) kuwapatia fedha zao za kujikimu.

Kwa kawaida wanafunzi hupewa fedha za kujikimu kila baada ya miezi miwili.
 
Makamu wa Rais wa serikali ya wanafunzi, Shamila Mshengema amesema mgomo huo ni matokeo ya taarifa zisizoeleweka zilizo kuwa zikitolewa na bodi juu ya lini fedha hizo zitatolewa.
 
Kwa kawaida pesa ya chakula huingiziwa kila baada ya siku 60 na mpaka sasa yapata wiki mbili pesa hiyo haijaingizwa
 
Mgomo huo unakuja zikiwa zimebaki siku mbili kabla ya Rais Magufuli Kuzulu chuo hicho kwa ajili ya uzinduzi wa jengo la Maktaba.

0 comments:

Post a Comment