Friday 15 September 2017

Wazee wa Kigoma Wamjia Juu Ndugai Wamtaka Kuacha Kiburi na Kusimamia Misingi ya Kuwaunganisha.

Wazee wa Kigoma wakiwakilishwa na Mwenyekiti wa Ngome ya Wazee ya Chama cha ACT Wazalendo, Alhaj Jaffar Kasisiko wamesikitishwa na kauli aliyotoa Spika Ndugai kuwa anaweza kumzuia Zitto Kabwe asiongee chochote mpaka ubunge wake utakapokwisha.

Wazee hao wanasema kitendo cha Spika kumzuia Zitto Kabwe kuongea bungeni ni sawa na kuwazuia wao wasiongee na shida zao zisiweze kutatuliwa na kudai inaonekana hiyo kauli imeshafanyiwa kazi na kitendo cha kumwita Zitto kwenye Kamati ni sawa na kupoteza muda tu na kudai jambo hilo halimtendei haki kijana wao Zitto Kabwe na wao wenyewe.
Aidha wazee hao wamemtaka Spika Job Ndugai na viongozi wengine wasiwe na kibri na watazame mambo ambayo yanawaonganisha kwa pamoja.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment