Wednesday, 10 January 2018

Wakili Kibatala ajitoa kesi ya Wema Sepetu.

Wakili Peter Kibatala ameiandikia barua Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, akiomba kujitoa kumuwakilisha msanii wa filamu nchini, Wema Sepetu katika kesi ya dawa za kulevya inayomkabili.

Hatua hiyo imekuja leo Jumatano, baada ya shauri lililopita Desemba 12, mwaka jana, mahakama hiyo kuelezwa kuwa wakili wa Wema hajafika  na kushindwa kuendelea kusikiliza kesi hiyo.

Mbali na wakili Kibatala kuomba kujitoa katika kesi hiyo,  mahakama hiyo imepokea barua kutoka kwa Wakili Albert Msando kuomba kumuwakilisha Wema katika kesi hiyo na kwamba aliomba apewe muda wa kupitia jalada hilo kabla ya kuendelea na kesi.

Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba anayesikiliza shauri hilo, amesema kuwa amepokea barua hizo Januari 9, mwaka huu na kuahirisha kesi hiyo hadi Februari 8, mwaka huu, itakaposikilizwa.
 
Washtakiwa wengine katika kesi hiyo ya kutumia dawa za kulevya ni Angelina Msigwa  na Matrida  Abbas.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Breaking News>>>Matokeo ya darasa la nne na kidato cha pili yatangazwa. Bofya Hapa Kuyatazama.

Baraza la Mitihani Tanzania (Necta) limetangaza matokeo ya mitihani ya upimaji wa darasa nne na kidato cha pili iliyofanyika Novemba 22 na 23 mwaka jana, huku idadi kubwa ya wanafunzi wakifanya vyema katika mitihani hiyo.

Akitangaza matokeo hayo leo Jumatatu Januari 8, Katibu Mtendaji wa Necta,  Dk Charles Msonde amesema jumla ya wanafunzi 1,086,156 waliofanya mtihani wa darasa la nne wamefaulu  kati ya 1,158,444 waliofanya upimaji huo.

Amesema  wanafunzi hao wamefaulu kwa kupata alama zenye madaraja ya A,B,C na D wakati wanafunzi 72,288 sawa na asilimilia 6.24 wamepata alama za daraja E, ambao ni ufaulu usioridhisha.

Kuhusu matokea ya upimaji wa kidato cha pili, Dk Msonde  amesema jumla ya wanafunzi 433,453 sawa na asilimia 82.32 kati ya 486,742 waliosajiliwa  kufanya mtihani huo wamepata ujuzi wa maarifa ya kuwawezesha kuendelea  na kidato cha tatu.

Dk Msonde alisema wanafunzi wa kidato cha pili  51,807 sawa na asilimia 10.68 wameshindwa kupata alama za kuwawezesha kuendelea na kidato cha tatu.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Joh Makini Afunguka Uhusiano Wake wa Kimapenzi na Mimi Mars.

Mwamba wa Kaskazini anayesumbua masikio ya wapenda burudani na ngoma ya 'Mipaka' Joh Makini amepangua tetesi za kujihusisha kimapenzi na mwanamuziki Mimi Mars ambaye pia ni mdogo wake msanii Vanesa Mdee.


Joh Makini amepangua tetesi hizo kwenye Friday Night Live ya EATV ambapo amesema kwamba tetesi hizo hazina ukweli wowote na kwamba yeye anamchukulia Mimi Mars kama mdogo wake kupitia heshima aliyojenga kwa wasanii hao ambao pia wanatokea kanda ya Kaskazini.

"A Big No. Mimi Mars ni kama mdogo wangu wa kike. Sisi ni familia moja aisee. Ni nani huyo ambaye anasambaza? alijibu Joh Makini kwa mtindo wa kuuliza.

Mbali na hayo Joh Makini amegoma kuweka wazi kuhusu mahusiano yanayodaiwa kuwa ni ya mdogo wake Nikki wa Pili na mpenzi wake Joan kwa madai kuwa hafahamu chochote.

Hata hivyo kumbukumbu zinaonyesha Joh Makini ni moja kati ya wasanii wachache hapa Bongo ambao amefanikiwa kuficha mahusiano yake kwa kipindi kirefu ambacho amesimama kwenye muziki.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Ole Sendeka Akanusha Sauti Inayosambaa Kwenye Mitandao ya Kijamii Asema Imetengenezwa na Wapinzani Ili Kumgombanisha.

Saa chache tu baada ya kusambaa kwenye mitandao ya kijamii sauti iliyodhaniwa kuwa ya Mkuu wa Mkoa wa Njombe Christopher Ole Sendeka akijadili namna ya utendaji wa Bunge na Awamu ya Tano ya Rais Magufuli mwenyewe ametolea ufafanuzi.

Ameeleza kuwa sauti hiyo siyo ya kwake na kwamba imetengenezwa na kuongeza kwamba sauti hiyo imetengenezwa na wapinzani ili kumfarakanisha yeye na viongozi wa serikali na walio chini yao.

“Naomba mzipuuze habari hizi kwa kiwango kinachostahili kwani zote ni uzushi mtupu , badala yake elekezeni macho, fikra na mikakati yenu katika uchaguzi unaokuja.” – RC Ole Sendeka

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Mrema Kudai Mabilioni ya Hela kwa Aliyemzushia Kifo.

Mwenyekti wa Bodi ya Parole nchini Mheshimiwa Agustino Lyatonga Mrema, amesema anaenda kufungua kesi ya madai ya mabilioni ya shilingi kwa watu waliomzushia taarifa za kifo hapo jana.


Akizungumza kwenye kipindi cha East Africa Breakfast kinachorushwa na East Africa Radio, Mrema amesema watu hao wamemletea tatizo kubwa sana la kushtua familia yake na watu wake wa karibu, hivyo anaelekea TCRA ili aweze kusaidiwa kuwabaini, na kuwapeleka polisi kuwafungulia kesi.

"Walivyotangaza jana Mrema amefariki kwanza nasikitika sana, kumtangazia mtu amekufa ni kweli nilihangaika jana, mke wangu alihangaika sana, watoto wangu, marafiki zangu wapenzi wangu walikuwa wanalia kwenye simu kufuatilia hizo habari kumbe ni uzushi, ni uongo habari za kijinga kabisa, nikitoka hapa sasa hivi naenda TCRA", amesema Mrema

Mrema ameendelea kwa kusema .."Nitakuwa kiongozi wa kwanza katika nchi hii kuchukua hatua kali, wanipe fidia inayostahili kwa kuniletea ujinga, nataka kujua huyu mtu aliyeanzisha huu uvumi na kuweka kwenye mitandao kwa ajili ya kunifedhehesha na kuniabisha, bilioni 20 wanilipe kwa usumbufu kwa aibu niliyopata jana".

Kwa upande mwengine Mheshimiwa Mrema amesema kitendo hiko kilimsaidia kujua ni watu gani wanampenda kweli na kina nani hawampendi, kutokana na reaction zao baada ya taarifa feki za kifo chake.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Sakata la Picha za Utupu Basata Aitawaacha Mastaa Hawa Salama.

Muda mfupi baada ya Naibu Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Juliana Daniel Shonza kumfungia msanii wa filamu na muziki wa Bongo Fleva, Suzan Michael ‘Pretty Kind’ kutojihusisha na masuala ya sanaa ikiwemo kutoweka picha yoyote mtandaoni huku akiwataka wasanii Jane Rimoy ‘Sanchi’ na Gift Stanford ‘Gigy Money’ wafike ofisini kwake, waziri huyo amesema orodha ni ndefu na huo ni mwanzo tu.

Katika mazungumzo maalum na Risasi Mchanganyiko, Naibu Waziri Shonza alisema wizara yake imefikia hatua hiyo baada ya kuona baadhi ya wasanii wakienda kinyume na maadili ya Kitanzania hivyo imelazimika kuingia kazini moja kwa moja kudhibiti mmomonyoko wa maadili.


Akijibu swali la msingi juu ya kwa nini ameamua kuanza na adhabu kali dhidi ya Pretty Kind na siyo wengine, Waziri Shonza alisema: “Unajua kabla ya kutoa adhabu hii sisi kama wizara tulitoa onyo kali kwa watu wanaoharibu maadili yetu kwa kuanika picha za ajabu mitandaoni, lakini yeye aliendelea kwa hatua mbaya zaidi, ndiyo maana tumeona tuanze naye kwa mtindo huo huenda akaelewa serikali inamaanisha nini kuzuia uchafu wa aina hiyo.”

Hata hivyo, Shonza ambaye ni Mbunge wa Viti Maalum akiwakilisha Mkoa wa Songwe, alisema orodha haijaishia hapo kwani mkononi mwake anayo majina ya wasanii wengi wanaotumia vibaya mitandao ya kijamii kuharibu maadili na kwamba muda siyo mrefu wanafuata kwenye kikaango vinginevyo wajirekebishe.


“Orodha ni ndefu na kama mnavyojua wasanii wetu wengi hususan wa kike sijui hudhani kujianika hovyo mitandaoni ndiyo ujuzi wa sanaa au sijui ni nini, sasa wapo wengi ambao muda siyo mrefu nitawafungia kazi kwa adhabu kali zaidi,” alisema Waziri Shonza.

Hata hivyo, Risasi Mchanganyiko ambalo ni namba moja kwa kudodosa habari kwa kina, lilitaka kujua ni adhabu gani watachukuliwa wahusika hao na ni nini kitatokea endapo Gigy Money na Sanchi watakaidi agizo la kufika ofisini kwake ambapo waziri huyo alisema:


“Huwezi kumtangazia adui aina ya silaha ulizonazo, wao kama wanaona tunatania basi waendelee kufanya uchafu wao na hao akina Gigy na mwenzake wasipofika ofisini kwangu kitakachowatokea kitajulikana hapohapo lakini niseme tu kwamba serikali kupitia wizara yangu imeamua kulinda na kupigania maadili ya nchi yetu kwa nguvu zote na hatuko tayari kuaibishwa na watu wachache.”

MASTAA HAWA HAPONI MTU

Licha ya Waziri Shonza kutotaja orodha ya majina ya mastaa wanaosubiri kikaango chao, gazeti hili limedadisi na kubaini kuwa kuna mastaa ambao kama hawatajirekebisha hawatapona. Mastaa hao ni kama vile Agness Mmasy, Amber Ruth, Amber Lulu, Sasha, Tunda, Kidoa na wengine wengi wenye hulka na kariba hizo.

KUTOKA RISASI

Gazeti hili linaipongeza kwa dhati kabisa Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo kupitia kwa Naibu Waziri Juliana Shonza kwa kuchukua hatua madhubuti kupambana na wasanii wanaotumia kazi yao kuharibu na kumomonyoa maadili yetu badala ya kujenga na kukuza utamaduni wa Kitanzania na tunawataka wasanii kujitambua kama vioo vya jamii.
Chanzo: Global Publishers

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Friday, 5 January 2018

Chege Akiri Kuathirika.

Msanii Mkogwe kutoka TMK Chege Chigunda amekiri kuwa aliathirika kisaikolojia baada ya kundi la TMK Wanaume Family kuanza kuvunjika.


Chege ametoa kauli hiyo leo akiwa ndani ya Planet Bongo ya East Africa radio na kusema kwamba boss wake ndiye aliyemtia  moyo nakumfanya azidi kupambana na kufikia mahali ambapo anapataka.

Akijibu swali la mtangazaji, Chege amesema kwamba "Nisiwe muongo kuvunjika kwa TMK Family kulinifanya niathirike kisaikolojia. Namshukuru sana Bosi wangu alinitia moyo na kuniambia kwamba nilikuwa pale kwa ajili ya kujitengeneza na siyo kumtegemea mtu aniimbie. Ujasiri wa maneno yale ndiyo yaliyonitia nguvu"

Akizungumzia kuhusu yeye na Temba kuonekana kuonekana maarufu ndani ya kundi kuliko wasanii wengine, Chege amesema kwamba kwenye kundi hakuwezi kuwa na watu maarufu wawili na kuongeza kwamba ndiyo maana yeye na Temba walibahatika.

Akizungumzia kuhusu wao wawili kuonekana na kusikika zaidi ikiwa ni pamoja na kutengeneza kombinesheni pamoja na Temba, Chege amesema kwamba muunganiko wao ulitengenezwa na wahindi ambao walipenda kazi yao na baadae kuamua kufanya kazi na muunganiko huo wa Chege na Temba.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Wachezaji Wanne Waongezewa Mkataba Manchester United.

Klabu ya soka ya Manchester United wamewaongezea mikataba wachezaji wake wanne ambao mikataba yao ilikuwa inafikia ukingoni.



Wachezaji hao ambao wameongezewa mikataba hiyo ni Juan Mata, Ander Herrera, Ashley Young na Daley Blind hadi mwisho wa msimu ujao. Wachezaji hao walikuwa wanatakiwa kuondoka bure mwishoni mwa msimu huu lakini United wamewapatia mikataba ya haraka wachezaji hao na kuimarisha ya maadili yao ya uhamisho kwa kuanzisha vifungu vinavyoongeza mikataba yao kwa miezi 12 hadi Juni 2019.

Mchezaji mwengine ambaye anatajwa kutaka kuongezewa mkataba ni Luke Shaw ambaye amewavutia sana mashabiki wa United kutokana na uwezo wake katika wiki za hivi karibuni na inawezekana kupewa mpaka mwisho wa msimu kuthibitisha thamani yake kabla ya uamuzi kufanywa juu yake.



Hata hivyo Marouane Fellaini amekataa kuongeza mkataba mpya na timu hiyo ambapo mwishoni mwa msimu huu atakuwa huru na timu ya Besitkas inaongoza katika mbio za kutaka kumsajili kiungo huyo wa Ubelgiji.

Mourinho hataki kumuuza Fellaini katika dirisha la uhamisho la majira ya baridi na amejiandaa kumpoteza wakati wa majira ya joto. licha ya matatizo yake ya sasa ya kuumia. Fellaini ameanza mechi moja tu tangu mwisho wa Septemba kwa sababu ya kuumia.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Watu Washtushwa na Muonekano Mpya wa Wowowo la Ruby.

Jana msanii wa Muziki wa Bongo Fleva, Ruby kupitia ukurasa wake wa Instagram aliposti picha ikimuonesha mwenye umbo kubwa tofauti na muonekano wake wa siku zote.

Picha hiyo ambayo ni ya kwanza kwa mwaka 2018 kwa msanii huyo kuonekana, Ruby aliiweka na kuwatakia mashabiki wake Kheri ya Mwaka mpya.

Watu wengi waliotoa maoni kwenye posti hiyo wameonekana kushangaa mabadiliko hayo ya ghafla huku wengine wakidai ametumia dawa za kuongeza makalio wengine wakiamini kuwa ametumia App ku’edit picha hiyo.

utamu_baby Mchina ruby huo yaan unatudangny hvhv wakat ulikua mwembamba kama mwiko Wa pilau😂😂
fasamalsaid Kweli hii mwaka mpya mambo mapya , hongera kwa mchina #wowowo
koiyarachel@laur_de_patrique katoa wapi huu msambwanda jomoni katuzidi hadi sisi. Kweli kati ya kiboko na mamba, mamba ndio kiboko!!! pooohhhh…
mamukimwanyaMara paah 2018 kitako icho
officialsiahshoo1Kwel uchaw upo had 2018 🙊🙊unalala slim unaamka na bonge la wowowo
mdogo_wake_hamisakama ni vigodoro duuuh wew umezidi umeweka kochi zima
Ukweli ni kwamba Ruby hajatumia dawa ya kichina wala kuvaa kigodoro bali picha hiyo imefanyiwa editing  kupitia Application maalumu zinazofanya kazi hiyo ya kuongeza maumbo kwenye picha.


Picha Orijino ya Ruby aliyopiga kabla ya kueditiwa.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Pendeza na Dar Empire Products: Badili Muonekano Wako na Kuweka Mwili Wako Sawa Bila Madhara yoyote.

PENDEZA NA DAR EMPIRE PRODUCTS: BADILI MUONEKANO WAKO NA KUWEKA MWILI WAKO SAWA KWA PRODUCT ZISIZO NA MADHARA YEYOTE WALA KEMIKALI, MATOKEO NI KWAARAKA.


  1)ONDOA NYAMA UZEMBE MIKONONI, KIUNONI KUPAK
2)TOA  KITAMBI KABISA
 3) PUNGUZA MWILI MZIMA KUANZIA KILO UNAZOITAJI WEWE
4) ONDOA MICHIRIZI ILIYO SHINDIKANA
 5) TOA MAKOVU, CHUNUSI, WEUSI KWENY MAPAJA KIKWAPAN
 6) KUWA MWEUPE WAKUPENDEZA
7) ONGEZA NGUVU ZA KIUME
  8) RUDISHA HAMU YA TENDO NA KUCHELEWA KUFIKA KILELE
9)ONDOA MAFUTA USONI
 10) ONDOA MIKUNJO USON

 TUNAPATIKAN DAR ES SALAAM:  PIGA CM

+255658 440 707

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

LIVE:Tundu Lissu azungumza na waandishi kutoka Hospitali ya Nairobi, Kenya.

Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa Mhe Freeman Mbowe na Mhe. Mwanasheria Mkuu wa Chadema Tundu Lissu watakuwa na mkutano na waandishi wa habari kutoka Nairobi Hospital .Mkutano huo utarushwa mubashara na KTN_News na Citizentvkenya , Saa nane kamili mchana

KUTOKA NAIROBI

Tundu Lissu anasema,


Kesho natimiza miezi minne tangu niletwe hapa Nairobi Hospital nikiwa sijutambui,nishukuru timu ya madaktari waliofanya kazi ya kuokoa maisha yangu".

Kwa namna ya kipekee kabisa niwashukuru wauguzi na madaktari wa Nairobi Hospital kwa kunifanya leo baada ya miezi minne niko hivi mnavyoniona.

Nilipigwa risasi 16 lakini mpaka sasa hakuna taarifa ya kukamatwa kwa mtuhumiwa yeyote wala sijahojiwa mbali na vitisho kwa Dereva wangu na kwa kifupi hakuna uchunguzi wowote kuhusu tukio hilo.

Kwa mara ya kwanza, kikundi cha watu wanaoitwa hawajulikani, walichukua bunduki za vita wakanifuata Bungeni, nilipotoka Bungeni mpaka nyumbani kwangu saa saba mchana kwa lengo la kuniua.

Kuna risasi moja nyuma ya uti wa mgongo. Madaktari wamesema ni hatari zaidi kuitoa kuliko ikibaki

Kilichofanyika dhidi yangu lilikuwa ni tukio la mauaji ya kisiasa moja kwa moja (Planned Political Assasination).

Sikupigwa Risasi za Bastola,walichukua bunduki za Vita wakanifwata kwa lengo la kuniua,ni kwa mara ya kwanza kutokea Tanzania.

Nilipigwa risasi 16 lakini mpaka sasa hakuna taarifa ya kukamatwa kwa mtuhumiwa yeyote wala sijahojiwa mbali na vitisho kwa Dereva wangu na kwa kifupi hakuna uchunguzi wowote kuhusu tukio hilo.

Jeshi la polisi kwa maoni yangu halipepelezi tukio hili kwa sababu wanajua njama za mauaji ya kisiasa kwa sababu nasumbua wakubwa wa Tanzania.

Serikali ya Tanzania na Jeshi la polisi lilifanya kila lililowezekana kuhakikisha watu hawalitaji jina la Tundu Lissu.

Haijawahi kutokea kwa mtu au kikundi cha watu kuchukua silaha na kwenda kumuua kiongozi wa kisiasa kwa sababu tu ya msimamo wake, hii ni mara ya kwanza katika historia.

Kosa kubwa la Tanzania ni kosa la uchochezi, ukiikosoa serikali ni mchochezi, ukimkosoa Rais ni mchochezi, ukimkosoa waziri ni mchochezi.

Sikushambuliwa na silaha za kawaida, nilishambuliwa na silaha za kivita.

Leo nazungumza hapa mbele yenu, Bunge la Tanzania halijatoa hata senti kumi kulipia gharama zangu za matibabu.

Serikali ambazo zina wajibu wa kulinda maisha ya raia wake, zinapoacha wajibu huo zinapaswa kuzomewa na dunia nzima.

Ni wakati wa vyombo vya habari kuihoji Serikali ya Tanzania.. Kwanini mnapiga watu risasi? Kwanini miili ya watu inapatikana ikielea baharini? Kwanini watu wanapotea?

Tangu nishambuliwe, Rais Magufuli hajasema chochote kuhusiana na tukio hili. nimeambiwa kuwa aliandika 'tweet', lakini siamini kama anaweza kutweet kama Rais Donald Trump.

Nimefanyiwa Oparesheni 17 na kwa sasa ninaweza kusema sio nimepata nafuu lakini nimepona kabisa.

Nashukuru Mwenyekiti wa CHADEMA kwa kunileta Nairobi. Serikali ilitaka nitibiwe Dar es Salaam ili niwe chini ya uangalizi wao mbovu.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Wastara amlilia Rais Magufuli baada ya kutapeliwa milioni 80 na kampuni ya simu.

Msanii wa filamu Wastara Juma amepaza sauti yake ya kutaka kusaidiwa pesa ya matibabu na Rais John Pombe Magufuli baada ya kutapeliwa na kampuni moja ya simu ambayo ilimteua kama balozi wa bidhaa zao.

Muigizaji huyo amedai ametapeliwa zaidi ya tsh milioni 80 na kampuni hiyo ya simu pesa ambayo amedai alikuwa anajichanga kwaajili ya matibabu ya mguu wake nchini India.

Taarifa ya Wastara.

    “RAIS MHE MAGUFULI
    MAKAMO MHE SAMIA SULUHU
    WAZIRI MKUU MHE KASIM MAJAALIWA
    MKUU  WA MKOA MHE POUL MAKONDA
    WATANZANIA WENZANGU

Mim Wastara juma muigizaji wa filamu tanzania naandika ujumbe huu mfupi sina budi sina jinsi nahitajika kurudi hosptal india Sifael hosptal tokea tal 12/02/2017 ambapo nilitakiwa nifanye matibabu kwa mda wa miaka 2 chini ya uwangilizi wa hosptal hiyo kabla ya kufanya maamuzi ya kufanyiwa operetion ya mgongo hivyo kila tal 12/ 2 natakiwa kurudi hosptal nimejitahidi kupambana peke yangu kutafuta pesa ya kunirudisha hosptal nimeshindwa

Mwezi 1 wachina wenye kampun ya simu ya KZG wamenikimbia nikiwadai milion 80 mwezi wa 2 muzambiq nimepoteza mzigo wa milon 19 kwenye vurugu la kufukuzwa watanzania
 
Mwezi wa 3 nimeenda nchini sweden kufanya filamu nimerudi mikono mitupu mwezi wa 4 nimedai pesa yangu steps tumeishia kwenda mahakamani bila kulipwa nilivyokuwa natarajia tokea hapo chchote ninachofanya kinachohusu pesa lazima tuishie polisi au mahakamani silipwi vile tunavyokubaliana na baya zaidi ninaofanya nao kazi awajui kuwa tokea nimerudi nchini toka sweden ninahaha kutafuta pesa ya matibabu,,

silali kwa maumivu makali ya mgongo na ninazimia kila mda hii imetokana na kuchelewa kurudi hosptal kufanya tiba ya mgongo na kubadilisha soberly skoner inayowekwa kwenye mguu kama tiba kuu ya kurudisha mgongo wangu ukae sawa matokeo yake mguu unavimba na kuchanika kila mara mgongo unauma kitu ambacho kinanikosesha raha kabisa na kuona sasa naathirika kiakili kwa maumivu sababu mda mwingi nakunywa dawa za maumivu bila kujua kama nimemeza dawa mara ngapi kwa siku hii sio nzuri kiafya

Kikubwa ninachoomba kutoka kwenu ni mim nirudi kwenye apointment yangu ya hospital sababu siwezi kurudisha mguu wangu kama zamani lakini ninaweza kuyakwepa maumivu kutokana na tiba ninayoweza kupata kupitia tatizo langu

Sihitaji msaada wa mtu nikiwa mahututi nikiwa siwezi kuandika sms kupokea sim au kumtambua mtu nahitaji sasa ninayo nguvu kidogo ya kuelewa hta nataka kutibiwa nin staki nisaidiwe kwa mtu kunisemea matatizo yangu wakati huo mim nimeshashindwa hta kuongea tena please watanzania wenzangu mficha uchi hazai sio mim mwenye matatizo pekee wapo wengi ila wanaona aibu najua mtajiuliza kiasiku wastara anauza nguo why?

anataka msaada sio kweli kuwa biashara ya mtandao inakidhi mahitaji yetu nimekuwa nikipost bidhaa kwa fujo bila kupost hta picha zangu nikiamini nitauza sana ili nirudi hosptal lakini sio kweli kabisa watu wanataka kuniona mim mitandaoni na sio mashati na magauni ninayouza ndio maana sifanyi vizuri upande huo ninaumia sana kuona mashabiki nawanyima haki ya kuniona lakini ninayo shida nahitaji niwe na afya njema nitembee vizuri nifurahi na watoto wangu na mashabiki zangu

afya yangu mim inauzwa tena kuanzia dollar 18000 pia mtajuliza why sioni aibu kusema shida zangu au kuomba msaada wakati mimi ni msanii na tafsir ya walio wengi wasanii ni watu wenye pesa sana sio kweli sanaaa yetu ndio kwanza inakuwa nimechoka kupost nikilalamika naumwa huku kesho mtu ananiona mzima nacheza mziki kumbe najilazimisha tu kuficha mateso yangu staki tena kuficha maumivu yangu natembea nanenepa huku nina maumivu makali

natamani nimmpe mtu huu mwili na ili jina ili niwe huru kwenye mateso ya kujificha huku naumia
 
nimejaribu sana kuongea na marafiki zangu wa karibu wanajua natania ninavyosema naumwa nahitaji msaada mtu aamini hata nikimwambia nichangie elfu 50 anaona nina pesa nyingi sana nadanganya No kabla haujafa haujaumbuka

nikiuza nyumba gari na chchote nilichonacho alafu nikafa watoto wangu wataishi wapi nin kitawasaidia mpka wapate pesa za kujikimu?? Jibu hakuna japo nimejaribu kunadi kilakitu nilichonacho ili mladi nipate pesa nirudi hosptal lakin mda umepita sana na naendelea kuumia mwili na kiakili pia sijafanikiwa please usinitafsir vibaya wala kunikejili wakati huna uwezo wa kunisaidia mim nimeamua kuwa muwazi kuwa nahitaji msaada ili niendelee na majukumu yangu watoto na watanzania waendelee kuniona

Pili ninaomba serikali inisaidie nipate pesa ninazowadai wachina mpka sasa zaidi ya milion 400 maana nilisain mkataba wa miaka miwili mpka leo ni mwaka 1 na miezi 2 na awajasitisha huo mkataba mpka leo kitu kinachoniuzia mim kufanya kazi na kampuny nyingine ya kuuza sim mpka mkataba wao uishe na awajanipa hta shilingi mia mpka sasa….

please wamenitoroka sina mkono mrefu wa kuwakamata zaidi ya huruma yenu na wanacho kiwanda kikubwa tu uko kwao china cha KZG kwasasa ninachohitaji kuliko chochote ni afya yangu kwanza
 
    Ukiguswa kwa chchote nipo na unanipata kwa no hii.
    0768666113
    0768666113

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

CCM yamsaka diwani wake aliyeipa kura UKAWA.

Wajumbe wa CCM wanaoingia kwenye Baraza la Madiwani la Jiji la Dar es Salaam, wamesema wapo katika hatua za mwisho za kumpata mjumbe mwenzao aliyesababisha wao kushindwa uchaguzi wa naibu meya wa jiji hilo.

Uchaguzi huo uliokuwa na mchuano mkali kutokana na kila upande kuwa na wajumbe kumi na moja, ulifanyika juzi katika ukumbi wa Karimjee na Mussa Kafana wa CUF akiungwa mkono na vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) aliibuka kidedea kwa kupata kura 12 dhidi ya 10 alizopata Mariam Lulida wa CCM.

Akizungumza kwa niaba ya wenzake, mjumbe baraza hilo CCM, Abdallah Chaurembo alisema tayari wanao ushahidi na wameshaanza kumbaini mjumbe ambaye alisababisha chama chao kushindwa katika uchaguzi huo.

“Tunataka kuirahisishia kazi kamati ya siasa ya mkoa kwa kumpata kwanza mjumbe huyu, halafu wao ndiyo watakaokuwa na jukumu la kumtangaza na kumchukulia anazostahili kwa mujibu wa makosa yake,” alisema Chaurembo.

Chaurembo ambaye pia ni Meya wa Temeke alisema walishaanza kumbaini mjumbe huyo kabla ya kazi ya kuhesabu halijakamilika na kudai kwamba hakuwa na nia ya dhati na CCM.

“Tulishakijua alichokuwa akikifanya, kwanza alikuwa anatetemeka wakati anaenda kupiga kura. Wakati yupo katika eneo la kupiga yeye ndiyo alitumia takriban dakika tano wakati wenzake nusu dakika.

“Hivi mtu unachukua takriban dakika tano nzima katika kupiga kura, una nini wewe, ina maana hujui kusoma wala kuandika? Alihoji Chaurembo. Nawaambia WanaCCM tutampata mtu huyo very soon (muda mfupi).

Alisema wameamua kushughulikia jambo hilo, ili iwe funzo kwa madiwani wengine wasiokitakia mema chama hicho na kwamba, hiyo itakuwa njia ya kuwaondoa wale viongozi wasio na masilahi na CCM.

Alieleza kuwa wajumbe wa CCM katika baraza hilo, wana imani wameshindwa katika uchaguzi kwa hoja mbili ambazo ni Ukawa kutumia utemi wakati kura mbili ziliharibika, na mjumbe mwenzao kuharibu kura na siyo kumpigia kura mgombea wa upinzani.

Katika uchaguzi huo, Chaurembo na meya mwenzake wa Ubungo (Chadema), Boniface Jacob nusura wazichape wakati wa shughuli ya kuhesabu kura kama si wajumbe wa uchaguzi huo kuwatenganisha.

Chaurembo aliendelea kwa kufafanua kuwa mjumbe huyo akishapatikana wajumbe wa CCM wa baraza ndiyo watakaokuwa mashahidi kwenye kamati ya siasa ya mkoa.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

BREAKING News>>Rugemarila Awataja Wezi wa Fedha za Escrow.

Leo January 5, 2017 Mfanyabiashara James Rugemarila anayekabiliwa na kesi ya utakatishaji fedha amewataja wezi wa fedha za Escrow katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kama alivyodai awali kuwa atawataja.

Wezi hao amewataja mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba baada ya Mwendesha Mashtaka wa TAKUKURU, Leornad Swai kueleza upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika, hivyo anaomba iahirishwe hadi tarehe nyingine.

“Mwizi ni Standard Chartered Tanzania Ltd na Standard Chartered Hong Kong ambao wameisababishia serikali hasara ya Trilioni 37, pia nimewapelekea TAKUKURU washiriki wengine wa fedha hizo, hivyo ninaomba niendelee kuwa hai ili nije kuwa shahidi mzuri wa upande wa mashtaka kuhusu wezi hao.” – James Rugemarila

Pia Rugemarila amedai kuwa wezi hao ndio wamemuibia hata kwenye kampuni anayoisimamia ya VIP ambayo inawadai Trillion 16. Wakili Swai alidai kuwa ni kweli Rugemarila aliwasilisha taarifa ofisini kwao na wanazifanyia kazi kisha watatoa majibu.

Tofauti na hayo Rugemarila pia ameiomba mahakama imkubalie akafanyiwe uchunguzi nchini India kwa sababu anasumbuliwa na ugonjwa wa saratani kwa miaka 9 sasa huku mshtakiwa mwingine ambaye ni mmiliki wa IPTL Harbinder Singh Sethi aliiambia Mahakama kuwa tatizo lake la ugonjwa linajulikana.

Kutokana na hatua, Hakimu Simba amesema afya za washtakiwa ni muhimu hivyo wafanyiwe uchunguzi, pia anautaka upande wa mashtaka ukamilishe upelelezi kwa wakati, ambapo ameahirisha kesi hiyo hadi January 19,2018.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Tunda: Nipo Tayari Kuwa Mke wa Mtu.

MUUZA nyago aliyejizolea umaarufu kutokana na vituko vyake, Tunda Sebastian, amefungukia kubadili muonekano wake kuwa, amefanya hivyo ili kukwepa kuonekana na mwili wa kitoto tena.

Akizungumza na Star Mix,Tunda alisema kuwa anapendezwa na muonekano ambao anaonekana hivi sasa kwa sababu angalau anaonekana mtu mzima hata mtu akimuoa anajua ana mke mkweli ndani.


“Nafurahia sana muonekano wangu wa sasa hivi nilivyo na kwa sasa nipo tayari kuitwa mke wa mtu maana hata nikiwekwa ndani kama mke nafaa kabisa, nilikuwa nakereka watu kunifananisha na katoto,” alisema Tunda.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Asante Kwasi Ang'aa Katika Mchezo wa Jana katika Michuano ya Mapinduzi.

Mlinzi mpya wa Simba raia wa Ghana Asante Kwasi jana amefanikiwa kufunga bao katika mchezo wake wa kwanza na klabu yake hiyo mpya kwenye michuano ya Mapinduzi na kuwazidi mabao baadhi ya washambuliaji msimu huu.


Asante Kwasi ambaye amesajiliwa na Simba kwenye dirisha dogo akitokea Lipuli FC amekuwa miongoni mwa walinzi wenye uwezo mkubwa wa kufunga. Baada ya jana usiku kufunga Kwasi sasa amefikisha mabao 6 msimu huu.

Akiwa na Lipuli FC Kwasi alifanikiwa kufunga mabao 5 katika mechi 11 za ligi kuu Tanzania bara alizocheza kabla ya dirisha dogo. Asante Kwasi sasa anakaa nyuma ya Emmanuel Okwi mwenye mabao 8 katika VPL na Habibu Kiombo mwenye mabao 7 kwenye VPL.

Mlinzi huyo anayemudu nafasi ya mlinzi wa kati na pembeni kushoto alifunga bao la tatu katika ushindi wa mabao 3-1 ilioupata Simba kwenye mechi yake ya pili kwenye michuano ya Mapinduzi 2018 uwanja wa Amaan.

Pia amekuwa ni miongoni mwa wachezaji wachache ambao wamefanikiwa kufunga bao katika mechi zao za kwanza na klabu mpya tena kwenye mashindano ambayo mchezaji anashiriki kwa mara ya kwanza

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Lucy Kombaa Kumzalia Mtoto Mzungu Wake.

MSANII wa filamu Bongo, Lucy Komba ambaye kipindi cha nyuma aliweka ngumu kumzalia mzungu wake, sasa anadaiwa kuwa kwenye mkakati mzito wa kusaka mtoto baada ya mwanaume huyo na familia yake kuchachamaa azae.

Akizungumza na Star Mix, mtoa ubuyu ambaye yupo karibu na bibie huyo alisema, japo kipindi cha nyuma aligoma kumzalia mzungu wake kwa madai kuwa bado anasoma sababu alijiunga na kozi mbalimbali, kwa sasa familia imemjia juu ikimtaka azae.

Baada ya kuunyaka ubuyu huo, Lucy anayeishi nchini Denmark na mumewe alivutiwa waya, alipopatikana alisema: “Mambo mengine ni ya kifamilia siwezi kuyaongelea, lakini kifupi tu ni kwamba sasa nipo kwenye mkakati wa kumpatia mtoto mume wangu.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Soma Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo.

Bonyeza Links zifuatazo Kusoma zaidi na Kuapply:


Vacancies Announcement at NMB Bank Plc, January 2018

Job Opportunities at Tanzania National Roads Agency (TANROADS)

Job Opportunity at Exact Manpower Consulting LTD, Legal Manager

Job Opportunity at PowerCorner Tanzania LTD, Electrical Technician

Job Opportunity at RTI International, Deputy Chief of Party

Higher Education Students' Loans Board: ORODHA YA WADAIWA SUGU JANUARY 2018

Job Opportunity at VisionPlus Integrated (VPI) Ltd, Accountant

Nafasi zingine za kazi ingia www.ajirayako.co.tz

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Aishi Manula Kufunga Ndoa Kesho.

Huku michuano ya Kombe la Mapinduzi ikiendelea kisiwani Zanzibar, kipa namba moja wa Simba, Aishi Manula hayupo katika kikosi hicho na anatarajiwa kufunga ndoa kesho Jumamosi.

Wakati Manula akifunga ndoa, timu yake itakuwa uwanjani kesho kuvaana na Azam FC kwenye michuano hiyo ikiwa ni mchezo wa makundi ambapo wote wapo Kundi A.

Kipa huyo alisema amefanya taratibu zote za kuomba ruhusa ili afanye namna ya kulimaliza suala hilo muhimu.

“Ni kweli sipo Zanzibar na timu kwa sababu nina ruhusa, Jumamosi ninatarajia kufunga ndoa ndiyo maana nimeshindwa kuungana na wenzangu kwa sasa kutokana na shughuli hiyo.

“Nawatakia kila la kheri wapambane na kufanya vyema, sijafahamu ni lini nitaweza kuungana na timu,” alisema Manula.

Taarifa zinaeleza, kama Simba itafika hatua za mwishoni, nusu fainali au fainali, Manula anaweza kuungana na wenzake kuipigania timu hiyo.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Meneja wa Wakala wa Majengo (TBA) Kigoma Akamatwa.

Jeshi la polisi linamshikilia Meneja wa Wakala wa Majengo (TBA), Mhandisi Mgalla Mashaka kwa tuhuma za kushindwa kukarabati Shule ya Sekondari Kigoma.

Meneja huyo alikamatwa akituhumiwa kushindwa kukarabati shule ya sekondari Kigoma kwa wakati licha ya kupewa zaidi ya shilingi milioni mia nne kati ya mia tisa tangu mwezi wa nane mwaka jana.

Mhandisi Mgalla amekamatwa baada ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Joyce Ndalichako, kufanya ukaguzi katika shule hiyo ambayo imeanza kupokea takribani wanafunzi elfu moja huku katika miezi mitano ya ukarabati hadi sasa ukarabati wa vyoo, mabweni, maabara na vyumba vya madarasa haujakamilika

Prof. Ndalichako amemuagiza Mkurugenzi Mkuu wa TBA kufika Kigoma kutatua tatizo hilo ili kuepusha maafa yanayoweza kutokea. Kutokana na hali hiyo serikali imeamua kujenga vyoo vya muda ili wanafunzi waweze kuanza masomo wiki ijayo.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Thursday, 4 January 2018

Simon Msuva Ametua Nchini kwa Mapumziko.

Kiungo mshambuliaji wa timu ya taifa ya Tanzania na klabu ya Difaa El Jadidi ya nchini Morocco, Simon Msuva ametua nchini kwa mapunziko ya muda mfupi huku akiwa na hari na hamasa kubwa ya kuhakikisha anacheza soka lakulipwa barani Ulaya.



Msuva ambaye awali alikuwa akiitumikia klabu ya Yanga kabla ya kusajiliwa nchini Morocco kwa kulipwa mshahara mnono unaokadiriwa dola 4,000 (takribani Sh milioni 9) amesema kuwa bado lengo lake kubwa ni kuhakikisha anacheza soka la kulipwa barani Ulaya.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Sherehe ya Kuchumbiwa Wolper Balaa..... Muoaji Afanya Kufuru ya Aina Yake.

SHEREHE ya kuchumbiwa kwa Staa wa sinema za Kibongo na Malkia wa Mavazi, Jacqueline Wolper imezua gumzo la aina yake baada ya muoaji kufanya kufuru ya aina yake, Amani linaripoti habari hii kwa mara ya kwanza (exclusive).

Sherehe hiyo iliyohusisha msafara mkubwa wa magari kutoka jijini Dar, ilifanyika Moshi, wikiendi iliyopita nyumbani kwa bibi yake kijijini Moshi.

Ili kutazama picha zote za tukio zima la kuchumbiwa kwa Wolper na mpenzi wake, Sadiki Athanasy Sanga ‘Engine’, ingia kwenye Application yetu ya Global Publishers sehemu ya magazeti.

Kama Huja-download fanya hivyo sasa, install kwa kupitia hizi Link uzitazame picha zote za kuchumbiwa kwa Wolper.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Baada ya Babu Seya na Mwanaye Kwenda Ikulu Mjadala Mkali Waibuka.

Inawezekana ilikuwa ni nia njema kwenda kumshuku Rais kwa kumpa msamaha uliomuepusha na kifungo cha maisha, lakini kitendo hicho cha Nguza Mbangu Viking na wanawe kimepokelewa kwa hisia tofauti.

Nguza, ambaye ni mtunzi wa wimbo maarufu wa “Seya” uliomfanya apachikwe jina la Babu Seya katika kesi ya kubaka na kulawiti wanafunzi wenye umri kati ya miaka sita na nane, na mwanae Johnson Nguza au Papii Kocha, walisamehewa na Rais John Magufuli pamoja na wafungwa wengine 8,150 siku ya Uhuru wa Tanganyika.

Alikuwa kitumikia kifungo cha maisha baada ya mahakama kumtia hatiani kwa kubaka na kulawiti watoto hao, na juhudi za kupangua hukumu hiyo Mahakama Kuu, Mahakama ya Rufani na nyuingine za nje hazikuweza kufanikiwa.

Lakini msamaha wa nadra kutokea kwa wafungwa wanaotumikia kifungo cha maisha na wenye makosa ya kubaka na kulawiti, ulimuepusha nyota huyo maarufu kwa kupiga gitaa la solo na mara tu alipotoka alisema angependa kuonana na Rais kwa ajili ya kumshukuru na akapata nafasi hiyo juzi.

Lakini kupokelewa kwake kumeibua hoja tofauti.

Wako wanaowaangalia waliofanyiwa vitendo hivyo miaka 13 iliyopita, ambao kwa sasa ni wasichana, na wengine wanaoangalia nafasi waliyoipata tofauti na wengine walionufaika na msamaha huo.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, watu waliohojiwa na gazeti hili walisema tukio la kwenda Ikulu halikupaswa kupambwa, pamoja na ukweli kwamba Katiba inampa Rais mamlaka ya kusamehe wafungwa wa aina yoyote.

“Sikuona haja ya Ikulu kulikuza suala la wanamuzi hao kwenda kuonana na Rais. Baada ya kusamehewa kwa nini wanageuzwa kama mashujaa?,” alihoji Wakili Onesmo Kyaule.

“Inawezekana kabisa hilo likawa na picha tofauti kwa watu waliofanya au watakaofanya makosa kama yao.”

Ikulu ilisambaza picha za Nguza na familia yake wakiwa wanatembea kuelekea Ikulu na baadaye wakiwa kwenye mazungumzo na Rais na nyingine zinazoonyesha wakisalimiana na baadaye wakitoka.

Dk Kyauke alisema licha ya sheria kumpa Rais mamlaka ya kusamehe, wanamuziki hao walipaswa kurejeshwa kwao baada ya kusamehewa.

Naye wakili mwingine wa kujitegemea, Alloyce Komba wa kampuni ya Haki Kwanza, alipinga kitendo cha wanamuziki hao kwenda Ikulu kwa maelezo kuwa licha ya kusamehewa kwao, bado wana hatia ya ubakaji.

Alisema lingekuwa jambo la maana kama wangeitisha mkutano na waandishi wa habari na kumshukuru Rais kuliko kwenda Ikulu na suala lao kutangazwa.

“Rais akisamehe wafungwa anakuwa na vigezo vyake ila katika hili la kina Babu Seya, nimeshtuka kidogo,” alisema.

Alibainisha kuwa Papii Kocha na Babu Seya walitiwa hatiani na hata walipokata rufaa walishindwa.

“Kwa kuwa tunaheshimu utawala wa sheria na Mahakama ndio yenye uamuzi wa mwisho na wahusika wameshindwa kwenye hizo ngazi zote, tunatakiwa tuheshimu,” alisema.

“Kwenda Ikulu kuna heshima, hawa heshima hii wameipata wapi? Aaah sisi tunaomuamini Mungu tunasema sawa ila katika sheria, sheria ni sheria.”

Alisema msamaha huo unaweza ukawa kikwazo kwa vyombo vya Serikali vinavyopambana kudhibiti makosa ya ubakaji na mengineyo.

Naye Profesa Mwesiga Baregu wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustino (Saut) alisema: “Sikutegemea kama wangeenda Ikulu kwa sababu msamaha wa Rais haufuti hukumu. Hauondoi jinai waliyofanya.

“Sijasikia kama wameomba radhi nasema hivi kwa sababu watoto waliotendewa vitendo hivyo pamoja na wazazi wao bado wapo na wanaliona suala hili.”

Alisema kama wanamuziki hao wangekaribishwa Ikulu sambamba na waliotendewa vitendo viovu walau ingeeleweka, “hata Serikali kufikiria fidia kwa waliotendewa vitendo vile nayo ingeweza kueleweka”.

Kwa upande wake, Dk James Jesse wa Shule Kuu ya Sheria Chuo Kikuu Dar es Salaam (UDSM) pia alisema msamaha haujafuta kosa.

“Unapopewa msahama sio kwamba kosa lako linafutwa. Rais ana mamlaka ya Kikatiba kufanya alichokifanya na kama watu watawaza tofauti huwezi kuwazuia,” alisema.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Penny Afunguka Kuwa na Gundu la Ndoa kwa Mwaka 2017.

MTANGAZAJI wa Runinga ya Magic Swahili kupitia kipindi cha Harusi Yetu, Penniel Mungilwa ‘Penny’amefunguka kuwa, kuna uwezekano alikuwa na gundu la kutoolewa mwaka 2017 lakini anaamini mwaka huu, 2018 ataolewa kwa uwezo wa Mungu.

Akizungumza na gazeti hili, Penny alisema mwaka huu yuko tayari kwa ndoa na kwa mwanaume sahihi kwani ameomba vya kutosha.

“Mwaka huu ni wa baraka kwangu na gundu nyingi zimeshaondoka 2017, mwaka huu kwangu ishallah shela litakaa mwilini mwangu, mwanaume yupo tayari,” alisema Penny bila kumtaja jina mwanaume wake.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa