Monday 26 February 2018

Waziri Ndalichako Atishia Kukifunga Chuo cha Mount Meru.

Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia, Prof.  Joyce Ndalichako amekitaka Chuo Kikuu cha Mount Meru kilichopo Jijini Arusha kuacha mara moja utaratibu wa kutoa alama za makisio kwa Wanafunzi wanosoma chuoni hapo na wakiendelea Serikali itakifunga chuo hicho mara moja kwa sababu utaratibu huo haujawahi kutumika katika Chuo chochote Duniani.

Waziri Ndalichako ametoa maagizo hayo alipotembelea katika Chuo hicho kuona miundo mbinu na namna wanavyo simamia utoaji wa elimu ya juu, ambapo amesema Wizara ilishatoa maelekezo kupitia Tume ya Vyuo Vikuu kuwa Chuo hicho kiwaondoe Wahadhiri ambao hawana sifa za kufundisha lakini agizo hilo mpka sasa halijatekelezwa. 

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment