Friday 24 February 2017

DONALD Trump Atangaza Kujenga Kinu Kikubwa Cha Silaha za Nyuklia Marekani.Fahamu zaidi hapa.

Rais wa Marekani, Donald Trump ametangaza kuwa anataka kujenga kinu kikubwa cha nyuklia nchini humo kuhakikisha kuwa taifa hilo lenye nguvu zaidi duniani linaendelea kuwa juu zaidi katika silaha za nyuklia.

Akizungumza leo katika mahojiano maalum na shirika la habari la Reuters, Rais Trump amesema kuwa Marekani sasa hivi iko nyuma katika uwezo wake wa silaha za atomiki.

Katika hatua nyingine, Reuters imemnukuu Trump akizungumza baada ya mahojiano hayo, ambapo alieleza kuwa anachukizwa sana na kitendo cha Korea Kaskazini kufanya majaribio ya silaha zake za maangamizi.

Alisema kuwa katika kuidhibiti Korea Kaskazini, Marekani inapaswa kutumia mfumo wa nchi marafiki kama Japani na Korea Kusini.



Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa


0 comments:

Post a Comment