Thursday 28 September 2017

Omog Ndiye Aliyeishikisha Adabu Yanga, Bado Anahitajika Simba Kuliko Yeye KulikoHata Anavyoihitaji Yeye- Manara.

Haji Manara amefunguka na kusema Kocha Mkuu wa Simba, Joseph Omog anahitajika zaidi na Simba kuliko hata yeye anavyohitaji Simba na kudai ni kocha pekee aliyeweza kuipa Simba vikombe viwili na kuifunga Yanga mara tatu katika mechi nne walizokutana.

Manara amesema hayo jana wakati akielezea mambo mbalimbali kuelekea mchezo wao na Stand United ambao unatarajiwa kupigwa katika uwanja wa Kambarage Shinyanga ambapo amedai wanaiheshimu timu hiyo lakini wao wanakwenda kwa lengo la kutafuta pointi tatu.

"Makocha watano wamekaa hapa Simba wameshindwa kutupa nafasi ya pili, wameshindwa kutupa kikombe lakini Omog katupa vikombe viwili na vyote kamnyang'anya Yanga kakutana na Yanga mara nne kampiga mara tatu, halafu kuna mtu mtaani anasema Omog hafai, Simba sasa hivi inamuhitaji zaidi Omoh kuliko Omog anavyoihitaji Simba kwa sasa" alisema Haji Manara

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment