Wednesday 14 February 2018

Mwana Aipongeza Serikali "Nguo za Heshima Ndio Kila Kitu".

MWANA-DASHOSTI wa Bongo Movies, Mwanaheri Ahmed ‘Mwana’ amefunguka kuwa kitendo cha Naibu Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Juliana Shonza kupiga marufuku mastaa wa kike kujiachia nusu utupu, ndiyo kila kitu katika kurudisha hadhi iliyopotea ya sinema za Kibongo.

Mwana alisema kuwa, baadhi ya mastaa, hasa wa filamu wanaojiachia nusu utupu ndiyo waliochangia kushuka kwa sanaa hivyo waziri amefanya jambo la maana kupiga marufuku na kuwachukulia hatua wale ambao wanaendelea kusambaza picha hizo za kihasara kwenye mitandao ya kijamii.

“Sijawahi kukaa nusu utupu na sidhani kama itatokea, ninaipongeza sana serikali kwa kupiga marufuku picha za nusu utupu zilizokuwa zikitupiwa mitandaoni na baadhi ya wasanii kwani zinaharibu maadili ya Kitanzania, ninaamini sasa hadhi ya filamu itarudi maana jamii ilitudharau kutokana na mambo kama hayo,” alisema Mwana.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment