Wednesday 28 February 2018

YANGA YAANDIKA HISTORIA MTWARA, YAICHARAZA NDANDA MABAO 2-1.

Young Africans imeandika historia ya kwanza katika Uwanja wa Nangwanda Sijaona baada ya kuifunga Ndanda FC kwa mabao 2-1, mchezo wa Ligi Kuu Bara.

Walikuwa Yanga walioanza kucheka na nyavu za Ndanda mapema kabisa kwenye dakika ya 6 ya mchezo, baada ya Pius Buswita kutumia vema madhaifu ya mabeki wa Ndanda kwa kfunga bao la kwanza.

Na katika dakika ya 29, Hassan Kessy, alifunga bao la pili kwa mguu wa kushoto katika eneo la hatari la wapinzani wao, na kuufanya mchezo uende mapumziko kwa mabao 2-0.

Kipindi cha pili, Ndanda walikuja na uhai wakipambana kupata mabao ya kusawazisha japo ammbo hayakuwa rahisi, lakini jitihada zao ziliwasaidia kupata bao la kufutia machozi katika dakika ya 83 kupitia kwa Nassor Kapama.

Mpaka dakika 90 zinamalizika, Ndanda FC 1-2 Young Africans.

Matokeo haya sasa yanaifanya Yanga kuwa na alama 40, nyuma ya Simba iliyo na 45.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment