Friday 18 November 2016

#MICHEZO>>>Simba yafunguka kuhusuujio wa Emmanuel Okwi na Kipre Tchetche.Fahamu zaidi hapa.

Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Klabu ya Simba Zacharia Hanspoppe amekanusha usajili wa washambuliaji Emmanuel Okwi na Kipre Herman Tchetche ndani ya klabu hiyo katika dirisha dogo la usajili.

Emmanuel Okwi na Kipre Tchetche.
Amesema habari zinazosambaa kuhusu usajili wa wachezaji hao siyo za kweli kwani kamati inakutana hii leo kwa ajili ya kupitia ripoti ya kocha na mara baada ya kikao hicho ndipo wataangalia mapendekezo ya kocha kuhusu usajili kwani mpaka sasa bado hawajafanya mazungumzo na mchezaji yoyote wa ndani au nje ya nchi.

Hanspoppe amesema, mshambuliaji Emmanuel Okwi kwa sasa yupo nchini Denmark na hakuna kiongozi ambaye ameshaenda kufanya mazungumzo naye kuhusu usajili, na kwa upande wa Kipre pia hawajawahi kufanya mazungumzo.
Zacharia Hanspoppe

Wakati huohuo Hans amesema, ndani ya klabu ya Simba hakuna mchezaji ambaye yupo katika mazungumzo na klabu yoyote kwani wachezaji hao wote wana mikataba ambayo inawafanya kuwa ni wachezaji halali wa Klabu hiyo.

Amesema, wachezaji  walio ndani ya klabu hiyo mikataba yao inaisha Juni 15 mwakani na wana uamuzi wa kuongea nao muda wowote na hata usajili unafanyika mara baada ya kumalizika kwa mkataba.



Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi


Bonyeza Hapa CLICK HERE

 

0 comments:

Post a Comment