Friday 15 September 2017

FIFA Imefanya Mabadiriko ya Mashindano ya Kombe la Dunia.

Shirikisho la soka la kimataifa FIFA limebadili utaratibu wa namna ya kupanga makundi katika fainali za Kombe la dunia 2018 nchini Urusi.

FIFA imesema wakati wa kupanga makundi itazingatia viwango vya soka ambavyo huwa inavitoa kila mwezi kwa timu za taifa ambapo sahani (pot) zote 4 zitapangwa kulingana na viwango kwenye orodha ya FIFA. Awali sahani ya kwanza pekee ndio ilikuwa inazaingatia viwango hivyo lakini sasa itakuwa ni kwa pot zote.
Pia FIFA imethibitisha kuwa itatumia viwango itakavyotoa mwezi Oktoba. Hii inamaanisha sahani ya kwanza huenda ikawa na timu za Ujerumani, Brazil, Ubeligji, Argentina, Ureno pamoja na wenyeji Urusi, lakini hadi sasa Brazil na Ubeligji pekee kwenye nchi za juu ndio zimefuzu.

Kuna dalili kubwa ya mataifa ya Uingereza, Hispania na Ufaransa yakawa katika sahani ya pili endapo yatafuzu. Afrika Mashariki katika kuwania kufuzu inawakilishwa na Uganda pekee ambayo ipo nafasi ya pili kwenye kundi E ikiwa na alama 7 nyuma ya Misri yenye alama 9. Uganda inashika nafasi ya 71 kwenye viwango vilivyotolewa jana na FIFA wakati Tanzania ikiwa nafasi ya 125.
TOA MAONI YAKO

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment