Thursday 22 February 2018

Baada ya Kuwasili Nchini Rais wa FIFA Amtaja Samatta.

RAIS wa Shirikisho la Soka Duniani (FIFA), Gianni Infantino amewasili nchini leo alfajiri Feb. 22, 2018 kwa ajili ya mkutano wa FIFA unaofanyika jijini Dar es Salaam.

Rais huyo wa FIFA akiwa uwanjani hapo baada ya kuwasili alipata fursa ya kuzungumza na waziri Mwakyembe ambapo alimtaja nahodha wa Taifa Stars, Mbwana Samatta, anayecheza soka la kulipwa KRC Genk ya Ubelgiji.

“Nilisikia mchezaji bora wa Afrika kutoka Tanzania, Mbwana Samatt, anayecheza Genk, hii ni nchi ya mpira licha ya changamoto za shirikisho siku za nyuma, lakini kwa sasa mpo kwenye mstari kutokana na uongozi mpya kwa kushirikiana na CAF  na FIFA,” alisema Infantino. 

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment