Thursday 1 March 2018

Bell 9 Aleta Kali Aifananisha Basata na Baba Asiyejua Jina la Mwanaye.

Msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Belle 9 amelishangaa Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) kwa kushindwa hata kuwajua wasanii japo hata kwa majina.


Belle 9 amesema hayo baada ya BASATA kuchanganya majina kwa kumtaja kwenye orodha ya wasanii waliofungiwa nyimbo zao jana Februari 28, 2018 badala ya kuweka jina la Roma Mkatoliki.

“Kwahiyo mimi ni Roma Mkatoliki haya basi tongwe record baby jei mada yo yo yo Roma!  Hii ni sawa na kua na baba ambaye akisikia umekosa ana kuhukumu lakini akiulizwa jina la mwanao anaitwa nani anajiuma uma halafu analitaja jina la mtoto wa jirani ambalo huwa analiskia akiwa anakuja kukuhukumu,“ameandika Belle 9 kwenye ukurasa wake wa Instagram.

Soma zaidi – TCRA yazifungia nyimbo 15, Diamond na Nay maumivu zaidi

BASATA walikosea kumtaja Belle 9 kwenye kipengele cha wimbo wa Kibamia ambapo waliandika Abemego Damiani a.k.a Roma Mkatoliki.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment