Wednesday 27 September 2017

Inasikitisha Binti wa Darasa la Tatu Apewa Mimba.

Mwanafunzi mwenye umri wa miaka 13 wa darasa la tatu katika shule ya msingi Makutano, kitongoji cha Igole kijiji cha Makutano wilayani Kilombero amelazimika kukatizwa masomo yake kwa kufukuzwa shule baada ya kupewa ujauzito.

Mtuhumiwa anayesadikiwa kutenda kosa hilo Samuel Daudi  ametoroka  na kwenda kusikojulikana.
Hali ya mimba za utotoni kwa wanafunzi wakiwemo wa shule za msingi wilayani Kilombero inadaiwa kuchangiwa na sababu mbalimbali ikiwemo vishawishi na kurubuniwa kwa wasichana wadogo kutokana na umbali wa shule hizo na makazi ya watu, ambapo wazazi wa binti huyo ambaye hutembea umbali mrefu sana kwenda shule, wamesema hawakugundua mapema kama kwa umri wake binti yao angeweza kubebeshwa ujauzito.
Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Makutano, Fabian Undole amesema wamekuwa na taratibu za kuwapima afya wanafunzi wa kike shuleni hapo kila baada ya miezi mitatu na kwamba jamii ya wafugaji imekuwa ikiongoza kwa matatizo hayo.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Kilombero Denis Londo amekiri changamoto kama hizo kujitokeza katika baadhi ya maeneo ingawa wameendelea kuchukua hatua kali na sasa wanaongeza nguvu kudhibiti kabisa hali hiyo.



TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment