Monday 26 February 2018

Mbao Yaitumia Salamu za Maaangamizi Simba Katika Mechi ya Leo.

Kikosi cha Mbao kimeamua kupeleka salamu kwa wapinzani wao Simba kuelekea mchezo wao wa leo Jumatatu utakaopigwa katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kwa kusema kuwa wamekuja jijini Dar es Salaam kupata ushindi na si vinginevyo.

Mwenyekiti wa timu hiyo, Solly Zephania Njashi, alisema kuwa maandalizi yao ya mchezo wa leo yapo vizuri na wamejiandaa vya kutosha na wamekuja kwa ajili ya kupata ushindi.

“Sisi tumejiandaa vizuri kwa ajili ya mchezo wetu wa kesho (leo) na mashabiki wafike kwa wingi kwani tuna uhakika tutaibuka na ushindi, tumejipanga kuhusu hilo.
“Sisi tumekuja kupata ushindi, siyo kupoteza, sema tatizo huwezi jua naye mpinzani wako amejipanga vipi kwenye mchezo huo, lakini sisi tupo vizuri na kikosi hakina majeruhi, bali kuna mmoja tu ambaye tulimpandisha kutoka kwenye academia, ila mwalimu atatoa ripoti kama atacheza au la,” alisema Njashi. 

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment