Tuesday, 13 December 2016

Haya Ndiyo Maamuzi Ya Halmashauri Kuu Ya Taifa Ya CCM Baada Ya Kikao Chake Cha Siku Moja.Fahamu zaidi hapa.

Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM imekutana leo tarehe 13/12/2016 jijini Dar es salaam kwa kikao cha siku moja cha kawaida. Kikao hicho kimeongozwa na Mwenyekiti wa Taifa wa CCM Dkt. John Pombe Magufuli.

Pamoja na mambo mengine, Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM imepokea taarifa ya Tathimini ya Uchaguzi mkuu wa mwaka 2015, baada ya kuitafakari taarifa hiyo, Halmashauri Kuu imeamua yafuatayo;-

1. Kupunguza idadi ya wajumbe wa vikao na idadi ya vikao vya Chama katika ngazi mbalimbali ili kuongeza ufanisi wa utendaji wa Chama na kuongeza muda wa viongozi wa Chama kufanya kazi za Chama kwa Umma badala ya kutumia muda mwingi vikaoni.

Ili kuwa  na vikao vya Chama vyenye tija imeamuliwa kama ifuatavyo:-

a). Halmashauri Kuu ya Taifa kwa sasa ina jumla ya wajumbe 388 idadi ambayo ni kubwa sana, hivyo imeamuliwa idadi hii ipunguzwe na kuwa wajumbe 158 kama  ifuatavyo:-

Wenyeviti wa Mikoa
Mikoa ya Bara           26x1    =      26
Mikoa ya Zanzibar      6x1   =          6

Wajumbe wa NEC wa Mikoa
 Mikoa ya Bara    26x1         =        26
 Mikoa ya Zanzibar   6x4         =        24
Wajumbe wa NEC wa Taifa
 Kutoka  Bara    =               15
 Kutoka  Zanzibar     =               15

Nafasi za Mwenyekiti   =                7

Wajumbe wa NEC wa Jumuiya
        UVCCM     =        5
        UWT   =        5
        WAZAZI    =        5
Wajumbe wa NEC kutoka Bungeni     =        5

Katibu wa Kamati ya Wabunge wa CCM      =       1

Wajumbe wa  NEC kutoka BLW   =       3

Katibu wa Kamati ya Wawakilishi =       1

Wajumbe wa NEC – wanaotokana na Nyadhifa zao
- Mwenyekiti wa CCM                  =       1
- Makamu Mwenyekiti (B)         =       1
-Makamu Mwenyekiti (Z)           =       1
- Makamu wa Rais                        =       1
-  Waziri Mkuu                               =       1
- Makamu wa Pili wa Rais (Z)   =       1
- Spika wa Bunge                          =       1
- Spika  wa  BLW                           =       1
- Mwenyekiti wa UWT                =       1
- Mwenyekiti wa WAZAZI          =       1
-Mwenyekiti wa UVCCM             =       1
- Katibu Mkuu – WAZAZI            =       1
- Katibu Mkuu – UWT                   =       1
- Katibu Mkuu – UVCCM              =       1
                                              Jumla:      158
#. Vikao vya kawaida vya Halmashauri Kuu ya Taifa vifanyike kila baada ya miezi sita badala ya miezi minne kama ilivyo sasa isipokuwa vinaweza kufanyika vikao maalum inapohitajika.

b). Kwa upande wa sasa imeamuliwa wajumbe wa Kamati Kuu wawe 24 badala ya 34 kama ifuatavyo:-

Mwenyekiti wa CCM.
Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara)
Makamu Mwenyekiti wa CCM        (Zanzibar)
Makamu wa  Rais
Katibu Mkuu wa CCM
Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Bara)
Naibu Katibu Mkuu wa CCM  (Zanzibar)
Waziri Mkuu
Makamu wa Pili wa Rais (Z)
Spika wa Bunge la Tanzania
Spika  wa BWL
Mwenyekiti  wa WAZAZI
Mwenyekiti  wa UWT
Mwenyekiti  wa UVCCM
Katibu wa   wa Halmashauri Kuu ya Taifa wa  Organaizesheni
Katibu wa   wa Halmashauri Kuu ya Taifa wa  Itikadi na Uenezi
Katibu wa   wa Halmashauri Kuu ya Taifa wa  Uchumi na Fedha
Katibu wa   wa Halmashauri Kuu ya Taifa wa  Mambo ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa
Wajumbe  watatu (3)  wa kuchaguliwa  na Halmashauri Kuu kutoka Tanzania

Wajumbe watatu  (3) wa kuchaguliwa  na Halmashauri Kuu kutoka Zanzibar.

#. Vikao vya kawaida vya Kamati Kuu vipunguzwe ili vifanyike kila baada  ya miezi minne badala ya miezi miwili isipokuwa vinaweza kufanyika vikao maalum inapohitajika.

c). Kwa ngazi ya mkoa, Wajumbe wa Kamati za Siasa za Mikoa wapunguzwe kwa kuondoa wajumbe  watatu ambao ni:-
Katibu wa Uchumi na Fedha wa Mkoa         -       1
Wajumbe wa kuchaguliwa na H/Mkoa        -       2

#. Vikao  vya kawaida vya Kamati ya Siasa ya Mkoa vifanyike kila baada ya miezi mitatu badala ya kila  mwezi kama ilivyo sasa isipokuwa vinaweza kufanyika vikao maalum inapohitajika.

d). Kwa upande wa Wilaya Wajumbe wa Kamati ya Siasa ya Wilaya wapunguzwe kwa kuwoandoa:-
 Katibu wa Uchumi na Fedha wa Wilaya    -       1
 Katibu wa Kamati ya Madiwani                   -       1
 Wajumbe wa kuchaguliwa na H/Kuu ya (W)-  2
  Jumla:  4

#.Vikao  vya kawaida  vya Kamati ya Siasa ya Wilaya  vifanyike kila baada ya miezi mitatu badala ya kila  mwezi isipokuwa vinaweza kufanyika vikao maalum inapohitajika.

#. Muundo wa Wilaya za Chama uendane na muundo wa sasa wa Serikali.

Kata,Tawi na Shina
Idadi ya kuanzisha Shina iwe wanachama 50  hadi 300.

Idadi ya kuanzisha Tawi iwe wanachama kuanzia 301 hadi 1,000.
Hata hivyo idadi hii izingatie eneo la kijiografia na wingi wa wanachama katika eneo hilo.

Vikao vya kawaida vya  Kamati za Siasa  za  ngazi hizi viwe vinafanyika mara moja kila baada ya miezi mitatu, isipokuwa vinaweza kufanyika vikao maalum inapohitajika.

#. Nafasi za Uongozi
Mwanachama anatakiwa kuwa na nafasi  moja tu ya uongozi wa kazi za muda wote kama ilivyoainishwa kwenye Kanuni za uchaguzi wa Chama Toleo la 2012 kifungu cha 22 na 23 ambazo zimetajwa kuwa ni:-
Mwenyekiti wa Tawi,Kijiji au Mitaa.
Mwenyekiti wa Kata/Wadi.
Mwenyekiti wa Jimbo, Wilaya na Mkoa.
Makatibu wa Halmashauri Kuu wa ngazi zote zinazohusika.
Mbunge, Mwakilishi na Diwani.

#. Viongozi wa kuchaguliwa waepuke kuwa watendaji badala yake waongoze na kusimamia shughuli za Chama kwa kuzingatia Katiba na Kanuni.

#.Vyeo ambavyo haviko kwenye Katiba
Vyeo  ambavyo havijatamkwa kwenye Katiba ya CCM haviruhusiwi katika Chama au Jumuiya zake mfano Umoja wa makundi mbalimbali kama Wenyeviti wa ngazi mbalimbali (mfano: Mwenyekiti wa Wenyeviti wa CCM n.k), Makamanda (UVCCM), Washauri (UWT) na Walezi (WAZAZI) katika ngazi zote.

#. Uhakiki wa Wanachama wa CCM
Halmashauri Kuu imeona ipo haja ya kufanya uhakiki wa wanachama wa CCM  na Jumuiya zake ili kujua idadi sahihi ya wanachama wetu kwa wakati huu.   Uhakiki huu uendane na kutoa kadi mpya za uanachama za kielektroniki ili kuwa na udhibiti wa usahihi wa wanachama na kuondoa wanachama HEWA. Aidha, Kadi za UWT, WAZAZI na UVCCM zifutwe ili tubaki na kadi za CCM tu.

#. Jumuiya za Chama Cha Mapinduzi
Jumuiya za CCM  zimetakiwa kufanya kazi zake kwa kuzingatia matakwa ya Katiba ya CCM na Kanuni za Jumuiya husika, kanuni za Jumuiya ziendane na  matakwa ya Katiba ya CCM.

#.Uaendeshaji  wa shughuli zote za Jumuiya za Chama na mali zake uwe chini ya usimamizi wa Chama Cha Mapinduzi. (Baraza la Wadhamini la Chama Cha Mapinduzi).
Makatibu Wakuu wa Jumuiya watakuwa wanateuliwa na Kamati Kuu  na  Manaibu Katibu Wakuu watateuliwa na Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya Taifa.

#. Wakati tukiendelea kubaki  na Bendera yenye rangi ya kijani na njano  na  alama ya jembe na nyundo, Halmashauri Kuu imeona ipo haja ya kuzifanya rangi hizo kuwa na muenekano wa kuvutia zaidi.

#. Utumishi  katika  Chama na Jumuiya zake. Katibu Mkuu wa CCM na Sekretarieti ipewe majukumu ya kusimamia ajira za Watumishi wa Chama na Jumuiya zake.

Nafasi za Makatibu Wasaidizi wa Mikoa na Wilaya zitaondolewa na badala yake kazi zao zitatekelezwa na Makatibu wa Jumuiya  za Chama wa Mikoa na Wilaya kwa utaratibu utakaopangwa.  Utaratibu huu utakipunguzia Chama Cha Mapinduzi gharama na kujenga umoja wa utendaji kazi wa Chama na Jumuiya zake katika Mikoa na Wilaya.

#. Tathimini ya hali ya Kisiasa na  Uchaguzi wa    Zanzibar .
Halmashauri Kuu ya Taifa imeagiza kuundwa kwa Kamati maalum ya kufanya tathimini ya kina kuhusu hali ya kisiasa Zanzibar kwa ujumla na masuala yanayohusu uchaguzi wa Zanzibar 2015.

# Mwenyekiti wa Kamati ya udhibiti na nidhamu ametakiwa akamilishe kazi ya taarifa ya udhibiti kwa wanachama waliokiuka mienendo ya kiuanachama kabla ya kuanza uchaguzi Mkuu wa Chama mwezi Februari 2017, Mikoa na Wilaya ambazo hazijaleta taarifa zao za kiudhibiti ziwe zimefikisha taarifa zao kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Udhibiti na Nidhamu kabla ya tarehe 30/01/2017.

#. Uhakiki wa Mali za Chama uendelee kufanyika kwa kina na uchambuzi zaidi ukikamilika Taarifa yake iwasilishwe kwa Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya Taifa mapema iwezekanavyo.

#. Maamuzi na mapendekezo haya yatapelekea kufanyika kwa mabadiliko ya Katiba ya Chama na Kanuni za Jumuiya  za Chama.

#. Kwa mambo yale ambayo yatahitaji mabadiliko ya Katiba, Mkutano Mkuu utaandaliwa mapema mwakani na kutafakari na kupitisha mabadiliko hayo ya Katiba.

Mwenyekiti wa CCM Dkt. John Pombe Joseph Magufuli ameteua wafuatao kujaza nafasi mbalimbali ndani ya sekretarieti ambazo zimekuwa wazi kutokana na waliokuwa wakizishikilia kupewa majukumu mengine ya kiserikali.

#.Ndg. Rodrick Mpogolo anakuwa Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara kuchukua nafasi iliyoachwa wazi na Ndg. Rajabu Luhwavi ambaye ameteuliwa kuwa balozi.
#. Col. Ngemela Eslom Lubinga- Kuwa Katibu NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa kujaza nafasi iliyoachwa wazi na Dr. Asha-Rose Migiro aliyeteuliwa kuwa Balozi
#. Humphrey Polepole kuwa Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi kujaza nafasi iliyoachwa wazi na Ndg. Nape Nnauye aliyeteuliwa kuwa Waziri.
#. Wajumbe wengine watabaki kama walivyo sasa.

Imetolewa na:-

NAPE NNAUYE
IDARA YA ITIKADI NA UENEZI
13/12/2016





Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi


Bonyeza Hapa CLICK HERE

 

MZEE wa Upako 'Kila mwandishi Aliyeniandika Vibaya ikifika Mwezi wa Tatu Akiwa Hai, Mimi Naacha Kuhubiri Naenda Kuuza Gongo'.Fahamu zaidi hapa.

Mchungaji wa Kanisa la Maombezi (GRC), Anthony Lusekelo, maarufu Mzee wa Upako amesema waandishi wote wanaoandika habari za kumchafua watakufa kabla ya kufika Machi mwakani.
mzee-wa-upako3

Kauli hiyo aliitoa jana ikiwa ni mwendelezo wa mahubiri yake ya nne katika wiki ya tatu mfululizo, akijibu yaliyoandikwa kwenye vyombo vya habari kuhusu kumfanyia fujo jirani yake na kulewa.

“Kila mwandishi aliyeniandika vibaya ikifika mwezi wa tatu akiwa hai, mimi naacha kuhubiri, nafunga virago nakwenda kuuza gongo, sasa Mungu ndiye ataamua kwamba ama niache kuhubiri mimi au wewe ufe …najua hata leo mpo humu mmekuja na mnasikiliza tu,” alisema.

Source: Mwananchi




Download  Application ya Hebron Male Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi


Bonyeza Hapa CLICK HERE

 

Monday, 12 December 2016

Ripoti ya Mtazamo wa Hali ya Haki za Kiraia na Kisiasa Tanzania.........LHRC Wametaja Mikoa 8 hatari kwa kukiuka haki za binadamu.Fahamu zaidi hapa.

Kituo cha Sheria na Haki za BInadamu (LHRC) kimetoa Ripoti ya Mtazamo wa Hali ya Kisiasa Tanzania kwa mwaka 2016 ambayo miongoni mwa mambo mengi yaliyoonyeshwa katika ripo hiyo ni pamoja na mikoa iliyokumbwa na matukio mengi ya ukiukwaji wa haki za binadamu.
 
Hapa chini ni orodha ya mikoa yenye hatari kwa wakazi wake kutokana na kukiuka haki za binadamu.

Simiyu na Kaskazini Unguja:

Mikoa hii miwili kwa mwaka 2016 imekumbwa na changamoto kubwa katika uhuru wa kujieleza, uhuru wa kukusanyika na haki ya kupiga kura. Lakini kwa upande mwingine mikoa hii imepata alama za juu zaidi katika matokeo ya mtazamo kuhusu haki za kiraia na kisiasa, hasa kwa upande wa haki ya kuishi.

Songwe, Tabora na Shinyanga:

Mikoa hii ilipata alama za chini zaidi ukilinganisha na mikoa mingine yote. Mikoa yote ilikuwa na alama za chini sana kwenye uhuru ya Kukusanyika na haki ya kuishi-mauaji na ukatili mikononi mwa vyombo vya dola. Kama serikali za mikoa zitaendelea kuminya uhuru wa kukusanyika, kushughulikia mauaji yanayotokana na imani za kishirikina na matukio ya kujichukulia sheria mikononi, basi itakua ngumu kupata mwenendo chanya katika mikoa hii.

Morogoro, Arusha na Manyara:

Katika mikoa hii kuna ongezeko kubwa la migogoro ya ardhi ambayo inaweza kupelekea watu kujichukulia sheria mkononi au mauaji yanayofanywa na vyombo vya dola. Migogoro hii hasa husababishwa na mvutano kati ya wakulima na wafugaji ambapo mara nyingi hupelekea vifo vya raia.
Mbali na mokoa hayo, kituo cha haki za binadamu pia kilitaja haki za raia zilizoongozwa kukiukwa kwa mwaka 2016 ambazo ni pamoja na;

Haki ya Kuishi-Kujichukulia Sheria Mkononi:

Mikoa ya Dar es Salaam na Morogoro, ambayo kwa sehemu kubwa ni mijini, iliongoza kwa kiasi kikubwa kwenye ukiukwaji wa haki hii. Kuna haja ya polisi na viongozi kurudisha imani ya wananchi juu yao ili kupunguza matuko ya kujichukulia sheria mkononi.

Uhuru wa Kutoa Maoni:

Athari ya Sheria ya Huduma za Vyombo vya Habari zitakuwa ni za muhimu sana kufanyiwa uchambuzi kwa mwaka 2017 hasa kwa kuwa uhuru wa vyombo vya habari umeelezwa kuwa miongoni mwa matatizo katika mikoa iliyopata alama za chini. 
Ukizingatia shinikizo ndani nan je ya nchi, itakuwa muhimu kuangalia kama Serikali itayafanyia kazi mapendekezo ya watetezi wa haki za 21 Matukio Makubwa yaliyotokea Mwaka 2016 Mtazamo wa Haki za Kiraia na Kisiasa 2016 Mikoa na Haki za Kuangalia mwaka 2017 Methodologia na Alama binadamu ya kurekebisha vipengele vya sheria hiyo vinavyominya haki.

Uhuru wa Kukusanyika:

Tumeshuhudia zuio la mikutano na mikusanyiko ya kisiasa kwa mwaka 2016, kitendo ambacho kimepelekea mtazamo kwamba uhuru wa kukusanyika imeminywa. Japokuwa Jeshi la Polisi baadae liliondoa zuio hilo, kitendo hicho kiliendelea kuathiri mtazamo kuhusu uhuru wa kukusanyika.

Haki ya Kuishi – Mauaji na Ukatili Mikononi mwa na Vyombo vya Dola:

Matukio ya mauaji yanayofanywa na vyombo vya dola yamechangia kwa kiasi kikubwa kushusha alama za haki katika mikoa mingi. 
Japokuwa kumekuwa na ongezeko la mashtaka ya mauaji yanayofanywa na vyombo vya dola, ikiwemo askari polisi wawili kukutwa na hatia ya mauaji hivi karibuni, kauli na matamko mbalimbali za viongozi wa serikali ambayo yanaweza kuchochea mauaji yanayofanywa na vyombo vya dola yanaweza kuwa chanzo cha mauaji pia.
Unaweza kupakua ripoti nzima hapa chini;
 
 



Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi


Bonyeza Hapa CLICK HERE

 

Wednesday, 7 December 2016

Mzee wa Miaka 75 Aweka Bango la Mke Anayemtaka.Fahamu zaidi hapa.

Katika  hali isiyo ya kawaida mzee mwenye umri wa miaka 75, Athuman Mchambua, mkazi wa Mtoni kwa Azizi Ally jijini Dar es Salaam amezua gumzo mtaani  baada ya kuamua kutafuta mke kwa kuweka bango barabarani.

Katika bango aliloliweka katikati ya barabara Mzee Mchambua alianisha sifa tano za mke anayemtaka pamoja na namba za simu za kuwasiliana naye.

Sifa hizo ni pamoja na awe mshika dini, uvumilivu wa ndoa, uwezo wa kilimo, apendo wa mume, watoto na wajukuu pamoja na usafi wa hali ya juu.
Mzee Mchambua ambaye alizungumza na Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC Swahili) hivi karibuni alisema alifanya uamuzi huo baada ya kufiwa na mke wake aliyezaa naye watoto 11 na kumwacha akiwa hana mtu wa kumsaidia kutunza familia na kufanya shughuli za shambani.

Katika mazungumzo na mwandishi wa BBC, alisema tayari wamejitokeza wanawake wanne waliotaka kuolewa naye lakini hakuna hata mmoja aliyekidhi vigezo alivyoainisha.

Alisema alilazimika kutumia njia ya tangazo kwa sababu anafiri kwa umri alionao hawezi kumpata mke kwa njia ya kawaida.

Alisema endapo njia hiyo itashindikana kumpata mke mwenye sifa anazotaka atalazimika kutumia madalali kumsaidia kumtafuta mke mwenye sifa.

BBC pia ilizungumza na mmoja wa watoto wa Mzee Mchambua, ambaye alisema anaona uamuzi wa baba yake ni sawa kwa sababu ameweka sifa za mwanamke anayemtaka.

Mtoto huyo alisema wapo tayari kumpokea mke mpya wa baba yao na watamheshimu kama mama yao mzazi.




Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi


Bonyeza Hapa CLICK HERE

 

Download wimbo mpya wa Vanessa Mdee unaoitwa "Cash Madame".

Download Vanessa Mdee - Cash Madame.





Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi


Bonyeza Hapa CLICK HERE

 

HASARA 5 za Ushauri wa Rafiki Kimapenzi.Fahamu zaidi hapa.

Watu wengi wamekuwa wepesi sana kukimbilia kwa rafiki zao ili kuomba msaada wa mawazo ya nini wafanye kwenye mapenzi. Imani iliyojengeka kwa watu wengi katika jamii yetu ni kuwa ushauri ni kitu muhimu sana kwa kila hatua.

Kwa mtazamo wa haraka haraka unaweza kuishia kwenye ukomo huo wa fikra na kuamini juu ya ushauri wa mtu kukufikisha mahali sahihi kwenye mapenzi. Unapokerwa na mpenzi unakimbilia kushauriwa na wakati mwingine hata unapotaka kuoa au kuachana na umpendaye, unamuomba rafiki yako ushauri.
Je, umeshawhi kufikiria hasara za kuomba ushauri wa kimapenzi kwa rafiki yako? Hebu ungana nami wiki hii ili nikumegee kidogo hasara za ushauri.

UTAKUPOTOSHA

Ni wazi kwamba kipimo cha uelewa kinatofautiana kutoka kwa mtu mmoja hadi mwingine. Ifahamike kuwa, uhodari wa mambo nao hutofautiana, mtu anaweza kuwa mahiri katika siasa na akaaminika kwenye jamii, lakini ukimpelekea suala la mapenzi anakuwa hajui kitu, hivyo ni rahisi kukupotosha.

Uchunguzi unaonyesha kuwa, wapenzi wengi sana hupotoshwa na rafiki zao wasiokuwa na uelewa wa kutosha juu ya tatizo au suala husika la kimapenzi. Ni vema kuwa makini unaposhauriwa.


UTARAHISISHA MAMBO

Mara nyingi washauri huwa si wao wanaokabiliana na mambo, hivyo ni rahisi kwao kupima vitu kwa juu juu tu na kushauri kirahisi rahisi. “Vipi kakupiga namna hii, aaa huyu si mwanaume kwa kweli ni bora ukaachana naye.” Anasema ni bora kuachana naye kwa sababu haumizwi na kuachana, unayeachana ni wewe anayekushauri.

“Mkubali tu bwana unalaza damu, hiyo tabia yake ya uhuni atabadilika, shosti unataka kuacha bahati ipite?” Kwa mshauri ni rahisi kusema hivyo lakini kumbuka ukubwa wa tatizo hatimaye utakabiliana nao wewe. Hii ina maana kwamba, unapofikiria kuhusu ushauri ufikirie pia kuhusu kushauriwa jambo kirahisi, ukiuvaa mkenge mwenye kuumia utakuwa ni wewe.

UTAKUGEUZA

Ulimwenguni kuna aina zaidi ya 1000 za mapenzi na kila mmoja anatajwa kupenda kwa staili zake. Mapenzi ni kama chembe hai nyekundu zilizopo kwenye damu ya mwanadamu ambazo zinaelezwa na wataalamu kuwa hazifanani hata kidogo. Uzoefu unaonyesha kuwa, washauri wengi hushauri kwa uzoefu wao, lakini je ni sahihi uzoefu huo uwe msaada kwa mtu mwingine?

Jibu ni hapana, kinachotokea mara nyingi kwenye ushauri ni mtu kumfanya mwenzake awe kama yeye alivyo, yaani apuuze aamue na apende kama staili yake, jambo ambalo haliwezekani kabisa kwenye mapenzi. Vipi Juma ageuke ghafla awe kama Hassan kwenye suala la mapenzi? Ushauri ni muhimu lakini upime kama unalingana na matakwa yako.

UTAKUONDOLEA UJASIRI

“Kwa maelezo hayo mumeo ni malaya sana, naona itakuwa vigumu kumbadilisha, ni bora ukaanza maisha yako kwa sababu kuna siku hali itakuwa mbaya.”
Huu ni ushauri ambao unaweza kumuondolea mtu ujasiri wa kukabiliana na tabia ya mumewe hadi kufikia hatua ya kumsaidia akaachana na tabia zake mbaya.

Ushauri huondoa ujasiri wa kukabili tatizo hasa pale anayekushauri atakapolipeleka suala lako kwenye njia ngumu isiyokuwa na ufumbuzi. Ikumbukwe kuwa anayeamini kushindwa ni mshauri lakini wewe kama mwanamke unaweza kusimama kutetea penzi lako na kuliweka sawa mpaka jamii ikasema: “Jamani huyu dada kamrekebisha kweli mumewe, hakuwa hivi alikuwa mlevi lakini sasa kaacha pombe.

UTAKUNYIMA FURSA

Kwenye mapenzi kuna fursa nyingi za mafanikio ambazo unaweza usizipate ukiwa mtu wa kusikiliza sana ushauri wa watu. Kuna wakati ambao unatakiwa usimame wewe kuamua kumpenda mtu ambaye jamii inaona kama utapotea.





Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi


Bonyeza Hapa CLICK HERE

 

Ripoti ya Madaktari kuhusu chanzo cha kifo cha mchezaji wa Mbao FC.Fahamu zaidi hapa.

Ripoti iliyotolewa na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Dk. Thoma Rutta na kusomwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, Augustine Ollomi inaeleza kuwa kusimama kwa moyo ghafla  ndio chanzo cha kifo chipukizi wa Mbao FC ya Mwanza, Ismail Khalfan Mrisho.

Taarifa hiyo ilitolewa jana na kamanda huyo alipokuwa akizungumza kuelezea chanzo cha kifo cha mchezaji huyo kilichotokea Jumapili wakati wa mchezo wa Mbao FC dhidi ya Mwadui FC ikiwa ni ligi ya vijana katika uwaja wa Kaitaba mkoani Kagera.

Daktari ametoa taarifa ya uchunguzi na kusema chanzo ni kusimama kwa moyo ghafla. Marehemu hakuwa na jeraha lolote, alisema Kamanda Ollomi.

Ismail Mrisho alizaliwa Mei 22, 1997 akiwa ni mtoto wa kwanza katika familia yao. Amesoma Shule ya Msingi Nyakabungo kuanzia mwaka 2006 hadi 2012. Mwana 2013 alijiunga na Sekondari ya Mwanza ambapo alihitimu mwaka 2016. Ismail alikuwa amepata ufadhili wa kwenda kusoma Chuo Kikuu cha Louisiana State nchini Marekani kuanzia mwakani.

Ismail lifikwa na mauti muda mfupi baada ya kugongana na mchezaji wa Mwadui, alipojaribu kusimama baada ya hapo alianguka tena ndipo alipokimbizwa hospitali mjini Bukoba lakini akafariki. 

Kabla ya kukumbwa na mauti hayo, aliifungia timu yake ya Mbao goli la kuongoza ambapo mchezo ulimalizika kwa Mbao kupata ushindi wa 2-0.




Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi


Bonyeza Hapa CLICK HERE

 

SABABU za Wanawake Kulia Baada ya Kufanya Mapenzi!..Fahamu zaidi hapa.

Kulia baada ya kushiriki ngono au kufanya mapenzi ni kawaida na hushuhudiwa sana kwa wanawake, ijapokuwa imesemekana kuwa wanaume hulia pia.

Kulingana na wataalam, kuna sababu kadhaa ambazo humfanya mwanamke kulia au kujawa na huzuni baada ya kushiriki ngono, na mojawapo ya sababu hizo ni homoni ambazo mwili wa binadamu hutoa wakati huo.

Umewahi kushiriki mapenzi na kugundua kuwa mpenzi wako amelia tu, baada ya kipindi kirefu cha kufurahisha?

Kulingana na wanasayansi, ni kawaida.

Utafiti mwingine umeonyesha kuwa kati ya asilimia saba nukta saba na asilimia thelathini na mbili nukta tisa ya wanawake wamewahi kulia baada ya kushiriki mapenzi.

Mara kwa mara, wanaume hulia pia.

Sababu za wanawake kulia baada ya kufanya mapenzi!

Mtaalam mmoja ameieleza hali hiyo kama 'hali ambayo mwanamke hushindwa kujidhibiti na kulia bila sababu, hasa baada ya kupandwa na raha ya kujamiana, au kufika katika upeo wa raha ya kujamiana (orgasm.)


Umewahi kudhani kuwa 'ustadi' wako ndio uliosababisha kulia kwa mwanamke baada ya kushiriki ngono? Pole sana!

Hata hivyo, mtaalam mwingine amesema kuwa ukweli wa mambo na mawazo yanayokuja punde baada ya kushiriki ngono kama woga, huweza kumfanya mwanamke kulia, ijapokuwa amesisitiza kuwa kulia kwa mwanamke baada ya kushiriki mapenzi ni kawaida!





Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi


Bonyeza Hapa CLICK HERE

 

Download wimbo mpya wa IYO Ft. Diamond Platnumz unaoitwa "Loving You".

Download IYO - Loving You Ft. Diamond Platnumz]



Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi


Bonyeza Hapa CLICK HERE

 

MATUMAINI UPYA KWA FARID MUSSA SAFARI YA HISPANIA, AANZA MAANDALIZI TENA.FAHAMU ZAIDI HAPA.

Kiungo kinda wa Azam FC, Farid Mussa ameanza maandalizi yake tena kujiandaa kwenda Hispania kujiunga na timu yake ya Derportivo Tenerife ya Hispania.


Tayari Farid amepata matumaini mapya baada ya leo kutinga kwenye ubalozi wa Hispania na kuanza kushughulikia kibali cha kufanya kazi nchini humo.

Msemaji wa Azam FC, Jaffar Iddi amethibitisha kwamba mambo yanakwenda vizuri.

"Kuna matumaini makubwa kwamba sasa mambo yataenda vizuri na Farid alikuwa ubalozini kwa kuwa tayari klabu ya Tenerife imeishawasiliana na ubalozi wa Hispania hapa nchini," alisema.

Awali kulikuwa na hofu ya kuua kipaji chake kwa kuwa suala la kibali kilionekana kuwa tatizo huku Farid akiendelea kukaa benchi kwa kuwa hawezi tena kuichezea Azam FC.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi


Bonyeza Hapa CLICK HERE

 

ZARI Athibitisha Yeye na Mama Mkwe Wake Bado Zinaiva.Fahamu zaidi hapa.

 Kuliwahi kuwepo uvumi kuwa Zari na mama yake Diamond Platnumz hawaelewani.

Tetesi hizo zilikuwa kubwa zaidi hivi karibuni baada ya Bi. Sandra kumchunia Zari kumpongeza kwenye siku yake ya kuzaliwa lakini akamtumia salamu ex wa mwanae, Wema Sepetu.

Lakini tangu Diamond na mama yake waende Pretoria, Afrika Kusini kwaajili ya kumwangalia Zari aliyejifungua Jumanne hii mtoto wa kiume, mambo yameonekana kuwa shwari.

Kwanza Diamond aliweka picha kwenye Instagram akiwa na wanawake hao wawili muhimu maisha mwake na mama yake kuirepost. Kwenye picha hiyo Diamond aliandika:

 Earlier today with my Favorite ladies, the ladies behind my success….. @kendrah_michael 💞 @zarithebosslady.”
Jumatano hii Zari ameweka picha na hiyo juu na kuandika: Snacking with mama in law @kendrah_michael what a laid back & chilled day.”

Ni furaha na amani tu kwenye familia ya Chibu kwa sasa.



Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi


Bonyeza Hapa CLICK HERE

 

Download wimbo mpya wa Navy Kenzo ft. Wildad unaoitwa "Feel Good".

Download Navy Kenzo - Feel Good ft. Wildad.





Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi


Bonyeza Hapa CLICK HERE

 

Rais Magufuli afanya mabadiliko kwenye Mikoa na Wizara......Amteua Ole Sendeka kuwa Mkuu wa Mkoa wa Njombe.Fahamu zaidi hapa.




Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi


Bonyeza Hapa CLICK HERE

 

YOUNG Dee Aeleza Sababu ya Kufanya Video na Mpenzi wake Tunda.Fahamu zaidi k hapa.

Rapa Young Dee ambaye kwa sasa anafanya vizuri na wimbo wake mpya 'Furaha' amefunguka na kuweka wazi sababu kubwa iliyompelekea yeye kufanya kazi na mwanamitindo Tunda

Young Dee akiwa kwenye kipindi cha Planet Bongo cha East Africa Radio alisema kuwa aliamua kufanya video hiyo na Tunda kwa sababu kwanza ni mtu ambaye yupo naye karibu hivyo kwake haikuwa kazi ngumu kumuitaji lakini pia adai alikutana na wanamitindo wengine ambao kwake walikuwa wakubwa sana akamua ngoja afanye na mtu wake wa karibu.

"Kwanza unajua sijafanya muda mrefu video ya mapenzi, hivyo nilifikiria nikaona Tunda ni mtu sahihi kwanza ni mtu wangu wa karibu hivyo nikaona akisimama yeye kwenye video hii ataleta maana zaidi kwa kile nilichokuwa nimelenga kukifikisha kwa jamii, maana nilikutana na wanamitindo wengine kwangu walikuwa wakubwa sana. Lakini pia nikiwa na Tunda muda wote kwangu ni furaha tu" alisema Young Dee.

Mbali na hilo anadai kuwa kipindi ambacho aliachia wimbo wake wa 'Hands up' ni kama alikuwa amewahi sana kwani alikuwa anajiona anahitaji kupumzika kwanza, kujijenga upya ili kuingia kwenye ushindani kweli na kufanya kazi rasmi.

"Kipindi kile kiukweli niliwahi sana maana tulikuwa na mizuka sana lakini kuna siku nilipost picha Instagram mimi mwenyewe nilijiona nimekonda kweli, nikaona nahitaji kupumzika, kulala vizuri na kufanya mazoezi ili nikirudi nirudi kweli ndiyo kama sasa nipo fiti kwa ushindani ndiyo maana nimekuja na hii kazi ya 'Furaha'" alisema Young Dee




Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi


Bonyeza Hapa CLICK HERE

 

Download wimbo mpya wa BEKABOY Ft Christina Shusho unaoitwa "Akutendee Nini".

Download BEKABOY-Akutendee Nini _ Christina Shusho.





Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi


Bonyeza Hapa CLICK HERE

 

Download wimbo mpya wa Darassa Ft. Ben Pol unaoitwa "Muziki".

Download Darassa Ft. Ben Pol - Muziki


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi


Bonyeza Hapa CLICK HERE

 

Rais Magufuli Aongoza Kikao cha Barazs la Mawaziri Ikulu Dar es Salaam.Fahamu zaidi hapa.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongoza Kikao cha Baraza la Mawaziri kilichofanyika leo tarehe 07 Desemba Ikulu jijini Dar es Salaam. Kikao hicho pia kilihudhuriwa na Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan pamoja na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa. PICHA NA IKULU.



Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi


Bonyeza Hapa CLICK HERE

 

SHILOLE na Mpenzi Wake Mpya Wavujisha Video Wakidendeka..Mashabiki Wauzika.Fahamu hapa.

Katika mitandao ya kijamii wiki hii imesambaa video inayomuonyesha msanii wa muziki, Shilole akiliwa denda ya kijana ambaye jina lake halikutambulika mara moja kitu ambacho kimewakera mashabiki wake.

Hii imekuwa ni tabia ya mastaa wengi kuvujisha video zao za siri hali ambayo inasababisha taharuki katika mitandao ya kijamii.

Baada ya kusambaa kwa video hiyo mashabiki wake wameonyesha kuchukizwa na kitendo hicho. Haya ni baadhi ya maoni ya mashabiki hao.

elizabethsommy
Shilole huna stress lkn my Dada duu cjawahi yaona haya kwako veeeepeeeeeee my sister wanaumeee haoo

zam_nasso
Hili lidada ni hayawani sana nawaonea huruma watt wake wanaona uchafu wa mama yao.

Da_dija
Afu aftr deiz utasikia wanajitia kupanick y hzo video zimerushwa without their willin’ wkt they keep a poz wanapojirecord, then hawachelewi kusema wamebakwa. anyways nilikuwa nauliza hizi sheria za mitandaoni zipo au zimetumbuliwa!!!!????.

ishaa_mashauzy
Eeeeee mungu huku tunakoendea mtatuonyesha hadi mkiwa mnakwichkwich alafu @shilolekiuno_badgirlshishi siuna watt wakike wakubwa unafikiri hawaoni haya looooooooooh

saratz
Anapenda vitoto uyu Dada tena bora kiwe kitoto cha umri wake sasa iki ni kidogo kuliko yeye VIDEO:




Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi


Bonyeza Hapa CLICK HERE

 

Mameja Jenerali Wapya Wavishwa Vyeo Vyao Makao Makiu ya JWTZ.Fahamu zaidi hapa.

 Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania Jenerali Davis Mwamunyange (kushoto) akimvisha cheo cha Meja Jenerali Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa Brigedia Jenerali Michael Isamuhyo, Makao Makuu JWTZ Upanga Dar es Salaam.
 Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania Jenerali Davis Mwamunyange (Kushoto), akimvisha cheo cha Meja Jenerali,Mkuu wa Kamandi ya Jeshi la Anga Brigedia Jenerali George William Ingram,Makao Makuu JWTZ Upanga Dar es Salaam.




Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi


Bonyeza Hapa CLICK HERE

 

MWIMBAJI Darasa Afichua Siri ya Nyimbo zake Kupendwa.Fahamu zaidi hapa.

Muimbaji huyo ameliambia gazeti la Mtanzania kuwa baada ya kushindwa kufanya vizuri kwenye nyimbo za ujumbe ndio akaangalia ni kitu gani mashabiki wanataka akaamua kubadilika.

“Mwanzo nilikuwa nikitoa nyimbo zenye vionjo vyenye ujumbe wa kutosha lakini hazikuwa zikipokelewa sana ila nilipokaa na kufikiria zaidi, nikatambua nini mashabiki wanataka na ndiyo maana muziki wangu upo juu sana tofauti na zamani,” amesema.

Rapper huyo kwa sasa anafanya vizuri na wimbo wa ‘Muziki’ uliogeuka kama wimbo wa taifa kwa sasa.



Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi


Bonyeza Hapa CLICK HERE

 

Monday, 5 December 2016

#YALIYOJIRI>>>Fundi Pancha Atupwa Jela Miaka 30 Kwa Kukutwa na Misokoto 601 ya Bangi.Fahamu zaidi hapa.

Fundi wa kuziba pancha, Harson Solomon (38), mkazi wa wilayani hapa amehukumiwa kifungo cha miaka 30 jela baada ya kutiwa hatiani kwa kupatikana na misokoto 601 ya bangi. 
Kifungo hicho kimeangukia sheria mpya ya udhibiti wa dawa za kulevya iliyosainiwa Mei 11, 2015 na aliyekuwa Rais wakati huo, Jakaya Kikwete. Imeelezwa Solomon ni miongoni mwa washtakiwa wa mwanzo kufungwa kwa sheria hiyo. 
Awali, sheria ilikuwa inatoa mwanya wa faini na mtu anaposhindwa kulipa ndipo hutumikia kifungo jela lakini hivi sasa anayepatikana na hatia ya kukutwa na kiwango kikubwa hutupwa jela. 
Kifungu cha 11(1) D cha sheria hiyo mpya, kinaeleza wazi mtu anayezalisha, kumiliki, kuuza, kununua au kusafirisha dawa za kulevya ikiwamo bangi, adhabu ya chini ni kifungo cha miaka 30 jela. 
Hukumu hiyo ilitolewa jana na Hakimu Mkazi Mfawidhi, Joachim Tiganga baada ya kuridhishwa bila kuacha shaka na ushahidi wa upande wa mashtaka. 
Wakili wa Serikali, Ignas Mwinuka alidai kortini kuwa Desemba 1, 2015 katika maeneo ya Mwika Kimangara, Moshi Vijijini mshitakiwa alipatikana na kiasi hicho cha bangi.
 Pia, anadaiwa kuruhusu eneo lake kutumika kuuza bangi na gongo. 
Akisoma hukumu, Hakimu Tiganga alisema matumizi ya dawa za kulevya yanazidi kuongezeka nchini na kuathiri jamii, hivyo Mahakama inatoa adhabu hiyo iwe fundisho kwa wengine. 
Katika kipindi chote tangu afikishwe kortini kwa mara ya kwanza Desemba 11 mwaka jana, mshtakiwa alikana mashtaka hadi alipotiwa hatiani na kuhukumiwa jana.



Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi


Bonyeza Hapa CLICK HERE

 

DEREVA Aliyeachia Usukani wa Basi Huku Akicheza Wimbo wa Darasa Mikononi Mwa Polisi Kwa Kuhatarisha Maisha ya Abiria.Fahamu zaidi hapa.

Yule Dereva aliyepagawa na nyimbo Mpya ya Darasa na kisha kuacha kuendesha Gari na kisha kuanza kucheza mziki huo huku gari hilo likiwa kwenye mwendo akamatwa na Polisi..
Hawa ndio wahusika walio kuwepo kwenye tukio hilo..

Dereva huyo ambaye ameonekana kwenye video akiwa anaendesha gari aina ya Coster ambayo inafanya safari zake Dodoma kwenda itigi akiwa anafanya kitendo cha hatari cha kuacha gari likiwa kwenye mwendo na kisha yeye kusimama na kuanza kucheza muziki huo akamatwa na Polisi na kesho atapandishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazo mkabili yeye pamoja na wenzake ambao alikuwa nao kwenye Gari hilo.
Kama Hujaona Hiyo Video Hii Hapa Chini:





Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi


Bonyeza Hapa CLICK HERE

 

#YALIYOJIRI>>>>PICHA: Ajali ya Lori na Hiace Yaua Watu 9 na Kujeruhi 18.

Watu tisa wamefariki dunia na wengine 18 kujeruhiwa katika ajali ya gari iliyotokea eneo la Ifunda mkoani Iringa jana baada ya lori kugonga gari dogo la abiria aina ya Toyota Hiace. 

Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza alisema dereva wa lori hilo lililokuwa likitokea Mbeya kuelekea Dar es Salaam, alishindwa kufunga breki na kuigonga Hiace hiyo iliyokuwa imeegeshwa pembeni ya barabara. 
“Lori limeharibika kabisa na Hiace pia imeharibika kabisa,” alisema Kamanda Masenza. 
“Lori hilo liliposhindwa kufunga breki liliigonga Hiace ambalo lilikuwa na abiria na kwenda mbele na kisha kugonga watembea kwa miguu,,” 
Masenza alisema katika ajali hiyo iliyotokea jana jioni, madereva wa magari hayo wote wamejeruhiwa na wamelazwa Hospitali ya Mkoa wa Iringa pamoja na majeruhi wengine. 
“Dereva mmoja yupo chumba cha upasuaji kwa kuwa mguu wake umevunjika na mwingine yupo wodini,” alisema