Sunday 25 February 2018

Ajali Mbaya ya Daladala Yatokea Kimara.

Basi la abiria (Daladala) linayofanya safari zake kati ya Mbezi na Makumbusho jijini Dar es Salaam limepinduka leo Jumatatu, Februari 26, 2018 asubuhi katika eneo la Kimara Korogwe.

Polisi wapo eneo la tukio kufanya jitihada za kuokoa watu waliokuwemo kwenye ajali hiyo ambapo basi limepinduka na kugeuka magurudumu yakawa juu.

Idadi ya majeruhi haijajulikana na iwapo kuna watu waliopoteza maisha kwenye ajali hiyo. Tutakupa taarifa zaidi baadaye. 

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment