Sunday, 25 June 2017

Manji amuomba radhi Rais Magufuli sakata la Coco Beach.

Mfanyabiashara maarufu na Diwani wa Mbagala, Yusuf Manji amemuomba radhi Rais John Magufuli kutokana na kesi aliyoifungua akidai kupewa haki ya uwekezaji katika eneo la Coco Beach jijini Dar es Salaam.

Manji ambaye pia ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Quality Group alishinda zabuni iliyotangazwa na Manispaa ya Kinondoni mwaka 2005, kwa ajili ya uwekezaji wa eneo la Coco Beach karibu na Bwalo la Maofisa wa Polisi lililopo Oysterbay.

Akizungumza kupitia taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari jana, Manji alisema licha ya kampuni yake kupitia kampuni tanzu ya Q-Consult kuingia makubaliano na Manispaa ya Kinondoni Desemba 21, 2007 kulikuwa na ucheleweshaji wa mradi huo.

“Hali hiyo ilisababisha kampuni yetu kutafuta njia ya sheria katika Mahakama Kuu Kitengo cha Ardhi, Desemba 17, 2007 na kufungua kesi ya ardhi namba 334 ya 2009 ambapo baada ya miezi sita Mahakama Kuu iliagiza Manispaa ya Kinondoni kutekeleza ahadi yake,” alisema Manji.

Hata hivyo, alisema baada ya Rais Magufuli kuingia madarakani alitangaza kusudio la kulifanya eneo hilo kubakia kuwa la matumizi ya wananchi kama lilivyo sasa.

“Kwa kutambua maelekezo ya Serikali ya Awamu ya Tano tunatii agizo na kuacha eneo hili liendelee kwa matumizi kama ambavyo linatumika sasa,” alisema Manji na kuongeza kuwa:

“Ninaomba radhi binafsi kwa Rais John Magufuli na Serikali yake kwa sintofahamu yoyote iliyojitokeza wakati wa ufuatiliaji wa jambo hili.”

Manji alisema wamewaagiza mawakili wao kujitoa kama wapinzani katika rufaa iliyowekwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali na kutodai gharama zozote walizoingia au hasara ya mapato kwa kuwa masilahi yao sio halali ukilinganisha na ya wananchi.

“Mwisho Quality Group Limited inatambua na kuunga mkono juhudi zote za Rais Magufuli za kizalendo katika kusimamia rasilimali za nchi yetu,” alisema Manji.

Desemba 5, 2015, Manji alimwandikia barua Rais Magufuli akimweleza usahihi wa mchakato wa zabuni ya kuendeleza Coco Beach.

Pia, katika barua hiyo alimwomba Rais afanye uchunguzi binafsi chini ya ofisi yake ambayo atashirikia nayo.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Download wimbo wa Cpwaa Ft. The Artist, Godzilla, One, Lord Eyez & Mabeste unaoitwa "Mission 12 O-Clock".

https://my.notjustok.com/track/download/id/235504



Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Waziri George Simbachawene Amemteua Profesa wa UDOM kuwa Diwani.

Dodoma. Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Tamisemi), George Simbachawene amemteua Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Profesa Davis Mwamfupe kuwa diwani katika Manispaa ya Dodoma.

Juzi Mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma Godwin Kunambi alimtaja Profesa Mwamfupe pamoja na wenzake wawili Roze Nitwa (CCM) na Vicent Tibalindwa (Chadema) kuwa waliteuliwa na Waziri kwa mujibu wa mamlaka aliyonayo.

Kunambi alisema Simbachawene aliteua majina sita kwa vyama vya Chadema na CCM ndipo wakayapigia kura likiwamo jina la Mwamfupe aliyetokea CCM.

“Waziri alitumia sheria namba 288 (24) (2d) ya Serikali za mitaa na kanuni za uteuzi za mwaka 2010 sura ya 4 (1) na 5 (1) vinavyompa mamlaka ya kufanya hivyo bila kuulizwa na humteua mtu ambaye ni mkazi wa eneo husika,” alisema Kunambi.

Manispaa ya Dodoma haina Meya baada ya Jaffary Mwanyemba kuondolewa na madiwani Machi mwaka huu kwa madai ya matumizi mabaya ya madaraka.

Hata hivyo, Mkurugenzi huyo alikana madai ya kumwandaa msomi huo wa uchumi katika nafasi ya Umeya ingawa alisema kila mtu mwenye sifa za kuwa diwani ana haki ya kugombea nafasi ya uongozi ikiwamo meya.

Mkurugenzi huyo aliwaondoa hofu waliokuwa wamejenga nyumba zao katika maeneo ambayo hayajapimwa kabla ya kuvunjwa kwa CDA akisema hawatasumbuliwa badala yake watarasimishwa huku akitoa tahadhari kwa wavamizi wa maeneo na viwanja kuwa lazima watavunjiwa.

Naibu Meya wa Manispaa ya Dodoma, Jumanne Ngede alisema baraza la madiwani halina shaka na uteuzi huo na kwamba watapewa ushirikiano katika kusukuma mbele gurudumu la maendeleo ikiwamo mchakato wa makao makuu.

Alisema mpango uliopo katika manispaa hiyo ni kujipanga kuwa na ugeni mkubwa ambao umeingia mkoani hapo ikiwemo maofisa wa serikali.

Mmoja wa madiwani ambaye hakupenda kutajwa jina lake alisema mpango wa uteuzi wa msomi huyo unaweza kuwagawa madiwani kwani kuna kila dalili za kuandaliwa kushika kiti hicho huku wengine wakitaka apewe nafasi katika kamati ya uchumi na fedha tu ili akaonyeshe uzoefu wake huko.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Siku Moja Tu watu wang’oa Bango la Mtaa wa Victor Wanyama.

Unaweza usiamini, jana tu ilitolewa zawadi ya mtaa, asubuhi ya leo tayari bango la Mtaa wa Victorr Wanyama limeng’olewa.

Taarifa zinaeleza wako ambao walitaka kuiba bango hilo kwa ajili ya vyuma chakavu lakini wengine wanaeleza, wako waliochukizwa Wanyama kupewa jina la mtaa Tanzania.

Jana, Meya wa Manispaa ya Ubongo Boniface Jacob, alimtunuku mtaa, Kiungo wa Tottenham ya England Victor Wanyama raia wa Kenya.

Jacob ambaye ni Meya akitokea Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), alimkabidhi Wanyama mtaa ambao awali ulikuwa unajulikana kama Viwandani na sasa utajulikana kama Victor Wanyama.

Mtaa huo uko Ubungo katika Wilaya ya Kinondoni mkoani Dar es Salaam.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Saida Karoli: ‘Urugambo’ inanikumbusha mpenzi wangu.

Mwanamuziki mkongwe wa nyimbo za asili, Saida Kalori, ambaye kwasasa anatamba na wimbo wake mpya ‘Urugambo’ ametoa ya moyoni kuwa wimbo huo unamkumbusha mpenzi wake wa zamani.

Saida anasema umaarufu wa wimbo huo umemsababishia kero kwa midume wakware ambao kila kukicha wanampigia simu.

Hata hivyo Saida amesema hataki kuwasikia kwani amechoshwa na tabia za wanaume wanaomfuata kwa malengo yao kisha humtema mara wanapofanikiwa malengo yao.

Alisema ni bora amtafute mpenzi wake wa zamani ambaye kila anapomfikiria anaumia kutokana na mapenzi mazito aliyonayo kwake.

Saida alianza kuwa maarufu miaka ya mwanzao ya 2000, baada wimbo wake ‘Salome’ kuwa maarufu ndani na nje ya nchi.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

HII Hapa Historia Fupi ya Freemasons Itakayokuacha Mdomo Wazi.

Ni shirika ambalo mambo yake ni siri kuu. Mimi nilifanya utafiki kwenye mitandao, nikafatilia historia yao kama inavyoonyeshwa mara kwa mara kwenye makala za historia katika televisheni za magharibi pamoja na kuongea na watu waliofuatilia kwa karibu mambo yao.
Kwenye maelezo yao kwa nje Free masons wanajitangaza kama shirika zuri tu.

Naomba niorodheshe mambo machache niliyoambiwa kuhusiana na Freemasonry.
1. Ni kweli Freemasonry kama ilivyo maana yake kwanza ilkuwa ni kundi la mafundi waashi (masons) au wajenzi kuwa lugha nyingine. Walikuwa ni wataalamu waliobobea kwenye masuala ya ujenzi wa mahekalu na mabenki ya zama hizo zinazoitwa kwa kizungu (medieval times).

Niliambiwa walikuwa ni watunzaji wa pesa za kanisa katoliki. Kwani walikuwa wanajenga mahekalu(cathedrals) za wakatoliki na mabenki/ mahandaki ya kuhifadhia pesa pamoja na kuzikia(catacombs).

Niliambiwa wanaweza kujenga hayo maandaki kwa utaalamu mkubwa kiasi kwamba ukiingia ndani ya hayo mahandaki bila ramani unaweza ukashindwa kutoka hata unaweza kupotelea humo humo ndani usiweze kutoka tena. Hicho ndicho kilichokuwa ni kiwango cha utaalamu wao.

2. Kwa kuwa walikuwa ni waashi ndiyo maana alama zao ni vifaa vya ujenzi, Pima maji n.k

3. Inasemekana mji mkuu wa marekani (Washington DC) ulisanifiwa na kujengwa na Freemasons. Na inasemekana ni mji makini ambao umejengwa ukizingatia pembe tatu zenye nyuzi zinazowakilisha u freemason.

4. Ikatokea kipindi ambapo hawa freemasons wakaasi kwa kuanza kujishirikisha na mambo ya nguvu za giza. Wengine wanasema walianza kuiba pesa za kanisa katoliki, lakini ukweli halisi haujulikani. Kutokana na sababu hizi na zinginezo ambazo ni siri kati ya kanisa katoliki na freemasons, Freemasons wakafukuzwa kutoka ukatoliki.

Ndio maana hakuna maelewano kati ya freemasons na wakatoliki. Wakatoliki wakaanzisha shirika jingine badala ya hao freemasons lijulikanalo kama Jesuits.

Jesuit Fathers ni mapadri wa katoliki wa daraja la juu sana wenye elimu ya juu zaidi ambao hufanya kazi za siri za utawala na udhibiti ndani ya kanisa katoliki.

5. Kuhusu imani yao (freemasons) nikaelezwa kwa kifupi kuwa wanaamini Yesu na Lucifer ni mtu na ndugu yake. wanaamini kuwa Lucifer ndiye mwema na mzuri lakini wanaamini kuwa Yesu ndiye mwenye mabaya. alimfanyia hila Lucifer aonekane mbaya.

6. Kinachoendelea ndani yake kuhusiana na ibada zake ni siri kwani kuna daraja ambazo muumini wa freemason anapanda kutokana na kubobea katika imani ikiwa ni pamoja na kutunza siri zao. Ninajua kuwa daraja ya juu kabisa ni nyuzi ya 33 (33rd degree)

7. Ni watu wenye nguvu mno na mambo yao ni makubwa mno na siri zao ni nzito mno. Ndiyo maana haziko wazi.

Wafuasi wa kiwango cha chini wala hawajui shirika hili linahusika na nini manake hata wao hawaambiwi kitu. Kwa wafuasi wa daraja ya chini wanakwenda ku socialize tu. Yaani kwa wasio jua kitu kule kwenye lodge zao ni kama ywca au wmca au club hivi. Kwenye nchi kama marekani watu wasio jua siri wanachukulia kama sehemu za kusocialize tu.

8. Freemasonry inawekwa pamoja na makundi mengine makubwa ya siri, yanayoendesha ulimwengu mzima kwa nguvu za kiuchumi, siasa na mambo ya utawala.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Picha: Jux ahitimu Chuo, China.

Msanii wa Bongo Fleva, Jux ameachia picha mtandaoni zikimuonyesha akiwa katika mafahali kitu ambacho kinaashiria kuwa amehitumu Chuo.
Muimbaji huyo wa RnB kwa kipindi kirefu amekuwa akidai anasoma nchini China lakini watu walikuwa wakihoji kwa nini hajapost hata picha akiwa Chuo. Sasa leo hii Jux amevunja ukimya huo kwa kuachia hizi picha tano na kuandika maneno mawili tu, ‘Finally done’.
Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Download wimbo mpya wa Chidi Benz ft Q Chilla unaoitwa "MUDA".

https://my.notjustok.com/track/download/id/235469


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Shangazi Yangu Ananisaga Kila Mara, Nifanyeje?.

Mimi naitwa NASRA na nina mika 24, hilo nalileta kwenu jambo lango wana-Udakuz naomba mnisaidie ushauri ili niwe kutatua tazizo hili linalonikabili hapa chini:

Baada ya mama yangu kufariki 2001 kuna shangazi yangu (ambaye ni mke wa mjomba wangu) alinichukua kwa minajil ya kunilea na kunisomesha ila amekuwa AKINISAGA tokea niko mdogo mpaka sasa! ambapo nikiwa mdogo wakati nimelala nilikuwa nashtuka yupo juu yangu na mimi nipo UCHI huku ananinyonya MATITI na sehemu nyingine za mwili na baadae alikuwa anapanda juu yangu na kunilalia huku akifanya vitu fulani mpaka ananimwagia vitu fulani katika sehemu zangu za siri na kuniambia ninyamaze nisimwambie mjomba "eti atanipa pesa ya kutumia shule na kunipeleka na gari, alipokuwa akimaliza baadae alikuwa akiniogesha na kuninunulia vitu VITAMUTAMU. Nilinyamaza maana sikujua jambo lile ila aliendelea kila mara mchezo wake huo.

Mpaka sasa Nimekuwa Lakini anaendelea mchezo huo na mimi nimeshajua na sometimes nasikia raha ila roho yangu haitaki kabisa mchezo huo , huwa naumia sana ...nataka niwe msichana wa kawaida ni date na wavulana na nisikie raha napokuwa na mvulana.....naombeni ushauri...

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Maneno ya Spika Ndugai baada ya wabunge kususia futari aliyoandaa.

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzani, Job Ndugai amewakumbusha wabunge wa vyama vya upinzani hasa vinavyounda UKAWA umuhimu wa jamii kukaa pamoja, kujadiliana na kumaliza tofauti zao.

Ndugai ambaye ni mmoja wa wabunge wa Bunge la 11 aliyasema hayo baada ya baadhi ya wabunge hasa wa upinzani kususia futari aliyoiandaa siku ya Jumanne kwa ajili ya wabunge wote. Kiongozi huyo wa juu wa mhimili huo alisema kuwa licha ya jukumu zito la kujadili na kupitish bajeti ya serikali ya 2017/2018, ushirikiano kwa jamii ni muhimu.

Jambo hilo lilmfanya asiwe na raha na kuamua kuzungumzia ndani ya bunge kwa upole kabisa ambapo alisema kuwa, baada ya kuhudhuria futari iliyoandaliwa na Waziri Mkuu Jumatatu, na baada ya kuwepo tetesi za kususia ya kwake alisema, amejifunza kuwa baadhi wamekatazana kuhudhuria shughuli kama hizo.

“Lakini nikajifunza kitu kimoja ambacho sikupenda kukisema, ila nikiseme hapa kidogo. Kuna wenzetu wamekatazana rasmi kuhudhuria shughuli kama hizi.”

Ndugai aliyasema hayo Jumanne wakati akihitimisha kipindi cha maswali na majibu kabla ya kupisha mapumziko na kisha kupigiwa kura kwa bajeti ya serikali.

"Bunge linaendeshwa kwa mawasiliano ya namna mbalimbali baina ya wabunge na uongozi.  Endapo kuna jambo linakwaza na kusababisha watu wasipate futari pamoja,  ni vizuri wakae pamoja na kuondoa jambo hilo," alizungumza Ndugai.

Licha ya kutoa tahadhari hiyo, Ndugai alisema kuwa wabunge hao wana uhuru wa kufanya hivyo (kutohudhuria) kama wanaona ni sawasawa.

“Siyo mwezi wa chuki na kubaguana. Niwakaribishe tena kwenye futari kwa watakaoweza kufika. Watakaoshindwa In Sha Allah, kila la heri. Tutaendelea kuwa pamoja mjengo huu huu,” alisema Spika Ndugai akihitimisha nasaha zake.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Lori lalipuka na kuteketeza watu 123, Pakistan.

Takribani watu 123 wamekufa kwa kuteketea kwa moto baada ya Lori lililokuwa limebeba mafuta kupata ajali na kulipuka nchini Pakistan.

Taarifa iliyotolewa na Serikali nchini humo imeeleza kuwa ajali hiyo imetokea katika mji wa Ahmedpur Sharqia katika jimbo la Punjap ambapo watu wengine kadhaa wameteketea vibaya, pale walipokuwa wakijaribu kuteka mafuta kutoka katika lori hilo la mafuta.

Waliojeruhiwa wanatibiwa hospitali huku kikosi cha zima moto kipo katika eneo la ajali kikikabiliana na moto huo.

Lori hilo la mafuta limedaiwa kuwa lilikuwa likiendeshwa kwa kasi hali iliyosababisha kuanguka na kisha kushika moto, huku mashuhuda wakieleza kuwa, baadhi ya watu waliofika katika eneo la ajali walikuwa wakivuta sigara, jambo ambalo linakisiwa kuwa chanzo cha moto huo.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

VIDEO: Diamond Kaongea Baada ya Rayvanny Kushindi Tuzo ya BET.

Ni Mwimbaji staa wa Bongo Fleva, makofi mengi amepigiwa kwenye utunzi wake pamoja na ukali wake wa melody, anaitwa Rayvanny kutoka WCB ambae June 24, 2017 ameshinda tuzo ya BET kipengele cha Viewers Choice Best New International Act Artist, Sasa leo June 25, 2017 Ayo TV na Millardayo.com imempata Diamond Platnumz kuzungumzia ushindi wa Rayvanny.

Itazame hii video hapa:


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Cristiano Ronaldo Hakamatiki..Haya Ndio Maajabu Mengine Aliyofanyia Nchi yake.

Cristiano Ronaldo akishangilia kibabe baada ya kuifungia Ureno bao la kwanza kwa penalti dakika ya 33 katika ushindi wa 4-0 dhidi ya New Zealand baada ya Danilo kuchewa rafu usiku wa Jumamosi Uwanja wa Krestovskyi mjini St Petersburg katika mchezo wa Kundi A Kombe la Mabara. Mabao mengine ya Ureno yalifungwa na Bernardo Silva dakika ya 37,  Andre Silva dakika ya 80 na Luis Nani dakika ya 90 na ushei. Matokeo hayo yanaifanya Ureno ifikishe pointi saba na kumalizana kileleni sawa na Mexico iliyomaliza na pointi saba pia baada ya kuifunga Urusi 2-1 na zote zinakwenda Nusu Fainali. Wenyeji Urusi wameungana na New Zealand kupanda jukwaani kitazama mechi za kumalizia michuano ya 2017

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Download wimbo mpya wa Nay Wa Mitego unaoitwa "Moto".

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Saturday, 24 June 2017

SOMA Nafasi za Ajira 535 Zilizotangazwa Leo Serikalini.

Bonyeza Links Zifuatazo Hapa chini:

535 Government Job Opportunities

Job Opportunity at Access Bank Tanzania

Nafasi zingine ingia www.ajirayako.com


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

SIMBA Waendelea Kuivunja Yanga Vipande Vipande...Sasa Wahamia Kwa Donald Ngoma.

SIMBA imeanza mazungumzo na straika wa Yanga, Donald Ngoma ambaye ameomba dola 80,000 sawa na Sh milioni 180 ili asaini mkataba wa kuichezea timu yao msimu ujao.

Kama Simba itafanikiwa katika dili hili la Ngoma raia wa Zimbabwe, itakuwa inamsajili mchezaji wa pili kutoka Yanga msimu huu kwani tayari inaye kiungo Haruna Niyonzima. Simba imenasa saini ya Niyonzima kwa dau la dola 60,000 (Sh milioni 132) na mshahara wa dola 3,000 sawa na Sh milioni 6.6.

Bosi mmoja wa Kamati ya Usajili ya Simba, ameliambia Championi Jumamosi kuwa, tayari wamemfuata Ngoma na amewaambia wazi kuwa wampe dola 80,000 ili asaini mkataba wao wa miaka miwili.

“Tunafanya usajili kwa ajili ya Kombe la Shirikisho Afrika na Ligi Kuu Bara msimu ujao, tunataka tufike mbali kwenye mechi za Caf (Shirikisho la Soka Afrika) pia tunataka ubingwa wa ligi yetu.

“Sasa ili tuwe na timu bora ni lazima tusajili vizuri, sasa tumemalizana na Niyonzima, tunaelekeza nguvu zetu kwa Ngoma tunayemuhitaji kwa ajili ya kuongeza nguvu.

“Ngoma anataka dola 80,000 ili asaini mkataba wetu, lakini sisi tutamuomba apunguze ili tukiafikiana tumpe hiyo fedha awe mchezaji wetu,” alisema bosi huyo kijana.

Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe hivi karibuni alililiambia gazeti hili kwamba, Niyonzima na Ngoma ni kati ya wachezaji anaowakubali na wana uwezo wa kuichezea timu yake.

Siku chache baada ya kauli hiyo ya Hans Poppe, kweli Simba ikamalizana na Niyonzima na sasa imeelekeza nguvu kwa Ngoma, straika anayesifika kwa ufungaji huku akimudu kutumia nguvu na akili uwanjani.

Imeelezwa kuwa, Simba imepata jeuri ya fedha iliyowawezesha kumbakisha kikosini nahodha Jonas Mkude baada ya mfanyabiashara Mohammed Dewji ‘Mo’ kutoa mkwanja mrefu.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

UJUMBE wa Kuua Polisi zaidi Waazidisha Hofu Kibiti.

Siku mbili tangu kuuawa kwa polisi wawili wa Kikosi cha Usalama Barabarani ambao walikuwa kazini katika Kijiji cha Bungu B, hali ya wasiwasi imezidi baada ya wauaji hao kusambaza ujumbe unaoeleza kuwa wanaendelea kusaka askari kwa kuwa ni wadhurumaji.

Watu hao wametuma ujumbe mfupi uliondikwa kwenye karatasi na kisha kuutuma katika mitandao ya kijamii, ukidai kuwa waliouawa (japo hawajatajwa majina yao) walidhulumu watu kwa kutumia kazi zao.

“Tunawatangazia wananchi tumewaua hawa kwa sababu wanadhulumu watu kwa kutumia kazi zao na yeyote atakayefanya kazi hapa au nje ya hapa tutamtafuta hata nyumbani kwake. Sisi tumejitolea kufa kuliko kuishi, kwa hiyo dereva au raia popote uwaonapo toa taarifa iwe nyumbani au kazini,” unasema ujumbe huo.

“Hakuna njia ya kumaliza dhuluma isipokuwa chuma tu, hapa chuma tuuu!”

Ujumbe huo ambao umeandikwa kwa mkono kwa kutumia kalamu ya rangi ya bluu unadaiwa kuwa unazungumzia vifo vya askari polisi wawili wa Kituo cha Polisi Kibiti, Sajent Salum na PC Masola waliouawa kwa kupigwa risasi wakiwa kazini.

Mmoja wa madiwani katika Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti (jina tunalo) alisema ujumbe huo unawalenga askari wa kawaida na wa Kikosi cha Usalama Barabarani.

Diwani huyo alisema kundi hilo linalofanya mauaji katika wilaya za Kibiti na Rufiji bado lipo na lina nguvu.

“Linaonyesha bado lina uwezo mkubwa wa kufanya mauaji na kutokomea kusikojulikana,” alisema.

Alisema kwa sasa Serikali inapaswa kuongeza nguvu zaidi ya wapelelezi ili kukomesha kikundi hicho ambacho hakijajulikana kinafanya hivyo kwa sababu zipi na wala kinakojificha.

Akizungumzia ujumbe huo, kamanda wa polisi wa Pwani, Onesmo Lyanga alisema Jeshi la Polisi litaendelea kuwasaka.

“Tutapambana nao tu,” alisema Kamanda Lyanga na kukata simu.

Mkuu w Jeshi la Polisi (IGP), Simon Sirro alisema wakati alipozungumza na wazee wa wilaya za Kibiti na Rufiji, kuwa wanaoendesha mauaji hayo watalipwa ubaya kama wao wanavyofanya.

IGP Sirro alisema daima hali ya mtu mtenda maovu ni kulipwa maovu, hivyo wauaji hao watapatikana na malipo yao yatafanyika ndani ya muda mfupi.

“Pelekeni salamu kwa wauaji hao kwamba ubaya huwa hauwi ubaya siku zote,” alisema.

Wilaya tatu za mkoani Pwani; Kibiti, Rufiji na Mkuranga zimekuwa zikikumbwa na mauaji ya viongozi wa vijiji, watendaji na polisi tangu Mei mwaka jana.

Hali ilionekana kuwa mbaya baada ya watu hao wasiojulikana kulishambulia kwa risasi gari la doria la Jeshi la Polisi na kuua askari tisa waliokuwa wakirejea kutoka zamu.

Askari wengine ambao ni maofisa, waliuawa katika mazingira tofauti; mmoja, Peter Kuponezya aliuawa wakati alipofika eneo ambalo watu hao waliteka kituo cha Idara ya Maliasili na kuagiza wananchi wachukue mali zilizokuwa zimekamatwa na wafanyakazi wa idara hiyo ambao pia baadaye waliuawa, na mwingine, Peter Kubezya aliuawa wakati kikosi cha polisi kilipokwenda kujaribu kukamata watuhumiwa wa uhalifu kwenye nyumba yao iliyo Vikindu.

Viongozi wa vijiji na watendaji wamekuwa wakiuawa kwa kushambulia kwa risasi baada ya kufuatwa na wauaji majumbani kwao nyakati za usiku au mashambani.

Wizara ya Mambo ya Ndani imependekeza kuundwa kwa kanda maalumu itakayoshughulikia wilaya hizo kujaribu kukabiliana na mauaji hayo.



Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

LEMA na Meya wa Arusha Wafunguka 'Tumechoshwa na Udhalimu na Uonevu Unaofanywa na DOLA Kwa Maagizo ya Viongozi" .

MBUNGE wa Arusha Mjini, Godbless Lema, Meya wa Jiji Kalist Lazaro na naibu wake, Viola Likindikoki, wamesema wamechoshwa na kile walichokiita udhalimu na uovu wanaofanyiwa na vyombo vya dola kwa maagizo ya viongozi mkoani hapa.

Kutokana na kufanyiwa vitendo hivyo, wamesema wameamua kwenda kuwashtaki viongozi hao kwa Rais John Magufuli.

Walisema hayo katika tamko la pamoja jijini hapa jana ikiwa siku mmoja tu baada ya polisi kumkamata na kumshikilia Naibu Meya Viola kwa tuhuma za kurekodi na kutoa nje siri za vikao vya kamati na vya Baraza la Madiwani.

Meya Lazaro alisema: “Nalaani kwa nguvu zote udhalilishaji dhidi ya viongozi wa upinzani kwa kisingizio cha amri tunazoambiwa zinatoka juu.
“Yaani viongozi wa serikali wanashindana kufanya uovu kwa kunyanyasa wapinzani.”

Alisema kwa mfano, Meya wa Ubungo alikamatwa kwa amri ya aina hiyo ikaonekana Arusha hawajafanya hivyo siku nyingi, ndiyo wakamkamata Naibu Meya. “Sasa tumechoka”.

Kwa upande wake, Lema alisema: “Tunasema tumechoka.” “Sisi ni binadamu, tuna nyama, tuna damu, tuna familia, tuna ndugu na jamaa.”
Alisema anajua hatakubaliwa na kuruhusiwa kuonana na Rais Magufuli ili kumweleza kilio chao cha kuonewa na viongozi hao, hasa vijana aliowateua.

“Tumeamua Mstahiki Meya ambaye ni Katibu wa Chama Mkoa aandike barua na aombe kukutana na Rais kumweleza kilio chetu,” alisema Lema.

Akizungumzia tukio la jana, Meya Lazaro alisema kitendo kilichofanywa na polisi kumkamata naibu wake kwa kosa ambalo kwa mujibu wa kanuni za uendeshaji wa Serikali za Mitaa lilipaswa kushughulikiwa na Kamati ya Maadili ya Baraza la Madiwani ni kulidhalilisha jeshi hilo.

“Polisi na hususani ofisi ya RCO (Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Mkoa) kitengo cha uchunguzi wa makosa ya mtandao hakihusiki na suala analotuhumiwa Naibu Meya kama kweli alitenda kosa hilo.

“Lakini hivi kwa akili ya kawaida Naibu Meya ni kiongozi wa vikao vya Baraza kama Meya hayupo, anasoma makabrasha hata yale yaliyopigwa mihuri ya siri, halafu anawezaje kuvujisha siri,” alihoji na kuongeza, “huku ni kujidhalilisha na kudhalilisha Jeshi la Polisi.”

Alisema kwa kuwa viongozi hawa wamezoea kukurupuka, Naibu Meya amemwandikia barua kumwomba aende akaonane na Rais Magufuli ili awachukulie hatua viongozi hawa ambao wengi historia zao zinafahamika kwa kukosa maadili.

Alidai hali hiyo inatokana na Baraza la Madiwani kuziba mianya yote ya ulaji kama vile kumpa mafuta ya gari Mkuu wa Mkoa na Mkuu wa Wilaya.

“Huko nyuma Halmashauri ya Jiji la Arusha lilikuwa shamba la bibi. Leo tumefanikiwa kupata hati safi, tumefanya vizuri kwenye sekta zote,” alisema.

Akizungumzia sababu za kukamatwa na kushikiliwa katika kituo kikuu cha polisi Arusha, Viola alisema pamoja na kushikiliwa kwa muda mrefu hakukuwa na mlalamikaji hadi polisi ilipompigia simu Mkurugenzi wa Jiji la Arusha, Athumani Kihamia, ambaye alitoa maelezo kama mlalamikaji.

“Hawa polisi na wale waliowatuma wamefanya mchezo wa aibu. Yaani mimi niko chini ya ulinzi wa polisi nawauliza kosa langu wanadai nimetoa siri za vikao. Nikauliza mlalamikaji ni nani na wao hawajui wanasema ni amri kutoka juu. Hii ni kweli?” alisema.

Aidha alisema atalishtaki mahakamani Jeshi la Polisi kwa kupoteza baadhi ya vitu vyake ikiwamo simu ya mkononi wakati wakitekeleza amri ya kumkamata.

“Tunajua hofu ya wakubwa hawa ni kwa sababu ya maovu waliyofanya, sasa tunawaambia vitisho vyao hatuviogopi na ni vya kawaida,” alisema.

Naibu Meya alikamatwa na kushikiliwa kwa muda pamoja na madiwani wawili wa viti maalumu, Sabina Peter na Happyness Chale kwa tuhuma za kutoa siri za vikao vya baraza la madiwani wa Jiji la Arusha.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

KIMENUKA..Shirika la Wanawake Barani Afrika Limemtaka Rais Magufuli Kuomba Msamaha.

Matamshi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli kuhusu wanafunzi wanaopata ujauzito kutoendelea na masomo yamezua gumzo kubwa na mijadala mbalimbali ndani na nje ya nchi.


Shirika la wanawake barani Afrika limemtaka Rais Magufuli kuomba msamaha kutokana na matamshi yake aliyoyatoa akiwa katika ziara ya kikazi Mkoani Pwani kuwa mwanafunzi atakayepata ujauzito katika utawala wake hataweza kuendelea na masomo.


Hata hivyo, katika sheria iliyopitishwa mwaka 2002 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuhusu suala la mtoto wa kike kupata ujauzito akiwa shule inaruhusu kufukuzwa shule na kifungo cha miaka 30 kwa yule aliyesababisha ujauzito huo.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Vigezo vya kupewa kitambulisho cha Uraia.

Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi imewatangazia wananchi wote wakazi wa Dar es salaam kuwa watapatiwa ofa maalum ya vitambulisho vya uraia siku ya maonyesho ya sababa ya 41 yanayotarajiwa kufanyikia katika viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini DSM.

Aidha,taarifa hiyo imeeleza kwamba usajili huo utafanyikia kwenye banda la NIDA kuanzia tarehe 28 Juni hadi Julai 10 mwaka huu.
 
==>Taarifa ya NIDA

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa