Monday 4 December 2017

MENEJA WA ULIMWENGU AELEZA NAMNA ALIVYOVUNJA MKATABA NA TIMU YA NDEMLA SWEDEN.

Jamal Kisongo ambaye ni meneja wa straika, Thomas Ulimwengu, yupo kwenye mchakato wa kuvunja mkataba wa mteja wake huyo dhidi ya timu ya AFC Eskilstuna iliyokuwa ikishiriki Ligi Kuu ya Sweden kufuatia kushuka daraja.

Timu hiyo ndiyo inayojiandaa kumchukua Said Ndemla ambaye amefuzu majaribio akitokea klabu ya Simba ya nchini.

Ulimwengu alijiunga na timu hiyo msimu uliopita ambapo alisaini mkataba wa miaka mitatu na hadi anafikia uamuzi huu hakuwahi kucheza mechi yoyote ya ligi kutokana na kusumbuliwa na majeraha ya goti anayouguza mpaka sasa.

Kisongo alisema kuwa kwa sasa yupo kwenye mchakato wa kumtafutia timu nyingine Ulimwengu ambapo anaamini mpaka Januari, mwakani, atakuwa amepata timu kubwa inayoshiriki ligi kuu na hatarejea Sweden tena.

Meneja huyo aliongeza kuwa kwa sasa Ulimwengu yupo nchini hapa akifanya mazoezi binafsi ya kujiimarisha baada ya kutoka Ubelgiji alikokuwa kwa mapumziko binafsi.

“Nipo kwenye mchakato wa kumtafutia timu Ulimwengu na ninaamini hadi kufika Januari nitakuwa nimepata ile ambayo inashiriki ligi kuu na hatarudi tena Sweden. Tunataka kuvunja mkataba na wale AFC Eskilstuna kwa kuwa imeshuka daraja licha ya kuwa tumebakiza miaka mawili kwenye mkataba,” alisema Kisongo.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment