Monday 27 March 2017

CCM yateua Makatibu wa Mikoa 31, wa Wilaya 155. ......Yaeleza msimamo wa chama kuhusu Makonda.Fahamu zaidi hapa.

Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika kuendelea kufanya mageuzi ya uongozi, muundo na mfumo, kimefanya uteuzi wa makatibu wa mikoa 31 wakiwamo wapya 20, na wa wilaya 155 ambao uteuzi wao unaanza mara moja kuanzia jana.

Pia chama hicho kimekiri kufanya mabadiliko ya kikatiba yanayolenga maeneo matatu ambayo ni misingi ya uongozi, muundo na mfumo pamoja na utawala na utendaji kwa lengo la kukijenga zaidi chama hicho, na hakuna sehemu yoyote kwenye Katiba hiyo iliyobadilishwa inayohusu Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020.

Akizungumza jana Dar es Salaam, Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) Itikadi na Uenezi, Humphrey Polepole alisema kati ya makatibu hao walioteuliwa wa mikoa 11 ni wale waliopandishwa hadhi kutokana na utendaji wao na 20 ni wapya kabisa.

Alisema katika orodha ya makatibu hao walioteuliwa, chama hicho kilizingatia sifa hizo ikiwemo maadili, weledi, jinsia na mpango wa kuachiana vijiti kwa kuzingatia rika.
 
Uteuzi wa Makatibu wa CCM Mikoa…
  1.     Arusha- ­ Elias Mpanda
  2.     Dar es Salaam-­ Saad Kusilawe
  3.     Dodoma- ­ Jamila Yusuf
  4.     Geita- ­ Adam Ngalawa
  5.     Iringa- ­ Christopher Magala
  6.     Kagera­- Rahel Degeleke
  7.     Katavi­- Kajoro Vyahoroka
  8.     Kigoma-­ Naomi Kapambala
  9.     Kilimanjaro-­ Jonathan Mabihya
  10.     Lindi­- Mwanamasoud Pazi
  11.     Manyara- ­Paza Mwamlima
  12.     Mara- ­Innocent Nanzabar
  13.     Mbeya- ­Wilson Nkhambaku
  14.     Morogoro-­ Kulwa Milonge
  15.     Mtwara- ­Zacharia Mwansasu
  16.     Mwanza-­ Raymond Mwangala
  17.     Njombe-­ Hossea Mpagike
  18.     Pwani-­ Anastanzia Amasi
  19.     Rukwa-­ Loth Ole Nesere
  20.     Ruvuma­- Amina Imbo
  21.     Shinyanga- ­Haula Kachambwa
  22.     Simiyu-­ Donald Etamya
  23.     Singida-­ Jimson Mhagama
  24.     Tabora-­ Janeth Kayanda
  25.     Tanga-­ Allan Kingazi.
“Makatibu wengi (20) tuliowateua ni wapya, hatuwezi kufanya mageuzi ya kuwa na CCM mpya na upya huo usionekane. Mageuzi ni fikra” amesema Polepole.

Lakini pia alisema katika orodha hiyo ya makatibu wa wilaya wa CCM 155, makatibu 76 ni wapya kutokana na vigezo vipya vilivyowekwa na chama hicho.

Aliwataja baadhi yao kuwa ni Mussa Matoroka anayekwenda Arumeru, aliyekuwa Katibu Mwenezi wa Mkoa wa Dar es Salaam, Juma Simba ‘Gaddafi’ (Longido), Joyce Mwenda (Namtumbo), Kombo Kamote (Bagamoyo), Grevas Ndaki (Momba), Othman Dunga (Hanang), Pili Augustino (Dodoma Mjini) na Martin Mwakitabu (Chamwino).

Wengine ni Aveline Ngwada (Bukombe), Nuru Ngeleja (Chato), Michael Mbaga (Iringa Mjini), Afidu Luambano (Temeke), Joyce Mkaugala (Ilala), Hanaf Msabaha (Kinondoni), Salum Kali (Ubungo), Robert Kalenge (Kigamboni), Ramadhan Dallo (Arusha) na Gulisha Mvanga (Monduli).

Kuhusu suala la Mkuu Mkoa wa Dar es Salaam, Polepole alisema, kwanza napenda kusema kuwa uhusiano wa CCM na vyombo vya habari ni wa kihistoria’… CCM inapenda kufuata utaratibu na ndio salama yetu kama yupo kiongozi wa chama amefanya jambo tuna utaratibu mzuri wa kuchunguza. Lakini pili, Mkuu wa Mkoa ni mteule wa Rais na anapomteua anamteua yeye peke yake na halazimiki kushauriana na mtu, hivyo badala ya kukaa na kumpangia Rais kitu cha kufanya, tumuache afanye kazi’.. “

Aidha, Humphrey Polepole akitolea ufafanuzi madai yanayoenezwa kuwa wamefanya mabadiliko kuwa Rais Magufuli ndiye atakayegombea 2020 bila kupingwa amesema kuwa, mabadiliko ya katiba waliyoyafanya katika mkutano mkuu maalum, hayakuhusu mchakato wa kumpata mgombea wa uchaguzi mwaka 2020. Hivyo tunawaomba wanachama wetu na watanzania wapuuze habari nyingine zinazoenezwa.

Katibu wa CCM itikadi na Uenezi ­Taifa


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment