Tuesday 12 December 2017

Msagasumu Awakata Ngebe Wanawake Wanaomshobokea " Nina Mke Wangu Acheni Shobo".

NGULI wa Muziki wa Singeli, Selemani Jabir ‘Msaga Sumu’, amewakata ngebe wanawake ambao wamekuwa wakimshobokea wakati yeye ana mke na watoto wawili.

Akizungumza na Full Shangwe, Msaga Sumu anayebamba na Ngoma ya Mwanaume Mashine alisema kuwa hana mpango na wanawake wanaomshobokea na haitakuja kutokea kwani ana ndoa yake anayoipenda.

“Imekuwa kero sasa, ninachoweza kuwaambia ni kwamba wanawake waache kunishobokea, Kwanza watambue kuwa ninaipenda familia yangu na kwa sasa ninatimiza miaka nane ya ndoa yangu, na nina watoto wawili, inshallah Mungu kanijalia,”alisema Msaga Sumu na kuongeza;

“Kwa sasa najipanga kuzindua rasmi Mwanaume Mashine ndani ya Dar Live hivyo soon nitatangaza.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment