Tuesday 31 May 2016

#MICHEZO>>>MAJIBU YA AZAM FC KUHUSU KIPRE TCHETCHE KUTIMKIA UARABUNI.Fahamu zaidi hapa.

Mtendaji Mkuu wa klabu ya Azam FC Saad Kawemba amekanusha taarifa za nyota wao Kipre Tchetche kusaini kwenye klabu moja ya nchi za falme za Kiarabu lakini akasema, wapo tayari kuzungumza na klabu yeyote ambayo inahitaji huduma ya mchezaji huyo.

“Taarifa hizo tumeziona na kwa maana ya wakati usajili hivyo ni vitu vya kawaida kwenye mpira, unasikiliza halafu unasubiri matokeo yake. Kwasasababu sisi ni klabu na nimeona kwenye mtandao mmoja amesema anamkataba na klabu na ni kweli bado tunamkataba naye wa mwaka mmoja”, amesema Saad Kawemba mtendaji mkuu wa klabu bya Azam FC alipohojiwa na Sports Extra ya Clouds FM.

“Kwahiyo tunaamini yeyote ambaye anamuhitaji atafika kwenye klabu yetu tuzungumze. Lakini katika kipindi hiki cha usajili tunategemea mambo kama hayo kutokea kwa wachezaji wengi na si yeye pekeyake.”

Jana pia zilitoka taarifa zinazomhusu raia huyo wa Ivory Coast kutakiwa na mabingwa VPL na FA Cup Dar Young Africans.

0 comments:

Post a Comment