Friday 15 September 2017

Kenyatta Ametaka Kufutwa kwa Kampeni ya Kumuondoa Jaji Mkuu Maraga.

Mgombea urais wa Kenya kupitia chama tawala cha Jubilee Uhuru Kenyatta, ametaka kufutwa kwa kampeni ya kuondoa Jaji Mkuu wa nchi hiyo David Maraga, iliyoanzishwa na mbunge wa chama hicho.

Uhuru Kenyatta amesema ni vyema kuacha Mahakama ifanye kazi zake na wao kuangalia zaidi kwenye uchaguzi wa urais unaofuatia ili kutetea nafasi ya chama hicho kubaki madarakani.

"Tumekubaliana kurudi kwa wapiga kura na masanduku ya kupigia kura, naelewa maumivu yenu na matendo yenu, lakini tuna uchaguzi wa kushinda Oktoba 17, hilo ndio linatakiwa liwe kipaumbele chetu, iacheni mahakama", amesema Uhuru Kenyatta.

Hapo jana mbunge wa chama cha Jubilee Ngunjiri Wambugu alianzisha kampeni ya kumuondoa madarakani Jaji Mkuu wa nchi hiyo David Maraga, kutokana na kile alichokiita utendaji mbaya baada ya kufuta matokeo ya uchaguzi wa urais nchini humo Septemba 1 mwaka huu, na kutaka urudiwe.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment